Bomu la IMTU limeshalipuka, bado la UDOM!

Bomu la IMTU limeshalipuka, bado la UDOM!

Labda umwelekeze wewe huenda akaelewa,halafu hata kufanya uchunguzi kidogo ili ajue kwamba walimu wanaofundisha MUHIMBILI ndio haohao wanaofundisha IMTU,BUGANDO jamani ujinga huu cjui utaisha na hapa ndipo ninapopata kuelewa sababu ya nchi yetu kutoendelea,ni kwa kujawa na wasomi vilaza jamii ya MENINGITIS......!JINGA KABISA
Leo hospitali ya IMTU imefungwa kwa kutokukidhi viwango.
Daktari mkuu wa hospitali hiyo ni Yasini Mgonda amabaye alikuwa daktari bigwa hapo Muhimbili.
 
Leo hospitali ya IMTU imefungwa kwa kutokukidhi viwango.
Daktari mkuu wa hospitali hiyo ni Yasini Mgonda amabaye alikuwa daktari bigwa hapo Muhimbili.

Bado anapiga kazi muhimbili+ regency + aga khan
 
Sasa mwenye huu uzi ni Maku kweli hapo UDOM inahusiana vipi na mkasa wa IMTU?hivi hast generalization itaisha lini!kama msomi lazima ufanye local analysis research ili uweze kufanya critical Evaluation bila kuwa na bias,kwa lengo la kupata fact Tunaojua Mkasa wa IMTU tupo cool.

Inaonekana huu jamaa mleta mada sijui ni daktari by professional, na kama ndio, basi inaonekana alisoma kwa shida sana,na anapoona watu wengine wanakuwa madaktari roho inamuuma vibaya.
 
Leo hospitali ya IMTU imefungwa kwa kutokukidhi viwango.
Daktari mkuu wa hospitali hiyo ni Yasini Mgonda amabaye alikuwa daktari bigwa hapo Muhimbili.
Utakuwa unamjua na professa Gesas wa UDOM ambaye alikuwa ni mwalimu wa anatomy Muchs!
 
Inaonekana huu jamaa mleta mada sijui ni daktari by professional, na kama ndio, basi inaonekana alisoma kwa shida sana,na anapoona watu wengine wanakuwa madaktari roho inamuuma vibaya.
Inauma kwa kuwa umma utateketea kwa mizaha yetu hii!
 
Tanganyika watu wana upeo mdogo sana leo mnabishana swala la ubora wa chuo Wakati kikwete kwa zarau anatibiwa nje ya nchi,Nyerere kafia london we unakauka koo wa muhas kweli we una kichwa kikubwa akiri NUKTA,ukikulia uswahilini lazima uathirike kiakiri,Pole sana Ukiama uswahilini ndio utaiona DUNIA ipo vp!Karibu DUNIANI toka huko polini hujui kwamba Tz bado poli ndo maana wageni bado wanagombania kuwekeza ?
 
Serikali ingewekeza katika vyuo vya utabibu kama vile KILOSA,KIBAHA,MVUMI na MACHAME tungeweza kuwa na vyuo bora sana kuliko IMTU lakini kwa kuwa serikali na jamii yetu inaamini mafanikio yanakuja kwa kukurupuka na bahati bahati haya ndio matokeo yake.

Roma haikujengwa kwa siku moja,vile vile taasisi kama MUHAS,UDSM,SUA,MUCCOBS hazikujengwa siku moja.

Leo hii unashuhudia chuo kama KAM MEDICS kinafundisha matabibu usishangae mwakani kinatoa degree ya udaktari,udaktari wa meno,pharmacy,na kozi nyingine lukuki bila kujipanga halafu unategemea ilinganishwe na MUHAS...huu ni uhuni.

Nasikia sikia kuwa UDSM ilianza kama kitivo cha sheria cha chuo kikuu cha EAST AFRICA leo hii ni university yenye courses lukuki sasa linganisha na UDOM na mikozi yake lukuki iliyoanza juzi juzi halafu uniambie itakuwa sawa na UDSM...what a joke?go to ARUSHA UNIVERSITY,MAKUMIRA UNIVERSITY n.k ujionee idadi ya course zilizopo kulinganisha na resources.

