Bodi ya Kimataifa ya Ushauri kwa Bodi ya Wakurugenzi na Watendaji ya Barrick Corporation Group...

kwani wameanza kuongoza baada ya hili sakata au??

ushabiki tu usio na maana


wanakuja Tanzania sasa!
 
Vyovyote vile Mimi baada ya malipo ule usafiri( Noah) waliosema kila kijana angekuwa nao!
Kama najiona vile naenda kwa wakwe kuposa binti na Noah yangu
Hio noah, kuna mtu anajiita "le"nani sijui naskia anayo
 
Kafanye tena research yako mkuu Barrick haiwezi kuwa na utajili wa dola bil 27 pekee
Kaka hii ni kulingana Consolidated Balance Sheet ya Barrick ya mwaka unaishia 31 dec. 2016 kwa miradi yao yote duniani inaonyesha net asset ni dola bil. 25 hii naweza nikakutumia
Kama Manchester united ina thamani ya Dola Bil 6.2 wazungu wanatushangaa hii ni figure kubwa sana sana ndio wanatuibia lakn sio kwa tune hiyo
 
Wamo mawaziri wa wizara ya ulinzi wawili wa marekani,mawaziri kutoka Canada,uingereza,spain
View attachment 523912
WATASHUGHULIKIWA KWA MUJIBU WA KATIBA NA SHERIA ZA NCHI HII, HAO SI WAKUWATETEMEKEA KAMA MLIVYOZOEA. ZAMA HIZI SI ZA KUWATETEMEKA HAO WAZUNGU NA WATAJUA SASA WAAFRIKA TUNA AKILI ZETU BWANA, HAKUNA CHA MAWAZIRI WASTAAFU WALA WAZUNGU WASTAAFU WATAKIONA CHA MTEMAKUNI.
 
WATASHUGHULIKIWA KWA MUJIBU WA KATIBA NA SHERIA ZA NCHI HII, HAO SI WAKUWATETEMEKEA KAMA MLIVYOZOEA. ZAMA HIZI SI ZA KUWATETEMEKA HAO WAZUNGU NA WATAJUA SASA WAAFRIKA TUNA AKILI ZETU BWANA, HAKUNA CHA MAWAZIRI WASTAAFU WALA WAZUNGU WASTAAFU WATAKIONA CHA MTEMAKUNI.
Hao jamaa huwezi kuwasimamisha mahakama za bongo,wana mahakama zao ulaya na marekani

Mkuu wewe wa wapi? Ukara?
 
Wenzetu mnaogopa sana wazungu sijui au nini? so what kama kuna mawaziri au malaika humo ndani.. you have to have confidence in your abilities. Ukisimama na wazungu usitetemeke hata kama wana macho ya bluu na nywele za dhahabu; usija ukadhani ni malaika!
Wakija dawa yao wanaongea chongereza we unawapiga chishwahili full lugha gongana na makontena hayatoki!!
 
Wakuu habarini...

Kutokana na jinsi kampuni mama ya Acacia Mining Company ambao ni Barrick Gold Cooperation walivolichukulia suala hili kwa uzito hadi Chairman wa Barrick Gold kuja kuonana na raisi ili kumaliza hili suala. Barrick wangeweza kuleta mtu yeyote ku-initiate the talks lakini Bosi mwenyewe kuja hapa inaonesha kua wao wamelichukulia kwa uzito unaostahili hii issue.

Kwa jinsi hali ilivyo ni wazi kuwa Barrick Gold na Accacia Mining Co wataunda timu ya watu wenye ushawishi ili kumaliza hili suala na hatimaye wao wajisafishe katika soko la kibiashara za kimataifa.
Kwanza tuanze kuangalia Barrick Gold na Acacia inaundwa na watu wa aina gani na potential waliyonayo, hii itasaidia kuona na sisi pia kwa upande wetu tuwe na watu wa aina gani watakao kaa meza moja na hawa mabwana.

Barrick Gold Cooperation
Ukiachilia mbali bodi ya wakurugenzi wa Barrick Gold, kuna Bodi ya kimataifa ya washauri inayoundwa na watu 12 ambayo kazi yake ni kushauri bodi kuu ya wakurugenzi wa Barrick katika masuala ya kisiasa na mikakati mingine inayoathiri kampuni. Bodi hiyo inaundwa na baadhi ya mawaziri wakuu wawili(2) na mawaziri watatu(3) kutoka nchi kubwa zilizoendelea kiuchumi.

Bodi hiyo inaongozwa na Former Prime minister of Canada 1984-1993 (Brian Mulroney), kuna member wengine kama:
Former spanish prime minister 1996-2004 (Jose Maria Aznar),
Former speaker of the US house of representatives 1995-1999 (Newt Gingrich, ambaye alikua kwenye timu ya kampeni ya Donald Trump),
Former Canadian Minister for Foreign affairs 2011-2015 (John R Baird),
Former US secretary of defence 1997-2001 (William S Cohen),
Former German Federal Minister of defence 2009-2011 (Karl-Theodor Guttenberg),
Former foreign policy advisor to UK prime minister 1983-1990(Margaret Thatcher),
Currently Member of UK's house of Lords (Lord Powell). Pia bodi hiyo ina watu wengine ambao ni wabobezi kwenye uongozi biashara za kimataifa. Pia mwenyekiti wa Barrick aliyekuja kuonana na Rais nae ni member wa bodi.

Kwa haraka haraka kutokana na website ya Barrick watu wa bodi hiyo hapo juu ndio wahusika wanaoshughulika na mambo kama hayo yanayoikumba kampuni, hivyo sio watu wa mchezo mchezo tena pale ambapo maslahi yao yanapototetereka.

Acacia Mining Company
wao bodi yao inaundwa na watu nane akiwemo mtanzania mmoja (Balozi Juma Mwapachu), bodi inaongozwa na rais wa barrick, CEO wa kampuni na member wengine.

Kwa mantiki hiyo basi timu watanzania inabidi iwe iliyoshiba ili kukabiliana vizuri na timu pinzani kwenye meza ya mazungumzo. Hata timu ya upande wa acacia isipokua na hivyo vichwa hapo basi ni wazi kua wowote watakaounda timu hiyo watafanya kazi chini ya maelekezo ya hao watu. Hivyo tujipange maana kwa kweli mazungumzo hayatakua mepesi.
 
Hapa kuna shida kubwa sana inayogusa kila idara inayoguswa. Ukurukupukaji.

CCM ilikurupuka na kupeleka miswada ya madini kwa hati ya dharura, ninini kilikuwa nyuma ya pazia cha kuwataka wabunge wapitishe niyo miswada kwa lazima bila ahta kuwapa nafasi ya kuisoma na kuielewa na hata kutafuta ufafanuzi wa kitaalamu katika masuala yaliyokuwa nje ya uelewa wao kabla hawajakaa kuijadili na kuipitisha? Ukurupukaji huu ulikuwa ni bahati mbaya ama kusudi?????????

CCM siku zote imekuwa ikikurupuka kuwazuia wawakilishi vya vyama vya upinzani kutoa mawazo yao ambayo kwa msingi huwa ni ya utetezi wa Watanzania. Bila tafakri kuwatukana na kuwadhalilisha makusudi, halafu baadaye matatizo yanatokea, wanaanza kurudi kule kule na kulaumu upinzani eti kwa nini hawasemi wakati walisema zamani wakadhalilishwa!. Huu ukurupupu ni kwasababu ya ufahamu mdogo wa wana CCM TWAWEZA 2015 au ni kukosa uzalendo kwao?

Sasa hivi tunaona wimbi la kufukuzwa kwa wapinzani bungeni kwa maelekezo kwamba wafukuzwe ili washughulikiwe nje ya bunge, eti kwa sababu tu wanatoa mawazo yasiyotakiwa na CCM hata kama ni ya ujenzi wa nchi. Hii bado ni nia njema ya CCM na serikali yake kwa Watanzania au ni uimarishaji wa pango la wanyang'anyi dhidi ya Tanzania?

