Boniface Jacob: Wakurugenzi wengi hawakuwa na sifa, wanaenda kuchezea pesa za umma

bagamoyo

JF-Expert Member
Jan 14, 2010
21,305
24,200


Meya na diwani wa zamani wa Kinondoni na Ubungo akiwa na ripoti za CAG mbele yake mezani studio ya Wasafi MEDIA na kuulizwa maswali na jopo la watangazaji na pia wasikilizaji anafafanua sababu za udhaifu wa kiuongozi ktk halmashauri za Dar es Salaam na nchini kwa ujumla.

Meya mstaafu Boniface Jacob aelezea jinsi wakaguzi wa ndani wa Halmashauri jinsi wanavyofanyiwa mizengwe kwa kunyimwa vitendea kazi ikiwemo usafiri na ofisi za Ukaguzi wa Ndani kuwekwa pembeni mbali na mkurugezi wa Halmashauri ili kuwakatisha tamaa na wasifurahie mazingira ya ofisi zao na kutishia ufanisi wa kazi yao nyeti ya ukaguzi .

Kada wa CHADEMA kamanda Boniface Jacob katika mahojiano exclusive na ya wazi ameelezea mapungufu makubwa ya wakurugenzi wa majiji na halmashauri za miji ambao hawana uzoefu lakini walipachikwa ktk nafasi za juu za uongozi na kusababisha CAG kuibua madhaifu mengi

Mfano ni ikiwemo matumizi mabaya ya kodi, kutofuata utaratibu, kulipa fedha za madawa Bohari Kuu ya Madawa MSD kisha Halmashauri hizo kutokwenda kuchukua mabilioni ya madawa na vifaa tiba vilivyolipiwa lakini havikuchukuliwa kupelekwa ktk mahospitali kutibu wananchi ....


Meya mstaafu alipoulizwa chini kuhusu kipindi halmashauri ya Kinondoni na Ubungo zilipokuwa na mameya na madiwani wengi wa CHADEMA hali ilikuwaje?

Meya Mstaafu Boniface Jacob anasema walidhibiti mianya ya upotevu wa Mali na matumizi mabaya ya mapato pia kodi hivyo kuibuka na hati safi kutoka kwa CAG na kusema hii ndiyo faida ya kuwa na sifa za kweli za vyama vingi Mali ya umma inalindwa kwani kuna macho ya vyama ktk baraza la udiwani, bungeni na vyombo huru vya habari kuhoji yaliyomo ktk ripoti ya CAG bila woga kama kipindi cha John Magufuli ambapo mahojiano hayo hayangewezekana na hata kama yangefanyika basi wangekuwa wamezingirwa nje ya ofisi na watu wasiojulikana kuwatisha na kuwatia nguvuni...

Kuhusu nini kifanyike ili halmshauri ziwe na wakurugenzi na wakuu wa idara thabiti walio na uwezo wa kufanya kazi kwa umahiri, meya mstaafu Boniface Jacob anasema wafanyakazi wa Halmashauri na idara za serikali waliofanya kazi kwa muda mrefu ndiyo wanatakiwa kupandishwa vyeo kuwa wakurugenzi au wakuu wa idara badala ya makada wa UVCCM na CCM kupachikwa ktk uongozi wakati hawana uzoefu ktk ofisi za umma.
 
1681832634747.png


Kamati maalum za Bunge za PAC na LAAC ni jukumu lao zibane Halmashauri baada ya ripoti hii ya CAG....
 
April 2023
Dar es Salaam , Tanzania

Ripoti ya CAG yaendelea kutikisa nchi, Meya Boniface aibuka ..... kufafanua kwa wananchi madudu ktk halmashauri​

img-20230411-wa0036.jpg

Date: April 11, 2023Author: mtezamedia0
ALIYEKUWA Meya wa Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni na Ubungo kwa nyakati tofauti, Boniface Jacobo, amewashauri wananchi wa mkoa Dar es Salaam kususia kulipia ushuru wa halmashauri tano za mkoa huo mpaka pale watakapochukuliwa hatua waliohusika na wizi wa fedha za halmashauri hizo zilizoibuliwa kwenye Ripoti ya Mzibithi na mkaguzi wa mahesabu za serikali(CAG).
img-20230411-wa0036.jpg

Jacob ametoa Rai hiyo leo jijini Dar es salaam wakati akizungumza na waandishi wa habari alipokuwa akichambua ya Ripoti ya CAG kwenye halmashauri tano za mkoa wa Dar es salaam.

