Tetesi: Brenda William Lukuvi kugombea ubunge jimbo la Isimani

Tetesi: Brenda William Lukuvi kugombea ubunge jimbo la Isimani

tpaul

Platinum Member
Joined
Feb 3, 2008
Posts
26,021
Reaction score
25,422
Katika kuonesha ari ya kupokea kijiti cha baba yake na kuendelea kuwatumikia wananchi wa jimbo la Isimani, mtoto wa marehemu William Lukuvi (Brenda Lukuvi) anatarajia kuchukua fomu ya kuwatumikia wapigakura wa jimbo la Isimani. Jimbo hili limekuwa likishikiliwa na baba yake kwa zaidi ya miaka 30 (1995-2026) kabla mbunge huyo nguli wa CCM kufariki dunia mwanzoni wa mwezi Machi, 2026.

"Kwa kuzingatia utamaduni wa chama chetu, kamati ya ushauri inapendekeza Brenda Lukuvi achukue fomu na kuendelea kuliongoza jimbo la Isimani amalizie kazi nzuri iliyofanywa na baba yake", alisema kigogo mmoja wa CCM kutoka Isimani ambaye hakupenda kuweka jina lake hadharani.
1000327064.jpg

Mh Brenda Lukuvi (mbunge wa Isimani ajaye)

MAONI YANGU
Mimi nashauri binti huyu akabidhiwe jimbo. Kwa kuwa baba yake amelifanyia mambo makubwa jimbo la Isimani, sioni sababu ya mtu mwingine kushika kijiti cha baba yake. Naunga mkono chama cha mapinduzi jimbo la Isimani kupendekeza jina la Brenda kuongoza jimbo la Isimani. Kwanza huyu ni msomi na amejifunza mambo mengi kutoka kwa baba yake. Namuunga mkono hoja 💯%.
 
Ubarikiwe
Isije ikawa kama wale jamaa wa demoghasia
Kile chama noma sana.. wale Covid19 karibu wote walikuwa chakula za wakubwa. Lissu mwenyewe alikuwa na dada yake mbunge wa viti maalum. Dr Slaa alikuwa na ka-mchepuko kake mbunge viti maalum, Ndesamburo alikuwa na binti yake viti maalum.. baba lao Mbowe haina hata haja ya kujadili.
 
Ni Brenda Rupia au Brenda Lukuvi? Kama ana sifa za kuwa mbunge apitie mchakato ndani ya chama akibahatika apeperushe bendera. Ila kutaka kulazimisha apewe ubunge sio sahihi. CCM sio chama cha kifalme.
Typing error. Ni Brenda Lukuvi mkuu.
 
Katika kuonesha ari ya kupokea kijiti cha baba yake na kuendelea kuwatumikia wananchi wa jimbo la Isimani, mtoto wa marehemu William Lukuvi (Brenda Lukuvi) anatarajia kuchukua fomu ya kuwatumikia wapigakura wa jimbo la Isimani. Jimbo hili limekuwa likishikiliwa na baba yake kwa zaidi ya miaka 30 (1995-2006) kabla mbunge huyo nguli wa CCM kufariki dunia mwanzoni wa mwezi Machi, 2006.

"Kwa kuzingatia utamaduni wa chama chetu, kamati ya ushauri inapendekeza Brenda Lukuvi achukue fomu na kuendelea kuliongoza jimbo la Isimani amalizie kazi nzuri iliyofanywa na baba yake", alisema kigogo mmoja wa CCM kutoka Isimani ambaye hakupenda kuweka jina lake hadharani.
View attachment 3564064
Mh Brenda Rupia (mbunge wa Isimani ajaye)

MAONI YANGU
Mimi nashauri binti huyu akabidhiwe jimbo. Kwa kuwa baba yake amelifanyia mambo makubwa jimbo la Isimani, sioni sababu ya mtu mwingine kushika kijiti cha baba yake. Naunga mkono chama cha mapinduzi jimbo la Isimani kupendekeza jina la Brenda kuongoza jimbo la Isimani. Kwanza huyu ni msomi na amejifunza mambo mengi kutoka kwa baba yake. Namuunga mkono 💯%.
HII MALISAFI nilikuwa naitolea macho sana kwenye hii tafrija kumbe tayari Manguli wa mjengoni washaipigia hesabu😂! Ama kweli CCM ni ukoo wa panya
 
Hakika upo sahihi ikizingatiwa baba yake alianza kutumikia chama cha TANU tangu mwaka 1954 akiwa kwenye korodani za mzee wake.

 
Back
Top Bottom