Smart911
Platinum Member
- Jan 3, 2014
- 175,289
- 193,279
BLOOD DEAL
Author: Teddy
Cont:0655 202 285.
Whatsapp :0756 202 284
KWA MWENYE UHITAJI WA RIWAYA HII, AWASILIANE NA MWANDISHI KWA NAMBA HIZO JUU.
SEHEMU YA 29
“okay , rudi nyuma ukate mkono wa kushoto , chumba cha kwanza “
“ahsante “,
alijihisi ushindi wa hali ya juu , alichokifanya ni kuingia uwani ,alibadili nguo kwa haraka sana , kisha alitoka kwa tahadhali sana , alinyosha moja kwa moja hadi mbele ya ofisi hiyo, akiwa na bastola pamoja na kisu ,kilichokuwa kiunoni , hakutaka kupoteza muda alifungua mlango, na kuingia ,macho yake yalipokelewa na zaidi ya watu wawili , waliokuwa wanazozana .
*****
Poul hakutaka kukubaliana na maneno ya MacDonald , aliona hafanyiwi haki , kwa jinsi alivyokuwa amewaka kwa hasira ilikuwa ni ngumu sana kumuelewesha ,
“ nyie mbona mnazozana ndani ya ofisi za watu ?,
Mtu aliyekuwa amesimama na bastola aliongea kwa lugha ya Kiswahili, akiwa anamtazama mmoja baada ya mwingine
“Poul nisa..mehe mwa..nangu …ni..nisam..ehe ta…”
“ funga kopo lako haraka , sihitaji ngojera zako hapa “,
mtu yule aliongea huku alivua kitambaa alichokuwa amejifunika usoni , lahaulla ! Alikuwa Ghati , alinyosha mkono wake sawasawa na uso wa David , mkono uliokuwa umeshikilia bastola , tayari kwa kumuua ,
“ sina muda wa kupoteza , rest in peace {pumzika kwa amani }paaaa!”
Maneno hayo aliyasindikiza kwa risasi , lakini risasi hiyo ilipiga talakilishi , mara baada ya mkono huo kupigwa teke na Omar ,
“ uyataka faya nini? This is our person , who send you?{ Huyu ni mtu wetu , nani kakutuma ?}, aliuliza Omar kwa Kiswahili kibovu , akiwa amemkamata vyema Ghati ,
“ hutakiwi kujua , ila tabua , mtu huyu hatakiwi kuishi , natekeleza agizo kutoka kwa boss “
“ boss! Who is your boss?[boss! Nani boss wako] ?”,
Poul naye aliyaingilia mazungumzo hayo , muda wote huo David alikuwa kimya ,kabisa ,moyoni aliomba miujiza itokee , ila kwa dalili zilizokuwepo mbele yake , ilikuwa ni ngumu sana kutokea hilo , mwili wote ulitweta kwa jasho , hakuwa akisikia hata maumivu ya kuchanwa kiganja chake , japo damu zilikuwa zikiendelea kutoka ,
“ binti usipousema ukweli utakufa “,
MacDonald aliongea huku akimuachia Poul na kumsogelea Ghati , alimkaba shingo yake kwa mkono wa kushoto , akiwa ameyatoa macho , mdomo wa bastola ukiwa usoni kwa Ghati,
“ semaaa”
“ sawa niachie “,
japo alikuwa amekabwa kwa nguvu lakini , hakudiriki kutetemeka , ilibidi asimulie nusu ya kisa , Poul kusikia jina la Vero , alijikuta akitoa chozi, picha na kumbukumbu zote zilirejea, alimkumbuka msichana huyo aliyekuwa akimlea vizuri , akimpeleka shule na kumfuata , akimchekesha pindi alipokwazika ,kila kitu kilirejea ndani ya akili yake .
“ Baba muachie , ni mtu mzuri sana “
“ kweli ?’
