CAG sio Muongo kwa vigezo hivi

CAG sio Muongo kwa vigezo hivi

Ukiumizwa/kuudhika na kauli za watu wa hovyohovyo na wewe unakuwa dhaifu,hao dawa yao ni kuwapuuza tu.
 
Kwanini Asaad kulidhalilisha bungu ughaibuni iwe sahihi lkn yeye akidhalilishwa isiwe sahihi? Mungu mwenye haki zote ANAWAONENI
Asaad
Kwanini Asaad kulidhalilisha bungu ughaibuni iwe sahihi lkn yeye akidhalilishwa isiwe sahihi? Mungu mwenye haki zote ANAWAONENI
Asaad hajalidhalilisha bunge wala hilo Bungu ulilokusudia.
Unaujua udhaifu maana yake?
 
Kwa hiyo sasa hivi inabidi tuongozwe kwa trust na sio uwazi na uwajibikaji!!?
Mkuu Dyuteromaikota, you are right, sasa ni mwendo wa trust tuu, mambo ya transparency na uwajibikaji waachie wengine, ndio maana Tanzania tumejitoa kwenye ule mkakati wa open government Initiatives.
P
 
Mimi naomba niendelee kumtia CAG wetu Profesa Assadi moyo.
Kanyaga twende Baba, Usicheke na kima.

Sisi wamasai hua tunaamini Dawa inayoponyesha ni ile chungu.
 
Mkuu Abdul Nondo, kwanza asante kwa nondo hii, sidhani kama mtu mzima mwenye akili timamu kichwani kwake anaweza kumuita CAG ni muongo, ujue tuna vichaa wengi kuliko tunavyojijua.

Kwa vile humu sio members wote wanaweza kusoma kila kitu, ni vema pia ungeweka ref ya aliyemuita CAG muongo kama hivi

Ila kwenye ripoti ya CAG, sio kila upotevu wa fedha za umma au matumizi makubwa ya fedha kwenye manunuzi bila kufuata taratibu ni matumizi mabaya ya fedha za umma au ni ufisadi.

CAG anakagua kufuatwa kwa sheria taratibu na kanuni za matumizi ya fedha za umma. Hivyo kuna maeneo ni kweli sheria taratibu na kanuni zilikiukwa lakini fedha zikatumika vizuri kwa ajili ya manufaa ya taifa mfano mzuri ni fedha za kununua zile ndege mpya, hazikufuata mchakato wa manunuzi wala taratibu za matumizi ya fedha za umma, ikiwemo kupangiwa bajet, kuidhinishwa na Bunge, CAG kusaini etc, kwa vile tumefanya manunuzi kwa utaratibu mpya wa Rais Magufuli unaoitwa kupiga tanchi, hatimaye ndege zimekuja na tumezishuhudia.

Hata matumizi makubwa kwenye Vote 20, japo hayakuidhinishwa na Bunge, lakini ni matumizi mazuri tuu, sote tunashuhudia rais wetu katika ziara zake, anatembea na mabulungutu ya hard cash na kugawa kwa wananchi.

Pia kuna maeneo ya matumizi makubwa, sheria taratibu na kanuni zote zimefuatwa, lakini huko ndiko tunapigwa.

Ukaguzi huanza kwa Entrance Meeting na kumalizika kwa Exit Meeting, hivyo inawezekana hadi CAG anafanya exit meeting, hizi sare za Polisi zilikuwa hazijaingia, lakini baadae ziliingia na ni kweli ziko ndani ya makontena.

Japo Ripoti ya CAG sio Masahafu au Bible, ila kiukweli kabisa aliyemuita CAG muongo, sikuzote ni kama kituko fulani.
P
Brother how do you know kama yalitumika kwa makusudi yaliyokusudiwa kama hakuna nyaraka? Usitetee kubadilisha matumizi ya fedha kama eti yalikua na nia nzuri simply because Kuna jambo jema limefanywa Hilo jambo jema nani anajua gharama halisi? "Government works on paper" kama no ivo Kuna haja gain ya kuwa name mpango wa matumizi?
Nini maana ya BUNGE kuwepo?

Usitetee ufisadi kwa kutaka cheo kama MUSIBA
 
Wewe nawe sijui nikuite Kilaza au nani!?!? Lugola kawa waziri wa mambo ya ndani tangu lini? Unabiwa ni issue ya 2015 November wakati hata serikali haijaanza kufanya kazi sawia. Muwe mnaficha ujinha wenu sometimes.
Tangu mwaka wa fedha 2015/2016, 2016/17 hadi 2017/2018 kumekuwa hakuna vielelezo!; Management responses za query hii hatuzijui na namna ya kuclear ni kuonyesha vielelezo vinavyotakiwa ni siyo vinginevyo. Naona kuna tatizo kubwa la kuchanganya siasa na uwajibikaji.Utetezi wa waziri bungeni hakufuti au kuondoa doa hili.
 
