Kitila Mkumbo
JF-Expert Member
- Feb 25, 2006
- 3,355
- 1,990
Mama Zk, kilimponza kupingana na hoja ya Slaa kiwazi wazi! Yeye pale angesema kweli shida ipo na tunaishughulikia badala ya kuungana na Balali, Six and the compony kusema tuhuma ni za uongo wakati alijua ni za kweli!
Mwanakijiji,
Hivyo ndivyo anavyotakiwa kufanya siku zote, ni sehemu ya majukumu yake. Sasa tumpongeze nini. Ila anapoboronga lazima kope zetu zinyanyuke.
...............Mtizamo wangu ni kama ifuatavyo:-
Serikali ilitoa Standing Order kwa BOT kulipa madeni ya EPA kadri fedha za kigeni zinavyopatikana.Unatoa standing order inaamisha kuwa benki inatekeleza tu haina haja ya kuconsult serikali(Pay Master General wala Waziri).Kwahiyo sioni sababu ya kuwaingiza Mhe Mramba na Mgonja(in his capacity kama Paymaster General).Kama responsibility ilipewa BOT then the BOT Board of Directors(hapa Mgonja yupo na sio Balali peke yake),Director of Economic Policy na watu wa kitengo cha Debt Management Unit. Hawa ndio wako direct responsible.Kwa jinsi hii summary inaonyesha kilichotokea ni Clear Fraud kati ya BOT na waliolipwa.Mimi pia ningependa sana either Mramba au Megji wajiuzulu lakini sidhani kama wako directly responsible.
Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali ndio mwenye jukuma la ku audit BOT, je kwa nini hakufanya hivyo yeye mwenyewe?Kama hakuwa hana uwezo(Technical Competence) wa kufanya hivyo, je ni kwa nini alikubali Delloite(CAG Agent)akubali kufukuzwa(kukatokea kutoelewa!!!!!! na BOT. Kwani Delloitte walipewa kazi na Board ya BOT au CAG?
CAG naye yuko responsible kwa kushinda kualert of a possible serious Audit breach on time.
Haya yalikuwa ni madeni ya muda mrefu mno inakuwaje BOT na Serikali kukubali kulipa kwa idhini(through Notarized Deeds of Assigmment). Huitaji kwenda shule kujua hii ndio ilikuwa loophole ya kuzitoa hizi fedha maana zilishakuwa unclaimed kwa muda mrefu na hata hao genuine wadai waliisha yafutilia mbali hayo madeni.Toka 1970 hujalipwa, huwezi kuendelea kuweka kwenye vitabu vyako.Haya makampuni 22(nina huakika hizi kampuni zote zilisajiliwa after 2004), yalitoa records hizi za madeni yaliyokufa hapo hapo BOT, wakaingia Samora, wakatengeneza letter head na deed of assignement, malawyer of Malegesi Calibre waka notarised hela ikatoka.Simple kama kumsukuma mlevi.
Roho inauma sana jamani.
Vyombo vya habari vimebaini kuwa Mkurugenzi wa kampuni inayohakiki makampuni yanayochimba dhahabu Alex Stewarts Assayers ni mtoto wa Mhe. Basil Pesambili Mramba aliyekuwa Waziri wa Fedha wakati kampuni hiyo ilpopata mkataba huo Juni 2003. Katika miaka miwili ya mkataba huo, kampuni hii imekuwa inalipwa dola 751,267 sawa na sh. 939 millioni kila mwezi. Kwa muda wa miaka miwili imejikusanyia dola milioni 18 sawa na sh. 22.5 bilioni. Kampuni hii pia ilisamehewa kodi kwa notisi za serikali za Novemba 25 2005 iliyotiwa saini na aliyekuwa Waziri wa Fedha. Ni wazi kuna mgongano wa manufaa (conflict of interest) ya Waziri wa fedha kuipa mkataba kampuni ambayo mtoto wake ni mkurugenzi na pia kuisamehe kodi. Mpaka hivi sasa serikali haijatoa maelezo ya kina kufafanua utata huu ambao unaashiria matumizi mabaya ya madaraka kunufaisha familia yako ambayo ni rushwa. Rais anawajibika kulichunguza suala hili kwa kina na ikiwa taarifa ambazo zimeandikwa katika vyombo vya habari na vielelezo vyake zina chembe ya ukweli, basi waziri awajibishwe kwa kufukuzwa kazi na Tume ya Kuzuia Rushwa ichukue hatua za kisheria kuwafikisha wahusika mahakamani.
Kutoka: http://cuf-tz.com/666.html
Meghji mnafiki mkubwa na ndo maana alitamani kumwozesha binti yake kwa JK.
Tuwapongeze mafisadi watuhumiwa kwa kuuchuna.
Pongezi kwa Mkapa unastahili pongezi!
Pongezi kwa Mramba
Pongezi kwa Yona
Pongezi kwa Jeetu Patel
Pongezi kwa Baba wa Richmonduli
Pongezi kwa Mastermind wa KAGODA
Pongezi kwa watuhumiwa mafisadi wengine.
Mmeonyesha uwezo wenu katika "KULA BATI"
Huyu mama aliyetupa ukweli (pamoja na kwamba hakuwepo kwenye mafisadi watuhumiwa) asipongezwe kwa kutupa habari za yaliyojiri.
Mramba! Mramba! Mramba! Mramba! Mramba!
Mhh huyu Basiri Mramba inaonekana anaogopwa sana na Kikwete. Yaani JK ameshindwa hata kutaja jina lake kwenye show yake ya kufukuza kazi mtu aliyejiuzulu!
Mramba watanzania wanaendelea kula nyasi kama ulivyotaka! swali ni je, nyasi zikiisha watakula nini? ...... nyama za watu I think