Waufukweni
JF-Expert Member
- May 16, 2024
- 4,438
- 14,672
Shirikisho la Vyama vya Madereva Bodaboda na Bajaji na Uongozi wa Machinga mkoa wa Dar es Salaam, wameahidi kutofanya kazi siku ya Disemba 9, 2025, kwa madai kuhofia kuingizwa kwenye mkumbo wa watu wanaofanya vurugu, kufuatia tetesi za kuwepo kwa maandamano yanayohamasishwa mitandaoni.
Viongozi wa Shirikisho hilo na wa Machinga mkoa wa Dar es Salaam, Said Kagomba na Namoto Yusuph wakitoa salamu zao katika Kongamano la kupongeza Hotuba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan, aliyoitoa wakati wa ufunguzi wa Bunge la 13 jijini Dodoma, wameweka wazi msimamo wao kuelekea siku ya Disemba 9, 2025.
Kauli hiyo imeungwa mkono na Mkuu wa wilaya ya Ilala na mwenyekiti wa kamati ya usalama ya wilaya hiyo Edward Mpogolo, aliyeahidi kulifikisha katika vikao husika, huku Kamanda wa Polisi mkoa wa Kipolisi Ilala Kamishna wa Polisi Yustino Mgonja, akieleza mikakati ya jeshi hilo katika kuwalinda raia na mali zao.
Viongozi wa Shirikisho hilo na wa Machinga mkoa wa Dar es Salaam, Said Kagomba na Namoto Yusuph wakitoa salamu zao katika Kongamano la kupongeza Hotuba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan, aliyoitoa wakati wa ufunguzi wa Bunge la 13 jijini Dodoma, wameweka wazi msimamo wao kuelekea siku ya Disemba 9, 2025.
Kauli hiyo imeungwa mkono na Mkuu wa wilaya ya Ilala na mwenyekiti wa kamati ya usalama ya wilaya hiyo Edward Mpogolo, aliyeahidi kulifikisha katika vikao husika, huku Kamanda wa Polisi mkoa wa Kipolisi Ilala Kamishna wa Polisi Yustino Mgonja, akieleza mikakati ya jeshi hilo katika kuwalinda raia na mali zao.