Nimeelewa.
Shukrani Mkuu Nondo kwa Nondo hizi
 
Mimi niliwahi kushauri viongozi wetu wapimwe afya ya akili from time to time, wanaweza kuingia wakiwa timamu, halafu ukichaa ukawapata, namna rahisi ya kutambua mushkeli wa afya ya akili zao ni kwa maneno yao na matendo yao.
P
Ushauri mujarabu sana huu naona wanasubiri hadi mheshimiwa mmoja avue nguo hadharani ndio wajue umuhimu wa kupima akili
 
Wapigaji wa madeal ktk jeshi la polisi ni wakubwa wa level ya makao makuu. Baada ya kuona CGA kawachungulia wamenyofoa sehemu kuokoa jahazi. Na hizo hela walizokimbiza kwenda kuleta hayo magwanda ni za activity nyingine. Akija tena CAG kwenye mwaka mwingine atakutana na gap lingine. Hela iliyopigwa ni kubwa kuiziba ni mgumu...hapo wanazungusha hela za Magu tu. Wamepigwa hoja ya Lugumi wakavuta hela ya magwanda wakaimbiza China kuleta vifaa, wamepigwa hoja ya magwanda wamenyofoa hela za kazi fulani wamekimbiza China kuleta magwanda, mwaka ujao watapigwa hoja ya hiyo hela... subirini!
 
Mkuu Abdul Nondo, kwanza asante kwa nondo hii, sidhani kama mtu mzima mwenye akili timamu kichwani kwake anaweza kumuita CAG ni muongo, ujue tuna vichaa wengi kuliko tunavyojijua.

Kwa vile humu sio members wote wanaweza kusoma kila kitu, ni vema pia ungeweka ref ya aliyemuita CAG muongo kama hivi

Ila kwenye ripoti ya CAG, sio kila upotevu wa fedha za umma au matumizi makubwa ya fedha kwenye manunuzi bila kufuata taratibu ni matumizi mabaya ya fedha za umma au ni ufisadi.

CAG anakagua kufuatwa kwa sheria taratibu na kanuni za matumizi ya fedha za umma. Hivyo kuna maeneo ni kweli sheria taratibu na kanuni zilikiukwa lakini fedha zikatumika vizuri kwa ajili ya manufaa ya taifa mfano mzuri ni fedha za kununua zile ndege mpya, hazikufuata mchakato wa manunuzi wala taratibu za matumizi ya fedha za umma, ikiwemo kupangiwa bajet, kuidhinishwa na Bunge, CAG kusaini etc, kwa vile tumefanya manunuzi kwa utaratibu mpya wa Rais Magufuli unaoitwa kupiga tanchi, hatimaye ndege zimekuja na tumezishuhudia.

Hata matumizi makubwa kwenye Vote 20, japo hayakuidhinishwa na Bunge, lakini ni matumizi mazuri tuu, sote tunashuhudia rais wetu katika ziara zake, anatembea na mabulungutu ya hard cash na kugawa kwa wananchi.

Pia kuna maeneo ya matumizi makubwa, sheria taratibu na kanuni zote zimefuatwa, lakini huko ndiko tunapigwa.

Ukaguzi huanza kwa Entrance Meeting na kumalizika kwa Exit Meeting, hivyo inawezekana hadi CAG anafanya exit meeting, hizi sare za Polisi zilikuwa hazijaingia, lakini baadae ziliingia na ni kweli ziko ndani ya makontena.

Japo Ripoti ya CAG sio Masahafu au Bible, ila kiukweli kabisa aliyemuita CAG muongo, sikuzote ni kama kituko fulani.
P
Copy n paste.
NIMEMSIKILIZA LUGOLA, KISHA NIKAREJEA RIPOTI YA CAG, NDIPO NIKAGUNDUA KWANINI LUGOLA ALITAKA KUVUA NGUO.

Ripoti ya CAG kuhusu sare za Jeshi ,Kurasa No. 310

" Kukosekana kwa nyaraka za kuthibitisha uletaji wa mzigo. Niliomba Hati ya kupokelea Shehena ya Mzigo Bandarini (Bill of Lading), Hati ya Madai kutoka kwa Mtengenezaji (Commercial Invoice), Hati ya Mzigo ulipotoka (Certificate of Origin), orodha za mali zilizopo kwenye meli (Packing List) na cheti cha ukaguzi wa bidhaa (Inspection Certificate) kutoka kwa Mzabuni Daissy General Traders kwa ajili ya kujiridhisha kama bidhaa husika zililetwa nchini. Hata hivyo, Mzabuni alishindwa kuwasilisha nyaraka hizo.

