Pole sana Daktari ambaye unajinadi kuwa upo Rwanda tena kwa mikoogo na ujuvi!
Hebu waulize hao madaktari wenye asili ya kinywaranda especially maspecialist wa hapo Rwanda walisoma wapi halafu utanijibu.
Kama kufanya kazi ya udaktari nje ya Tanzania ndio kigezo chako cha ubora wa Bugando basi nenda Botswana utawakuta wana MUCHS wako wizarani,nenda south Africa utawakuta wana MUCHS wanamiliki hospitali.
Ni hulka hii hii ya kudharau ukweli mchungu kwamba Muhimbili au UDSM ni centers of excellency ndio imepelekea kuibuka kwa vyuo vya kata.Ni hulka hii ndiyo imefanya eti hata vilaza kujilinganisha na vipanga na kuona mambo ni marahisi tu!Ni hulka hii inayomkosesha mwanafunzi wa shule ya msingi ama sekondari anakosa role model!
Ni hulka hii inayoipa nguvu wizara ya afya au elimu ambapo kwa kiasi kikubwa wamejaa wataalamu wenye elimu za kuungaunga kuona kwamba yoyote aweza kuwa daktari,nurse,muhudumu wa afya kutoka chuo chochote tu,by the way Muhimbili wanacomplicate tu halafu mshahara si ule ule!!
Ni hulka hii inayofanya kupaona Agha Khani na hospitali za private ni bora sanaa kuliko Muhimbili kisa Uzuri wa majengo lakini ikishindikana wanarefer Muhimbili.
Ni hulka inayonikera kweli kweli ya kutokukubali kuwa kuna 1 na 9,kuna mwanga na giza,kuna juu na chini,kuna vipanga na vilaza,kuna DAR na Mtwara!
Hivi ni kwa nini hatupendi kuukubali ukweli huu mchungu...ambao mimi nimeusema na nitaendelea kuusema,mchukie au mfurahi au mtukane.
Bwa Dr wa abroad(rwanda) naona ulisikia sikia kuwa machifu wa muhimbili hawapiti mawodini na hivyo mentorship ni tatizo!porojo zile zile!mwambie aliyekuhadithia akusumulie vizuri!hivi chifu wa firm one akiondoka unakatazwa kwenda firm two?Anyways sihitaji kuingia into detailed experience ya uwepo wangu Muhimbili,Imtu,Udom n.k
Mimi ninapoendaga mahospitalini kule wanapopelekwa interns huwa siwaulizi MO au Residents kuhusu ubora wa interns bali nawauliza wahudumu na manesi na wagonjwa na majibu ninayoyapata ndio basis ya msimamo wangu huu ambao nilitarajia kuwa mtauita ni 'arrogance'
HOJA YANGU HUIFAHAMU?aunataka kusympathize na madaktari,wanafunzi wa IMTU?
Kama Muhimbili bado hajafikia kiwango sahau kuhusu taasisi hizo nyingine huu ni ukweli mchungu!
Unaongelea maadili ya udaktari?Hapo ndio umenikumbusha kitu....kwa taarifa nilizonazo ni kwamba somo la medical ethics halipo kwenye mitaala ya hivyo vyuo vya kata !
Daktari wa Rwanda karibu kwa mjadala.