Buriani John Nash na kiu ya kufahamu ni nini kinakosekana kwa Wasanii wetu hapa Bongo

JOTO LA MOTO

JF-Expert Member
Apr 11, 2018
758
555
1602184486293.png

John Lester Nash-1940-2020

Nikiwa bado Bw mdogo nyumbani alifika Baba yangu mdogo mmoja akiwa na kaseti kadhaa alizotoka nazo ng'ambo..miongoni mwa nyimbo zilizonivutia kwenye moja ya kaseti ni ngoma ya "rock me baby"

Sikujali sana ni nani aliyeimba kibao hicho ila baadae nilikuja kujua kimeimbwa na John Nash...nakumbuka siku moja kulikuwa na pati kwa jirani nikawapelekea hiyo kaseti, hii ngoma ilivyoanza tu karibia Watu wote waliokuwa nje wakaingia ndani.

John Nash amefariki jumanne iliyopita, tarehe 6 mwezi huu wa kumi. Pumziko La Amani apate Mwendazake.

Ni miaka 30 iliyopita lakini bado ukisikiliza vocal za hawa 'Waswahili' wenzetu waliozamia huko ughaibuni na ukilinganisha na Wasanii wetu ni kama kuna utofauti mkubwa...sasa huwa najiuliza kama Watu wa jamii hiyo hiyo kwa nini vocal za aina hiyo zisipatikane pia hapa Bongo?.

Huwa nasikiliza Wasanii kama Gregory Abbort, Bill Ocean, Luther Vandros na wengine wengi wenye asili ya Africa na kujaribu kuzitafuta vocal za aina hiyo hapa nyumbani bongo

Hivyo bado huwa najiuliza kama tunao Wasanii wa kaliba hiyo au ni mpaka nao wahamie huko ughaibuni?.

 

Attachments

  • search.jpg
    search.jpg
    3.5 KB · Views: 2
Old is gold, vitu vingi vinabadilika kwa kadri ya nyakati... kwenye muziki kuna zama ulikuwa muziki kweli na huenda zisijirudie.

RIP Johnny Nash, .....the world no more!
 
Ni kama uisikilize Nightshift ya group la ''The Commodores'' la kina Lionel Richie then ulinganishe na vya sasa....big different.
 
Ni kama uisikilize Nightshift ya group la ''The Commodores'' la kina Lionel Richie then ulinganishe na vya sasa....big different.
Pointi yangu si haswa kulinganisha muziki wa wakati ule na wa sasa la hasha.

Ni kutaka kujua Wao wa kule wana nini ambacho huku kinakosekana ili hali nao chimbuko lao ni huku huku Africa?.

Hebu tuwe wa kweli, sikiliza hizo nyimbo ni za miaka thelathini iliyopita na bado huwezi kuzilinganisha na za kwetu za sasa hivi, kunzia uzalishaji, mpangilio, vocals n.k.

Kwa mfano Tanzania tuna wimbo ambao umevuka mipaka, wimbo wa "malaika nakupenda malaika".....lakini kilichovuka ni ile tungo tu si muziki na Mtunzi wake...wengi watakuimbia malaika lakini hawana habari ni nani Mtunzi.

Sasa je ni kwa nini Wanamuziki wetu hawana nafasi ya kuwa wa kimataifa "international" kama walivyo hao wa huko?.

Mfano angalia ile project ya R Kell ya one8, ilikuwa kama vile R Kelly anafanya kazi na Wanafunzi wake badala ya Wanamuziki wenzake.
 
Back
Top Bottom