Bora nikaoe Tanga

Bora nikaoe Tanga

Hapo mikanjuni ulipotaja pana demu wangu anaitwa Khadija ni kungwi huyu wa kufundwa wari, sasa ole wako ukamchukue usije sema sikukukanya.
 
JIBU LA SHAHIRI..NIOE TANGA.
Na Wenyewe twajijua,siri ya mke wa pwani,
shanga zilizozagaa,mguni na kiunoni,
Hawahitaji chapaa, zitokazo mashineni,
Kaoe baba kaoe, Nyumbani tanga kunani!.

Siri ni ngoma ya ndani, siyo ya mkidigeni ,
hufunziwa kitandani, siyo yenu hadharani,
Huchoma ndani miyoni,kufurahisha machoni,
Kaoe baba kaoe,Nyumbani tanga kunani!.

Huzifunga zao shanga,kiuno bigili ndani,
huzivunja zao chaga, kwa ile shuhuri ndani,
kama mtoto mchanga,kilio cha dirishani,
Kaoe baba kaoe, Nyumbani tanga kunani! .

Waja leo ondoka leo,Ni msemo wa zamani,
waja leo wala leo, ufunuliwe vya ndani,
wala usinywe kileo,ili upate mwandani,
Kaoe baba kaoe,Nyumbani tanga kunani! .

Oa makorora sikoni, wala si wa mikanjuni,
si muheza si handeni, kote kumeja mapenzi,
wakuacha simuoni, vyote vya utamu ndani,
Kaoe baba kaoe, Nyumbani tanga kunani! .
 
Mkuu wewe ni mtunzi mzuri, endeleza kipaji chako
 
Bora nikaoe Tanga, tena binti wa Pangani,
Yule anovaa kanga, na mitandio kichwani,
Aongee kwa kuringa, na lafudhi ya kipwani,
Awe na kauli njema, kwangu na kwa ikhwani

Pangani nikimkosa, natafuta wa Handeni,
Niweze peleka posa, nioe niweke ndani,
Naenda haraka hasa, nisichelewe njiani,
Nitampenda kwa dhati, upendo kutoka moyoni.

Au nishuke Muheza, nikamsake mwandani,
Apate kuniliwaza, na uchovu wa kazini,
Najua hatanikwaza, kuniumiza moyoni,
Niliwazwe hasahasa, ili niwe wa thamani.

Au awe wa Lushoto, tena kule mlimani,
Alozoea msoto, kupanda kushuka chini,
Azijua changamoto, zilizopo maishani,
Siku nikisema sina, asiende kwa jirani.

Au niende Korogwe, nimpate wa ubani,
Mchuzi atie ngogwe, nyanya chungu za mjini,
Nisemwe au nirogwe, sisikii na sioni,
Nitalia kwa makeke akimtwaa fulani.

Wakilindi simpiti, na yeye namthamini,
Aweze kunidhibiti, ili nisitoke ndani,
Masham matashtiti, kwa udi pia ubani,
Katu asinisaliti, nikiwa na hali duni.

Ndugu zangu wa Mkinga, naomba nipokeeni,
Nakuja kutia nanga, nimsake wa moyoni,
Asiwe wa kujivunga, aishike sana dini,
Sio kama nabagua, hiyo yangu tamaduni.

Au nibakie Tanga, nioe pale mjini,
Walipojaa nyakanga, wafundao wari ndani,
Panauzwa hadi shanga, sijui za kazi gani,
Kama nyumba nitajenga, hata kule Mikanjuni.

Hapa sasa naishia, mawazo tele kichwani,
Wapi nitajipatia, mke yule mwenye shani,
Nipate furahia, raha ya ndoa ndoani,
Ila atokee Tanga, mjini au wilayani.
Hongera mkuu umetisha ila kuhusu kupanda milima siku hiz wote tunapanda mlima! wengine wanaruka hadi ukuta! afadhal hata anaepanda mliman labda atarud na kuni kuliko tunao tafuta kitu ambacho hatukioni wala kukipata!
 
Hongera mkuu umetisha ila kuhusu kupanda milima siku hiz wote tunapanda mlima! wengine wanaruka hadi ukuta! afadhal hata anaepanda mliman labda atarud na kuni kuliko tunao tafuta kitu ambacho hatukioni wala kukipata!
Ahsante mkuu, hahahahaha anaepanda mlima labda atarudi na kuni
 
Mabinti Wa Kitanga Wanasifika Sana Kwenye Mapenzi Na Mie Nijongee Nikatafute Wangu Wa Maishani
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom