CC ya CCM haikuwa na jipya

CC ya CCM haikuwa na jipya

Kama kuna ulazima wa kunukuu...basi hata nukuu maneno machache.

Ni kweli mkuu, unakuta thread imekuja jamaa amekuwa wa kwanza ku-comment, ajabu ana-quote kwanza. Nafikiri watu hatujui nini maana ya Quote!
 
Hivi kikao sikinakaliwa leo ss mleta uzi mbona umetoa taarifa kabla ya kikao kuketi? Au nimaono!
 
Hata Nyerere ASINGE MFUKUZA Lowassa miezi 9 kabla ya uchaguzi

Haya sijui Lowassa kajadiliwa,sijui kafukuzwa ni mbwembwe tu

Unamfukuza Lowassa kwakosa gani? Huyu ni mwanaCCM wa ukweli hamna shaka na atabakia kuwa hivyo.
 
Hivi mnafikiri kunaweza kuwa na jipya katika ccm hii! Nothing number ni zilezile na huyo mwenyeiti wao ni kama kondoo hawezi fanya chochote.
 
Agenda ya masai kumbe uwongo!

Kumbe wewe ulitegemea wamjadili kwa ubavu upi? Nao wana akili wanajua wajumbe wote kuanzia mkutano mkuu, halimashauri kuu hadi kamati kuu robo tatu ya wajumbe wake wapo kwa Edo sasa hio hoja itapitia wapi? Na aliekudanganya J.K. hayupo na Edo ni nani?
 
Huyu jamaa mpuuzi na muongo wa kutupwa kazi yake kutunga uongo tu cc wanakaa leo hicho anachosema kimekaa jana labda aliitisha petro mselewa ila siyo jk

Wewe hujui kuwa kuna kikao nje ya kikao? Au unadhani kikao lazima kiwe kile cha ukumbini pekee?
 
Ukiwa muongo lazima kwanza kabla ya kuleta uongo wako uwe unajitahidi kuangalia ukweli wa suala unalotaka kulitengenezea uwongo

Eti Kamati Kuu ya CCM ilikaa na kuwaongelea wagombea wa Urai na uchaguzi wa serikali za mitaa.

Tatizo lenu vijana wa BAVICHA mnadhani mnafamu wakati hamfahamu lolote. Hata wanaokubaliana na uwongo wako ni kundi lenye fikra kama zako.

Kwa taarifa yako kikao kilichofanyika juzi ni Kamati Kuu Maalum ya NEC.

Inayofafanya kikao leo ni Kamati Kuu.

Hivi ni vikao viwili tofauti ambavyo vina wajumbe tofauti na majukumu tofauti.

Kwa mwanaCCM hai yoyote anafahamu tofauti yake achilia mbali mfanyakazi wa CCM.

Huyu eti ndiyo anawadanganya ni mfanyakazi wa CCM na wao wanakubali.

Wajinga ndiyo waliwao
Nakuunga mkono uzushi umezidi CC inakutana leo na watu hawajui hats protocol za chama wanatunga hata utunz kuwa kinana alisoma mashtaka mapya sio kazi take hiyo no kazi ya mangula.kutunga kwa lengo LA kuchafua watu no jambo bays sana
 
Kamati Kuu ya CCM iliyoketi leo Kisiwandui,Zanzibar ilitawaliwa na pongezi pamoja na maagizo ya hapa na pale ya kichama. Taarifa za kuaminika toka ndani ya kikao husika zinaonesha kuwa CC imepitisha karibu maazimio yote ya Kamati ya Komredi Mangula.

CC imepongeza ushindi kwenye Serikali za Mitaa. Pia CC imeipongeza Kamati Maalum ya Maadili chini ya Komredi Mangula kwa kuwabana na kuwarekebisha wagombea watarajiwa wa Urais.

"Hapo CC imesifu na kupongeza mwenendo wa wahusika kwasasa na kuwaona wanaofuata taratibu za chama. Hakukuwa na mjadala mkali kama ilivyotarajiwa" kilisema chanzo hicho toka Kisiwandui.

CC pia imempongeza na kumpa baraka Rais na Mwenyekiti wa CCM Taifa kwa jinsi anavyoendelea kulishughulikia kwa weledi sakata la Escrow. Mwenyekiti ameahidi kuwa makini na mtenda haki katika hilo.

CC imeiagiza Sekretarieti ya CCM kufanya maandalizi kabambe ya Kura ya Maoni na uchaguzi mkuu kwa kutoa Ripoti mara kwa mara juu ya mikakati inayoendelea. Sekretarieti imeruhusiwa kuunda kamati mbalimbali za wataalamu ili kufanikisha maandalizi hayo.

CC imetambua na kupongeza ziara za kuimarisha chama na kukagua utekelezaji wa Ilani zilizofanywa na Sekretarieti chini ya Katibu Mkuu Kinana.

"Hayo ndiyo makubwa humo. Kikao hakikuwa na mjadala mkalí. Kilitawaliwa na busara" kimesema chanzo cha taarifa hii.

Mzee Tupatupa wa Lumumba,Dar es Salaam
 
kwi kwi kwi kwa kwa Ushindi wakati miji yote mikubwa wamepoteza haya katiba itawatokea puani sijamona aliyejirekebisha zaidi ya kuendelea kutoa pesa na mtoa pesa katumia magazeti kuwatisha wameufyata chezea jamabazi la Richimond , Epa nakadharika
 
Hata sikutegemea lolote la zaidi kutoka kwenye vikao vyao.
 
Kikao hicho kinathibitisha ule msemo unaosema ukishangaa ya Mussa utayaona ya Firauni!

Hivi watanzania wataielewaje CC ya CCM, wanapoisikia inaibuka na tamko la kumpongeza JK, wakati kiporo chake cha Muhongo, kuhusiana na Escrow account, ambacho aliahidi 'kukitafuna' baada ya siku 2. baada ya kile kikao chake na wazee wa Dar, hivi sasa inakatika wiki ya tatu, kiporo hicho JK ameshindwa 'kukitafuna' kwa kuwa 'kimechacha' ile mbaya?!
 
Hakuna jipya poleni sana mliopoteza ndugu zenu kwa kukosa dawa pale Sewa na Mwaisela huku watu wakila raha Kisiwandui.
 
Ina maana CCM hawakuona hata chembe ya sehemu wanapostahili kujirekebisha, zaidi ya pongezi tu. Kweli hiki chama changu sasa kimekwisha.
Tatizo la kuwa na watu wote wanaomuogopa Mhe, Rais. Hakuna hata mmoja anayeweza kuthubutu kumwambia ukweli wa hali halisi uku nje.
Nimekatishwa tamaa sana. Bussness as usual..!!
 
Back
Top Bottom