Bunge kusitisha uuzwaji UDA? 270 Milioni zaingizwa akaunti ya Idi Simba

...Iliyobakia hapa ni huyo "kidume cha mbegu" Robert Kisena kumfuata Iddi Simba na kumpa mkong'oto wa kufwa mutu kama alivyomfanyia yule OCD au sijui ODC kule Shinyanga. Maana ni wazi ishatoka hiyoo!! Milioni 270 alizolipa hatarudishiwa. Safi sana!
Wabongo mbona mnaingizwa mikenge kirahisi wajameni? Yani unaamini mtu mwenye milioni 270 hana sophistication ya kujua kwamba huwezi kununua hata kiatu, acha kampuni ya milioni 270, viatu vya yebo yebo kwa kuweka hela kwenye akaunti ya mtu binafsi ambae si mmliki hiyo mali? Kweli mnaamini hawa wawili lao si moja?

Na kuingiza hela kwenye akaunti, especially transaction ya magnitude kubwa kama hiyo, ku deposit huwa ni hatua za mwisho kabisa za mikataba ya mauzo, lazima kuna paperwork ndefu ilifanyika na kubadilishana kabla hujampa mtu milioni 270, hizo paperwork zinasemaje, alipewa karatasi gani huyo anaejifanya kaibiwa? Kama hakuna paperwork kwenye transaction ya mil 270 basi ni mchoro tu huu, wanawachezea Watanzania wadanganyika.
 
Tatizo sijawasikia wabunge waliokuwa wanapigia kelele fedha za Jairo!!! where are they at!?
 
  • Thanks
Reactions: FJM
Shenzi sana huyu Iddi Simba

huyu katika kwao Kigoma huko na Khalifa Khamisi wakaja kutaka kutuulia klabu yetu ya SAIGON

wangekuja kutulliza sie wana Saigon tulivyowatimua. Kila mtu anayemjua Iddi Simba anajua alivyo anavyooona pesa

I just hope Ridhwani knows what he is up do and who he has been dealing with
 
Wingu zito lazidi kutanda UDA
Tuesday, 02 August 2011 19:57

Habel Chidawali, Dodoma
Mwananchi

WINGU zito bado limeugubika mkataba wa uuzwaji wa hisa za Serikali ndani ya Shirila la Usafiri Dar es Salaam (Uda), kufuatia wanaodai kuwa wamiliki wake kujitokeza hadharani tangu kuanza kwa mvutano ambao umekuwa ukizihusisha pande tofauti.
Wamiliki hao ni Kampuni ya Simon Group Ltd ambao jana waliwambia waandishi wa habari mjini Dodoma kuwa umiliki wake umekidhi vigezo vyote katika kumiliki Hisa kwa asilimia 52.53.

Hata hivyo, Kamati ya Bunge ya Hesabu za Mashirika ya Umma (POAC) jana hiyohiyo ilirusha kombora na kusema kuwa mkataba huo ni batili na kwamba fedha zote zipo kwenye akaunti ya kada wa Chama Cha Mapinduzi na mwanasiasa wa siku nyingi (jina tunalihifadhi kwa sasa).

Mwenyekiti wa bodi ya wakurugenzi wa Simon Group, Robert Kisera alisema kampuni yake ilifuata vigezo vyote vilivyotakiwa na kwamba imejidhatiti kuliendesha Uda bila wasiwasi.

Kisera alisema kuwa hadi sasa kampuni yake imekwishawekeza kiasi cha Sh760 milioni na kwamba kiasi kilichobaki cha Sh500 kinatarajia kulipwa kabla ya mwisho wa mwezi huu.

Msimamo wa POAC
Kwa upande wake, Mwenyekiti POAC, Zitto Kabwe aliitisha mkutano wa Waandishi wa habari katika Viwanja vya Bunge na kueleza kuwa mkataba wa Uda na Simon ni kizungumkuti na kutahadharisha kuwa aliyeingia mkataba huo amejiingiza matatani mwenyewe.

Zitto alisema kuwa kilichofanyika ndani ya mkataba huo ni ufisadi mtupu na akaeleza kuwa tayari kamati yake ilishabaini kuwa yako madudu makubwa hivyo ikaomba Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali kuingilia kati kwa ajili ya kufanya ukaguzi kwa kina.
“Taratibu hazikufuatwa,na uamuzi wowote utakaofanyika ni batili kwa kuwa tayari sisi tumeshaanza mchakato wa kubaini kilichopo ndani ya mkataba huo ikiwa ni pamoja kumuagiza CAG na tayari Spika ana taarifa hizo,’’alisema Zitto.

