Bukoba vs Moshi

Bukoba vs Moshi

Status
Not open for further replies.
Unavyofikiria sivyo mji Wa bukoba una kilometa za mraba 90 huku moshi ikiwa na 59 hivyo kiukubwa bukoba ni kubwa kuliko moshi. Kwa location bukoba iko location nzuri ukizingatia imepakana na Uganda. Rwanda,Burundi, na Kenya kupitia ziwani,kimzunguko Wa pesa ni mkubwa hasa uwepo Wa bandari, nchi nyingi zilizozunguka,vyuo vingi saut,jocuko,katoke,na open.pia viwanda ni vingi tanika,bunena water,Victoria chalks,vicfish,chai yetu,asilia water,Kabanga water, Mali juice,viwanda vya mafuta ya kujipaka,kagera sugar,viwanda vya maziwa,na balimi,.tena bk IPO katikati ya mwanza na mtukula ambayo miji kuna masoko ya Africa mashariki,biachara ya ndizi ndo usiseme watu ni wengi na bukoba bado INA sehemu kubwa ya kujenga nyumba kuliko moshi ambayo imebanwa na vijiji. Nakushangaa usemapo moshi itangazwe jiji ?
Nikuulize tu, Je ulishawahi fika Kilimanjaro kama ndio ni wapi ?
 
Kilimanjaro ni mkoa wenye mandondocha mengi kutokana na kuwatumia Kibiashara. Na ivi mwezi umeandama, inawezekana watu wakawa wanabishana na watu wa mwezi mchanga
Baki huko huko msewe uendelee kuota ya moshi eti mamdondocha khaaa sasa si wangetisha aiseee inshot mkuu punguza wivu kajenge kwenu watz ndo tulivyo badala ya kujenga kwako unakaa kusema ya wenzio
 
maendeleo cyo kuwa na majengo marefu,wakazi wengi wa mkoa kagera wanaishi vijijini na hii kutokana na kuwepo na huduma zote muhimu za kijamii,mkoa umejariwa ardhi yenye rutuba kuna haja gani ya kwenda kujazana mjini
Hivi kwa uopeo wako wewe moshi vs bk ipi ina huduma nyingi za kijamii maana unaongea kwa fact za upande mmoja punguza u much know mzee
 
AuY-M0FCIAAwUPI.jpeg
nakumatt moshi
 
Ila ndugu zangu wachaga punguzeni kuwageuza watoto matahira kisa utajiri nyumba nyingi za wachaga hukosi taahira kuweni na huruma hapa mjini nawaona wengi ukienda uko uchagani vijijini khali mbaya badilikeni hilo linatia sana doa mkoa wenu
Zunguka maduka yao k.koo pia kila duka yuko taahira na ndondoncha ..kwa kafara acha kabisa hawa watu
 
Moshi pamoja na kuwa kitovu cha utalii wa mlima ila kiukweli hamjaweza kutumia hiyo fursa na ndo maana mnapambanishwa na miji ambayo haina hata vitu vya kitalii sana na mnaonekana sawa tu. Kwa mapato yanayotokana na mlima ule, kwa kutokupata misuko suko ya mabalaa kama Kagera halafu bado mko karibu sawa kiasi hiki kusema kweli mko nyuma. Kuna kujisifu uko wa kwanza kumbe unakuwa wa kwanza kwa wajinga.

Sihitaji kuwa mnafiki, nawapongeza mlioweka picha hapa kwani mmetusaidia sana lakini zaidi niwapongeze wenye kuwekeza Kagera kwani mbali ya misuko suko yoote inayoukumba mkoa lakini bado hamjakosa cha kuonesha. Mwanaume baada ya vita unatizamiwa uwe na makovu mengi sana mithiri ya Sikamona wa Zawadi ya Ushindi, lakini ukiwa mshindi wa vita. Kagera inapitia magumu mengi sana na bado haiko nyuma ya mstari, jitihada zipo na zinaonekana.

