Kakole
JF-Expert Member
- Jul 29, 2015
- 2,094
- 1,743
Kama umetunga mwenyewe basi big up sana mzee wa Tanga kwa njeka.ahsante kiongozi
Kama umetunga mwenyewe basi big up sana mzee wa Tanga kwa njeka.ahsante kiongozi
I LOVE YOU Sky EclatKaribu bwana shemeji uoe Tanga.
Bora nikaoe Tanga, tena binti wa Pangani,
Yule anovaa kanga, na mitandio kichwani,
Aongee kwa kuringa, na lafudhi ya kipwani,
Awe na kauli njema, kwangu na kwa ikhwani.
Pangani nikimkosa, natafuta wa Handeni,
Niweze peleka posa, nioe niweke ndani,
Naenda haraka hasa, nisichelewe njiani,
Nitampenda kwa dhati, upendo kutoka moyoni.
Au nishuke Muheza, nikamsake mwandani,
Apate kuniliwaza, na uchovu wa kazini,
Najua hatanikwaza, kuniumiza moyoni,
Niliwazwe hasahasa, ili niwe wa thamani.
Au awe wa Lushoto, tena kule mlimani,
Alozoea msoto, kupanda kushuka chini,
Azijua changamoto, zilizopo maishani,
Siku nikisema sina, asiende kwa jirani.
Au niende Korogwe, nimpate wa ubani,
Mchuzi atie ngogwe, nyanya chungu za mjini,
Nisemwe au nirogwe, sisikii na sioni,
Nitalia kwa makeke akimtwaa fulani.
Wakilindi simpiti, na yeye namthamini,
Aweze kunidhibiti, ili nisitoke ndani,
Masham matashtiti, kwa udi pia ubani,
Katu asinisaliti, nikiwa na hali duni.
Ndugu zangu wa Mkinga, naomba nipokeeni,
Nakuja kutia nanga, nimsake wa moyoni,
Asiwe wa kujivunga, aishike sana dini,
Sio kama nabagua, hiyo yangu tamaduni.
Au nibakie Tanga, nioe pale mjini,
Walipojaa nyakanga, wafundao wari ndani,
Panauzwa hadi shanga, sijui za kazi gani,
Kama nyumba nitajenga, hata kule Mikanjuni.
Hapa sasa naishia, mawazo tele kichwani,
Wapi nitajipatia, mke yule mwenye shani,
Nipate furahia, raha ya ndoa ndoani,
Ila atokee Tanga, mjini au wilayani.
Kaoe tanga ujute, na kilio cha hudhuniBora nikaoe Tanga, tena binti wa Pangani,
Yule anovaa kanga, na mitandio kichwani,
Aongee kwa kuringa, na lafudhi ya kipwani,
Awe na kauli njema, kwangu na kwa ikhwani.
Pangani nikimkosa, natafuta wa Handeni,
Niweze peleka posa, nioe niweke ndani,
Naenda haraka hasa, nisichelewe njiani,
Nitampenda kwa dhati, upendo kutoka moyoni.
Au nishuke Muheza, nikamsake mwandani,
Apate kuniliwaza, na uchovu wa kazini,
Najua hatanikwaza, kuniumiza moyoni,
Niliwazwe hasahasa, ili niwe wa thamani.
Au awe wa Lushoto, tena kule mlimani,
Alozoea msoto, kupanda kushuka chini,
Azijua changamoto, zilizopo maishani,
Siku nikisema sina, asiende kwa jirani.
Au niende Korogwe, nimpate wa ubani,
Mchuzi atie ngogwe, nyanya chungu za mjini,
Nisemwe au nirogwe, sisikii na sioni,
Nitalia kwa makeke akimtwaa fulani.
Wakilindi simpiti, na yeye namthamini,
Aweze kunidhibiti, ili nisitoke ndani,
Masham matashtiti, kwa udi pia ubani,
Katu asinisaliti, nikiwa na hali duni.
Ndugu zangu wa Mkinga, naomba nipokeeni,
Nakuja kutia nanga, nimsake wa moyoni,
Asiwe wa kujivunga, aishike sana dini,
Sio kama nabagua, hiyo yangu tamaduni.
Au nibakie Tanga, nioe pale mjini,
Walipojaa nyakanga, wafundao wari ndani,
Panauzwa hadi shanga, sijui za kazi gani,
Kama nyumba nitajenga, hata kule Mikanjuni.
Hapa sasa naishia, mawazo tele kichwani,
Wapi nitajipatia, mke yule mwenye shani,
Nipate furahia, raha ya ndoa ndoani,
Ila atokee Tanga, mjini au wilayani.
Hahahahahahaa WanaKuLaga thuHapo mikanjuni ulipotaja pana demu wangu anaitwa Khadija ni kungwi huyu wa kufundwa wari, sasa ole wako ukamchukue usije sema sikukukanya.
Hahaa bweni kwa ma mwiny hasa bweni ndogoNenda Pangani na hasa Bweni