Best home tutor
Senior Member
- May 8, 2026
- 194
- 262
Naitwa Batuli Selemani Kiberenge, Mwalimu wa shule ya sekondari Mirijo na mkazi wa kijiji cha Mrijo wilaya ya Chemba. Mnamo tarehe 2 Julai 2026 binti yangu mwenye umri wa miaka 8 (jina nalihifadhi ili kulinda faragha yake), mwanafunzi wa darasa la 4 shule ya msingi Sanzawa, alitekwa na kisha kubakwa na kutelekezwa akiwa katika maumivu makali sana.
Tulimpeleka kituo cha Afya Mrijo kwa ajili ya matibabu. Taarifa ya daktari ikathibitisha kuwa binti yangu amebakwa. Tuliripoti tukio hilo kituo cha polisi Mrijo na kufunguliwa jalada RB/MRJ/364/2026 na msako wa kumtafuta mtuhumiwa ukaanza. Mtuhumiwa anaitwa Abdul Yassin, mkazi wa Mrijo wilaya ya Chemba. Kwa kushirikiana na wananchi, tulifanikiwa kumkamata mtuhumiwa tarehe 3 Julai 2026.
Mtuhumiwa alifikishwa kituo cha polisi Mrijo, ili hatua nyingine za kisheria ziweze kuchukuliwa. Kwa kuwa ushahidi ulikuwa wa kujitosheleza, mtuhumiwa alitakiwa kupelekwa Mahakamani jana tarehe 06 Julai 2026. Lakini katika hali ya kushangaza, hakufikishwa mahakamani na polisi walipoulizwa walidai kwamba alitoroka akiwa kituoni.
Najiuliza mtuhumiwa anawezaje kutoroka akiwa kituo cha polisi chenye ulinzi mkali wa askari wenye silaha? Tena Mtuhumiwa wa kesi kubwa kama hii? Na kwa nini atoroke siku ya kupelekwa mahakamani? Sijaridhika na maelezo ya polisi. Naomba unisaidie kupaza sauti ili haki ya mwanangu ipatikane.!
Tulimpeleka kituo cha Afya Mrijo kwa ajili ya matibabu. Taarifa ya daktari ikathibitisha kuwa binti yangu amebakwa. Tuliripoti tukio hilo kituo cha polisi Mrijo na kufunguliwa jalada RB/MRJ/364/2026 na msako wa kumtafuta mtuhumiwa ukaanza. Mtuhumiwa anaitwa Abdul Yassin, mkazi wa Mrijo wilaya ya Chemba. Kwa kushirikiana na wananchi, tulifanikiwa kumkamata mtuhumiwa tarehe 3 Julai 2026.
Mtuhumiwa alifikishwa kituo cha polisi Mrijo, ili hatua nyingine za kisheria ziweze kuchukuliwa. Kwa kuwa ushahidi ulikuwa wa kujitosheleza, mtuhumiwa alitakiwa kupelekwa Mahakamani jana tarehe 06 Julai 2026. Lakini katika hali ya kushangaza, hakufikishwa mahakamani na polisi walipoulizwa walidai kwamba alitoroka akiwa kituoni.
Najiuliza mtuhumiwa anawezaje kutoroka akiwa kituo cha polisi chenye ulinzi mkali wa askari wenye silaha? Tena Mtuhumiwa wa kesi kubwa kama hii? Na kwa nini atoroke siku ya kupelekwa mahakamani? Sijaridhika na maelezo ya polisi. Naomba unisaidie kupaza sauti ili haki ya mwanangu ipatikane.!