Bomu hatari duniani lipo Russia!!

Bomu hatari duniani lipo Russia!!

Nao tumewachoka kila siku mabomu watu wanakufa na Kansa na ukimwi wanakalia mabomu tu usenge huo kama kweli wanaume walete dawa ya Kansa na ukimwi tutaanza kuwapigia magoti siyo mabomu yann sasa walilipue jua basi tujue wao wanaume
 
SATAN-2 Made in Russia likionyeshwa live tarehe 27/10/2016,hili kombora ndio hatari zaidi kwa sasa duniani limetengenezwa kwa advanced technology ni inter-continental linafika popote duniani na kwa muda mfupi tuu kwa kasi ya ajabu,lina uzito wa tani zaidi ya 100,linabeba mabomu 10-15 ya atomic,kombora kama hili moja linaweza kuigeuza majivu nchi yote ya UFARANSA.Makombora kama haya 54 yanaweza kuiangamiza USA kabisa.

Pamoja na silaha nyingine kali za kivita ndio maana Rais wa Russia kwa kujiamini kabisa alisema hivi
"we have the best army in world"

lilishawahi kuigeuza majivu nchi gan kwa mfano?!
 
Hawa nao labda wasbr vita vya nuclear ndo watatisha, vita visivyo vya nuclear wakae pembeni..... Maneno mengiiii mwisho wa siku anakuja kukumutwa kama dogo tu. Atulie tu na sio kujisifu. Naendelea kushangazwa tangu kusikia Russia ina aircraft carrier moja tu in service.

We jamaa vipi? unaleta za utotoni za vua kwanza mabuti kabla ya kupigana? kwenye vita huwezi kumpangia mtu silaha ya kutumia na ndio maana US anamuogopa Mrusi kwenye kipengere hicho.
 
Labda huijui tuu ww2 ilivoenda. Russia alisha surrender na parts kubwa ya russia ya ulaya ilikuwa imetekwa.na walishaanza kujenga maandaki kuulinda mji wa moskow maana germans walikuwa wanakaribia.wajerumani walichokosea ni kudivert wanajeshi wengi kuiteka kiev na kingine kuwa na maadui wengi.wao wakiwa wachache.na kama lengo lao la vita lingekuwa kuiteka urusi.wangeiteka tuu.maana walikuwa na more advanced weapon

Hizo tamthilia umezihibua wapi!!! kwenye archives za CNN au VOA?
 
Yaani yote hii tunashangilia watu kuuana na kupoteza maisha hii nguvu ingewekezwa kuleta mbinu za kurefusha maisha..nawaza tu..
 
Jenerali mmoja wa kimarekani, nadhan ni General Miller alisema ni ujinga kuanza Kupigana na nchi ingine ambayo mnajua mna nguvu sawa nayo kijeshi. Nilimpendea hapo

Majenerali wenye akili nzuri kama Miller ndio wanafaa kuwa included kwenye safu ya Uongozi wa Trump.

Ukijaribu kufatilia CVs za Majenerali kama Miller utakuta ni wasomi wa fani ya Sayansi au Engineering, wanajua fika wakijitia kimbelembele na kujaribu kuishambulia Urusi kwa kushtukiza au kikawaida matokeo yake yanaweza kuwa balaa kubwa kwa nchi zote mbili bila kujali nani kaanzisha timbwili, lakini I can assure you Uncle SAM atapata a lion's share ya maangamizi.

Warusi awana utamaduni wa kuchokoza watu wala kijitapatapa lakini ukitishia Taifa lao uwezi kubaki salama i.e huo ndio unakuwa mwisho wa utawala au Taifa lako - awana mchezo,
mifano ya kuthibitisha ukweli huo hipo sana - someni historia ya Mataifa yote yaliyo wahi kuivamia Urusi yalishia wapi, kitu gani kinawafanya kuamini kwamba safari hii mambo yatakuwa tofauti - watu awajui tu.

Ukichunguza kwa umakini utabaini kwamba kundi ambalo ni very vocal na bellicose ni Majenerali mbumbumbu wasio kuwa na background yoyote kwenye masuala ya sayansi au Engineering watu kama hao si rahisi comprehend how devastating WMD can be - yapo yapo tu yanasukumwa/shinikizwa na owners wa Military Industry Complex, ma Bankers na maneocon ili yatafute sababu/visingizio vya kuanzisha WW3 au another arm race/cold war yakiwa na lengo la kupiga pesa ndefu - hayana habari kwamba WW3 ikitokea nayo hayana pa kukimbilia - wao na vizazi vyao watahangamia kwenye conflagration kama wengine.

Watu wabishi na wenye mawazo ya ajabu kama hayo wapo pia hapa JF - mtu anasema eti walijuaje kama kombola moja linaweza kuhangamiza Ufaransa nzima - yaani wanafikiri ma Nuclear Physicists wanashindwa kufanya mahesabu kujua nuclear war head moja yenye payload ya Megatonne kihasi fulani ina uwezo wa kuhangamiza square kilometer ngapi za aridhi/nchi?
 