Huu ukurupukaji wa makinikia ambao sasa unalaizmishiwa kwamba mabadiliko yafanyike ili kodi ya madini iongezeke kwa 1%, ni kitu gani hiki ndiugu zangu??????

Juzi serikali imekaa na kiongozi wa Barrick kwenye mazungumzo ambayo kumbe ni premature, lakini muda huo huo tukaona ukurupukaji wa kueneza habari kwenye mitandao kwamba BARRICk wamekubali kulipa hayo matrillion, kitu ambacho kukmbe ni uwongo!. Hii ni nini lakini? Kuna uharaka gani wa kukimbila mitandaoni kueneza habari za upotoshaji halafu leo kumbe mechi ndiyo inaanza na inaonekane kuna sintofahmu kubwa baara ya hao hao waenye migodi "KUKANUSHA INSTANTLY KWAMBA TAARIFA ZA MAPATANO NA KWAMBA WAMEKUBALI KULIPA NI ZA UWONGO". Hii ni aibu ilioje?

Hivi hii tabia ya ukurupupu inalenga nini hasa? Kuwafanya Watanzan wapumbvue ili wakae kimya hata kama hakuna kitu wanaona kikibadilka? Ni namna ya kutafuta sifa kwa majitu majininga ili yashangilie na kuwasifu viongozi kwa jinsi isiyo sahihi? Ni nini haswa kinatafutwa?

Tabia za ukurpupu huu, zinaligharimu taifa kwa kiwango gani? Maisha mangapi y awananchi ayanapotea kama moto wa mishummaa kwa maamuzi haya yanayofanyika kwa ukurupupu?

KWA KWELI INAUMIZA NA KUSIKITISHA SANA. MUNGU WASIMAMIE WATANZANIA WANYONGE WANAOONEWA, WAJINGA WASIOJIELEWA UWAWEKE MBALI NA ATHALI ZA WATU WAPUMBAVUE!
 
CHADEMA mbona waoga mpo chini ya Uangalizi wa Magufuli acheni Uoga!
Tutarudi hapa baada ya muda (usiojulikana) kufanya tathmini ya huu uzi shujaa. Kwa sasa tuvumilie tu maoni ya mtoa hoja hawezi kueleweka sasa tukiwa kwenye lindi la "hamasa" na "matumaini" mapya.
 
Mleta uzi, weka source maana umeiba hiyo news kwenye print media moja ya Leo.


Ila kuhusu migodi lazima wakae chini Hakuna porojo mbele za JPM.

With JPM, from 2015 - 2025
 
IMG-20170616-WA0021.jpg
pia haya makampuni japo ni ya watu binafsi,lakini ni mawakala wa nchi husika zinazofaidika nayo,ikiwemo marekani,uingereza,Canada,hapa tunajaribu kuutingisha uchumi na siasa za nchi hizo tunakozunguka kuomba msaada usiku na mchana

Tujue na tujipange kwa full-scale economic war na hawa jamaa,na vita yao huwa hawajali hata kama itachukua miaka 50

Angalia Ghadafi kagombana na wazungu miaka tele zaidi ya 30,baadae wakaelewana akajua yameisha,kumbe wenzetu hawajui kusamehe wala kusahau!

Angalia Mugabe,sasa miaka zaidi ya 20 wana bifu nae,they never forgive and forget!

Mpaka leo NATO unahangaika kuizunguka Russia! Japo waliiangusha USSR

Mpaka leo watu hawa wana urafiki wa mashaka na China!!

Saddam Hussein walimpiga vita ya kwanza ya ghuba,wakashindwa kumtoa,wakarudi tena!!

Tujipange sana,na tujiangalie,mashirika makubwa kama haya hukopa benki ya dunia na IMF kupata mitaji ya kufungua migodi na wana sauti sana katika mashirika haya!

Tunapambana na mgodi mkubwa kwa utajiri duniani,Barrick Corporation
 
Back
Top Bottom