BLOOD DEAL
Author: Teddy
Cont:0655 202 285.
Whatsapp :0756 202 284
KWA MWENYE UHITAJI WA RIWAYA HII, AWASILIANE NA MWANDISHI KWA NAMBA HIZO JUU.
SEHEMU YA 10.
Dk. Eddyson alikata simu na kubaki amesimama, moyo wake ulijaa furaha, hakuamini kama zoezi hilo lingekamilika salama, hakutaka tena kukaa neno hilo ,alianza kujiandaa kuelekea kwake, moyoni akiwa na amani sasa. Usiku mzima ulikuwa wa furuha kupita maelezo, hadi kunapambazukua alikuwa na tabasamu tu, hali hiyo ilimshangaza hata mke wake, lakini hakuweza kumuuliza .
Safari ya kwanza, asubuhi hiyo ilikuwa ni kuelekea Nyakato national majanini, huko alikutana na David, aliekuwa amemsubili muda mrefu.
"Nakupa nyumba hii, ila hati sitakupatia leo, utazipata baada ya kifo cha Janiphar, hapo ndipo nitakapoamini, na kuanzia muda huu, umeshakuwa rafiki kwangu na ndani ya Blood deal, hutakiwi kukataa kufanya chochote, ukienda nje ya utaratibu, kichwa chako kitakuwa chakula cha hii "
David alizungumza huku, akitoa bastola ndani ya suruali yake, wote wakiwa ndani ya gari lake, alianza kuipangusa pangusa, akiwa ameitumbulia macho, upande wa Dk. Eddyson, hali haikuwa nzuri, kulikuwa na nafsi iliyoanza kumbeza na kumsunta, muda mwingine alijuta kukutana na David, kukubali kufanya kazi yake, alidhani mambo yatakuwa rahisi sana! Masikini Dk Eddyson alianza kutetemeka, bila mwenyewe kutegemea.
"Sasa unatetemeka nini? Mbona unakuwa kama mwanamke! Daima mwanaume huishi popote, hufanya lolote, na tambua mwanajeshi hachagui adui wa kumshambulia hata mtoto mdogo anaweza kushambuliwa akiwa upande wa adui, wewe mwanaume kaza mjomba " alizungumza maneno hayo David akiwa anakipiga piga kifua cha Dk Eddyson, kilichokuwa kidogo na cha kawaida sana .
"Lakini makubaliano yetu hayakuwa hivyo? "Alizungumza kwa unyonge, muda mwingine alitamani kuitoa damu yenye maambukizi ya virusi vya Ukimwi ndani ya mwili wa Janiphar, lakini haikuwezeka, tayari maji yalikuwa yamemwangika ndani ya bahari, na ni ngumu sana kuyachota yaleyale, lazima utoke na mengine, majuto ambaye ni mjukuu tayari ,alikuwa rafiki yake kuanzia dakika hiyo.
"hahaha Dk Eddyson!! Hahahaha! Unanifurahisha kweli baadala ufu....."
David alicheka kwa furaha, huku akiongea, aliyakata maneno yake, baada ya kuchukua mzinga wa konyangi, aliutikisa tikisa kama dakika moja, huku macho yake yakiendelea kumtathimini Dk. Eddyson ,aliekuwa mnyonge kupita maelezo ,
"puuuuh! Sikiliza bwana mkubwa, siku zote ahadi huvunjwa kutokana na sababu za kila mmoja, hujawahi kuona penzi la watu waliokuwa wakipendana sana, na kila mtu akiwatamani lakini mwisho wa siku wanaachana? Na hata wakikutana hawasemeshani? "
"kweli "
"sasa Kama ni kweli!, Je mimi nitakuachaje, na tayari umeshafahamu kila kitu changu, ukitaka nikuache labda nikuue "
"nini? "Dk. Eddyson alipayuka kupita maelezo,
"ndio lazima ufe, ndipo utakuwa huru la sivyo karibu ndani ya Blood deal, kuna swali?"
"ha.... hap... aaana "
Alijikuta akishindwa kujibu vyema, zaidi ya kuendelea kutetemeka, ile furaha ya asubuhi aliyoamka nayo ilotoweka ghafla.
"Basi kama hakuna, karibu kwako, unaweza ukarudi kuishi hapa kuanzia leo, fanya usafi, tutazidi kuwasiliana, unaweza kuondoka chukua pikipiki wahi hofisini "
David alimkabidhi noti tatu za elfu tano tano mpya, Kama nauli.
