Bunge ndicho chombo kikuu cha jamhuri ya muungano ambacho kitakuwa na madaraka,kwa niaba ya wananchi,kuisimamia na kuishauri serikali ya jamhuri ya muungano na vyombo vyake vyote katika utekelezaji wa majukumu yake..... hayo ni maneno ya katiba ya JMT siyo yangu.
Wabunge wote ni wawakilishi wa wananchi wapo pale kwa niaba yetu kwa sababu haiwezekani Watanzania wote kuingia bungeni ndio maana tumechagua wachache wetu kutoka miongoni mwetu kwenda bungeni kwa niaba yetu kutuwakilisha.
Kilichopo sasa ni serikali inajisimamia yenyewe na inajishauri yenyewe kibaya zaidi inalisimamia pia bunge,bunge limekuwa kama kifaranga cha kuku na serikali imekuwa mwewe,serikali imekuwa juu ya bunge linapanga hoja ya kujadili na pia linafuta hoja ambayo hawaipendi.
Wabunge wengi wa CCM wanajiona kama nao ni sehemu ya serikali niliwahi kumsikia mbunge mmoja wa CCM(ambaye si waziri wala mkuu wa mkoa) akisema na yeye ni kiongozi wa serikali.
Kwahiyo kwa sababu bunge hili chini ya spika Makinda linasimamiwa na linashauriwa na serikali na si la wananchi basi hakuna haja ya kuwa nalo kwa sababu kuwa nalo ni kujiongezea gharama tu.tuiache serikali ijishauri na ijisimamie yenyewe kuliko kuwa na bunge la serikali.