Mbona taasisi kama DIT imebakia kuwa tech college na inatoa wahitimu wazuri tu bila hata kujipachika u-UNIVERSITY?

Tuache utani wa elimu hasa hasa elimu inayohusu afya.

Miaka takribani 15 tumeshuhudia wanafunzi wa sekondari wakifeli masomo ya sayansi vibaya sana PCB ikiwemo halafu linganisha na idadi ya wanafunzi wa udaktari katika kipindi hicho(waweza kuta zinalingana au hata kuwa kubwa kwa wahitimu wa elimu za afya) sasa utajiuliza wametokea wapi?

Muhimbili ilikuwa inadahili wanafunzi kati ya 70-150 kipindi kile cha watoto wakifaulu vizuri na nusu au robo tatu kati yao walikuwa wanadisco sasa leo hii Muhimbili anatoa 200,KCMC 100,Bugando 70,IMTU 90 n.k hii akili ya ukubwani au vyuoni imetokea wapi ghaflaghafla?....Tunaendekeza siasa ee?tunajidanganya wenyewe!

Siamini kama ni number ya watumishi wa afya waliopikwa nusu ndio imetuletea matokeo mazuri tunayoyaona kwenye afya kwa sasa bali ni juhudi za USA na wenzake.

Matokeo ya elimu hii ya kata ni uwepo wa semina nyiingi zinazoenda kwa jina la 'ON JOB TRAINING" hii inadhihirisha kuwa mabomu yaliyotegwa na vyuo vyetu inabidi yateguliwe..swali ni kwamba tutaweza kuyategua yote kwa wakati kabla hayajalipuka?...jibu ni hapana na mengine ndio hayoo yanalipuka!
 
Huwa najiuliza kwanini wanajf wengi ni wapumbavu sipati jibu.

Ukienda jukwaa la elimu ndo utaumia zaidi.

Hakuna mijadala ya kitaaluma zaidi ya matusi na kashifa.

Unaelekeza hawaelewi,unabaki kucheka kwa huzuni tu.

Asante mkuu, kumbe wanaoliona hili wapo wengi!! Wajinga ni wengi sana aisee!
 
Tatizo madaktari wengi haswa waliosoma muhimbili mmekua wachoyo wa taluma hamtaki kabisa kusikia madaktari kutoka vyuo vingine ila ukweli ni kwamba vyuo hivi ni best kuliko muhimbili huko imebaki jina tu
Kwanza malecturer wenu ndo wanashinda kwenye korido za vyuo kama imtu, hkmu na vingine wakoomba ajira
Acheni ubaguzi
Hamuwezi kumaliza kutibu watz wenyewe
 
Sasa mkuu kama walimu wa UDOM ndo hao kutoka muhimbili basi tatizo lianzie muhimbili huko huko.
walimu wa Udom wengi wao ni juniors katika uzoefu wa kutibu na kufundisha,ndio kwanza wameanza!wengine wako Makerere wanasoma ili warudi kufundisha kwa ufasaha.
 
Pole sana Daktari ambaye unajinadi kuwa upo Rwanda tena kwa mikoogo na ujuvi!

Hebu waulize hao madaktari wenye asili ya kinywaranda especially maspecialist wa hapo Rwanda walisoma wapi halafu utanijibu.

Kama kufanya kazi ya udaktari nje ya Tanzania ndio kigezo chako cha ubora wa Bugando basi nenda Botswana utawakuta wana MUCHS wako wizarani,nenda south Africa utawakuta wana MUCHS wanamiliki hospitali.

Ni hulka hii hii ya kudharau ukweli mchungu kwamba Muhimbili au UDSM ni centers of excellency ndio imepelekea kuibuka kwa vyuo vya kata.Ni hulka hii ndiyo imefanya eti hata vilaza kujilinganisha na vipanga na kuona mambo ni marahisi tu!Ni hulka hii inayomkosesha mwanafunzi wa shule ya msingi ama sekondari anakosa role model!

Ni hulka hii inayoipa nguvu wizara ya afya au elimu ambapo kwa kiasi kikubwa wamejaa wataalamu wenye elimu za kuungaunga kuona kwamba yoyote aweza kuwa daktari,nurse,muhudumu wa afya kutoka chuo chochote tu,by the way Muhimbili wanacomplicate tu halafu mshahara si ule ule!!