Aidha, nilipitia Mfumo wa Forodha (TANCIS) wMamlaka ya Mapato (TRA) na kubaini kuwa hapakuwa na shehena yoyote kutoka kwa Mzabuni Daissy General Traders mwezi Novemba 2015. d) Vilevile, nilifanya mahojiano na Maofisa wa Bohari kuu ya Jeshi la Polisi na kubaini hakukuwa na Sare zozote zilizoletwa na Mzabuni Daisy General Traders mwezi Novemba 2015. Hivyo, Serikali imepata hasara kubwa kwa kufanya malipo ya Sare za Polisi ambazo hazikuletwa na Mzabuni. Kuhusu suala hili, nashauri Mzabuni Daissy General Traders arejeshe kiasi alicholipwa kwa kutoleta Sare za Polisi na hatua stahiki za kinidhamu na kisheria zichukuliwe kwa Maofisa wote wa Jeshi la Polisi kwa kuisababishia Serikali hasara. "
 
Asante bwana Madelu kwa kumchimbua huyu dogo toka mafichoni na kumbambikia kesi. Wengi wetu tulikua hatumjui.

Mwaga nondo kijana...sisi tunaotumia akili tu ndio tutaelewa ila wasio na akili hawezi kuelewa kinaongelewa nini.
 
Hivi kwani kangi hayupo humi kweli aje atuambie hizo pumba anazo ongea ni za mpunga au mahindi
 
Kwa hiyo sasa hivi inabidi tuongozwe kwa trust na sio uwazi na uwajibikaji!!?
Pascally unaibagaza tu taaluma yako ya uandishi kwa kusema kila akisemacho Rais ni kweli tupu, nae ni mwanadamu pia kama wewe anaweza asiseme kweli wakati fulani for a political circumstances,

Hata albashir wa Sudan alikuwa Rais na upo uwezekano wakati fulani aliwaaminisha wananchi wake kwamba yeye ni muadilifu na sio mwizi wa mali za umma, lakini wanasudan walivyokinukisha tuliona maburungutu ya madolari na mapaundi aliyoyaficha nyumbani kwake.

So sio kisa ni Rais tumuamini kwa kila kitu yeye sio mungu. Jikite kwenye ufisadi wa jeshi la polisi, huku kwa Rais unaibagaza taaluma yako tu.
 
Nina Amini Kwamba Wengi Wenu Mmeanza Kuziona Report za CAG Awamu Hii, Sio Kosa Letu, Tecno Zenu zinawafanya Mnakuwa na High Sessional Ya Kuongea Kila Jambo.
 
Mkuu, huwa naamini sana katika busara zako ila hapa nadhani umepotoka au unataka kupotosha japo sidhani Kama una maslahi yoyote katika kufanya hivyo.

Unasema report ya CAG sio msahafu, hii ni kweli maana report inaweza kuwa na mapungufu kadha wa kadha. Ila ambacho sikubaliani na wewe ni hapo unapobariki manunuzi yasiyofuata kanuni, taratibu na sheria za fedha eti kwa kigezo kwamba manunuzi hayo yalifanyika kwa manufaa ya umma na umetolea mfano manunuzi ya ndege. Hii sio sawa mkuu.

Kama tuliweka taratibu/kanuni/sheria za manunuzi basi ni lazima zifuatwe na mtu akiacha kuzifuata anapaswa kuwajibishwa kwa maana kutofuata sheria halali zilizowekwa ni kosa kisheria na huwa tunasema no one is above the law, hata rais mwenyewe hayupo juu ya sheria.

Najua kuna ideology mbili katika kufanya maamuzi ambazo ni rule based na result based, wewe umebase kwenye result based, kwamba japo sheria hazikufuatwa ila results zimekuwa nzuri Sasa swali ni je vipi ingetokea result mbaya, mfano tungekuwa tumepigwa, ungekuwa na msimamo huo huo?

Halafu Kama unaongozwa na good will kwanini usifuate taratibu katika manunuzi? Watu wasio safi ndio mara nyingi huwa hawafuatwi sheria. Nahitimisha kwa kusema japo report ya CAG sio msahafu ila kwa kuwa nyaraka za manunuzi hazipo na taratibu zilisiginwa basi ni lazima watu wawajibishwe no matter results walizo deliver. Na hizo ndege naamini tumepigwa na ipo siku ukweli utaelezwa na inshaalah wote waliohusika watawekwa behind bars.
Ndugu dawa yenu

Pascal Mayalla ni verified user na sio kama mimi na wewe. Kwahiyo msome vizuri.

Pascal ni yuleyule na hajabadirika na alichokiandika kisome vizuri, utagundua hoja zake ndio haswa ni kile ulichokisema wewe. Huna haja ya kupingana nae, msome vizuri kwenye mistari yake huku ukizingatia "inayo trend kwa sasa" nina amini utamuelewa

Usisahau aliwahi kutuhumiwa na kuitwa mzobe mzobe kwa kosa dogo tu la mtu kutoizingatia alama ya kiulizo matokeo yake maoni yake huru yenye maneno zaidi ya mia mbili yote yakaharibika kwa kukosewa tu kuiona alama ya kiulizo. Watu zaidi ya 300 walioaminiwa na watanzania kutusimamia mambo yetu wote walipata upofu hawakuiona hiyo alama ilhali iliendelea kuwepo.

Kamati yenye wataalam wakatumia muda wao hadhim wa kufanya mambo muhimu kwa kujikita kuhukumu jambo kwa kushindwa tu kuiona alama ya kiulizo.
 
Back
Top Bottom