Bodi ya Ithibati yawataka waandishi wa habari kujisajili ili watambuliwe rasmi

Bodi ya Ithibati yawataka waandishi wa habari kujisajili ili watambuliwe rasmi

Just Pray

JF-Expert Member
Joined
Nov 7, 2023
Posts
2,142
Reaction score
4,779
Mwenyekiti wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Tido Mhando, ameongea na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam, akitangaza kuanzishwa kwa mfumo mpya wa kidigitali wa kupata Ithibati na Kitambulisho cha Uandishi wa Habari (Press Card).
Kupitia mfumo wa TAl-Habari, waandishi sasa wataweza kujisajili mtandaoni kwa urahisi zaidi .

Mambo muhimu anayopaswa kuwa nayo mwombaji ni pamoja na:
  • Picha ndogo (passport size)
  • Vyeti vya elimu
  • Kitambulisho cha Taifa (NIDA)
  • Barua ya utambulisho kutoka taasisi au kama ni freelancer
  • Ada ya Ithibati ya TZS 50,000

Baada ya kujisajili, mwombaji atapokea msimbo wa
SMS na barua pepe ili kuendelea na hatua za kujaza taarifa, kufanya malipo, na kuwasilisha ombi lake.
Kitambulisho hiki kinatumika sehemu yoyote ya shughuli za kihabari - ndani na nje ya taasisi.

Ni kwa mujibu wa Kanuni ya 17(a) ya Sheria ya Huduma za Habari, inayowalenga Wahariri, Watangazaji, Waandishi wa kujitegemea, Wapiga picha, Waandaaji wa vinindi, Wanafunzi wa uandishi, na hata Wa. V shi wa Habari wa kigeni.

 


Na Mwandishi Wetu, JAB.

Wakati Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) ikiufungua rasmi mfumo wa usajili wa Waandishi wa Habari wa https://taihabari.go.tz ili kuomba kuthibitishwa na kupatiwa Kitambulisho cha Uandishi wa Habari (Press Cards) Mwenyekiti wa Bodi hiyo Ndg. Tido Mhando amewaonya wenye nia ya kutumia vyeti visivyo halali wakati wa kujaza taarifa zao.

Mhando alitoa tahadhali hiyo tarehe 19 Mei, 2025 wakati akizungumza na Wahariri na Waandishi wa Habari wa vyombo mbalimbali vya Habari katika ofisi za Bodi hiyo zilizopo Mtaa wa Jamhuri jijini Dar es Salaam.



“Ndugu zangu Waandishi wa Habari, Bodi hii itaanza kutoa ithibati kwa waandishi wa habari wote kupitia mtandao na kutoa vitambulisho vya kidijiitali (digital Press Card). Maombi ya ithibati Press Cards yatafanyika kupitia Mfumo unaoitwa TAI-Habari”, alisema.

Mhando alisema mahitaji muhimu wakati wa kujaza taarifa katika mfumo huo kuwa ni pamoja na namba ya simu na barua pepe vinavyofanya kazi, picha ndogo (passport size) iliyoskaniwa barua ya utambulisho kutoka taasisi anayotoka au anakopeleka kazi zake ikiwa ni mwandishi wa kujitegemea (Freelancer), nakala ya Kitambulisho cha Taifa (NIDA) na ada ya ithibati shilingi Elfu Hamsini (50,000).




“Mahitaji mengine ni vyeti vya elimu vilivyoskaniwa kwa mfumo wa PDF na kuthibitishwa na Mamlaka husika (kama chuo kikuu vithibitishwe na TCU na kama ni vyuo vya kati vithibitishwe na NACTVET), na katika hili nisisitize tafadhali sana usiweke cheti ‘feki’ jambo hilo linakiuka siyo tu linakiuka maadili ya taaluma habari, bali pia ni makosa yanatakayodhibitiwa kwa mujibu wa Sheria za nchi,” alisema Mhando.

Mhando alisema mahitaji hayo ni muhimu ili kukamilisha mchakato wa maombi kwa mafanikio na kwamba ni hatua inayolenga kuboresha huduma, kuimarisha usimamizi wa taaluma ya Uandishi wa Habari na kurahisisha upatikanaji wa vitambulisho kwa waandishi waliothibitishwa.

Aliomba Wahariri, Waandishi na wadau wote wakiwemo waajiri kutambua umuhimu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari katika kuimarisha weledi, maadili, na uwajibikaji wa taaluma ya uandishi wa habari nchini, na hivyo watoe ushirikiano wa hali ya juu katika kukuza na kuendeleza taaluma hiyo muhimu kwa taifa.


Akijibu maswali ya waandishi wa Habari kuhusu watu walio kwenye tasnia bila kuwa na vyeti vya Elimu ya Uandishi wa Habari, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi hiyo Wakili Patrick Kipangula alisema Sheria ilitoa muda wa miaka mitano kwa watu waliokuwa hawana sifa ili wakasome na kutimiza vigezo vya kisheria.

Alisema baada ya muda huo kuisha Waziri aliongeza muda wa mwaka mmoja na kwamba tangu Waziri aongeze mwaka mmoja ni miaka miwili imeshapita na kufanya jumla ya miaka nane na hivyo hakutakuwa na muda wa nyongeza tena.
 
Hii si taaluma ya kuundiwa bodi. Hapa wamechemka pakubwa. Hii taaluma ni kubwa na pana na inakua kwa kasi ya ajabu ni ngumu kuiundia ithibati. Sijui ni nani kaingiza siasa kwenye taaluma hii!
 
Hii si taaluma ya kuundiwa bodi. Hapa wamechemka pakubwa. Hii taaluma ni kubwa na pana na inakua kwa kasi ya ajabu ni ngumu kuiundia ithibati. Sijui ni nani kaingiza siasa kwenye taaluma hii!
Taaluma ikiwa kubwa na pana si ndiyo inahitaji uthibiti mkuu? au unataka iendelee kuwa holela? Unafurahi kuona wachekeshaji nao wanafanya kazi za habari bila kujua misingi na maadili yale?
 
Taaluma ikiwa kubwa na pana si ndiyo inahitaji uthibiti mkuu? au unataka iendelee kuwa holela? Unafurahi kuona wachekeshaji nao wanafanya kazi za habari bila kujua misingi na maadili yale?
hapana
 
Back
Top Bottom