Leo napata kutoa jibu langu kwenu wazalendo juu ya CCM iliyojaa mi...bunge iliyojaa woga,hofu na mashaka.WAZALENDO WENZANGU,MUNGU huchukia sana mwanadamu mwenye tabia hizo tatu.BADALA YAKE huwapenda wanadamu waliojawa na Upendo,Ujasiri na Matumaini.Wazalendo wenzangu,kundi hili la pili daima hudumu katika uzalendo.Hivi tukitoa Quiz pale Bungeni kwa wawakikilishi wetu individually kwa swali"TOA MAANA MBILI ZA NENO MZALENDO",je tusingepata majibu ya vioja? Tukumbuke mwaka 1995 mzee John Malecela alipata kutoa salaam kwa spika kwa niaba ya ccm,alisema"Mheshimiwa spika kwa niaba yangu na chama cha mapinduzi,napenda nikuhahakishie kwamba hoja yoyote itakayoletwa humu bunge na serikali hii ccm,TUTAIPITISHA TU".Ndugu WAZALENDO,maneno hayo ya Mzee John ni dhahiri wazi kwamba wabunge wa ccm wamejawa na 'anti-citizenry elements',nini maana yake? Maana yake ni kwamba wabunge hawa wana mioyo miwili[uchama 52% na uzalendo 48%],kwa maana hiyo,wabunge wa ccm ni waumini wa sera za woga,hofu na mashaka ambazo huanzia kwenye 'party caucos' ambapo watoa mada hutumia lugha za vitisho kuwazuia wabunge walioaminika kuwa ni wazalendo.Tujiulize wako wapi wabunge hawa?DEO FILIKUNJOMBE,ANNA KILANGO,SAMWEL SITTA na wengine kwa muktadha?Itachukua muda mfupi ujao Mwenyeenzi Mungu asikie kilio cha Wazalendo kwamba atupe wabunge wenye upendo na nchi yao,wenye ujasiri wa kutetea rasilimali za nchi yao na wenye matumaini ya kubadiliisha hali ya nchi kiuchumi,kisiasa,kijamii,kiutamaduni na kiulinzi.Ndugu wazalendo kila mmoja anayetaka kugombea nafasi ya ubunge kupitia ccm afahamu kabisa atageuka roboti wa kulinda maslahi ya chama kwanza kabla ya uzalendo.MWAKA 2015 hakika tutashuhudia katika maeneo mengi Wazalendo[nje ya ccm] wakiibuka washindi kwa kuwa mgombea mzuri na makini lazima atoke ccm.NACHUKIA WOGA,HOFU NA MASHAKA.