Aisee. This is beyond any acceptable irrational...if at all there's...what a poor thinking. Hii hatua inapaswa kupingwa kwa nguvu za hoja zote zilizopo, ama itazidi kuugharimu sana huu mhimili, hasa viongozi wake.
Hii haiwezi kuwa namna sahihi ya kuficha udhaifu mkubwa wa serikali bungeni na uzembe wa bunge na wabunge, hasa wale wengi wa CCM!
Dkt. Thomas na wenzako, Watanzania si mabwege tena. Take it or live it, si wajinga tena. Wanajua mnachotaka kuficha. Wanajua mnaficha uchafh chini ya zulia. Nani hajui. Hata watoto wa chekechea wanajua hii move maana yake ni nini!
Naomba kumnukuu Lissu, mchague, ama bunge iwe sehemu ya mijadala ya afya au bunge lisiwepo kabisa, wananchi wajue moja.
Bunge ambalo haliwezi kufanya kazi yake kwa mujibu wa katiba, kisha linaanza kutafuta sababu kama hizi za kupuuzwa, linafunga ushahidi wa uzembe wake na ukibogoyo linaoung'ang'ania kwa faida ya CCM na serikali yake.
Dkt. Thomas, CCM imeshavunjika miguu. Kinachosubiriwa sasa hivi ni ama kuisukuma tu iangike kwa haraka, ama kuishikilia na kuisaidia ianguke polepole, huku wananchi wakiendelea kuumia. Wenye akili hawawezi kuthubutu kuitibu hiyo miguu.
Where do u stand! Ni ama unasimama pamoja na Watanzania wanaotaka kuona haki, matumaini na uwajibikaji kama moja ya misingi muhimu kwa amani na utulivu kisha maendeleo tunayoyatamani, ama unasimama kinyume nao, maana yake unasimama upande wa CCM.
Nani amewadanganya kuwa kutoonesha live vipindi vya bunge ndiyo njia itakayowapatia ushindi kwa kusimama katikati ya udhalimu na ukandamizaji. It is either u stand with the the oppressor (s) or the oppressed. Uamuzi huu unawatambulisha mko upande gani.
You are gone too...