BodaBoda date-out or delivery?

BodaBoda date-out or delivery?

realMamy

JF-Expert Member
Joined
Apr 28, 2024
Posts
7,304
Reaction score
18,229
Nimekutana na utani mwingi huko Tiktok unaosema kuwa

“Unatoka out na mpenzi wako afu mnapanda bodaboda? Sasa io ni out au delivery mwanetu????" 😂
1000142817.jpg


Kwa mimi ninavyoelewa Boda boda au Pikipiki ni usafiri wa abiria wenye gharama nafuu kama 3k-5k.

Na wengine hutumia usafiri huo kwenda nao kazini na katika shughuli nyinginezo.

Usafiri huu wakati mwingine una kadhia nyingi mfano mnaweza kuloa na mvua, vumbi, na kuchomwa na jua. Hakuna AC, hakuna privacy.

Mnafikia destination mkiwa na macho mekundu na nywele zimeharibika. Sio gari, sio Uber, ni usafiri wa mwananchi wa kawaida kabisa.

Sasa hapa ndipo ugomvi unapoanzia:

Timu ya "Hii ni Delivery tu"

Wanasema out ina hadhi yake. Inatakiwa iwe na mipango, gari, restaurant, na kumpa mwanamke wako “privacy”.

Wanasema kutoka out na boda ni sawa na ku-order food, si date.


Timu ya "Out ni nia, sio gari”
Wanasema Upendo unapimwa na muda na malengo, sio na gari wala tax.Kuna watu walioanza na boda boda leo wana nyumba na magari.

Wanaongeza kuwa kama mnaelewana kweli hata usafiri waboda boda utakuwa kumbukumbu tamu. Kumpa mtu shida ya gharama kila mara ndio kunaua uhusiano.

Swali
1. Vigezo vya "Out" kwako ni nini?

2. Kama mpenzi anakualika "twende out" kwa usafiri wa boda boda utaenda au utagoma?

3. Wanaume unaweza kumchukua malkia wako kwa kutumia usafiri wa boda boda bila kujisikia vibaya?
1000142815.jpg
 
Nimekutana na utani mwingi huko Tiktok unaosema kuwa

“Unatoka out na mpenzi wako afu mnapanda bodaboda? Sasa io ni out au delivery mwanetu????" 😂
View attachment 3642089

Kwa mimi ninavyoelewa Boda boda au Pikipiki ni usafiri wa abiria wenye gharama nafuu kama 3k-5k.

Na wengine hutumia usafiri huo kwenda nao kazini na katika shughuli nyinginezo.

Usafiri huu wakati mwingine una kadhia nyingi mfano mnaweza kuloa na mvua, vumbi, na kuchomwa na jua. Hakuna AC, hakuna privacy.

Mnafikia destination mkiwa na macho mekundu na nywele zimeharibika. Sio gari, sio Uber, ni usafiri wa mwananchi wa kawaida kabisa.

Sasa hapa ndipo ugomvi unapoanzia:

Timu ya "Hii ni Delivery tu"

Wanasema out ina hadhi yake. Inatakiwa iwe na mipango, gari, restaurant, na kumpa mwanamke wako “privacy”.

Wanasema kutoka out na boda ni sawa na ku-order food, si date.


Timu ya "Out ni nia, sio gari”
Wanasema Upendo unapimwa na muda na malengo, sio na gari wala tax.Kuna watu walioanza na boda boda leo wana nyumba na magari.

Wanaongeza kuwa kama mnaelewana kweli hata usafiri waboda boda utakuwa kumbukumbu tamu. Kumpa mtu shida ya gharama kila mara ndio kunaua uhusiano.

Swali
1. Vigezo vya "Out" kwako ni nini?

2. Kama mpenzi anakualika "twende out" kwa usafiri wa boda boda utaenda au utagoma?

3. Wanaume unaweza kumchukua malkia wako kwa kutumia usafiri wa boda boda bila kujisikia vibaya?View attachment 3642087
Achana na date.

Mimi hata kwa usafiri wa kawaida tu sijawahi na nafikiri sitapanda bodaboda.

Bora hata Bajaji.
 
Achana na date.

Mimi hata kwa usafiri wa kawaida tu sijawahi na nafikiri sitapanda bodaboda.

Bora hata Bajaji.
Dala dala boda boda miyeyusho kichizi

Mara elfu ya boda+ kuliko dala dala

Unatokea home umependeza unashuka ukiwa una nuka jasho nguo yote uliyoipiga pasi inakuwa imekunjana kunjana kama imetapikwa
 
Dala dala boda boda miyeyusho kichizi

Mara elfu ya boda+ kuliko dala dala

Unatokea home umependeza unashuka ukiwa una nuka jasho nguo yote uliyoipiga pasi inakuwa imekunjana kunjana kama imetapikwa
Bodaboda zinaua sana.

Bora hata daladala kunuka jasho kwa Mtanzania si jambo la ajabu.
 
Tunazipanda na hamtuambii kitu, kila mtu kwa urefu wa kamba yake, wa boda apande, wa bajaj nae na mwenye uwezo wa kiyoyozi nae apande, muhimu tumetoka date, tumekula tukashiba halafu tukaenda kula...

Wa kiyoyozi nae kala halafu akaenda kula...ngoma droo!
 
Bodaboda zinaua sana.

Bora hata daladala kunuka jasho kwa Mtanzania si jambo la ajabu.
Kwa suala la usalama boda boda hapana Kwa kweli , Bora hata upate ajali then ufe unaweza kupata ajali kufa haufi ukaishia kukatwa mguu au ukapatwa na stroke ya kudumu ukaishia kuishi kwenye mateso mazito maisha Yako yote

Eti Kuna jasho Kwa watanzania 😆😆🙌
 
Back
Top Bottom