Bomu la IMTU limeshalipuka, bado la UDOM!

Bomu la IMTU limeshalipuka, bado la UDOM!

Yaani nimepata hasira kuu mkuu! Basi tu....

Haina haja blaza ni binadamu tu na hulka zetu!!!!!
Kama mtu haoni sababu ya CO kusomea udaktari wakati wakiingia huko wanatumia mtaala mmoja na wanamaliza wote leo anakuambia "kubebeshwa mzigo mzito" huyu kajiweka wazi dhamira na
itikadi yake!!!!!

Kaambiwa habari ya wahitimu walioenda nje na kukutana na chngamoto, badala ya kujibu kaleta sarakasi za lugha na kuchomoka halafu anasukuma lawama kwingine,huyu wa kukuumiza kichwa???!!

One arrogant chap, shunner, obsessed with social credo and segregative tendencies!!!!!
 
Mkuu ni kweli nimechafukwa kwani tunapoelekea ni kubaya !

I appreciate mchango wa wahudumu,manesi,clinicians na bila kusahau wahisani wa marekani et al katika sekta ya afya.

I personally have trained AMOs,COs Nurses and the like on TB,HIV,IMCI and the like,but the inflammatory fact is, they can never be an alternative to the real healthcare professionals.

Hapo tulikuwa tunazima moto tu kama mwalimu alipoanzisha kada ya AMO na leo hii tunahitaji MO !

Tusjidanganye kwa kurudia kosa,eti tufyatue MO wa kutosha hata kama hawana kiwango...ni kosa linalojirudia!

Tunahitaji MO na specialists wenye viwango for sustainability of the healthcare system.
Asubuhi njema kwako Daktari wangu.
Ni ukweli usofichika ya kuwa tunahitaji watu ambayo ni well qualified katika nyanja ya afya na naamini jitihada zimeanza kuonekana kutokana na kuanzishwa kwa vyuo vikuu vingi zaidi.
Naamini ni kweli kabisa kuwa kuna kada ambazo baada ya muda itabidi zifutike katika sheria kwani tutakuwa tumeshapiga hatua ya kuweza kuzalisha watu wa kutosha ku replace hizo kada.
Tupo katika kipindi cha mpito na with time tuta stabilize ingawa naamini wanaowafundisha hao ambao unaona ni kulipuliwa si ajabu ni wahitimu wa Chuo kitukufu kama Muhimbili;nani alaumiwe?
 
Yani huu ni upuuzi.si ajabu ni mabonzo yaliyojaa humu yanayoendelea kupromote vyuo walivyosoma tuwaone wa maana.mimi naamini utendaji wa kazi unategema individualy.wewe kama ni kilaza mvivu mzembe umesoma UDSM.utabaki kuwa kilaza tuu.mfano hai shule ya kwanza kitaifa matokeo ya form six mbona ni shule ndogo tuu imepita shule kubwa ngapi.??kwa hiyo usiishi kwa kukariri historia.soma dogo uje kuwa competent kazini..usitegemee kuja na ukilaza wako ujitete umesoma MUHAS uonekane wa maana.tutasema Dr fulani ni kilaza..wala sio Dr kutoka UDOM au DR kutoka BUGANDO.Tena muache mijadala isiyo na tija wala faida.bali ni discrimination zisizo na maana.kama wewe unajihisi ni Dr wa maana na genius kuliko wenzako tuambie lipya ulilofanya kwa taifa.
Tena inaonesha wengi ni vitoto hata rotation hawajamaliza vimetawaliwa na mawazo na tabia za kisecondary..competation na majigambo ya ajabu ajabu.mnajidhalilisha.

Pamoja na makosa madogo madogo ya kiuandishi. Unapoint kijana, kimsingi mpaka hivi sasa hakuna chuo kinachotoa madaktari bora zaidi ya Bugando hapa Tanzania.Hii ni kuanzia undergraduate mpaka post graduate.

MUHAS wamebaki na jina tu. Waalimu wako bize na vijiwe mjini hawana muda wa kutosha kutoa mentorship kwa vijana. Kutwa wapo TUMAINI, HINDUMANDAL, AGAKHAN NA VIJIWE VINGINE. Vijana unawakuta wanarandarand mawodini bila usimqmizi na muongozo wa kutosha. Waalimu ni arrogant kam MENINGITIS alivyo arrogant. Wanajisifia tu..utasikia i am the only so and so in TANZANIA, Sasa unakuwa proud kuwa peke yako? akimaanisha kuw a ni intelligent zaidi wakati tunawajua wameanzia diploma...na kwa pespective ya MENINGITIS kuanzia diploma ni UKILAZA.

Huu ni wakati MUHAS kupokea changamoto kutoka vyuo vingine positively na kujifanyia self evaluation na kuchukua hatu madhubuti.

Ukija kwenye usimamizi katika research dissertations kwa wanafunzi wa postgraduates ni worse. Waalimu hawanamuda wa kusoma dissertion ya mwanafunzi. Kutwa kukimbizana n vijiwe mjini, waalimu wamejawa hofu ya kunyang'anywa vijiwe na wanafunzi wao, hivyo wanahakikish wanagraduate wakiwa na as little knowledge as possible. HIYO NDIYO MUHAS YA LEO BWA MDOGO MENINGITIS.

Ndugu meningitis nenda mahospitalini ambako madaktari intern kutoka vyuo mbalimbali wanafanya internship, nenda ongea na ma MO au Residents wanaofanya nao kazi, watakuambi wanafunzi wa MUHAS wakoje hivi sasa. Acha kuongea bla bla hapa. Na bahti nzuri wote wanafanya intern katika hospitali hizo hizo chini ya wasimamizi wale walewale na wanakuwa recommended for regiatration na watu hao hao kwa ajili ya registration kwenye bodi hiyohiyo.

Sasa unaposema kuna madaktar wanasajiliwa na kupewa vyeti vya udaktari wakati hawana sifa nashindwa kuelelewa msingi wa hoja yako ni nini?. Unataka tuende mbali na kuanza kuangalia huyu daktar anaenitibu alifaulu vipi huko chuoni, kwamba nikikuta ulipata C kwenye OBGY basi hunizalishii mke wangu. Daktar jitazame, zingatia kanuni na miiko ya taaluma yako. Usipende ku create hofu kwa wananchi pasipokuwa na sababu za msingi.

Niko RWANDA Huku kuna madaktari wamesoma BUGANDO hakik they are doing wonderfull and i am proud of them as fellow TANZANIAN.
 
UDOM ndio usiseme,maana hata wakufunzi wao ni vituko!!unakuta lecturer anashindwa challenge kidogo tu toka kwa wanafunzi,maana anakua hanatofauti yoyote ya ufahamu wa mambo kulinganisha na wanafunzi wake.hili nalo ni bomu lingine kaka.

basi elimu ya tz ni ovyo in general.....coz 99% of the lecturers in tz wamesoma UD
 
Mkuu analysti nashukuru kwa mchango wako. Ubarikiwe huko na hao mabalozi wetu huko wape salamu na shukurani juu ya hayo wafanyayo!!!!!
 
Last edited by a moderator:
Kuna rafiki yangu mmoja alisomea udaktari Muhimbili,akaenda Marekani kwa lengo la kufanya kazi kama daktari.Baada ya kukutana na vikwazo vya mitihani ya bodi,akaamua atafute kazi nyingine na sasa ni mfanyabiashara.

Rafiki yangu mwingine naye alisomea udaktari hapo hapo Muhimbili.Baadaye akafanya specialization(ubingwa)Muhimbili au Bugando kwa muda wa miaka miwili au mitatu kama sikosei.Sasa yuko nchi moja Ulaya mwaka wa pili anahangaika kurudia kozi za udaktari upya na kisha anatakiwa afanye mitihani ya udaktari ya wizara ya afya ya nchi husika au bodi ya madaktari, na kama atafaulu ndipo atapewa leseni ya kumruhusu kutibu wagonjwa.

Halafu hapa watu wanajisifia kuwa chuo chao cha Muhimbili ni bora zaidi.Kama nyie wazuri,mbona mkiletewa kesi mnazi refer India na South Africa?Vifaa hakuna na wataalam hakuna;kwasababu kama huna vifaa vya kutosha na vya kisasa shuleni,hutaweza pia kutengeneza wataalam wazuri.

Tufanyeje ili tutoke?Tufanyeje walau na sisi tuwe na wataalam competent na hospitali hata 3 tu nchi nzima zenye viwango kama vya India na South Africa?Tufanyeje ili India na Ulaya nao siku moja watamani kuleta wagonjwa wao Tanzania iliyosheheni wataalam wenye sifa zinazoheshimika duniani kote?Nadhani haya ndiyo yakujadili kama tunataka kuboresha sekta ya afya nchini.

Huwezi kusema wewe ni bora kuliko IMTU au UDOM wakati kwenye soko la dunia wote mnatupwa kapu moja na ili mpate ajira ya udaktari,wote mnalazimishwa kufuata utaratibu unaofanana kulingana na nchi mliyosomea udaktari wenu.
Kamata LIKE mkuu. Umemaliza kila kitu. Siendelei kusoma thread ya kipuuzi kama hii.
 
Teh teh teh! Madaktari wenyewe ndio nyie, operesheni ya kichwa mnapasua mguu. Eti Muhimbili the best.. Mnatoa madaktari au ushuzi?
 
Teh teh teh! Madaktari wenyewe ndio nyie, operesheni ya kichwa mnapasua mguu. Eti Muhimbili the best.. Mnatoa madaktari au ushuzi?
Mkuu jaribu kufuatilia mambo kwa kina, kosa la upasuaji Lilikua la kimawasiliano sio lakitechnical...it happens everywhere, atahuko America mnapopasifia pia yanatokea, mtu anaenda kutahiriwa anaishia kukatwa uume mzima Imetokea Huko jimbo la Alabama hivi majuzi, kwa uwezo wako wa kufikiria utasema huyo daktari pia amesoma MUHAS
 
Ni kweli mimi ni mfuasi wa ligi tajwa,na sababu ya msingi ni moja tu...I believe in quality and not quantity.

Ni heri kuwa na vichwa mia moja kuliko vihiyo millioni moja.

Unatumia standard gani kuhukumu hivyo vyuo unavyosema vinatoa quantity na sio watu walioelimika, eleza na udhaifu wa vyuo ulivyotaja. Kuhusu rafikiyo aliefeli kidato cha nne, watu kuna kipindi hufanya vibaya na baadae kurekebisha makosa yao na vice versa. Mfano tu Charles Darwin alikua ovyo mpaka walimu wake na baba yake wakasema akili yake iko below standard..
 
Teh teh teh! Madaktari wenyewe ndio nyie, operesheni ya kichwa mnapasua mguu. Eti Muhimbili the best.. Mnatoa madaktari au ushuzi?

Na hospital zetu hapa bongo ukienda unaomba Mungu upone otherwise ni majanga watu wangekuja na point nini kifanyike kurekebisha tatizo mana naona elimu ya Tanzania inapumulia machine hamna bora hapo
 
Sasa mwenye huu uzi ni Maku kweli hapo UDOM inahusiana vipi na mkasa wa IMTU?hivi hast generalization itaisha lini!kama msomi lazima ufanye local analysis research ili uweze kufanya critical Evaluation bila kuwa na bias,kwa lengo la kupata fact Tunaojua Mkasa wa IMTU tupo cool.
 
Tunaposema huu upuuzi wa vyuo vya kata hautakiwi watu wanasema tuna dharau bora jamii inajionea yenyewe.
Ati mtu alifeli kidato cha nne leo hii anapewa cheti cha kuwa daktari...ukiuliza nini eti ooh tunapunguza uhaba wa madaktari...pambaff sana.



MY TAKE


  • SERIKALI INATAFUTA KURA
  • G.ABACHORI ANASAKA NOTI
  • MLALAHOI ANASAKA AJIRA YA URAHISI

Fallacy of generalization.
Ukiwa mjinga ficha ujinga wako lau kwa kukaa kimya.
 
Kweli wewe unaumwa UTI wa MGONGO,..chuo ni material ulionayo kichwani na siyo UDOM,SUA au UDSM.Ndo maana mnakosa kazi kwa sababu unadhani ukisoma UDSM ndio kuajiliwa badala ya kujibidiisha.Kuwa na mtazamo mpana other wise utakuwa unapiga kwenzi ncha ya mkuki.
 
pamoja na makosa madogo madogo ya kiuandishi. Unapoint kijana, kimsingi mpaka hivi sasa hakuna chuo kinachotoa madaktari bora zaidi ya bugando hapa tanzania.hii ni kuanzia undergraduate mpaka post graduate.

Muhas wamebaki na jina tu. Waalimu wako bize na vijiwe mjini hawana muda wa kutosha kutoa mentorship kwa vijana. Kutwa wapo tumaini, hindumandal, agakhan na vijiwe vingine. Vijana unawakuta wanarandarand mawodini bila usimqmizi na muongozo wa kutosha. Waalimu ni arrogant kam meningitis alivyo arrogant. Wanajisifia tu..utasikia i am the only so and so in tanzania, sasa unakuwa proud kuwa peke yako? Akimaanisha kuw a ni intelligent zaidi wakati tunawajua wameanzia diploma...na kwa pespective ya meningitis kuanzia diploma ni ukilaza.

Huu ni wakati muhas kupokea changamoto kutoka vyuo vingine positively na kujifanyia self evaluation na kuchukua hatu madhubuti.

Ukija kwenye usimamizi katika research dissertations kwa wanafunzi wa postgraduates ni worse. Waalimu hawanamuda wa kusoma dissertion ya mwanafunzi. Kutwa kukimbizana n vijiwe mjini, waalimu wamejawa hofu ya kunyang'anywa vijiwe na wanafunzi wao, hivyo wanahakikish wanagraduate wakiwa na as little knowledge as possible. Hiyo ndiyo muhas ya leo bwa mdogo meningitis.

Ndugu meningitis nenda mahospitalini ambako madaktari intern kutoka vyuo mbalimbali wanafanya internship, nenda ongea na ma mo au residents wanaofanya nao kazi, watakuambi wanafunzi wa muhas wakoje hivi sasa. Acha kuongea bla bla hapa. Na bahti nzuri wote wanafanya intern katika hospitali hizo hizo chini ya wasimamizi wale walewale na wanakuwa recommended for regiatration na watu hao hao kwa ajili ya registration kwenye bodi hiyohiyo.

Sasa unaposema kuna madaktar wanasajiliwa na kupewa vyeti vya udaktari wakati hawana sifa nashindwa kuelelewa msingi wa hoja yako ni nini?. Unataka tuende mbali na kuanza kuangalia huyu daktar anaenitibu alifaulu vipi huko chuoni, kwamba nikikuta ulipata c kwenye obgy basi hunizalishii mke wangu. Daktar jitazame, zingatia kanuni na miiko ya taaluma yako. Usipende ku create hofu kwa wananchi pasipokuwa na sababu za msingi.

Niko rwanda huku kuna madaktari wamesoma bugando hakik they are doing wonderfull and i am proud of them as fellow tanzanian.

,,!tunahitaji raisi makini,
jk elimu halikua chaguo lake.
..,,.,, thread closed...
 
Mleta mada unaonekana kuwa na mawazo ya kizamani yaliyokwisha kupitwa na wakati,

Badala ya ku focus kwenye tatizo ambalo halihusiani kabisa na Academics za wanafunzi hawa likiwemo hili la Negligence iliyofanywa na IMTU administration unaishia kuwashambulia wanafunzi wasiokuwa na hatia.

Kwa mawazo yako hayo finyu nimeshapata kujua wewe ni mtu wa aina gani pamoja na dharau zako zilizopitiliza unaonekana kuwa mtu usiyependa kuona mwingine amesoma na kufanikiwa katika hii field ya Afya, sasa sijui ulitaka familia yenu peke yenu iwe na madokta hata sijakuelewa,.

Acha majungu yasiyokuwa na tija, fanya kazi kwa bidii uendeshe maisha yako na familia kama unayo.[/QUO
Ucjali sana mkuu,yanaonekana wazi huyu bwana kahitimu na wala hajaelimika maana kama anashindwa kujua kwamba utupaji wa takataka sio kazi ya mwanafunzi wa chuo nashindwa kuelewa ni chuo gani amesoma,pia yapaswa ajue kwamba "EDUCTION IS WHATS REMAIN AFTER LEARNING HAS GONE" sasa yeye bado yupo kulekule zilipendwa ( 90 za kwenye karatasi but no skills at hands ) Halafu hizo UD products anazozisifia si ndio hawa wakina MULUGO,KAPUYA,CHENGE.......! wamesaidia nini nchi hii,kwangu mimi only skills and competence on the professionalism do matter not name of the institute underwent,as long as wote tunakesha huku miguu ikiwa kwenye beseni la maji hana huna jipya
 
Asubuhi njema kwako Daktari wangu.
Ni ukweli usofichika ya kuwa tunahitaji watu ambayo ni well qualified katika nyanja ya afya na naamini jitihada zimeanza kuonekana kutokana na kuanzishwa kwa vyuo vikuu vingi zaidi.
Naamini ni kweli kabisa kuwa kuna kada ambazo baada ya muda itabidi zifutike katika sheria kwani tutakuwa tumeshapiga hatua ya kuweza kuzalisha watu wa kutosha ku replace hizo kada.
Tupo katika kipindi cha mpito na with time tuta stabilize ingawa naamini wanaowafundisha hao ambao unaona ni kulipuliwa si ajabu ni wahitimu wa Chuo kitukufu kama Muhimbili;nani alaumiwe?

Labda umwelekeze wewe huenda akaelewa,halafu hata kufanya uchunguzi kidogo ili ajue kwamba walimu wanaofundisha MUHIMBILI ndio haohao wanaofundisha IMTU,BUGANDO jamani ujinga huu cjui utaisha na hapa ndipo ninapopata kuelewa sababu ya nchi yetu kutoendelea,ni kwa kujawa na wasomi vilaza jamii ya MENINGITIS......!JINGA KABISA
 
Pamoja na makosa madogo madogo ya kiuandishi. Unapoint kijana, kimsingi mpaka hivi sasa hakuna chuo kinachotoa madaktari bora zaidi ya Bugando hapa Tanzania.Hii ni kuanzia undergraduate mpaka post graduate.

MUHAS wamebaki na jina tu. Waalimu wako bize na vijiwe mjini hawana muda wa kutosha kutoa mentorship kwa vijana. Kutwa wapo TUMAINI, HINDUMANDAL, AGAKHAN NA VIJIWE VINGINE. Vijana unawakuta wanarandarand mawodini bila usimqmizi na muongozo wa kutosha. Waalimu ni arrogant kam MENINGITIS alivyo arrogant. Wanajisifia tu..utasikia i am the only so and so in TANZANIA, Sasa unakuwa proud kuwa peke yako? akimaanisha kuw a ni intelligent zaidi wakati tunawajua wameanzia diploma...na kwa pespective ya MENINGITIS kuanzia diploma ni UKILAZA.

Huu ni wakati MUHAS kupokea changamoto kutoka vyuo vingine positively na kujifanyia self evaluation na kuchukua hatu madhubuti.

Ukija kwenye usimamizi katika research dissertations kwa wanafunzi wa postgraduates ni worse. Waalimu hawanamuda wa kusoma dissertion ya mwanafunzi. Kutwa kukimbizana n vijiwe mjini, waalimu wamejawa hofu ya kunyang'anywa vijiwe na wanafunzi wao, hivyo wanahakikish wanagraduate wakiwa na as little knowledge as possible. HIYO NDIYO MUHAS YA LEO BWA MDOGO MENINGITIS.

Ndugu meningitis nenda mahospitalini ambako madaktari intern kutoka vyuo mbalimbali wanafanya internship, nenda ongea na ma MO au Residents wanaofanya nao kazi, watakuambi wanafunzi wa MUHAS wakoje hivi sasa. Acha kuongea bla bla hapa. Na bahti nzuri wote wanafanya intern katika hospitali hizo hizo chini ya wasimamizi wale walewale na wanakuwa recommended for regiatration na watu hao hao kwa ajili ya registration kwenye bodi hiyohiyo.