*****
Usiku mzima hakuna alieshituka, zaidi ya kujigeuza geuza, saa kumi na mbili, Poul alikuwa wa kwanza kuamka, aliyafuta macho yake ili kuiondoa hali ya usingizi singizi, kisha alinyanyuka na kuketi, hakutaka kumuamsha mama yake, muda huo, alichofanya alishuka taratibu hadi chini alikoanza kufanya mazoezi kama Dk. Atanasi alivyokuwa amemweleza,
"Mama nataka kuoga "
Poul alimuongelesha Mama yake, huku mikono yake ikimtikisa tikisa, dakika mbili alishituka akiwa mchovu mchovu sana,
"shikimoo Mama "
Mar- haba ,umeamka salama? "
"Ndio mama, wewe je? "
"Salama ila nahisi, mwili mchovu, na mkono unauma hapa "aliongea huku akipashika shika eneo lililokuwa likimuuma, hakujua ni kipi kilimpata zaidi ya kuhisi uchovu tu, hakuta kulala tena, alimchukua mwanae na kumpeleka bafuni alimsafisha, kisha nae alijisafisha, baada ya kumrudisha chumbani huko,dakika kumi wasalimiaji waliingia, hata kabla hawajakaa Dk. Atanasi alifka chumbani humo kumjulia hali rafiki yake Poul, aliwaomba wampishe kidogo na baada ya vipimo aliondoka, akiahidi kurudi mchana huku akiwapa matumaini ya kuondoka siku chache.
Ilikuwa jumatano asubuhi Janiphar alikuwa akijiandaa kuelekea kazini, baada ya wao kuruhusiwa kutoka hospitali siku tano nyuma, hakuwa na furaha hata kidogo, kutokana na upweke uliokuwa ukimsumbua, siku zote alizoea kuondoka na mmewe ,tena wakiwa wanacheka kwa furaha,
"mpenzi nilikuzoea sana, sikujua kama siku moja utaniacha peke yangu, nilijua tutaishi milele ndani ya vicheko na tabasamu zisizo na kikomo, leo umeondoka na kuniachia mtoto, leo umeondoka na kuniachia lawama na hata uaduni, laiti ningekuwa na uwezo ningekufuata, nit...... "Janiphar alishindwa kuongea, alijikuta akilia sana huku akiwa ameikumbatia picha ya mmewe, siku wakifunga ndoa, miaka mitatu nyuma, hakiri yake, moyo wake vyote vilishindwa kuzoea kabisa, kila siku kwake kilikuwa kilio,tena kibichi, muda mwingine alidhani ni ndoto, ama yuko Safari na siku moja angelejea, lakini haikuwa hivyo, Emanuel alikuwa ameshafariki! Na asingeonekana tena ndani ya uso wa dunia.
Taratibu aliitoa picha hiyo kifunia kwake, aliibusu, kisha aliirudisha ndani ya kabati lake la nguo, hakutaka tena kuiona kwa muda huo,
"bwana nipe uvumilivu "papo hapo alichukua funguo za gari lake aina ya BMW ,mkoba mkono wa kushoto na kutoka chumbani humo, aliwaga ndugu waliokuwepo kisha aliondoka, bila kuyafuta machozi yaliyokuwa yamesambaza sambaza powder yake.
Kila mtu alifurahi kumuona, neno Pole ndilo aliloshinda nalo masikioni mwake, siku hiyo alishinda mnyonge sana, lakini kadri siku zilivyozidi kusonga alijikuta akianza kuzoea zoea na kusahau ,ndani ya miezi mitatu alikuwa keshazoea, kule kulia lia kulipungua kiasi, tabasamu likaanza tena kuonekana usoni mwake, ngozi nayo ikaanza kukujuka na kurudi katika muonekano wake, wa kawaida.
Mwezi wa sita alianza kuugua ugua hovyo hovyo, muda mwingine alihisi ni maralia hivyo alinunua dawa, ama aliongea na Dk. Atanasi aliemshauri cha kufanya, lakini hakupona akawa mtu wa homa homa baada ya muda mfupi, hali ilivyozidi kuendelea ilibidi aende Aghakhan kuchukua vipimo.
"Janiphar Emanuel! "
" Abeee Dk "
Akiitika Janiphar huku akinyanyuka na kuelekea chumba alichokuwa Dk Larry, raia wa Hindia
"karibu Janiphar "Dk. Larry aliongea kiswali chenye rafudhi ya kihindi hindi huku akimtazama machoni ,
"ahsante "
Kimya kilitawala huku Dk. Larry akikagua kagua karatasi zake,
"Dk. niambie vipi namaralia sugu nini ? "
Aliuliza Janiphar baada ya kuona kimya kimetawala muda mrefu.
Dk Larry hakutaka kuongea chochote zaidi ya kumtazama kama dakika tatu, kisha aliachia kikohozi kikavu kutengezeza koo lake,
"Janiphar "alianza kwa kuita, kisha akiendelea
"majibu yako utapata, ondoa wasiwasi, hebu niambie mmeo alikufa kwa ugonjwa gani? "
"aaaah! Aliuawa nchini Afghanistan, kwa ufupi hakufa kwa ugonjwa wowote "
"sawa, na kabla ya kifo chake, aliwahi kuugua ugua kitu chochote?"