Aidha,Jacobo amesema kupitia Ripoti hiyo imeonesha ufisadi mkubwa kwenye halmashauri ya Ubungo,Halmashauri ya jiji la Dar es salaam pamoja na kigamboni .

“Natoa rai kwa wakazi wote wa Dar es salaam kususia kulipa ushuru zote za manispaa ,haiwezekani watanzania walipe ushuru halafu pesa zinaliwa na wajanja kwenye hizi halmashauri”Amesema Jacobo.

Ameongeza kuwa atatumia nafasi yake ya uanachama wa chama cha demokrasia na maendeleo Chadema kuitisha mikutano ya hadhara mkoa wa Dar es salaam kuwahimiza wananchi na wakazi wake kususia kulipa ushuru mpaka wahusika wachukuliwe hatua.

Kadhalika,Jacobo amesema katika Ripoti ya CAG kumeonesha ufisadi mkubwa ikiwemo kupoteza fedha za miradi,fedha za mikopo kwa vijana,kuchelewa kwa miradi.

Pamoja na hayo Jacobo amesema hatua alizochukua Rais wa Jamhuri wa Muungano,Samia Suluhu Hassani,kuhusu wahusika waliotajwa kwenye Ripoti ya CAG na kusema hatua hiyo ni ndogo kwani hatua zaidi zinahitajika

Source : Ripoti ya CAG yaendelea kutikisa nchi, Meya Boniface aibuka atangaza mgomo huu mzito.
 
18 April 2023
Namanyele Nkasi
Rukwa, Tanzania

Rose Mayemba - Fedha Zilizoibiwa Zote Zirejeshwe



Katika ziara ya kikazi ya viongozi CHADEMA kanda ya Nyasa, mwenyekiti wa Chadema, Mkoa wa Njombe, Rose Mayemba ..... baada ya 2020 wananchi wameshindwa kupata taarifa za CAG kwa uwazi na kuzijadili kwa kina madhara yake kwa jamii nzima .... lakini juhudi hizo za kuifanya CCM ibakie pekee yake ktk uwanja wa siasa zimefeli na sasa tunakuja kwenu wananchi kuwashukuru kwa uvumilivu na kupata wasaa wa kujadili mustaktabali wa nchi yetu ikiwemo ripoti hii ya CAG ...
 
GWAMAKA MBUGHI - HALMASHAURI NA MAJIJI YALIZEMBEA



Jiji la Mbeya, halmashauri ya Chunya, Ileje, Busokelo, Wangingombe, Iringa mjini pia Nkasi ripoti ya CAG yaelezea matumizi ya mashaka na upotevu mkubwa..

Viongozi wa CHADEMA wanaendelea kuchambua ripoti ya CAG mbele ya wananchi na vyombo vya habari nchini kote ...
 
19 April 2023
Mwanza, Tanzania

Ezekia Wenje ataka waliokula fedha za umma wakamatwe

Mwenyekiti wa Chadema Kanda ya Victoria, Ezekia Wenje ameonyesha kukerwa na tabia ya baadhi ya viongozi ambao kazi yao ni kusifia kila linalofanyika katika Serikali hata kama ni jambo lenye madhara kwa maslahi kwa Umma.

Pia amesema watanzania wengi wamezoea mateso jambo linalosababisha wasichukue hatua wanapoona ubadhilifu wa fedha za Umma na matumizi mabovu ya rasilimali za Umma.

Hivyo kuwataka wananchi kuwa mstari wa mbele kupiga kelele pale fedha za umma zinapofanyiwa ubadhirifu kama ripoti ya CAG iliyotelewa ikionesha hali hiyo mbaya
 
17 April 2023

SUGU ALICHANA BUNGE KUHUSU RIPOTI YA CAG "HALIJISHUGHULISHI NA MAMBO YA WANANCHI WANAPELEKAJE NOVEMBER "

 


Meya na diwani wa zamani wa Kinondoni na Ubungo akiwa na ripoti za CAG mbele yake mezani studio ya Wasafi MEDIA na kuulizwa maswali na jopo la watangazaji na pia wasikilizaji anafafanua sababu za udhaifu wa kiuongozi ktk halmashauri za Dar es Salaam na nchini kwa ujumla.