Ni hulka hii inayofanya kupaona Agha Khani na hospitali za private ni bora sanaa kuliko Muhimbili kisa Uzuri wa majengo lakini ikishindikana wanarefer Muhimbili.

Ni hulka inayonikera kweli kweli ya kutokukubali kuwa kuna 1 na 9,kuna mwanga na giza,kuna juu na chini,kuna vipanga na vilaza,kuna DAR na Mtwara!
Hivi ni kwa nini hatupendi kuukubali ukweli huu mchungu...ambao mimi nimeusema na nitaendelea kuusema,mchukie au mfurahi au mtukane.

Bwa Dr wa abroad(rwanda) naona ulisikia sikia kuwa machifu wa muhimbili hawapiti mawodini na hivyo mentorship ni tatizo!porojo zile zile!mwambie aliyekuhadithia akusumulie vizuri!hivi chifu wa firm one akiondoka unakatazwa kwenda firm two?Anyways sihitaji kuingia into detailed experience ya uwepo wangu Muhimbili,Imtu,Udom n.k

Mimi ninapoendaga mahospitalini kule wanapopelekwa interns huwa siwaulizi MO au Residents kuhusu ubora wa interns bali nawauliza wahudumu na manesi na wagonjwa na majibu ninayoyapata ndio basis ya msimamo wangu huu ambao nilitarajia kuwa mtauita ni 'arrogance'

HOJA YANGU HUIFAHAMU?aunataka kusympathize na madaktari,wanafunzi wa IMTU?

Kama Muhimbili bado hajafikia kiwango sahau kuhusu taasisi hizo nyingine huu ni ukweli mchungu!

Unaongelea maadili ya udaktari?Hapo ndio umenikumbusha kitu....kwa taarifa nilizonazo ni kwamba somo la medical ethics halipo kwenye mitaala ya hivyo vyuo vya kata !

Daktari wa Rwanda karibu kwa mjadala.

Nakupa taarifa Daktari bora kuliko wote Tanzania yaani uti wa mgongo from MUHAS hakuna medicine kisichofundisha Medical Ethics.
 
Tatizo madaktari wengi haswa waliosoma muhimbili mmekua wachoyo wa taluma hamtaki kabisa kusikia madaktari kutoka vyuo vingine ila ukweli ni kwamba vyuo hivi ni best kuliko muhimbili huko imebaki jina tu
Kwanza malecturer wenu ndo wanashinda kwenye korido za vyuo kama imtu, hkmu na vingine wakoomba ajira
Acheni ubaguzi
Hamuwezi kumaliza kutibu watz wenyewe
wachoyo lakini wanafundisha!
Unamaanisha nini hasa?
Kweli Tanzania ni zaidi ya uijuavyo.
 
Nakupa taarifa Daktari bora kuliko wote Tanzania yaani uti wa mgongo from MUHAS hakuna medicine kisichofundisha Medical Ethics.
Taarifa naipokea !hahaha hebu niambie kuhusu forensic medicine na psychiatry!
 
The issue at hand is tatizo la msingi kuhusu elimu yetu lipo hususan ubora wa elimu itolewayo siyo tu katika higher learning institutions bali karibia ngazi zote!!siku hizi wanafunzi wa vyuo vikuu wasio jua kiingereza vizuri ni wengi mno ingawa wanafundishwa kwa kiingereza! Nenda UDOM, SUA, MZUMBE, STELLA MARIS,SAUTI,MT MERU na tatizo la ubora wa walimu lipo! hii imesababishwa na ongezeko la vyuo vikuu kuwa kubwa kuliko maandalizi ya walimu bora wenye uwezo wa kufundisha katika vyuo hivyo!! kinacho takiwa kama Taifa tungekuwa na watu wenye uwezo pale wazarani wafanye kitu kiitwacho EDUCATIONAL AUDITING ILI KUBAINI UBORA WA ELIMU ITOLEWAYO, UBORA WA WALIMU WALIOPO,NA HATA MINIMUM STANDARDS ZA CHUO HUSIKA KAMA ZIMETIMIA.
 
Back
Top Bottom