Bodaboda hawana Haki

Bodaboda hizi na sasa hivi naona bajaj zinachukua kasi
Hawa nao ni wale wale. Ukibahatika pita njia kama Moroko nwenge au daraja la Tanzanite unakuta kushoto bajaj kulia bajaj wote mwendo mmoja hawakupishi . Wanaboa sana kama vile njia ni yao tu. Au pita mtaa wa samora vile vinavyotoka feri mpaka stesheni ni kero tupu.
 
Hayo uliyoandika ni sahii kabisa ila in advanced level.
Ajali nyingi za bodaboda huwa ni issue ya common sense kabisa na wala siyo elimu ya kufundishwa.
 
Kiukweli nachukizwa sana na wengi wa mabodaboda wabavyo behave

Huwa tunawasubiri hadi kwenye zebra wanakupigia honi, in short kwenye barabarani huwa sina tahadhari sana na magari kama ambavyo huwa nachukua kwenye hawa watu boda boda

Nimeshuhudia wakimgonga bimdada mmoja zebra, can you imagine mtu anagongwa zebra, afu wenzake wanamtetea eti bi Dada alivuka kwa mapozi sana, hivi zebra mtu anaweza tumia zaidi ya sekunde 30 kuvuka?? Sasa una haraka gani hiyo hadi ya 30s kuwa barrier kwako

Wajirekebishe
 
Bodaboda huwa hawajali sheria za barabarani unakuta taa hazijaruhusu wao wanapita tu tena bila tahadhari yoyote. Mara nyingi wanagongwa na mwendokasi pale mataa ya Shekilango.
 
Boda boda wa DSM ndo kundi la wajinga zaidi bro , matrafiki wanatakiwa wawekeze nguvu Zaid Kwa hawa watu, usidhubutu kupanda boda katika any busiest road Dar es salaam
 
Boda ni janga la Taifa hawasimami kwenye taa nyekundu sijui uwa wanawahi wapi?
 
Mkuu
Ukiwa unapanda haya mabus ya mwendokasi kila siku, na ukawa unakaa pale mbele kabisa na dereva, utakubaliana na mimi kabisa kuwa bodaboda ni wapumbavu.

Na mbaya zaidi huwa wanajiaminisha kwamba hawezi kupatwa na hatari..
Gari ishatoka kasi, anaenda kujichomeka anavyopenda.

Mwendokasi huwa wanajitahidi mno kuwakwepa,
Muda mwingine hadi hupelekea gari lililobeba mamia ya watu kuyumba, kwa sababu ya mtu Moja aliyeamua kujitoa ufahamu na kukatiza bila mpangilio.


Kama mna ndugu zenu bodaboda na mnawapenda, tafadhali washaurini washikilie akili zao, badala ya kuziweka mfukoni.


Mwendokasi ina mapungufu mengi mno ila siyo kwa upande wa uendeshaji wa madereva .
Madereva wake wapo makini sana..
Laiti wangekuwa rafu kama wa daladala, ama wangekuwa na akili kama za bodaboda
Akiyanani kungekuwa na mamia ya misiba kila siku.
Sent from my TECNO CG6 using JamiiForums mobile app
 
Kuna siku dereva alikwepa bodaboda aliyejipachika
Gari iliyumba mno.

Siku nyingine tena hii ni last month..
Niligonga kichwa kwenye kiti cha mbele..
Hapo waliosimama sijui walikuwa na hali gani, kama siyo kuangukiana hovyo.
Yote Kwa sababu ya mtu aliyeamua kukatisha ghafla mahala ambapo taa hazijamruhusu.

Madereva wa mwendokasi ni wavumilivu mno,
Bodaboda wanatia hasira mno.

Sent from my TECNO CG6 using JamiiForums mobile app
 
Namnukuu Godbless Lema..

"Boda boda ni Laana"

Na mimi naongezea kwamba, Uafrika hasa utanzania ni laana.

Kwa nchi zilizo endelea, First world countries, Bodaboda ni uchafu mjini.

Na si bodaboda tu, hata Bajaji ni takataka.

Zinachafua miji.
 
Sio DIT kabisa ni nyuma kidogo pale kwenye mataa ambapo kuna barabara ya kwenda Lumumba kama sijakosea.. Muda mwingine madereva wa mwendokasi wanadharau mataa.
Pale Zanzibar reassurance bodaboda hujikatizia tu wanavyotaka bila hata mataa kuwaruhusu.


Hao mwendokasi unasema hawafuati mataa si kweli.
Na kama wapo, basi ni asilimia 0.5

Bodaboda asilimia 99 ni vichaa huko Morogoro road.


Sent from my TECNO CG6 using JamiiForums mobile app
 
Hii ajari nimeishuhudia live. Tukiwa tumesimama kusubiria kwasababu taa zilikuwa zimeruhusu Mwendokasi zipite, boda boda yule akaona anachelewa, akaangalia upande mmoja akaona kweupe akataka kukatisha kuingia Lumbumba hamadi Mwendokasi hii hapa. Mengine ni history. Ni uzembe wa bodaboda kwa asilimia zote
 
Namnukuu Godbless Lema..

"Boda boda ni Laana"

Na mimi naongezea kwamba, Uafrika hasa utanzania ni laana.

Kwa nchi zilizo endelea, First world countries, Bodaboda ni uchafu mjini.

Na si bodaboda tu, hata Bajaji ni takataka.

Zinachafua miji.
Ningepewa nafasi ya kuishauri serikali
Ningeishauri bodaboda na Bajaj vitolewe kabisa main road hasa hii Morogoro Road.

Yaani boda ni vichaa namba Moja kwenye hii barabara.


Kijijini kwao wanajua mtoto anapambana
Yeye anakuja kujikatizia tu kwenye mataa anavyotaka.

Bodaboda asilimia kubwa hawajitambui.
Serikali iingilie kati iwaokoe hawa watu Kwa kuwapiga marufuku hizi barabara kubwa..
Waendeshe ndanindani tu.
Vinginevyo wataendelea kulimwa vichwa na kusababishia watu wengine majanga Kwa upumbavu wao wa kutotii Sheria.

Sent from my TECNO CG6 using JamiiForums mobile app
 
Kwahyo boda boda wana haki ya kupita kwenye barabara za mabasi yaendayo kasi? Angalia ajali nyingi za boda lazima kuna tatizo mtu wa gari hawezi kuchomeka gari au kupenya kwenye foleni
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…