Bwana Mtei matatani kwa kumchukua mwanamke msukule

Bwana Mtei matatani kwa kumchukua mwanamke msukule

52ded72bba96f9dbd3893b9bb3869cf5.jpg

Haika tulia kesho upige pesa
 
Najiuliza tu mwemyewe hivi kama ni ukweli hiyo familia ingekuja hapa kusema ni kweli?
 
Issue ya misukule ni uongo wa hali ya juu kuwasadikisha watu kuwa mtu anaweza kufa/kuchukuliwa msukule mbali na makazi ya binadamu ili afanyishwe kazi na kisha mganga mashuhuri ( wa kufufua misukule) au mhubiri mashuhuri (kama afanyavyo gwajima) aweza kumfufua na kumrejesha katika utu wa kawaida!this is a satanic illusion! Baya zaidi jamii zetu za kiafrika zimekumbatia sana imani hii na kuendelea kutapeliwa kila siku
Ungeongezea nyama kidogo kwenye maelezo yako kwa nini unaamini kwamba imani hiyo ni uongozi kuliko kutoa maelezo ya jumla.
 
Wakuu sijapenda treatment aliyofanyiwa huyo mdada
It is obviously a mental retarded case
Anaonekana amedhoofu kwa njaa na kiu badala ya kumsetiri na kumhudumia kwanza wanambwaga kwenye gari na kupiga picha
Hakika mungu anawaona kwa kukosa kwao ubinadamu
Pia hatujui huko mbele alikopelekwa(polisi) watamhudumia au ndio watamtreat kama wanavyowafanyia vibaka?

Hivi kweli hadi leo bado watu wana fikra za Msukule? Ama kutuhumu mtu kwa kiasi hicho? NO!

Mungu teremsha mikono yako uwafumbue maarifa binadamu hawa na kuokoa kiumbe wako
 
Aisee watu wa Gogoni, Kibamba, Kiluvya toeni taarifa kamili naona hatujapata ukweli
 
huyo dada inasemakana sio msukule bali ana matatizo ya akili juzi alienda kituo cha polisi mbezi akaingia chooni akakaa muda sana baadae askali wa kike wakamuogesha na kumsitili na akawakimbia
anawezekana akili yake inamtuma kukaa chooni tuu
Mtei naona unajitetea kiaina tehe tehe tehe.
 
Ngoja siku wakichukua ndo utakja ku
Issue ya misukule ni uongo wa hali ya juu kuwasadikisha watu kuwa mtu anaweza kufa/kuchukuliwa msukule mbali na makazi ya binadamu ili afanyishwe kazi na kisha mganga mashuhuri ( wa kufufua misukule) au mhubiri mashuhuri (kama afanyavyo gwajima) aweza kumfufua na kumrejesha katika utu wa kawaida!this is a satanic illusion! Baya zaidi jamii zetu za kiafrika zimekumbatia sana imani hii na kuendelea kutapeliwa kila siku
amini
 
Hayo Mambo huwa yapo Sana kiafrica Sema ukimfanyia hvo ndugu nikijua Tu umekwisha na wewe .yani kafanywa kama mnyama vile.
Aisee Kama yangu lazima tuonane wabaya.
 
Issue ya misukule ni uongo wa hali ya juu kuwasadikisha watu kuwa mtu anaweza kufa/kuchukuliwa msukule mbali na makazi ya binadamu ili afanyishwe kazi na kisha mganga mashuhuri ( wa kufufua misukule) au mhubiri mashuhuri (kama afanyavyo gwajima) aweza kumfufua na kumrejesha katika utu wa kawaida!this is a satanic illusion! Baya zaidi jamii zetu za kiafrika zimekumbatia sana imani hii na kuendelea kutapeliwa kila siku
Unazan hii ni kwa africa tu,uko wrong mkuu.bara la asia ni balaaa kwa haya mambo.kwa kifupi hata marekan ushirikina na hiz man zipo na uko ndo wanaongoza.sio tu africa mkuu.ss africa hta kwa uchawi ni wa mwisho
 
Wenzetu wakiokota mbwa kakonda wanamhifadhi na kumpa joto na kumpa chakula halafu kumtibu.
Lakini huku ndio kwanza anatupwa kama mzoga na kuangaliwa kama filamu bila haya, sijui wanawaza nini kwa ufupi tuna watu zaidi ya wanyama
 
Dah hizi pesa lakini ?? Mtu unamficha mwenzako utafikiria ume muumba wewe
 
Mmhh mbona inasikitisha? Tatizo kubwa la watu na hii mitandao ya sasa ni kuwahi kutuma picha au kuandika kitu asicho na uhakika nacho. Hebu yeyote mwenye taarifa sahihi kwa tukio hili alitolee maelezo vizuri. Na si ustaarabu kupiga picha zisizo staha na kuziweka vile. Na kwa muonekano wa picha hakuwa na madhara maana yupo karibu na watu hivyo ni rahisi kumsitiri. Hebu jiulize ikadhibitishwa kuwa ni mgonjwa wa akili aliyepotea huko kwao wewe uliyewaza msukule au nini utajisikiaje nafsini mwako? Kwa muonekano wa picha tu yawezekana alidumbukia labda kwa bahati mbaya na kwa sababu hajitambui ndo ikawa hivyo. Na pili vyombo vyetu vya usalama wa raia, ishu kama hii waipatapo wanatakiwa kuifanyia kazi na kutolea ufafanuzi ili isiwaathiri watu wengine.
 
Ila jamani watanzania huku tuendako sasa ni pabaya! ! Hiyo mijimama hapo na mivitenge yao imeshindwa kumsitiri huyu mwanamke? Eti watanzania ni wakarimu!!?!

Halafu huyo mbona anaonekana kwamba alishawahi kuwa na mimba (kujifungua)? Hilo tumbo na hayo maziwa ni kama a kuna viumbe wamevitumia! Bado anaonekana sio mtu mzima sana na pia nywele sio mbaya sana ila MWILI umetumika sana plus kukosa lishe.

Mambo ya uchawi kwa Tanzania yetu wala sio la kuonea haya!! Siku hizi mabinti wadogo sana na vijana (baadhi) kimbilio Lao ni kwa babu (ukiangalia conversations zao instagram). Kwa wafanya biashara huko ndo kumeoza! ! Asilimia kubwa sana ya wafanyabiashara wanatumia ndumba ila wanatafautiana viwango vya kafara na wala hii sio siri!!

Tunavyozidi kujifanya eti "tupo Karen ya 21 hakuna mambo ya kichawi"...ndipo wenye fani zao wanafanya yao!!

**Kuna siku nilikua naenda kazini na wenzangu shift ya alfajiri ( saa tisa na nusu usiku) tukapita mitaa ya steers ya zamani Posta, tukiwa kwenye gari tuliona mbele yetu watu watatu mmoja kakaa chini wale wawili wanammwagia ma vitu (kama majani mengi), driver wetu akazima taa za gari fasta na kupunguza mwendo ili tusiwashtue (gari ilikua black) tukiwa tumekaribia hatua chache kutoka walipo tukaona yule alikua amekaa kasimama then anapewa nazi na wale wenzie akawa anavunja na kusema maneno kwa sauti (hatukuyaelewa), wengine tuliokuwa nao kwenye gari wakaanza kuogopa (mmoja muhindi alianza kulia) ikabidi driver aondoshe gari pale tukawapita pembeni kuwaangalia vizuri kumbe ni wanawake (mijimama) imevaa maderaa na mitandio imejifunika!! Hata hawakustuka!!!
 
Back
Top Bottom