Meya mstaafu Boniface Jacob aelezea jinsi wakaguzi wa ndani wa Halmashauri jinsi wanavyofanyiwa mizengwe kwa kunyimwa vitendea kazi ikiwemo usafiri na ofisi za Ukaguzi wa Ndani kuwekwa pembeni mbali na mkurugezi wa Halmashauri ili kuwakatisha tamaa na wasifurahie mazingira ya ofisi zao na kutishia ufanisi wa kazi yao nyeti ya ukaguzi .

Kada wa CHADEMA kamanda Boniface Jacob katika mahojiano exclusive na ya wazi ameelezea mapungufu makubwa ya wakurugenzi wa majiji na halmashauri za miji ambao hawana uzoefu lakini walipachikwa ktk nafasi za juu za uongozi na kusababisha CAG kuibua madhaifu mengi

Mfano ni ikiwemo matumizi mabaya ya kodi, kutofuata utaratibu, kulipa fedha za madawa Bohari Kuu ya Madawa MSD kisha Halmashauri hizo kutokwenda kuchukua mabilioni ya madawa na vifaa tiba vilivyolipiwa lakini havikuchukuliwa kupelekwa ktk mahospitali kutibu wananchi ....


Meya mstaafu alipoulizwa chini kuhusu kipindi halmashauri ya Kinondoni na Ubungo zilipokuwa na mameya na madiwani wengi wa CHADEMA hali ilikuwaje?

Meya Mstaafu Boniface Jacob anasema walidhibiti mianya ya upotevu wa Mali na matumizi mabaya ya mapato pia kodi hivyo kuibuka na hati safi kutoka kwa CAG na kusema hii ndiyo faida ya kuwa na sifa za kweli za vyama vingi Mali ya umma inalindwa kwani kuna macho ya vyama ktk baraza la udiwani, bungeni na vyombo huru vya habari kuhoji yaliyomo ktk ripoti ya CAG bila woga kama kipindi cha John Magufuli ambapo mahojiano hayo hayangewezekana na hata kama yangefanyika basi wangekuwa wamezingirwa nje ya ofisi na watu wasiojulikana kuwatisha na kuwatia nguvuni...

Kuhusu nini kifanyike ili halmshauri ziwe na wakurugenzi na wakuu wa idara thabiti walio na uwezo wa kufanya kazi kwa umahiri, meya mstaafu Boniface Jacob anasema wafanyakazi wa Halmashauri na idara za serikali waliofanya kazi kwa muda mrefu ndiyo wanatakiwa kupandishwa vyeo kuwa wakurugenzi au wakuu wa idara badala ya makada wa UVCCM na CCM kupachikwa ktk uongozi wakati hawana uzoefu ktk ofisi za umma.

Hawa ndio madiwani sasa.
 
DC ARUSHA : HALMASHAURI UWEZO MDOGO, AKILI ZIKIGOTA TUNAINGILIA,



Mkuu wa wilaya Ya Arusha Ferician Mtahengerwa ameelza ameshangazwa na kitendo cha Mmbunge wa Arusha mjini Mrisho Mashaka Gambo kuongea kila mahali anapopata nafasi ikiwemo Bungeni kuwa kunaudhaifu wa usimamizi wa fedha za miradi na ubadhilifu wa fedha hizo katika jiji la Arusha huku akituhumu ofisi ya Mkuu wa Mkoa na Mkuu wa Wilaya kuwa zinabariki mambo hayo kutokea Mkuu wa Wilaya Mtahengerwa ameeleza kuwa tuhuma za Mbunge Gambo ni siasa za kitoto kwa kuwa serikali ilishachukua hatua za Kali kwa watumishi waliohusika na yeye Mbungaje anafahamu lakin bado anatumia mambo hayo kama kiki kisiasa.
Source : Global TV online
 
Back
Top Bottom