Kuna watu walitaka kusema kimapato Kilimanjaro iko juu lakini chanzo cha mapato hayo naamini kinaeleweka hata kwa mtoto mchanga, utalii wa mlima. Ukiondoa huo mlima sioni mtaizidi wapi kagera, pili kwa idadi ya watu. Kagera yenye watu 2.3ml hauwezi ukaibeza eti pato dogo kisa mwenye watu 1.6ml yuko juu per capital. Idadi ya watu ni kigezo no.1. Haina tofauti sana ukalinganisha kipato cha mkazi wa Znz na aliyeko bara kama nchi per capital. Znz ina watu kiasi gani? Lakini ninachoamini siku ziwa (econ.factor) ya kanda ya ziwa (kagera) ikianza kuwa na meli za kusafirisha abiria na mizigo na zikaanza ruti pale kama itakuja kusemwa tena eti vimikoa fulani fulani viko juu kimapato kupita mikoa ya ukanda wa ziwa, kwa anayebisha tutakwenda kwa data pia. Hii ni sawa na mtu leo kusema bandari ya dar iondolewe halafu unambie itaendelea kuwa na uchumi ule ule, nitakubishia kwa data. Na kwa Tz bajeti ya serikali bado ilikuwa inatengwa kimikoa kutokana na per capital ya mkoa husika na ndo sababu utakuta miradi mkoa fulani itaendelea kuhudumiwa na kwa wingi zaidi kuliko mingine kisa ni tofauti ya mapato kutoka mikoa husika.

Naishia hapa na nimewapa changamoto wenzetu wa Kilimanjaro, nyinyi hamtakiwi kuwa hapo mlipo kwasababu mna sababu nyingi za kuwavusha na mkilemaa mikoa mingine imeamka na mtapotezwa.
 
Moshi pamoja na kuwa kitovu cha utalii wa mlima ila kiukweli hamjaweza kutumia hiyo fursa na ndo maana mnapambanishwa na miji ambayo haina hata vitu vya kitalii sana na mnaonekana sasa tu. Kwa mapato yanayotokana na mlima ule, kwa kutokupata misuko suko ya mabalaa kama Kagera halafu bado mko karibu sawa kiasi hiki kusema kweli mko nyuma. Kuna kujisifu uko wa kwanza kumbe unakuwa wa kwanza kwa wajinga.

Sihitaji kuwa mnafiki, nawapongeza mlioweka picha hapa kwani mmetusaidia sana lakini zaidi niwapongeze wenye kuwekeza Kagera kwani mbali ya misuko suko yoote inayoukumba mkoa lakini bado hamjakosa cha kuonesha. Mwanaume baada ya vita unatizamiwa uwe na makovu mengi sana mithiri ya sikamona lakini ukiwa mshindi wa vita. Kagera inapitia magumu mengi sana na bado haiko nyuma ya mstari, jitihada zipo na zinaonekana.

Kuna watu walitaka kusema mapato Kilimanjaro iko juu lakini chanzo cha mapato hayo naamini kinaeleweka hata kwa mtoto mchanga, utalii wa mlima. Ukiondoa huo mlima sioni mtaizidi wapi kagera, pili kwa idadi ya watu. Kagera yenye watu 2.3ml hauwezi ukaibeza eti pato dogo kisa mwenye watu 1.6ml yuko juu per capital. Idadi ya watu ni kigezo no.1. Haina tofauti sana ukalinganisha kipato cha mkazi wa Znz na aliyeko bara kama nchi per capital. Znz ina watu kiasi gani? Lakini ninachoamini siku ziwa (econ.factor) ya kanda ya ziwa (kagera) ikianza kuwa na meli za kusafirisha abiria na mizigo na zikaanza ruti pale kama itakuja kusemwa tena eti vimikoa fulani fulani viko juu kimapato kupita mikoa ya ukanda wa ziwa, kwa anayebisha tutakwenda kwa data pia. Hii ni sawa na mtu leo kusema bandari ya dar iondolewe halafu unambie itaendelea kuwa na uchumi ule ule, nitakubishia kwa data. Na kwa Tz bajeti ya serikali bado ilikuwa inatengwa kimikoa kutokana na per capital ya mkoa husika na ndo sababu utakuta miradi mkoa fulani itaendelea kuhudumiwa na kwa wingi zaidi kuliko mingine kisa ni tofauti ya mapato kutoka mikoa husika.

Naishia hapa na nimewapa changamoto wenzetu wa Kilimanjaro, nyinyi hamtakiwi kuwa hapo mlipo kwasababu mna sababu nyingi za kuwavusha na mkilemaa mikoa mingine imeamka na mtapotezwa.
Sindano imewaingia watu wa kilimanjaro na dawa inafanya kazi tayari. Kilimanjaro wanabebwa na serikali kutokana na mlima na kulingana watu wengi wa kule uelewa mdogo inafikia hata kutangaza mlima wanashindwa mpaka wategemee watu kutoka Dar es salaam ndio wautangaze mlima, mpaka Tanzania breweries limited wamejaribu lakini bado. Elimu ni kitu kizuri na kujitambua. Kagera aipewi msaada wowote na serikali lakini ina watu makini wenye uwezo wa kupambana na matatizo ya kawaida na majanga ya asilia.
Meli ya Mv. Bukoba ilianguka watu zaidi ya 1000 walifariki lakini watu wamesimama kiuchumi na pato Lao, mashamba yalikumbwa na kunyauka lakini watu wamesimama kimapato