“ Ndiyo “
Ghati alipoachiwa alimfuata David , alimpiga ngumi ya kifua hali iliyopelekea kuinama kidogo , kwa jinsi alivyokuwa amenywea hata hakupata wazo la kuchukua bastola yake , alikuwa mdogo mithili ya pilitoni , kitu alichokuwa akikiwaza ni miujiza tu , alitamani kupiga kelele lakini hakuweza,
“ anatakiwa apelekwe sehemu nzuri kwa mahojiano zaidi “,
Ghati aliongea , huku akiwatazama wenzake , mawazo hayo yalionekana kufaa sana , ilibidi wampe somo la kujikaza pindi atakapotoka nje , na kama angeleta usumbufu kifo kilikuwa halali yake , hakuwa na ubishi alijikaza na kuanza kuongoza njia mbele akitanguliwa na Omar pamoja na Ghati aliyekuwa bado na mavazi yake yale yale mekundu , hakujali kama angeweza kushitukiwa , kisha alifuta Poul na nyuma kabisa alikuwa MacDonald ,
“ Linda nakuja “
“ sawa boss “,
msichana wa mapokezi alijibu huku akiwa amemkazia macho boss wake huyo , hakujua kipi kilikuwa kinaendelea , hadi wanatoka nje ya jengo hilo hakuna mtu aliye fahamu , japo walinzi toka shirika la Kk security walikuwa eneo hilo ,lakini hawakufahamu nini kilikuwa kikiendelea .
Baada ya kumuingiza ndani ya gari lake aina ya Prando hapo ndipo walipomfunga uso kwa kitambaa cheusi safari ya kuelekea Geita ndani ya pori la matete ilianza , Omar ndiye alikuwa dereva , aliendesha gari hadi kigongo feri ,kwa muongozo wa Ghati pamoja na Poul , akipitia barabara ya Shinyanga , walifuata utaratibu wote hapo kivukoni kisha waliendelea na safari yao .
Majira ya saa kumi jioni walikuwa ndani ya pori hilo ,walimshusha na kuanza kumvuta kuingia ndani zaidi ,
“unachotakiwa ni kuongea ukweli , ukifanya hivyo utakuwa umejiwekea uwezekano wa wewe kuendelea kuishi “,
Poul aliongea huku akimchanja chanja na ncha ya kisu chake , mgongoni, chanja chanja hiyo ilipelekea shati lake uchanika chanika , japo alikuwa akimuomba msamaha ,lakini Poul hakuwa na roho ya kutoa msamaha huo ,
“ mpe hii karatasi aandike sababu ya kuua”,
MacDonald aliongea huku akitoa kipande cha karatasi na kumpatia Poul ,naye alikifikisha moja kwa moja kwa David ,
“ andika ukweli wote , ukipindisha , kifo halali yako, pia orodhesha mali zote na unirithishe mimi “
“zote !”
“ Ndiyo ?”
“ Ha..ha..hapana mwanagu ,mie nitaishije lakini ?”
“ kwani mali zako? , Jasho la baba yangu ,ama hufahamu hilo paaaa!”
Aliongea kwa hasira , kitendo cha David kukataa kumrithisha mali ,kilimkera sana , ilibidi ampinge makofi ya usoni ili kumuweka sawa , makofi hayo hayakubadili nia ya David aliendelea kukataa tu ! Hapo ndipo msichana Ghati alipopandwa na hasira alimsukuma Poul na kumsogerea David ,
“ Omar nipatie huo mkasi , anaona tunacheka .“
Baada ya kupewa alianza kumbana kila sehemu ya mwili , muda mwingine alidriki kutoka na kiasi kidogo cha nyama , japo aliumia na kutoa machozi lakini msimamo ulikiuwa ule ule , mali hakutaka kuachia ,
“ sasa nakufanyia kitu mbaya , nakuoa meno bila ganzi “,
MacDonald aliongea kwa kichina , lugha ambayo ilikuwa ngeni kwa David na Ghati pekee yao , alimtoa Ghati na kumpiga ngumi moja tu iliyopelekea meno yake mawili ya mbele kutoka , yakiacha damu zikichuruzika ,
“ bado unagoma ?’
“ Naaaandikaaaa”,
aliongea kwa maumivu makali sana, ilibidi akubali , hali aliyokuwa nayo ilimtisha , tayari alishatambua nia ya watu hao , kukataa kwake kungepelekea hata kifo .
