Bunge kusitisha kurusha 'LIVE' vikao vyake!

Bunge kusitisha kurusha 'LIVE' vikao vyake!

Halafu "oooh, Tanzania ni nchi yenye uhuru wa habari".

Nyoooo.

Nani ataondoa hoja "zisizo za msingi"? Kwa muongozo gani?

Kama kuna wabunge wenye "hoja zisizo za msingi" kwa nini bunfe lisiache wananchi waone wabunge wao wanavyotoa "hoja zisizo za msingi" live ili kuwaelewa zaidi na kuweza kuamua vizuri zaidi kama wataendelea kuwachagua au watawamwaga uchaguzi ujao?

Kwa nini bunge linaingilia uhuru wa vyombo vya habari?

Kwa nini wanahabari wasilishitaki bunge mahakamani?

Kwa nini wabunge wasitunge sheria ya "freedom of information" itakayohakikisha bunge haliwezi kupitisha maazimio ya kidikteta kama haya?
yahani mkuu katika hali hii na jitihada wanazofanya kuficha taarifa unatarajia bunge hilo hilohilo litunge sheria ya huhuru wa vyombo vya habari? Nadhan atakaye peleka hoja hiyo atazuiwa kuvuka mipaka ya mkoa wa dodoma!
 
Very simple kwa Wabunge wa Upinzani!! Kama sheria bado zitakuwa zinavunjwa, la msingi ni kuzuia vikao kuendelea. At the end tutajua kulikoni. Si juzi wabunge wa Upinzani walikataa kutoka nje na kuanza kupiga kelele. Sasa wakikataa kutoka nje na kuamua kufanya walivyofanya juzi, mtu anadhani live coverage itazuia wasifanye hivyo. Issue hapa ni kanuni kufuatwa na kuruhusu mijadala yenye maslahi kwa taifa kujadiliwa. Huwezi ficha uozo kwa kutorusha matangazo. Yasiporushwa na kanuni zikaendelea kukiukwa, serikali na spika watakuwa na wakati mgumu zaidi wa ku-counter kitu chochote wapinzani watakacholeta kwa wananchi. Hapa ni busara tu na spika aache kuilinda serikali. Afanye kazi yake. Kizazi cha sasa ni tofauti na kile cha miaka 30 iliyopita.
 
Wanatunyima uhuru wetu wa habari kama wapiga kura wao..Inawapasa kutambua hasara za maamuzi hayo
 
Hii ni hoja ya Wasira ili awe na muda wa kuchapa usingizi. Mtu mwanazuoni kama Kashilila kuongea mataptap kama haya ni kudhalilisha elimu yake na taaluma aliyo nayo. Umaarufu hautafutwi bungeni. Unakuja automatically kwa wanao ona unavyojitoa kwa jamii na busara ulizo nazo. Je na U tube utawafungia? Akili ndogo kuongoza akili kubwa.
 
Kwahiyo wanataka kutuaminisha kwamba bunge lisipoonyeshwa live hakutakuwa na ukiukwaji wa kanuni sio?
Miaka ile ya zama za giza tuliweza kuwafahamu wabunge machachari sana kama Mzindakaya kupitia gazeti la mfanyakazi na redio Tanzania sembuse wakati huu wa dot.com kiruninga zaidi!
Nachojua mimi ni kwamba kama mtu ana hoja mfano Tundu Lissu na John Mnyika kwa kutaja wachache, hawahitaji live streaming ili kuongea bungeni, tena nahisi hapo ndipo watakuwa wakali zaidi.
 
Katibu wa Bunge naye katumwa kama anavyotumwa Anne, tunahitaji namba yake tumweleze hisia zetu.
 
akili ndogo ndongo zinapojaribu kutawala akili kubwa kubwa,matokeo yake ndio haya,wanadhani kwa kulikimbia tatizo,ndio wana solve tatizo.
 
kama bunge limeshindwa kusimamia sheria za ndani ya bunge,kimsingi haliwezi kusimamia utekelezaji wa sheria za nchi,linapaswa kuhakikisha kanuni na sheria zinafuatwa na kila mbunge,kinyume na hapo wanataka kuhakikisha wananchi wanashindwa kupata taarifa juu ya maamuzi yanayofanywa ndani ya bunge ktk wakati unaotakiwa.
 