“Kutokana na hilo, hapa jamaa kaingia choo cha kike na kwa vyovyote vile lazima ametapeliwa na wajanja kwa kuwa kamati ilishamwambia mapema lakini anashindwa kuelewa kuwa Kamati ya Hesabu za Mashirika ya Umma ndiyo yenye jukumu la kubinafsisha mashirika zaidi ya hapo ni hakuna.’’

Kwa upande wake Makamu mwenyekiti wa kamati hiyo, Deo Filikunjombe (Ludewa-CCM) alisema kuwa kinachoyatafuna mashirika ya umma ni Msajili wa Hazina ambaye ameshindwa kutimiza wajibu wake kwa zaidi ya miaka 10.

Filikunjombe alisema kuwa kwa zaidi ya Miaka 10 Msajili ameshindwa kuteua bodi jambo linaloonyesha kuwa uwezo wake ni mdogo sana ambao hata kwa dawa asingeweza kujinusuru zaidi ya kusababisha migogoro kila kunapokucha.

Alisema kutokuwapo kwa bodi kulifanya uamuzi kufanyika kiholela holela jambo ambalo limeifanya Kamati hiyo kuwa na shaka.Mbunge huyo alisema kuwa kuna uzembe ndani ya serikali ambao umekuwa ukisababisha baadhi ya wachache kuendelea kutafuna mali za umma wakati nchi ikibaki maskini.

“Kwa mfano angalieni tarehe hizi 2/9/2009 ziliingia Sh 250,00 milioni ziliingia Benki M’, Makambako tarehe 26/11/2009 ziliingizwa Sh 20 milioni Benk M’ Songea kabla ya tarehe 9/12/2009 kuingizwa kiasi cha Sh 30 milioni katika tawi la Mlimani City zote zikiwa ni akaunti za (anamtaja mwanasiasa huyo),".

Alisema kumekuwapo maneno ya kuichafua kamati hiyo kwamba inafanya kazi chini ya mwamvuli wa vigogo walioko ndani ya Serikali jambo alilokanusha.

“Kwanza Watanzania naomba watambue kuwa Simon haijanunua Uda, bali kilichopo ni kwamba Simon ilinunua zile hisa ambazo hazikuwa zimelipiwa na kuwa hakuna kigogo yeyote nyuma ya kampuni hii na huyo wanayemtaja mimi simfahamu," alisema Kisera.

Shutuma nyingi alizirusha kwa Mbunge wa Ubungo, John Mnyika ambaye alisema kuwa kuwa ndiye amekuwa akiichafua Simon Group na kumtaka mbunge huyo kufunga mdomo ili asiingilie mambo yoyote kuhusu mkataba huo.Kwa mujibu wa Kisera, kitendo cha Mnyika kuandika barua kwenye ukusara wa ‘face book’ akielekeza shutuma kwa Simon ni kitendo cha uonevu na manyanyaso kwa mwekezaji mzawa.

Mnyika aliingilia kati mvutano ulioko kati ya Meya wa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam, Dk Didas Masaburi na Meneja wa Uda, Victor Milanzi, akisema hakuna mwenye haki ya kumnyooshea mwingine kidole, kwani wote wawili ni sehemu ya matatizo yanayolikabili shirika hilo.

“…Wote wawili wameshiriki kwa kiwango kikubwa katika kukiuka sheria, kanuni na taratibu kwenye uendeshaji wa Uda bila kuzingatia kwa ukamilifu maslahi ya wasafiri na walipa kodi,” alisema Mnyika katika taarifa yake kwa vyombo vya habari aliyoitoa kupitia mtandao wa face book.
 
kumbe pride inaendeshwa na pesa za ujanja ujanja ..... duh ..... Robert Kisena umekwisha .... nakushauri ukatafute sangoma fasta
 
Tatizo sijawasikia wabunge waliokuwa wanapigia kelele fedha za Jairo!!! where are they at!?
Hapa ndipo kwenye tatizo, kumbe nawe umeona eeh!. Naomba tusifurahi haraka ushindi huu kwa sababu hii ni hatua ya mwanzo tu, swali ni tumejiandaaje watakapobadili kibao?. Mengi tu yameshafanikiwa kufumuliwa ila yamegeuzwa mpaka yameonekana yalikuwa sawa tu na wala hapakuwa na tatizo, sasa hili nalo halitaangukia huko huko?, juhudi na kazi kubwa ya vyombo vyetu vinavyotakiwa kusimamia haki na sheria inatumika katika kugeuza na kuhalalisha scandal za ajabu ajabu kama hizi. Mfano ni huu ulioutoa, muda si mrefu hakuna atakayezungumzia tena habari za Jairo wakati kimsingi ni jambo lilopashwa kuitikisa serekali. Rushwa katika ngazi ya juu kiasi hiki, watu walitakiwa wawe wamejiuzulu wangine wamefukuzwa lakini kimyaaaaaa!
 
ccm at work. Yani tunaibiwa mpaka sasa tumekuwa paranoid na deal lolote! Huwezi kusinzia hata kidogo sasa. Maana ukifumba macho tu, utaweza kukuta hata nyumba yako imeuzwa ukiwa umesinzia hapo ndani! hahahaha
Ivi ikulu bado ni ya nchi hii?
Hatuna imani na chombo chochote cha serikali. Nafuu ivunjwe tu...
 