*****
“ Huu ndi…o.. ukw…eliiiiii, na..kuomba…usiniue …mwana..ngu”,
alizungumza kwa taabu sana ,kutokana na maumivu makali aliyokuwa akiyasikia , Poul alishindwa kuvumilia pindi alipoyasoma maamdishi hayo ,ilikuwa kama katoneshwa donda alilia sana ,
“ ahsante , kwa ukweli wako ila tambua sitakuacha hai “
“ ha.pa..na .. nisa..mehe ..nai..acha ..fami..lia…yang..na..nani?”
“ Hahahaha! Ulipowaua wazazi wangu ulitegemea nitaishi na nani ?, Unastahili kufa, nitawasaidia mie “,
Poul hakutaka tena kuongea alianza kumchana chana kila sehemu ya mwili , jinsi alivyokuwa amevimba kwa hasira na uchungu ilikuwa ngumu mtu yeyote kumkataza , hakuishia kumchana chana tu, alianza kumkata kidole kimoja baada ya kingine , David alilia kama mtoto mdogo , maumivu aliyokuwa akiyasikia aliyafahamu mwenye ,
“ hadi unakufa nakukata kiungo kimoja baada ya kingine , jinsi unavyoumia na kuhangahika kwa maumivu makali na machungu tambua hata wao walihangaika vivyo , waliumia vivyo “ ,
aliongea huku akihamia vidole vya miguuni nako alikata kimoja baada ya kingine kwa kutumia kisu chake , muda wote huo wenzake walikuwa kimya wakikitazama kitendo hicho , hakuna aliyeweza kumuonea huruma David ,
“ sasa zamu ya kukata masikio , pua na mdomo “
“ boraaa un..iue..tu ..kuliko ..ku.ni..fa..ny..ia..hiviiiiiiiiiiiii”
“ hahahah !” Poul alicheka kwa dharau iliyochanganyikana na hasira , hakujali maneno yake alimkata sikio la kushoto na kuliweka pembeni , na la kushoto alifanya vivyo hivyo , alihakikisha kila kiungo amekitoa katika mwili huo ,
“ hebu mmalizie tuondoke “
“ sawa “ ,
papo hapo alimchoma kisu cha tumboni kama mara tatu , akichoma na kuchomoa , hakuna kilichosika zaidi ya kilio cha maumivu kisha David alipoteza maisha papo hapo ,
“ tunamzika ?”
“ Hana haja ya kuzikwa , baba yangu alilala barabarani usiku mzima akiwa amekufa , atakuwa chakula cha fisi , tuondokeni “.
Poul alihisi kutua kitu flani kizito ndani ya mwili wake , alijihisi mwepesi kabisa , kitu kilichokuwepo mbele yake ni kufikisha ujumbe huo kwa babu na bibi yake ambao sasa walikuwa wakiishi katika nyumba ya wazazi wake hapo Bugando . Walisafiri hadi mwanza jioni hiyo hiyo , majira ya saa nne usiku walikuwa kivuko cha kigongo feri , walisubili kwa muda wa dakika kumi na tano , ndipo feri hiyo ilifika , waliingiza gari lao ambalo lilikuwa la marehemu David , na baada ya dakika kumi na tano walikuwa upande wa pili , dakika arobaini na tano tayari walikuwa ndani ya jiji la mwanza ,
“ sasa mie nasepa “
“ wapi tena ?”
“ Kitwima hoteli , kesho asubuhi ya saa kumi na moja naingia Tarime “
“ hapana dada Ghati , naomba kesho twende sote nyumbani kwetu aghalau ukawaone wazee wangu ,nadhani watafurahi sana kukuona , na utanisaidia kuwaelewesha “
“ nini haraka , ila kwa kuwa umeongea wewe nitakuwa bega kwa bega nawe “ ,
yalikuwa maongezi kati Vero na Poul wakiwa nje ya mwanza hoteli usiku huo .Vero aliagana nao kisha akaondoka , kwa miadi ya kukutana siku ilifuata .
****
Hatimae David kauliwa na Poul (Mototo wa kaka yake)...
Ila nahisi Poul hatoishi kwa raha, misukosuko lazima itamuandama... Kuua siyo jambo dogo...
Cc: mahondaw