Wakudadavuwa
JF-Expert Member
- Feb 17, 2016
- 17,506
- 15,997
Hivi waarabu hawakuwa wakoloni?
Ed...
Historia ya ukombozi wa Tanganyika inaambatana na Uislam kwa kuwa Wazungu waliofika walikuwa Wamishionari na azma yao kuu ilikuwa kueneza Injili katika "dark continent."
Lakini mathalan Krapf alipofika kwa Chief Kimweri Vuga kamkuta anajua kusoma na kuandika yeye na wanae wake wote.
Kimweri akisoma na kuandika kwa herufi za Kiarabu.
Haya yaliwadhihirishia Wamishionari kuwa ile fikra ya kuwa wanakuja kustaarabisha watu haikuwa sahihi kwani Uislam umewatangulia.
Wamishionari wakafungua njia kwa wakoloni na kwa pamoja wakaanza kuupiga vita Uislam.
Walichofanya Waislam ndiyo haya tunayojadili hapa sasa takriban mwaka wa 10.