Tetemeko la aridhi limepiga lakini watu wapo strong kipato,

Kagera ni sawa na Taifa la Israel watu wanapata majanga lakini kipato na maisha wapo vizuri sana na kiakili ndio usiseme

Pamoja na propaganda zote za watu wasioipenda kagera, lakini bado inasimama kama Israel
 
Ndu
Sindano imewaingia watu wa kilimanjaro na dawa inafanya kazi tayari. Kilimanjaro wanabebwa na serikali kutokana na mlima na kulingana watu wengi wa kule uelewa mdogo inafikia hata kutangaza mlima wanashindwa mpaka wategemee watu kutoka Dar es salaam ndio wautangaze mlima, mpaka Tanzania breweries limited wamejaribu lakini bado. Elimu ni kitu kizuri na kujitambua. Kagera aipewi msaada wowote na serikali lakini ina watu makini wenye uwezo wa kupambana na matatizo ya kawaida na majanga ya asilia.
Meli ya Mv. Bukoba ilianguka watu zaidi ya 1000 walifariki lakini watu wamesimama kiuchumi na pato Lao, mashamba yalikumbwa na kunyauka lakini watu wamesimama kimapato

Tetemeko la aridhi limepiga lakini watu wapo strong kipato,

Kagera ni sawa na Taifa la Israel watu wanapata majanga lakini kipato na maisha wapo vizuri sana na kiakili ndio usiseme

Pamoja na propaganda zote za watu wasioipenda kagera, lakini bado inasimama kama Israel
Ndugu yangu nimeona watu wanazunguka tu na ukiona mtu anaanza kuzunguka zunguka mpaka anaokoteza basi ujue kazi imekwisha. Ukitumia data huitaji kuzunguka saana kihivyo, weka data. Machungu yanayopitiwa na wanakagera ni mangapi? Nimeona mwingine anauliza eti ni majanga yapi wamtajie. Ukimwona mtu wa hivi basi usishangae ukaja kujua hata Kagera haijuhi na kufika ndo kwanza analisikia leo.

Ni nani angevumilia hayo machungu kiasi kile? Halafu leo bado hujionei aibu kujilinganisha nae, really? Ni sawa na mtu aliyekuwa akihara wiki nzima mkiwa na uzito sawa, leo kuharisha kukome halafu unataka mkapime uzito na ukishamzidi unaanza kufurahi, kuruka ruka na kushangilia, unakuwa kama Zuzu hivi. Na ukiweza kuona pengine unamzidi 1kg tu, jitizame, wewe ndo utakuwa unaumwa na hujajitambua make huyu asingehara wiki nzima usitegemee mngekuwa sawa tena.

Wakifikiri kujilinganisha na Kagera leo ndo furaha yao, basi wamejikwaa. Ule mkoa ni sleeping giant, sitaki kusema ila mwenye kuelewa ameelewa na siku ikifika ukaamka wasianze watu kutafutana.
 
Hii ni Machame Moshi hapo lakini ni kama ulaya
images
images
images
images


Haya ndio mazingira yanayowapa Wachagga kiburi cha kujenga na kurudi kwao December
 
Ni kwa nia nzuri tu ya kuijua Tanzania ilivyo lakini sio kuilinganisha na sehemu inayoitwa kagera hapana kapsa hili tulishalimaliza
 
Kwa kweli Moshi inavutia tuwe wakweli
images
images
images
images
protea-hotel-aishi-machame.jpg
images

Machame panavutia sana zidini kutunza mazingira yetu
 
Wazungu wakifika huku huwa wanakimbilia kwenye mabegi yao kukagua tickets zao upya kama ni kweli ndege haikupotea njia na kuwapeleka Ulaya Frankfort
search
hotel-pool.jpg
machame1.jpg
machame-nkweshoo-cultural.jpg
Mountain5.jpg
Tony-diTomasoKili-210.jpg

Mpaka mzungu aje akuelewe na aamini kapsa kama yupo Africa huwa ni kazi ngumu yenye changamoto mingi sana kwa kweli.
 
Tuijue zaidi Moshi vijijini
machame%20gate.jpg
9194_kilemakyaro-mountain-lodge%20DSC01664.JPG
filename-lodge-jpg-thumbnail0.jpg
53.jpg
machame-walking-rain-forest.jpg
30622903.jpg

Kizuri hakiitaji nguvu nyingi kukipamba ukweli mnao moyoni Kilimanjaro ni tunu ya taifa.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom