Bomu la IMTU limeshalipuka, bado la UDOM!

Bomu la IMTU limeshalipuka, bado la UDOM!

Kuna rafiki yangu mmoja alisomea udaktari Muhimbili,akaenda Marekani kwa lengo la kufanya kazi kama daktari.Baada ya kukutana na vikwazo vya mitihani ya bodi,akaamua atafute kazi nyingine na sasa ni mfanyabiashara.

Rafiki yangu mwingine naye alisomea udaktari hapo hapo Muhimbili.Baadaye akafanya specialization(ubingwa)Muhimbili au Bugando kwa muda wa miaka miwili au mitatu kama sikosei.Sasa yuko nchi moja Ulaya mwaka wa pili anahangaika kurudia kozi za udaktari upya na kisha anatakiwa afanye mitihani ya udaktari ya wizara ya afya ya nchi husika au bodi ya madaktari, na kama atafaulu ndipo atapewa leseni ya kumruhusu kutibu wagonjwa.

Halafu hapa watu wanajisifia kuwa chuo chao cha Muhimbili ni bora zaidi.Kama nyie wazuri,mbona mkiletewa kesi mnazi refer India na South Africa?Vifaa hakuna na wataalam hakuna;kwasababu kama huna vifaa vya kutosha na vya kisasa shuleni,hutaweza pia kutengeneza wataalam wazuri.

Tufanyeje ili tutoke?Tufanyeje walau na sisi tuwe na wataalam competent na hospitali hata 3 tu nchi nzima zenye viwango kama vya India na South Africa?Tufanyeje ili India na Ulaya nao siku moja watamani kuleta wagonjwa wao Tanzania iliyosheheni wataalam wenye sifa zinazoheshimika duniani kote?Nadhani haya ndiyo yakujadili kama tunataka kuboresha sekta ya afya nchini.

Huwezi kusema wewe ni bora kuliko IMTU au UDOM wakati kwenye soko la dunia wote mnatupwa kapu moja na ili mpate ajira ya udaktari,wote mnalazimishwa kufuata utaratibu unaofanana kulingana na nchi mliyosomea udaktari wenu.

Safi sana mkuu kwa kuelewa somo langu!waingereza au wamarekani hawataki kabisa kuruhusu uchakachuaji wa fani ya udaktari au afya kwa ujumla.

Ni haki yao kuiita MUHAS,UDOM,IMTU n.k kama vyuo visivyo na viwango kulingana na viwango walivyojiwekea.sasa nakushangaa sana unapochukia kuona watanzania tukiita IMTU haijakidhi viwango vya kitanzania.
Kuna kipindi ilikuwa ni lazima kupita internship Muhimbili kama hukusomea udaktari hapo Muhimbili!sasa ni bora liende!
 
Sioni uhusiano wa kichwa cha habari na content, pia mwandishi anaonekana ni mfuasi wa ligi za vyuo plus hakipendi UDOM, binafsi nimesoma UDOM na nafurahi kuwa msaada kazini na kwa jamii inayonizunguka kutokana na maarifa niliyopata. Swala la IMTU linaonekana lilikua la cost saving na kubanwa na deadline ya ukaguzi, sijui wanafunzi wao wanaingiaje hapo. Mwisho wa siku muhusika anaenda kusimamia uwezo wake na chuo alichotoka kitakua hakina msaada. Hata UDSM ina watu wametoka pale na kuwa msaada mkubwa sana kwa hii nchi lakini kuna wengine wametoka pale kama wametumwa kuwakatisha tamaa Watanzania.

Ni kweli mimi ni mfuasi wa ligi tajwa,na sababu ya msingi ni moja tu...I believe in quality and not quantity.

Ni heri kuwa na vichwa mia moja kuliko vihiyo millioni moja.
 
Labda hata mzee wako analo analolijua au hata wangu pia lakini kuna vitu wewe unajua zaid yao wote !!!!

Sio ajabu mimi kujua pia zaid yako!!!!!

Mkubwa wako akikueleza sikiliza!
Naijua MUCHS,KCMC,BUGANDO,KAIRUKI,IFAKARA,IMTU,UDOM,MBARARA,MAKERERE,NAIROBI!!

Lakini leo tunaongelea IMTU na UDOM!!

Iko siku tutaiongelea MUHAS VS MUCHS
 
Eti kufeli ni accelerator ya kufanya vizuri!
Kufeli ni kufeli tu hata ukibadilisha jina!
Kwa hiyo mmewaambia walimu wafelishe ili baadae watu wafaulu?

Yaani umefeli shule ya msingi,sekondari halafu leo umeibuka na PHD!
Hii iko Tanzania tu na ndio maana tunajionea vimbwanga!

UDOM na IMTU limekuwa kimbilio la wale walioshindwa na kuingia makazini kwa kada za clinical officers,AMO,n.k

ilitakiwa kuwe na program tofauti ya kuwaendeleza watu hawa na sio kuwapa elimu nzito ya udaktari kisa wanataka kupandishwa vyeo!

Hapa ni sawa na issue ya kila kijana kutaka kuimba bongo fleva hata kama ni bubu!

Now i can believe that your brain is being inflammed,...
 
Sarungi profesa,daktari wa mifupa?Vipi ilikuwaje ishu yake kwani?
Alisomea east europe na aliporudi akakutana na sera hizo za kudharauliana lakini at the end the day akawa profesa mzuri kuliko hata hao wa kujisikia (nilisimuliwa na Daktari mmoja marehemu sasa).
 
Safi sana mkuu kwa kuelewa somo langu!waingereza au wamarekani hawataki kabisa kuruhusu uchakachuaji wa fani ya udaktari au afya kwa ujumla.

Ni haki yao kuiita MUHAS,UDOM,IMTU n.k kama vyuo visivyo na viwango kulingana na viwango walivyojiwekea.sasa nakushangaa sana unapochukia kuona watanzania tukiita IMTU haijakidhi viwango vya kitanzania.
Kuna kipindi ilikuwa ni lazima kupita internship Muhimbili kama hukusomea udaktari hapo Muhimbili!sasa ni bora liende!

Nakushangaa kuwaita IMTU hawana viwango wakati na mwenyewe wa Muhimbili huna viwango.Kama IMTU,nawe huna kiwango kwavile hukufundishwa na wataalam competent na wakutosha kwenye hospitali zenye vifaa vya kutosha na vya kisasa.Na ndiyo maana ukiletewa complex case pamoja na uMuhimbili wako,unakuwa huna tofauti na IMTU;Kwa vile wote mtai refer nje kwenye wataalam competent wenye vifaa vya kutosha na vya kisasa.

Kwahiyo hata kwa viwango vya kitanzania,huwezi kumcheka mtu wa IMTU kwavile hata yeye ana uwezo wa kutibu malaria kama wewe tu.Au labda useme wewe daktari wa Muhimbili unaweza kutibu ugonjwa gani ambao daktari wa IMTU hawezi kutibu?
 
Nakushangaa kuwaita IMTU hawana viwango wakati na mwenyewe wa Muhimbili huna viwango.Kama IMTU,nawe huna kiwango kwavile hukufundishwa na wataalam competent na wakutosha kwenye hospitali zenye vifaa vya kutosha na vya kisasa.Na ndiyo maana ukiletewa complex case pamoja na uMuhimbili wako,unakuwa huna tofauti na IMTU;Kwa vile wote mtai refer nje kwenye wataalam competent wenye vifaa vya kutosha na vya kisasa.

Kwahiyo hata kwa viwango vya kitanzania,huwezi kumcheka mtu wa IMTU kwavile hata yeye ana uwezo wa kutibu malaria kama wewe tu.Au labda useme wewe daktari wa Muhimbili unaweza kutibu ugonjwa gani ambao daktari wa IMTU hawezi kutibu?
Ukielewa maana halisi ya 'kutibu' ndio utaweza kuwatofautisha wa Muhimbili na wa kata!kutibu malaria sio sawa na kuprescribe ant-malarials
 
Ni kweli mimi ni mfuasi wa ligi tajwa,na sababu ya msingi ni moja tu...I believe in quality and not quantity.

Ni heri kuwa na vichwa mia moja kuliko vihiyo millioni moja.
Daktari mwenzangu naona umecharuka!!!
Je unajua ya kuwa kuna nchi zimepunguza mortality si kuzalisha highly qualified doctors lakini kwa ku train village health workers tu?
Je unajua ya kuwa mafanikio yote ya kudhibiti TB na leprosy ni chini ya DTLC na RTLC ambao majority ni mere AMOs?
Je unajua ya kuwa kuna kitu kinaitwa fursa,inaweza ukawa na pass nzuri lakini ukakosa fursa na ikiw afursa hiyo utaipatia Russia au Cuba bado unaweza kuwa daktari bora kuliko hao wa Muhimbili.
Nimefanya kazi na fourth and fifth year medical students kutoka nchi za magharibi lakini sikuona manufaa makubwa zaidi ya kuwa mbele katika ku interpret vitu kama ECG.
Retreat kidogo utafakari msimamo wako.
Jioni njema.
 
Alisomea east europe na aliporudi akakutana na sera hizo za kudharauliana lakini at the end the day akawa profesa mzuri kuliko hata hao wa kujisikia (nilisimuliwa na Daktari mmoja marehemu sasa).

nimekupata mkuu..hawa jamaa wenyewe ni wababaishaji halafu wanadharau wenzao
 
Ukielewa maana halisi ya 'kutibu' ndio utaweza kuwatofautisha wa Muhimbili na wa kata!kutibu malaria sio sawa na kuprescribe ant-malarials

nipe tofauti ya 'kutibu' malaria na magonjwa mengine kati ya muhitimu wa Muhimbili na wa IMTU.Kuna mtu ameandika hapa kuwa ana jamaa zake waliohitimu IMTU wapo muhimbili wanatibu;basi wasingeruhusiwa kutibu hapo kama hawakidhi viwango?

Mbona hatujawahi kusikia zile kesi zilizoshindikana Tanzania na kupelekwa South Africa au India,zinabakizwa Tanzania kwavile tuna madaktari wazuri waliosomea Muhimbili wana uwezo wakuzi manage kesi hizo?
 
Daktari mwenzangu naona umecharuka!!!
Je unajua ya kuwa kuna nchi zimepunguza mortality si kuzalisha highly qualified doctors lakini kwa ku train village health workers tu?
Je unajua ya kuwa mafanikio yote ya kudhibiti TB na leprosy ni chini ya DTLC na RTLC ambao majority ni mere AMOs?
Je unajua ya kuwa kuna kitu kinaitwa fursa,inaweza ukawa na pass nzuri lakini ukakosa fursa na ikiw afursa hiyo utaipatia Russia au Cuba bado unaweza kuwa daktari bora kuliko hao wa Muhimbili.
Nimefanya kazi na fourth and fifth year medical students kutoka nchi za magharibi lakini sikuona manufaa makubwa zaidi ya kuwa mbele katika ku interpret vitu kama ECG.
Retreat kidogo utafakari msimamo wako.
Jioni njema.

Mkuu ni kweli nimechafukwa kwani tunapoelekea ni kubaya !

I appreciate mchango wa wahudumu,manesi,clinicians na bila kusahau wahisani wa marekani et al katika sekta ya afya.

I personally have trained AMOs,COs Nurses and the like on TB,HIV,IMCI and the like,but the inflammatory fact is, they can never be an alternative to the real healthcare professionals.

Hapo tulikuwa tunazima moto tu kama mwalimu alipoanzisha kada ya AMO na leo hii tunahitaji MO !

Tusjidanganye kwa kurudia kosa,eti tufyatue MO wa kutosha hata kama hawana kiwango...ni kosa linalojirudia!

Tunahitaji MO na specialists wenye viwango for sustainability of the healthcare system.
 
Eti kufeli ni accelerator ya kufanya vizuri!
Kufeli ni kufeli tu hata ukibadilisha jina!
Kwa hiyo mmewaambia walimu wafelishe ili baadae watu wafaulu?

Yaani umefeli shule ya msingi,sekondari halafu leo umeibuka na PHD!
Hii iko Tanzania tu na ndio maana tunajionea vimbwanga!