"mmmmmh! Hapana, mme wangu hakuwa na tabia ya kuugua hovyo hovyo, kwani vipi? "
"hakuna tatizo, nilikuwa nataka kujua tu, je wew hukuwa ukiugua chochote? "
"hapo nyuma hapana!, ila miezi mitano ama sita baada ya mme wangu kufariki, mwili wangu ulianza kuumwa umwa hovyo, mwanzo nilijua mawazo, lakini hali iliendelea endelea tu "
"ok sawa, samahani kwa swali hili, sina nia mbaya, je baada ya kufiwa uliwahi kushiriki tendo la ndoa na mtu mwingine? ".Safari hii Janiphar alishituka, hakujua kwanini Daktari huyo alikuwa na maswali, mengi kiasi hicho!.
"Hapana sijawahi, na siko tayari kwa muda huu, nampenda mme wangu sana, je nimeonekana na Ukimwi? "
"mmmmmh! Janiphar ondoa wasiwasi, bado tunashughulikia vipimo, na hatuwezi tukakueleza, kuwa umeambukizwa ila njoo baada ya miezi mitatu tutajua zaidi "
Maneno ya Dk. Larry alimchanganya sana Janiphar, hakutaka kuendelea kukaa tena ,chumbani humo alitoka mbio mbio hadi ndani ya gari lake, safari ya kuelekea mwananchi hospital ilianza, njia nzima alikuwa akitoa machozi, hakujua alifikaje hapo, alipaki gari lake mbele ya jengo la zamani la Tanesco,alishuka haraka, huku akikimbia kukifuata kijia cha kuingia soko la makoroboi, lakini hakufika huko ,alikunja mkono wa kushoto na kuingia ndani ya hospitali hiyo iliyojificha ficha, kwa mtu mgeni jiji la mwanza ni vigumu sana kuifahamu.
"Agines ninaukimwi! "Janiphar aliongea bila hata kukaa, Wifi yake Agines aliekuwa daktari mpya ndani ya hospitali hiyo alimshangaa, haikuwa kawaida ya Janiphar kwenda pale bila kumtarifu.
"nani kakueleza wifi? "Agnesi aliuliza kwa upole, huku akiacha kumuhudumia mgonjwa aliekuwemo ndani,
"nimetoka Aghakhan dakika hii nimeelezwa, ninaukimwi wifiiii, na nani kaniambukizaaaa"Janiphar alishindwa kuongea vizuri, zaidi ya kulia, alikiona kifo kikimkabili muda si mrefu , kifua nacho kilichemka kupita maelezo .
"Mamy tulia Kwanza, acha nimalizie kumuhudumia huyu nije tujue zaidi " Agnes alizungumza hayo, huku akimalizia kumuhudumia mgonjwa wake, dakika kumi alianza kuongea na wifi yake ,Janiphar alianza kumuelezea kila kitu, huku akitia huruma,
"acha tuchukue kipimo ".
Papo hapo alichukua damu kutoka kwa Janiphar, na kuipeleka sehemu husika, dakika mbili alilejea kuongea na wifi yake, akimtia moyo, kidogo Janiphar akianza kufarijika, wakiwa wamezama ndani ya mazungumzo, majibu ya Janiphar yaliletwa na kukabidhiwa Dk. Agines ambaye ni wifi yake kabisa, kabla hajafanya chochote Janiphar alimnyakua na kuyasoma, papo hapo alidondoka chini kama mzigo puuuu, na kupasuka kichwa upande wa kisogoni, Agines alibaki amepigwa bubuwazi, hakujua afanye nini, zaidi ya sekunde arobani na tano alikuwa hajielewi ,alikuja kushituka baada ya kuona damu nyingi zikiipamba taizi, kelele akizozipiga zilichangia kujaza watu, dakika saba ndizo zilizotumika kumsaidia Janiphar aliekuwa akihema kwa mbali sana ,huku akiwa amepoteza fahamu , huduma ya kwanza ilitolewa ,kabla ya kwenda Bugando hospitali kwa uchunguzi zaidi.
Machozi na kamasi nyepesi nyepesi hazikukatika machoni, na puani kwa Agines pindi alipogundua majibu ya wifi yake, yaliyokuwa yakionesha maambukizi ya virusi vya ukimwi, hakujua muda gani walifika Bugando, wakiwa bado getini Janiphar alipandisha kifua juu, macho yakiwa yametoka, huku mdomo ukiachama na alipokuja kushusha kifua tayari alikuwa amefariki, kila mtu ndani ya ambulance hiyo hakuamini hasa hasa wifi yake, alieona kama maigizo flani lakini ukweli ndo ulikuwa huo.