Wooow!!!.....m'kijiji a lot of kudos goes to you from your fellow tanzanian,I have a feeling that your articles on UDA shed some light to a lot of concerned citizen.
He has a lot of explaining to do!

Who, Simba ? You are wrong Kobello, it is the system that has become a breeding ground for fisadis of all types, shapes and sizes you name it, a system that at times you, Kobello, have gone out of your way to defend. If there is any explaining to be done, we will demand it not only of Simbas, Kusenas and Jairos but Kobellos and the like who continue to defend the status quo as the nation sinks deeper and deeper into filth. It is just a matter of time Kobello, just a matter of time !
 
Kha...Ivi una imani na chombo chochote cha state? Bunge, mahakama na serikali?
 
Who, Simba ? You are wrong Kobello, it is the system that has become a breeding ground for fisadis of all types, shapes and sizes you name it, a system that at times you, Kobello, have gone out of your way to defend. If there is any explaining to be done, we will demand it not only of Simbas, Kusenas and Jairos but Kobellos and the like who continue to defend the status quo as the nation sinks deeper and deeper into filth. It is just a matter of time Kobello, just a matter of time !
Defend what system?....Dude,I will never be a CDM member not even a fan.If that makes me fisadi,be it!
But there are things that really bother me,indigeneous investors who are raping Tanzania is one of them.So,since he got 270mil in his account from Kusena,let him explain exactly what that money was for,with supporting documents.
That system crap is so 90s!
 
HUYU MTU ANAYEAMINI UNAWEZA KUNUNUA SHIRIKA LA UMA KWA KUWEKA HELA KWENYE AKAUNTI BINAFSI, KWELI ANGEWEZA KULIENDESHA HILI SHIRIKA. Na huyu Mzee niliamini kasharidhika< Kumbe bado anaendelea kupiga dili. NIMEAMINI HII NDIO TANZANIA. usanii unaanzania ngazi ya familia mpaka JUU KABISA
 
Defend what system?....Dude,I will never be a CDM member not even a fan.If that makes me fisadi,be it!
But there are things that really bother me,indigeneous investors who are raping Tanzania is one of them.So,since he got 270mil in his account from Kusena,let him explain exactly what that money was for,with supporting documents.
That system crap is so 90s!

See what I mean ? How does Chadema come into this ! Of course you are very right to call the issue of system crap because the likes of Symbion, like all parasites, cannot survive on their own. If you shelter filth, dont blame the flies and the cockroaches that come for a visit and end up settling permanently because of the comfort and security accorded them. Since you have chosen not to lay any blame on the system that owns the habitat for fisadis to flourish, what more can I say - good luck though not for long young man !
 
huyu kisena nae chizi tu.iweje aweke pesa kwenye akaunt ya mtu binafs bila kudadisi eti kisa management ya UDA imesema!!!!

halafu huyu kisema ni rafiki mkubwa sana na ridhiwan kweli wameingizwa choo cha kike......huyu huyu idd simba ni mwizi toka zaman hata hiyo pride tanzania anaiendesha kiwizi wizi tu
 
Hivi watanzania tuna matatizo gani?
Si huyu Iddi Simba ndo alikuwa mhubiri mkubwa wa sera za uzawa?
Jamani mi nina wasiwasi na ubongo wa wabongo kama uko katika viwango stahili vya binadamu wa kawaida.
 
Huu sasa ni UMIMINISHAJI siyo UBINAFSISHAJI. Naona mzee SIMBA aliamua kutekeleza sera kipenzi ya chama chao cha "Chukua Chako Mapema" ili kufanikisha "the so called" usafirishaji. Ama kweli nchi hii itajengwa na wenye moyo na kuliwa na wenye meno na visu vikali vya kukata mapande makubwa makubwa ya nyama.
 
Defend what system?....Dude,I will never be a CDM member not even a fan.If that makes me fisadi,be it!
But there are things that really bother me,indigeneous investors who are raping Tanzania is one of them.So,since he got 270mil in his account from Kusena,let him explain exactly what that money was for,with supporting documents.
That system crap is so 90s!

That's where you lost the direction.

Chadema inaingiaje tena hapa?? watu mnaiogopa chadema kiasi kwamba kila kitu lazima mki-associate nayo??
 
Back
Top Bottom