UDOM na IMTU limekuwa kimbilio la wale walioshindwa na kuingia makazini kwa kada za clinical officers,AMO,n.k

ilitakiwa kuwe na program tofauti ya kuwaendeleza watu hawa na sio kuwapa elimu nzito ya udaktari kisa wanataka kupandishwa vyeo!

Hapa ni sawa na issue ya kila kijana kutaka kuimba bongo fleva hata kama ni bubu!

Conservatisim na desperation zinakutesa sana we jamaa.
 
Aliyeleta mada hii naye ni BOMU linalosubiri kulipuka, hoja yake ni 'fallacy of generalisation" kwani sioni mahusiano yaliyopo kati ya tukio hili la IMTU na UDOM, tuacheni kuongea vitu kishabiki, inawezekana ni kweli UDOM panaweza pakawa na changamoto zake kutokana na uchanga wa chuo hicho, lakini sidhani kama changamoto zile zinaweza zikawa ni sababu ya kutosha ya kuibeza serikali kwa kukianzisha! Kwani wanaofanya mambo sivyo wote walisoma UDOM? Hao madaktari waliopasua kichwa badala ya goti la mgonjwa nao walisoma UDOM ama IMTU? Hivi kwani SUA au UDSM nazo si zilianza zikiwa changa kama UDOM? Lakini pia vyuo hivi vikongwe navyo si vinamapungufu yake, ama vimekamilika kabisa na tunaweza kuvifananisha na OXFORD ama HARVAD? Na zaidi, mbona UDOM ilianzishwa na walimu wengi tu toka SUA, UDSM na kwingineko, au nao waliishiwa maarifa walipofika UDOM? Mkuu mleta mada acha mawazo mgando! Mbona tunashuhudia vijana wengi tu toka UDOM wakiwa na perfomance nzuri tu maofisini, na saa ingine wanawazidi wale waliosoma vyuo vikongwe? Aaaaargh......!
 
Eti kufeli ni accelerator ya kufanya vizuri!
Kufeli ni kufeli tu hata ukibadilisha jina!
Kwa hiyo mmewaambia walimu wafelishe ili baadae watu wafaulu?

Yaani umefeli shule ya msingi,sekondari halafu leo umeibuka na PHD!
Hii iko Tanzania tu na ndio maana tunajionea vimbwanga!

UDOM na IMTU limekuwa kimbilio la wale walioshindwa na kuingia makazini kwa kada za clinical officers,AMO,n.k

ilitakiwa kuwe na program tofauti ya kuwaendeleza watu hawa na sio kuwapa elimu nzito ya udaktari kisa wanataka kupandishwa vyeo!

Hapa ni sawa na issue ya kila kijana kutaka kuimba bongo fleva hata kama ni bubu!

Nilielewa kuwa u punguani na hauwezi kunielewa.

Kuna vigezo vinavyotumika kuwadahili na hivyo hujaviweka, kwa hiyo argument yako ni upuuzi mtupu unless utuoneshe kuwa kuna vigezo vya udahili vilikiukwa amma kwa makusudi, amma kwa bahati mbaya amma kwa wadahiliwa kughushi amma kwa wadahili kufumba macho kwa sababu yoyote ile. Bila hivyo, hiyo yako ni hoja muflis na kama ni mahakamani kesi imeshatupiliwa mbali zamani na gharama zote unalipa.
 
Tunaposema huu upuuzi wa vyuo vya kata hautakiwi watu wanasema tuna dharau bora jamii inajionea yenyewe.
Ati mtu alifeli kidato cha nne leo hii anapewa cheti cha kuwa daktari...ukiuliza nini eti ooh tunapunguza uhaba wa madaktari...pambaff sana.



MY TAKE


  • SERIKALI INATAFUTA KURA
  • G.ABACHORI ANASAKA NOTI
  • MLALAHOI ANASAKA AJIRA YA URAHISI
Hahaha duh salsa wewe hebu jenga hoja nzito ,tupe matukio yanayothibitisha kuwa IMTU in chuo kibovu(cha kata)
 
Back
Top Bottom