Labda huijui tuu ww2 ilivoenda. Russia alisha surrender na parts kubwa ya russia ya ulaya ilikuwa imetekwa.na walishaanza kujenga maandaki kuulinda mji wa moskow maana germans walikuwa wanakaribia.wajerumani walichokosea ni kudivert wanajeshi wengi kuiteka kiev na kingine kuwa na maadui wengi.wao wakiwa wachache.na kama lengo lao la vita lingekuwa kuiteka urusi.wangeiteka tuu.maana walikuwa na more advanced weapon
WWII huijui kasome "Operation Barbarossa". Hitler ailikuwa na axis tatu zikiongozwa na Gen. Von Runsdet kaskazini, Gen. Von Gott at the Center na Gen. Paulus South. Na hawa walikuwa the most combat experienced commanders wa Hitler na hiyo ilikuwa 1942. Operation hii iliendelea hadi katika viunga vya Moscow. Lakini Marshall Zhukov ndiyo aliyeongoza successful counter attack na siyo "kosa" la wajerumani kudivert majeshi. Hicho ukachokisema wewe si sahihi kwa kuwa mission aliyopewa Gen. Paulus na Gen. Guderian (Tank forces) ilikuwa kwenda kuviteka visima vya mafuta ili kuinyima Urusi nishati hiyo ya kuyawezesha majeshi yake Kusonga mbele. Hata hivyo majeshi ya Urusi chini ya Gen. Vasily Chuikov ( 3rd Army) aliwasambaratisha wajerumani pale Stalingrad ( kati ya Askari 300,000 wa Germany ni 90,000 tu ndiyo waliachwa hai na kutekwa. Gen. Paulus aliomba msaada na ndiyo hicho unachokizungumza na baadaye Paulus aliomba kujisalimisha kwa warusi lakini Hitler alimkatalia na akampandisha na Cheo kuwa Field Marshal akitegemea kuwa Paulus atajinyonga (kama ilivyotakiwa na Hitler kwa kamanda mwenye cheo hicho) kuliko kukubali kutekwa na Warusi. Paulus hakutekeleza ombi hilo la Hitler akasurrender kwa Gen. Chuikov and General na baadaye Marshal Vasily Chuikov ndiye aliyeongoza 3rd Army na ndiye aliyeiteka Berlin. Hao Wamarekani wako waliingia hiyo vita 1944 na nia ilikuwa kumzuia mrusi asiiteke Berlin na siyo vita. Nakukumbusha kuwa Hitler aliingia Paris anapiga bendi.
 
Nimetaja wapi america hapo.kama ujeruman alikuwa ameelemewa ilikuwaje alifika hadi moscow? Na ni kwanini warus walianza kujenga maandaki ya kuukinga moskow?sikatai baadae kilichofuata ni ujeruman alianza kushambuliwa vikali na warus.lakin warus walisha shindwa wazuia.just imagine ile vita ingekuwa ni german dhid ya urusi pekee.kwamba hamna nchi zingine je urusi angeweza mtiti wa hitler.
 
We jamaa vipi? unaleta za utotoni za vua kwanza mabuti kabla ya kupigana? kwenye vita huwezi kumpangia mtu silaha ya kutumia na ndio maana US anamuogopa Mrusi kwenye kipengere hicho.
Kuna kitu kinaitwa No first Use, sijui unaelewa au ndo upro russia usokuwa na maana!!
 
SATAN-2 Made in Russia likionyeshwa live tarehe 27/10/2016,hili kombora ndio hatari zaidi kwa sasa duniani limetengenezwa kwa advanced technology ni inter-continental linafika popote duniani na kwa muda mfupi tuu kwa kasi ya ajabu,lina uzito wa tani zaidi ya 100,linabeba mabomu 10-15 ya atomic,kombora kama hili moja linaweza kuigeuza majivu nchi yote ya UFARANSA.Makombora kama haya 54 yanaweza kuiangamiza USA kabisa.

Pamoja na silaha nyingine kali za kivita ndio maana Rais wa Russia kwa kujiamini kabisa alisema hivi
"we have the best army in world"
Kuna siku,warussi watakula hayo mabomu.
 
Kuna kitu kinaitwa No first Use, sijui unaelewa au ndo upro russia usokuwa na maana!!

We jamaa unajifanyaga unajua sana, wakati mwingine logic ndogo tu inahitajika kuelewa mambo. Pamoja na NFU pledge/policy ipo lakini haina meno mkuu. Hadi sasa ni China na India pekee ndo walioipledge 100%. NATO wenyewe waliikataa., Russia alisema yeye atatumia iwapo kuna mtu atam-nuke au hata kama mtu atamuattack conventionally. Na hiyo ndio sababu nikasema huwezi kumuamulia mtu silaha ya kutumia.
No First Use policy ni butu.
 
We jamaa unajifanyaga unajua sana, wakati mwingine logic ndogo tu inahitajika kuelewa mambo. Pamoja na NFU pledge/policy ipo lakini haina meno mkuu. Hadi sasa ni China na India pekee ndo walioipledge 100%. NATO wenyewe waliikataa., Russia alisema yeye atatumia iwapo kuna mtu atam-nuke au hata kama mtu atamuattack conventionally. Na hiyo ndio sababu nikasema huwezi kumuamulia mtu silaha ya kutumia.
No First Use policy ni butu.
Kwani si ulisema huwezi kumpangia mtu weapon ya kutumia? All nations wana avoid nuke war because they know the consequences. Russia alisema yeye atatumia iwapo kuna mtu atam nuke, ndo pale pale No first use, Hao Nato wao wenyewe hawawezi kum nuke anyone at first. Wewe unasema butu but its in effect. Tumia hio hio Logic unayotaka nitumie. Tangu US adondoshe Nuclear nambie one war ambayo Nuclear weapon imetumika tena.
 
Back
Top Bottom