hizo ni kelele za wapumbavu wa CDM, hakuna lolote hapo. Mwisho wa maneno ni kwenye kupiga kura na hapo ndio mtajua nini maana ya kuwa na wabunge wachache.
CCM ndio dume lenu nyie.
Mkuu
Mimi siyo mwanachama wa CCM na wala CDM, na pia si mwanachama wa chama chochote cha siasa. Niliwahi kuwa TANU/CCM kwa vile ilikuwa mjibu wa sheria enzi hizo. Baada ya mfumo wa vyama vingi baadhi ya watumishi wa umma hawakutakiwa kujiunga na vyama vya siasa, na tangu wakati huo sijajiunga na chama chochote. nimeleza yote haya ili kuonyesha kuwa siyo kila mtu kwenye jamvi hili ni CCM au CDM n.k.
Sasa napenda kutoa mchango wangu wa mawazo kuwa kama kweli sisi ni watanzania tunaoipenda nchi yetu, ushabiki wa vyama vya siasa hautatufikisha popote. CCM kwa kuwa na wabunge wengi bungeni ndio chanzo cha kiburi,jeuri na tabia ya kuupuuza watanzania.
Wabunge wengi wa CCM wapo kukiwakilisha chama chao zaidi kuliko kuwakilisha majimbo yao,jambo ambalo limedumaza maendeleo ya watanzania kwa muda mrefu. vurugu nyingi wizi wa kura hulenga kuweka wabunge wengi ndani ya bunge hata kama hawana mchango wowote kwa taifa na utumiaji wa vyombo vya dola kukandamiza upinzani nao ni mbinu itumiwayo na CCM jambo hili haliyusaidii ndugu zanguni huku ni kukandamiza demokrasia ya kweli. Na hii ndo jeuri ya kujiita dume lenu wakati ni dume kibogoyo"toothless bull".
Kazi ya chama cha upinzani huwa ni kukosoa na kushauri kipi kifanyike kwa lengo la kuboresha maendeleo ya wananchi na nchi kwa ujumla,dhana ambayo kwa mtizamo wangu CCM inalichukulia kama unafiki au mashindano. Ikumbukwe leo kwamba leo kama huko upinzani kesho unaweza kuwa ndo mpinzani kwani hakuna dhibitisho kuwa CCM itadumu milele madarakani.Kaunda hakutegemea Chiluba angemwondoa madarakani.
Ushauri wangu kwa wana CCM wakumbuke usemi wa zamani kuwa "cheo ni dhamana", fanyeni mambo kwa kuzingatia kuwa kuna kesho.
Kwenu watu wa vyama vya siasa (upinzani), matatizo na vikwazo mnavyopata ni tatizo la katiba ambayo inatoa mwanya mkubwa wa kuwabana k.m
uhalali wa tume ya uchaguzi,matumizi ya vyombo vya dola dhidi ya upinzani (wakati Sugu anapowekwa chini ya ulinzi kwa kosa la kawaida,mbunge mwingine anayetishia kuua anaombewa ruhusa/kibali kwa mwanasheria au mkurugenzi wa mashitaka cha kukamatwa. Bunge lenye tabaka la wabunge). Hayo ni matatizo ya kikatiba, sasa mkazo mkubwa uwekwe kwenye kuikwamua nchi na wananchi kwenye katiba inayotoa mwanya kwa mkuu wa nchi kuchagua refa,washika vibendela kuchezesha ligi ya uchaguzi (Tume ya Uchaguzi). Kweli ndugu zangu "Fisi akiwa hakimu Mbuzi ana sheria"?.Ushauri wangu ni kwamba lekebisheni maswala ambayo yamekuwa vipingamizi vya ushindi wenu baadala ya kukimbilia Ikulu. Kwani mkikimbilia Ikulu bila maandalizi haya mkini kunaweza kusiwepo na tofauti yoyote.
Great Thinkers nasi tutoe mchango wa mawazo tukizingatia utanzania/utaifa zaidi badala ya itikadi zetu, katika hilo tutaweza kutoa mawazo yasiyo base/fungamana na chama chochote cha siasa. Ni hapo tu, tutakapoweza kusaidia taifa letu. hebu tufike mahala jembe tuliite jembe na si shoka.