Sasa unaposema kuna madaktar wanasajiliwa na kupewa vyeti vya udaktari wakati hawana sifa nashindwa kuelelewa msingi wa hoja yako ni nini?. Unataka tuende mbali na kuanza kuangalia huyu daktar anaenitibu alifaulu vipi huko chuoni, kwamba nikikuta ulipata C kwenye OBGY basi hunizalishii mke wangu. Daktar jitazame, zingatia kanuni na miiko ya taaluma yako. Usipende ku create hofu kwa wananchi pasipokuwa na sababu za msingi.

Niko RWANDA Huku kuna madaktari wamesoma BUGANDO hakik they are doing wonderfull and i am proud of them as fellow TANZANIAN.
Pole sana Daktari ambaye unajinadi kuwa upo Rwanda tena kwa mikoogo na ujuvi!

Hebu waulize hao madaktari wenye asili ya kinywaranda especially maspecialist wa hapo Rwanda walisoma wapi halafu utanijibu.

Kama kufanya kazi ya udaktari nje ya Tanzania ndio kigezo chako cha ubora wa Bugando basi nenda Botswana utawakuta wana MUCHS wako wizarani,nenda south Africa utawakuta wana MUCHS wanamiliki hospitali.

Ni hulka hii hii ya kudharau ukweli mchungu kwamba Muhimbili au UDSM ni centers of excellency ndio imepelekea kuibuka kwa vyuo vya kata.Ni hulka hii ndiyo imefanya eti hata vilaza kujilinganisha na vipanga na kuona mambo ni marahisi tu!Ni hulka hii inayomkosesha mwanafunzi wa shule ya msingi ama sekondari anakosa role model!

Ni hulka hii inayoipa nguvu wizara ya afya au elimu ambapo kwa kiasi kikubwa wamejaa wataalamu wenye elimu za kuungaunga kuona kwamba yoyote aweza kuwa daktari,nurse,muhudumu wa afya kutoka chuo chochote tu,by the way Muhimbili wanacomplicate tu halafu mshahara si ule ule!!

Ni hulka hii inayofanya kupaona Agha Khani na hospitali za private ni bora sanaa kuliko Muhimbili kisa Uzuri wa majengo lakini ikishindikana wanarefer Muhimbili.

Ni hulka inayonikera kweli kweli ya kutokukubali kuwa kuna 1 na 9,kuna mwanga na giza,kuna juu na chini,kuna vipanga na vilaza,kuna DAR na Mtwara!
Hivi ni kwa nini hatupendi kuukubali ukweli huu mchungu...ambao mimi nimeusema na nitaendelea kuusema,mchukie au mfurahi au mtukane.

Bwa Dr wa abroad(rwanda) naona ulisikia sikia kuwa machifu wa muhimbili hawapiti mawodini na hivyo mentorship ni tatizo!porojo zile zile!mwambie aliyekuhadithia akusumulie vizuri!hivi chifu wa firm one akiondoka unakatazwa kwenda firm two?Anyways sihitaji kuingia into detailed experience ya uwepo wangu Muhimbili,Imtu,Udom n.k

Mimi ninapoendaga mahospitalini kule wanapopelekwa interns huwa siwaulizi MO au Residents kuhusu ubora wa interns bali nawauliza wahudumu na manesi na wagonjwa na majibu ninayoyapata ndio basis ya msimamo wangu huu ambao nilitarajia kuwa mtauita ni 'arrogance'

HOJA YANGU HUIFAHAMU?aunataka kusympathize na madaktari,wanafunzi wa IMTU?

Kama Muhimbili bado hajafikia kiwango sahau kuhusu taasisi hizo nyingine huu ni ukweli mchungu!

Unaongelea maadili ya udaktari?Hapo ndio umenikumbusha kitu....kwa taarifa nilizonazo ni kwamba somo la medical ethics halipo kwenye mitaala ya hivyo vyuo vya kata !

Daktari wa Rwanda karibu kwa mjadala.
 
Back
Top Bottom