Kwahiyo hat ule utaratibu wa zamani wa kurusha kwa kutumia Radio Tanzania(by then) nao hautokuwepo?
Hata kwenye taarifa ya habari huenda wakakataza isionyeshwe video ya kutoka Bungeni.
 
Na budget ya matangazo katibu wa bunge atuambie imepelekwa wapi kwakuwa tayari ilishapitishwa.
 
yahani mkuu katika hali hii na jitihada wanazofanya kuficha taarifa unatarajia bunge hilo hilohilo litunge sheria ya huhuru wa vyombo vya habari? Nadhan atakaye peleka hoja hiyo atazuiwa kuvuka mipaka ya mkoa wa dodoma!

Upinzani nao upo katika njama hizi?

Kama haupo kwa nini hatuoni upinzani ukianzisha hoja hii tuone utakavyopingwa?
 
Wakifanya hivyo, itakuwa turufu nyingine kwa Chadema! Too short sighted, Makinda and the team!! 2015 ni karibu na ndio woga wa CCM unazidi!!
 
Baada ya kwenda mbele tunarudi nyuma what silly country is this? 21st century bado unasema tutawaletea recorded and edited events that's shame for our young democracy, I can't believe this is happening.
Je ni lini tutawafikia kama jirani zetu kama kenya ambapo wameweza kufanya live debate for presidential contestants kama bunge tu linakatazwa kurushwa life.
 
nahisi huyo katibu ndio amejichanganya sana sasa kama wanavunja kanuni kwa makusudi hii si ndio hukumu kwa wananchi? maana wananchi ndio watajua ukweli kama kweli wamevunja kanuni kamkusudi na dawa yao ni kuwahukumu kwenye kura tu. sasa mkiwaficha wanaokiuka kanuni kwa makusudi sisi wananchi tutajuaje? hii ni danganya toto kabisa wasitufanye sisi wajinga, wangesema tu kuwa serikali inakuwa na kigugumizi pale inapotakiwa kujibu hoja kwa ufasaha, yaani tunarudi tena nyuma zama za zamani jamani? bunge la uingereza ukilitazama vizuri bila kujua kinachoendelea utahisi hawana adabu hata kidogo hata huyo pm cameroon anavyoongea kwenye bunge ni tofauti kabisa na anavyokuwa nje ya bunge full mapovu ila anaongea kwa point, ccm badilikeni jamani.
 
Safii wafute vipindi vya bunge watuwekee miziki full tyme hata taarifa ya habari nayo ifutwe tule bataaaaa
 
hizi ndizo mbinu mpya za akina Kinana na Mangula kulinda chama mfu na serikali yao dhaifu! nani kawaambia sisi walipa kodi ambazo zinalipia kila kitu kuanzia mishahara,marupurupu,matangazo,nk tunataka kusikiliza makombo badala ya kuwasikiliza moja kwa moja wawakilishi wetu wanatuwakilisha vipi bungeni? Ukifika hapo unajiuliza,watu aina ya Salim Hamed Salim na Prof. Anna Tibaijuka wanawezaje kujiunga na watu wenye akili ndogo kiasi hiki!!! Nimeamini mwisho wa CCM ukaribu kuliko nilvyo waza mwanzo.
 
Watanzania tunazidi kuchezewa kila kitu ni siri TBC inaendeshwa na kodi za wananchi na sisi ndio inatakiwa tuwaambie tunataka kuona nini...hawa watawala baada ya kuamua kwa maslahi ya Taifa wanaamua kwa maslahi ya Chama...hivi hatuwezi kutafuta sahihi kama milioni 10 kusema tunataka POAC irudi na BUNGE live hatuwezi kweli? Maana kulalamika hawa jamaa hawajali kabisaaa...Tuchukue hatua
 
Back
Top Bottom