second9
JF-Expert Member
- Jun 22, 2016
- 294
- 628
Wakuu baada ya jana kusikiliza vijana pale bungeni wakijibu hoja za Gwajima nikajikuta natafakari kuhusu bunge kwa muda mfupi na hii ni namna ambayo nimeliona Bunge kwa mtazamo wangu.
Bunge la Tanzania.
Je nikisema lile jengo la Dodoma ni jengo la wezi wa kura, machawa wa rais, makutano ya wateuzi makatili wanaotukana wananchi ntakuwa nakosea ni mtazamo wangu unaweza kuusahihisha.
Bunge la Tanzania.
- Ni Bunge la Rais (SSH) sio la wananchi kwani hoja zao kila mara ni za kumsifia rais na kumtetea hata anapokosea wananchi, hakuna namna hata ndogo jamaa wanakuja na hoja za kumrekebisha Rais ... hata Gwajima amefanya press hajataka kutumia kofia ya ubunge.
- Ni Bunge lenye wabunge wote wakuteuliwa na Rais Magufuli na sio kwa kura za wananchi kwa maana mi ninavyojua waliiba kura hawakushinda kihalali.
- Ni Bunge ambalo wabunge wake asilimia kubwa hawana elimu ya kutosha na wenye elimu wamekuwa brainwashed hii ndio sababu wakitaka kukosoa wanakuja kuongelea nje ya bunge maana hata hawa wenye uelewa kidogo wanaona ndani ya lile jengo kuna vilaza hawawezi kuelewana.
- Ni Bunge ambalo wabunge wake wanaweza kutukana wananchi kama vile afanyavyo Rais kwa maana ukimuita mtu kenge ni tusi na ni mfano wa Rais aliyeita watu Mbwa na Lijitu.
Je nikisema lile jengo la Dodoma ni jengo la wezi wa kura, machawa wa rais, makutano ya wateuzi makatili wanaotukana wananchi ntakuwa nakosea ni mtazamo wangu unaweza kuusahihisha.