Bongo Star Search 2009: Burudani kweli!?

P-Funk ni yule chotara mwenye macho ya bangi bangi? Kama ni yule hafai kuwa judge. Nashangaa kwa nini Madame Ritta hajatambua hilo. Anafanya kipindi kizima kionekane useless. Idea nzima ya Bongo Star Search sio mbaya, ila wakae watu sober zaidi pale kama judges. Huyo Salama naona amejirekebisha kidogo, bila shaka baada ya kupata exposure kidogo. Hivi alikuwa wapi vile?
 
ila kwa sasa wamejirekebisha sana. wako poa sana. Na hivi wamemleta salama mambo swafi.
 
BSS wamefanikiwa kwa kiasi kikubwa kutoa lugha za kejeli na maudhi na wakasahau kabisa kuwa jukumu kubwa ni kuibua kipaji cha mshiriki katika muziki. Tangu kipindi hiki kianze hakuna mshiriki (aliyeshinda) ambaye ameweza kwenda sambamba na kina AY, Banana Zoro, Stara T etc. Angalia vipindi kama American Idol, You got talent etc product zinazotoka ni za uhakika (acha tuhuma za hivi karibuni dhidi ya AI). Majaji wako objective hata kama comment zao ni za maudhi lakini utaona jinsi mwisho wa siku mshindi anavyoweza kutamba nje ya AI kwa kupata recording contracts na kutoa nyimbo maridhawa. Nafikiri ni ufahamu mdogo wa majaji katika dhima nzima ya BSS
 
Hatimae zile mbio za kumkimbiza catherine ntepa kutoka BSS ZIMEFANIKIWA NA LEO HII MTU ALIE NA FURAHA KUPITA WOTE SI MWINGINE BALI NI BI MKUBWA SALAMA JABIR ALIEJITAHIDI SANA KUTOMPA SUPPORT TOKA MWANZONI WA MASHINDANO
DA CATHE KILA LA KHERI WE UNA KIPAJI...
 
Nafikiri Catherine ametoka kwa kura chache kuliko washiriki wenzake watano. Na mimi naona kosa litakuwa la kwake mwenyewe. Ni kweli ana kipaji, lakini uamuzi unafanywa na wapiga kura ambao si wataalamu wa muziki, hivyo yeye alipaswa aimbe nyimbo ambazo ni maarufu na zinafahamika na wapiga kura.
 
thread ya mwaka 2009.
kipindi hicho madam rita alikuwa mrembo kweli kweli. alikula sana pesa za mzee mengi.

dah kweli kila nyakati na kumbukumbu zake.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom