Blood deal

Blood deal

Madame S

JF-Expert Member
Joined
Mar 4, 2015
Posts
17,190
Reaction score
34,526
SEHEMU YA 1.

Ndege kubwa toka shirika la ndege duniani Qutar ilionekana ikitafuta uelekeo mzuri wa kutua ndani ya uwanja wa kimataifa wa Hamid karzai international airport ndani ya mji wa kabul Afghanistan, kabla ya kutua taratibu ilishusha matairi ya mbele na kisha ya nyuma huku teyari abiria wote ndani ya ndege hiyo wakiwa wamefunga mikanda na kutulia katika viti vyao ,huku wengine wakiomba taratibu mioyoni mwao kumsihi mungu wao awasimamie katika nafasi hiyo iliyokuwa imesalia katika safari yao.
"Tunapenda kuwatakia mapumziko mema na shughuri njema ndani ya nchi ya Afghanistan "
Sauti nyororo ya msichana aliyekadriwa kuwa chini ya miaka ishirini na tano ilisikika ikipenya taratibu ndani ya kila ngoma za masikio ya kila abiria aliyekuwa ndani ya ndege hiyo. Lugha hiyo ilizungumzwa kwa kiarabu lakini ilitafasiliwa kwa lugha zaidi ya nne kiswahili, kingereza, kifarasa, na, kichina hali hiyo ilisaidia baadhi ya abilia waliokuwa wangeni na lugha ya kiarabu kuelewa kilichozungumzwa .
Taratibu ilianza kushuka chini kwa Kasi huku tairi zote zikiwa nje teyari kuikanyanga aridhi ya nchi hiyo na kabla ya kusimama ilianza kuseleleka kwa kasi huku ikiendelea kupungunza kasi hiyo kisha ilisimama ,mlango ulifunguliwa huku ngazi ikiwa teyari .
"so tutaonana lini Ema?"
"aaaah!! sijui... "
"stop Ema ndo unataka sema hatutaonana tena ?"
Juliet aliongea kwa madeko sana kana kwamba walikuwa wanafahamiana kwa muda mrefu, yale mazoea mafupi na kufahamiana kwa muda mfupi ndani ya ndege hiyo yalimfanya Juliet kuwa karibu sana na Bwana Emanuel
"tutaongea"alijibu kwa ufupi huku akinyanyuka kitini hapo
"basi nipe contact zako "Safari hii Juliet aliongea kwa madeko zaidi macho akiwa ameyarembua akiyapa hali ya usingizi usingizi ili tu kumkoleza Emanuel, sura yake yenye umbo la yai ikiwa imezawadiwa mashavu meupe na makubwa kiasi yakiwa na vishimo pindi alipocheka ilimfanya azidi kuvutia zaidi.
"+25575620228.."
"ahsante sana "
"usijali"
"Mhhhh! samahani ulisema utakuwa hoteli gani?
"intercontinetal"
"waooo! kumbe upo hapa hapa Kabul, mie naelekea Ghazni"
"vyema zaidi"
Kadri muda ulivyozidi ndivyo maongezi na mazoea yalizidi kuongezeka hali hiyo ilimfanya kila mtu kumuamini mwenzake, kwakuwa ulikuwa wakati wa kutoka ndani ya ndege hiyo ilibidi wakatishe mazungumzo na kufuata taratibu zote zikiwemo za ugongewaji wa passport
"kimepotelea wapi hiki? Emanuel alijiuuliza peke yake akiwa anasukuma kitoroli kilichokuwa na begi Lake dogo pamoja na kifuko kidogo, shingo yake aliipa kazi ya kuzunguka huku na huko kumtafuta Juliet akiwa na lengo la kumuaga kabla ya kuondoka ndani ya uwanja huo
"samahani kaka tunaweza tukachunguza begi lako? "aliongea mmoja wa askari waliokuwa eneo la lango kubwa, kwa lugha ya kingereza
"hakuna shaka angalieni tu! "
Kwa kuwa hakuwa na wasiwasi wowote juu ya mizingo yake aliwapa begi lake huku akiwasaidia kufungua, macho yake yalishituka kidogo baada ya kukutana na nguo tofauti na iliyokuwa imewekwa juu na mkewe
"nini hiki? "
"s... si... jui"
Alijikuta akipata mshituko wa hali ya juu baada ya kutolewa mfuko mkubwa wa rambo rangi nyeusi ukiwa umefungashiwa vitu mithili ya unga
"drugs abuse(madawa ya kulevya) "
Askari aliekuwa akiufungua mfuko huo alijikuta akishituka Sana
"hapana begi hili silo langu! "
"kiaje wakati umekamatwa nalo wewe? " ilibidi askari asimame huku akimsogelea Emmanuel aliekuwa bado akilikagua kagua begi hilo ambalo lilikuwa lake kwa kila kitu kuanzia kimdori kidogo kilichokuwa pembeni alama iliyokuwa ubavuni lakini alichanganyikiwa na mzigo uliokuwemo ndani yake ,kwa macho yake mawili alishuhudia mkewe akipanga nguo moja baada ya nyingine huku yeye akiwa amejilaza pembeni akimtania,
"sasa madawa yameingiaje? "alizidi kuumiza kichwa chake bila kupata jawabu sahihi.
"kuanzia muda huu upo chini ya ulinzi? "alinzungumza askari aliekuwa akifahamika kwa jina la Nurdin , papo hapo alifungwa pingu mikononi na kutolewa nje ya uwanja huo akiwa chini ya ulinzi mkali sana
"lakini sihusiki na mzigo huu "
"hayo hatujui sie wewe subili ukifika pahali sahihi utaongea"
Emanuel alipakizwa ndani ya gari la polisi akiwa haamini tukio hilo ambalo aliliona kama ndoto ya mchana muda mfupi angeshituka, kutoka uwanjani hapo hadi kituo cha polisi hakukuwa na umbali mrefu walijikuta wakitumia dakika saba tu
"shuka"
Taratibu alishuka na kuanza kuelekea ndani ya kituo hicho kilichokuwa kikifahamika kwa jina la muhazrat police station.
"inakuaje raia wa Tanzania unaingia na madawa ya kulevya hapa ili hali nchi yako inasifika kwa amani, utulivu na kila kitu chema? " Asikari polisi aliekuwa amesimama nyuma ya meza kubwa aliongea huku akimtazama machoni, japo alikuwa amevaa miwani lakini macho yake makubwa na mekundu yalionekana dhahili
"si.. hu.. siki... na... tukio hili! "
"acha kudanganya kaka hapa si Tanzania ,tambua uko Afghanistan hatuna tamaa ya rushwa kama asksri wenu wasiotekeleza kazi zao,hebu lete na hiyo passport yako yawezekana umegushi "
Emanuel alimpatia huku akianza kuingiwa na woga, aliijua vyema nchi hiyo, teyari alianza kujihesabu mfungwa mpya nje ya nchi yake hakika aliumia sana, maneno matamu aliyoyapata toka kwa mkewe Janiphar pamoja na kijana wake Mdogo Poul wakiwa uwanja wa ndenge wa mwanza yalimuumiza sana
"Baba utaniletea baskeli ?"
"ndioo baba, tena niache aaaah! masihara hayo ".Alijikuta akikumbuka na kumfanya atoe machozi namna ushahidi ulivyokuwa wazi dhahili gereza lilikuwa halali yake.
Baada ya mahojiano hayo aliamriwa kuvua kila kitu kisha alipelekwa mahabusu.
******
"haloo "
"ndio niambie umefanikisha? "
"aaaah! mie tena ,andaaa pesa yangu tu "
"poa "
Simu ilikatwa huku kila mtu akiwa na furaha ndani ya moyo wake, kiasi cha milioni kumi kwa kazi ndogo kama hiyo kilimfanya dada huyo kucheka na kufurahi, teyari alikuwa tajiri mtoto
"kwanza nanua gari, nguo za kufa mtu watanikoma mwanza hahaha "
Aliongea peke yake akiwa kitandani ndani ya hoteli ya Intercontinetal ghorofa ya kumi na mbili chumba na 231 ,kwa furaha aliyokuwa nayo ilimrazimu kuanza fakamia vinywaji vilivyokuwa ndani ya jokovu ndogo. Ghafla alisikia mlango ukingongwa taratibu alinyanyuka huku mkononi akiwa na chupa ya kileo ,mwili wake mweupe akiufunga taulo lililoishia katikati ya mapaja
"nani? "
"mhudumu "
Jibu hilo lilimfanya afungue haraka bila kuwa na wasiwasi wowote
"shiii! kaa kimya "
Alijikuta akiamriwa baada ya kukutana na watu wawili wakiwa wamevaa mavazi yaliyowaficha sura zao, walimsukumia ndani ya chumba bila kuongea chochote huku mwingine akiwa ameshikilia bastola aina ya m-32
"sikia binti wewe ni mzuri sana kama hutaki kufa tupe penzi "Homayoun aliongea huku akumsogelea karibu kisha alilivuta taulo hali iliyopelekea wote kutoa macho na udenda baada ya kukutana na mwili mweupe ukiwa na ngozi nyororo
"naanza mimi "
"wapi acha nianze mie "
Walianza kubishana kwa lugha ya kiarabu ambayo ilikuwa ngeni masikioni mwa binti huyo aliekuwa akitetemeka Sana
"basi tukose wote paaaaaa! "
Murtaza aliongea huku akiyasindikiza maneno hayo na risasi moja iliyokifyatua vyema kichwa cha binti huyo.
"sasa nini? "
"kazi yetu ilikuwa kuua si vingine tuondoke "
Walitoka kwa tahadhari wakipitia mlango wa nyuma bila kuinewa na mtu yeyote.

"Juliet unatakiwa usafiri hadi Afghanistan na Emanuel hakikisha unakuwa nae karibu sana ili asije shituka kwa lolote sawa? "
"sawa boss vipi malipo yangu lakini tambua kazi ya kwanza hujanipatia " Juliet aliongea huku akinyanyua glass ya bia iliyokuwa mezani ndani ya mwanza hoteli na kuipeleka mdomoni alikunywa fundo moja kisha aliirudisha glass hiyo pahali pake na kumtazama David usoni
"pole Juliet malipo yote nitayaunganisha nitakupa milioni kumi keshi "
David alizungumza huku akimtazama machoni akisindikiza na tabasamu bashasha ili kumteka Juliet alikuwa ameshamjulia udhaifu wake
"sawa so lini ataondoka? "
"kesho na ndege ya saa mbili asubhi na nzuri zaidi nimekukatia kiti kimoja na yeye unatakiwa umchangamkie maana namjua hana tabia ya kuongea ongea "
"hilo niachie mie mmakonde halisi natema checheka kama sijielewi hahaha! "
Juliet aliongea huku akikitikisa kifua chake kilichojaliwa chuchu kubwa kiasi kulingana na mwili wake ,maneno hayo yalizidi kumpa faraja ya ushindi bwana David. Waliongea mengi sana na jambo kubwa kuliko yote lilikuwa ni kumkamata bwana Emanuel msukuma toka wilaya ya Simiyu mkoani shinyanga tajiri kupindukia akiwa chini ya miaka thelathini na tano ,alikuwa akiishi jijini mwanza wilaya ya nyamagana maeneo ya Bugando karibu kabisa na chuo cha udaktari Bugando.
Japo alikuwa tajiri sana hakuwa na moyo wa kichoyo kuanzia nyumbani kwao alikowajengea wazazi wake nyumba ya kisasa kabisa huku wadogo zake wawili mmoja wa kiume aliekuwa hajaoa alimshirikisha katika biashara zake, Dada yake alikuwa bado mwanafunzi ndani ya chuo cha udaktari Bugando.
Katika umri huo alikuwa teyari na familia mke na mtoto mmoja aliefahamika kwa jina la Poul, mkewe aliitwa Janiphar mwenyeji wa mkoa wa Moshi wilaya ya Rombo kijiji cha mashati, kutokana na upendo na uchapakazi kati ya wanandoa hao walijikuta wakifanikiwa sana kila iitwapo leo, utajiri wao haukuishia kuwasaidia wazazi na ndugu pekee bali kila iitwapo jumapili hawakusita kutoa misaada kwa wafungwa ndani ya gereza la Butimba na baadhi ya vituo vya kulelea watoto yatima pia jumamosi hawakusita kusambaza misaada kwa wazee na watoto waliokuwa wakiishi maisha ya mtaani arimarufu kama ombaomba vitendo vyote hivyo vilimfanya apendwe na kila mtu si mkubwa ama mdogo pia jina lake lilikuwa mswaki ndani ya vinywa vya wakazi wa mwanza na mkoani shinyanga.
*****
 
BLOOD DEAL
Author: Teddy
Cont:0655 202 285.
Whatsapp :0756 202 284
KWA MWENYE UHITAJI WA RIWAYA HII, AWASILIANE NA MWANDISHI KWA NAMBA HIZO JUU.

SEHEMU YA 2

Katika umri huo alikuwa teyari na familia mke na mtoto mmoja aliefahamika kwa jina la Poul, mkewe aliitwa Janiphar mwenyeji wa mkoa wa Moshi wilaya ya Rombo kijiji cha mashati, kutokana na upendo na uchapakazi kati ya wanandoa hao walijikuta wakifanikiwa sana kila iitwapo leo, utajiri wao haukuishia kuwasaidia wazazi na ndugu pekee bali kila iitwapo jumapili hawakusita kutoa misaada kwa wafungwa ndani ya gereza la Butimba na baadhi ya vituo vya kulelea watoto yatima pia jumamosi hawakusita kusambaza misaada kwa wazee na watoto waliokuwa wakiishi maisha ya mtaani arimarufu kama ombaomba vitendo vyote hivyo vilimfanya apendwe na kila mtu si mkubwa ama mdogo pia jina lake lilikuwa mswaki ndani ya vinywa vya wakazi wa mwanza na mkoani shinyanga.
*****
Saa moja na dakika kumi na tano Emanuel aliondoka nyumbani kwake akiwa na mdogo wake pamoja na familia yake ndani ya gari lake la kifahari aina ya Vorvu
"inatakiwa ufanye kazi kwa nguvu, utii, moyo wa kujituma na heshima lazima ufanikiwe tu "
"kweli kaka "
Hadi wanafika uwanja wa ndege walikuwa wakizungumzia maswala ya Kazi
"nitakukumbuka Sana mpenzi " Janiphar aliongea huku kichwa chake akikilaza juu ya bega la kushoto la mmewe Emanuel
"usijali mama siku tano tu "
"baba utaniletea baiskeli? "
"ndio baba wewe tena masihara nisipoleta"
Baada ya maongezi hayo Emanuel aliangana na familia yake kisha alielekea chumba cha ukaguzi na baada ya zoezi hilo kukamilika aliiendea ndege.
Akiwa katika mawazo dhidi ya familia yake ghafla alitokea msichana aliekuja kukaa pembeni yake na Safari ikawa imeanza hadi wanaingia Nairobi hakuna akiemsemesha mwenzie lakini baada ya kutoka Nairobi msichana aliekuwa pembeni yake alijifanya akiumwa tumbo tena lenye maumivu makali sana hali hiyo ilimfanya Emanuel kushituka sana papo hapo alianza kutoa huduma ya kwanza kabla ya wahusika maarumu
"ahsante kaka" Juliet aliongea mara baada ya kupatiwa msaada
"usijali duniani kusaidizana leo kwako kesho kwangu, "
"kweli kabisa"
Kimya kilichukua nafasi tena kama dakika kumi kisha Juliet alianzisha mazungumzo tena
"naitwa Juliet naelekea Afghanistan kibiashara sijui mwenzangu nani? "alizungumza huku akimtazama machoni
"Emanuel pia naelekea huko huko uendako ".
Huo ndio ukawa mwanzo wa urafiki wao hadi wanaingia mjini Kabul walikuwa marafiki kabisa hali hiyo ilimfurahisha sana Juliet aliemshukuru muumba wake, baada ya kutoka ndani ya ndege hiyo alijichanganya na abilia waliokuwa wakitembea makundi makundi kuelekea sehemu ya kuchukulia mizigo haraka sana alichukua begi la Emanuel lililokuwa likifanana kila kitu na lake alilokuwa amelijaza madawa ya kulevya kazi aliyopewa na bwana David aliefananisha begi hilo na la Emanuel ,kazi aliyoifanya akishirikiana na mmoja wa wafanyakazi wa uwanja wa ndege mjini mwanza kuyapitisha madawa hayo.
"kushi nei kafie mbele "Juliet aliongea peke yake akiwa anamtazama Emanuel aliekuwa bado akimtafuta yeye, pia alishuhudia tukio la uchukuaji begi hilo, papo hapo alielekea getini alikokwenda kuongea na askari kisha aliondoka akitumainia ushindi mkubwa.Kweli Emanuel alipofika eneo hilo alikaguliwa na kukutwa na mzingo mkubwa wa madawa ya kulevya.
Juliet alikuwa na shauku ya kupata milioni kumi mara baada kufika ndani ya hoteli ya intercontinetal iliyokuwa katikati ya mji wa Kabul mji mkubwa kwa shughuri mbalimbali za taifa hilo alimpigia simu David kumpa taarifa hiyo kisha alianza kujiburudisha na vileo vilivyokuwa vimesheheni ndani ya jokovu dogo la kisasa.
*****
"Hamayoun uko wapi? "
"niko internet house " Hamayoun akijibu ujumbe huo ulioingia ndani ya simu yake kupitia njia ya whatsapp
"naomba uelekee intercontinental hoteli ghorofa ya kumi na mbili chumba no 231 ukammalize msichana unaemuona kwenye picha hiyo "
"sawa malipo je? "
"nishawaeka dolla elfu tatu ndani ya acount yako "
Baada ya mawasiliano hayo kutoka Tanzania hadi Afghanistan Hamayoun aliondoka eneo hilo akikodi pikipiki hadi nyumbani kwa rafiki yake Murtaza mtaa wa tano toka eneo hilo. Murtaza alikuwa jambazi na mafia mkubwa aliekuwa akifanya kazi na kundi la Taliban lililokuwa tishio sana nchini humo,
"mwanangu twende dili limewaka "
"kweli? "
Aliuliza Murtaz akiwa haamini habari hiyo kwani alikuwa na siku tatu bila kuingiza pesa zaidi ya kuzitumia, aliitupa sigara yake chini na kuikanyanga kisha alivaa suruali nyeusi pamoja na koti lake na mwisho kabisa aliichomeka bastola yake kiunoni kisha walitoka nje wakiliendea gari lake
" tunahitaji vyumba Kwa matumizi ya masaa matano tu " aliongea Hamayoun na dada aliekuwa mapokezi
"vipo dolla mia saba tu! "
"poa "
Hamayoun alilipia kisha walipandisha ngazi hadi ngazi ya pili toka hapo kisha walichukua lifti iliyowapeleka gharofa ya kumi na mbili
"tufanyeje sasa? "
"we subili utaona "
Murtaza alizungumza huku akitembea kuelekea mbele akikipita chumba cha Juliet hata kabla hajafika mwisho akitokea mfanyakazi aliekuwa na mashuka machafu dhahili alionekana alikuwa mfanya usafi.
"samahani dada "
"bila samahani " alijibu msichana huyo huku akiizuia miguu yake kusonga mbele hilo likawa kosa kubwa sana
" tunaomba ukatusaidiea kuongea na mgeni aliomo ndani ya chumba kile "
Murtaza alisema huku mdomo wa bastola yake ukiwa kichwani mwa msichana huyo aliekuwa ameanza kutetemeka
"sawa nitaenda "
"twende "
Ashirafa aliongoza hadi mlangoni mwa chumba hicho na kugonga waliposikia kitasa kikiguswa walimtoa Ashirafa mlangoni hapo akiwa amemfunikwa puani na kitambaa cheupe sekunde kumi tu alianza kulegea akikosa nguvu papo hapo Hamayoun alimlaza chini karibu kabisa na chumba hicho kisha alilejea kwa mwenzake aliekuwa amesimama katika ya mlango akigojewa kufunguliwa.
" boss teyari "
"basi sawa "
Alijibu David huku akikenua meno ishara ya ushindi. Japo aliishi Tanzania lakini kazi zake kokote duniani zilifanyika tena kwa wepesi.Usiku mzima aliumaliza akitafuna nyama choma na bia ndani ya Tilapia Hoteli pembeni akiwa na wapambe pamoja na wasichana watatu waliokuwa wakimlisha, kumbusu na kila aina ya mapenzi.
*****
Kukamatwa kwa mtanzania nchini Afghanistan akiwa na madawa ya kulevya kulienea kwa kasi sana kila kona ya dunia mithili ya moto wa kifuu, David alikuwa na hamu ya kumuona Emanuel akiwa nyuma ya nondo kweli katika taarifa ya habari ya saa mbili usiku kupitia ITV na radio one habari hiyo ilitangazwa hadhalani hapo ndipo furaha yake ilizidi kuongezeka mara dufu alijiona mshindi kupita maelezo.
"shemu mme wangu amekamatwa jamaniiiiii! "
"nini? "
"kweli eti na madawa ya kulevyaa jamaniii "
Mama Poul aliongea huku akianza kulengwa lengwa na machozi hakuamini tukio hilo
"Yesu na Maria Shemu njoo nyumbani jamaniiiii" alizidi kulalamika ndani ya simu akimsihi David kufika nyumbani kwake Bugando usiku huo huo hata chakula kitamu alichokuwa akikila kilikwama akawa wa kulia peke yake akiongea kichanga,
" ilikuwaje shemu?" aliuliza David mara baada ya kufika nyumbani hapo akijifanya kuchanganyikiwa sana, ilibidi Mama poul aelezee tukio zima jinsi alivyoshuhudia huku akiendelea kububujikwa na machozi kila alipotoa neno
" shemu jikaze atatoka tu "
"nashindwa kuelewa madawa hayo yamefikaje ndani ya begi lake ilihali nguo nilimpangia mwenywe "
" hata mie nashangaa ila amini atatoka tu, na kesho itabidi nisafiri "
"wapi tena ?"
" huko huko shemu nikajue cha kufanya "
" kweli shemu"
" basi itabidi uanadae pesa za kutosha shemu "
" usijali Shemu hata nyumba nitauza ili mme wangu atoke "Janiphar alikuwa radhi kupoteza kila kitu ili ampate mmewe aliempenda kupita Maelezo
"basi sawa "
Baada ya mazungumzo hayo David aliondoka huku wakiahidiana kuonana kesho.

"Jamani mie sihusuki kwa lolote jamani "
" kijana usilete ujanja kwa hiki na hapa hakuna cha kutafuta uchunguzi wowote kuhusu hili ushahidi uko wazi na kesho jiandae kuelekea mahakamani "
Aliongea mmoja wa Askari aliekuwa zamu usiku huo wa siku ya pili, japo balozi wa Tanzania nchini Afghanistan alijitahidi sana kumsaidia raia wa nchi yake lakini ilishindikana kabisa hivyo bwana Emanuel akawa amesubili kifungo tu, usiku huo aliutumia kumuomba mungu ili amuepushe na hukumu iliyokuwa mbele yake lakini haikuwezekana siku iliyofuata ambayo ilikuwa jumatatu alipelekwa mahakamani kusomewa shitaka lililompeleka jela miaka saba, hakuwa na ndugu ama rafiki yeyote wa kumfariji alilia peke yake kadri alivyoweza, ama kumuwekea dhamana.
" sikuwahi fikiria siku moja ningeingia gerezani tena nje ya nchi yangu, leo hii mie Emanuel nafungwa na kudhalilishwa kwa tuhuma za uuzaji madawa ya kulevya, heshima yote imevunjika nani ataniamini tena ,namuacha mwanangu mdogo bila penzi la baba je siku akijua aibu hii sura yangu nitaificha wapi? "
Yalikuwa maneno ya kuhuzunisha sana aliyoyatamka Emanuel akiwa ndani ya gari la wafungwa tayari kwenda kutumikia kifungo cha miaka saba katika gereza la Guantanamo mjini Kabul, ilikuwa imepita miaka mingi sana bila kundondosha chozi lakini siku hiyo alilia kama mtoto mdogo, machozi hayo yalitoka si kwa kifungo hicho lahasha! aliwalilia wazazi wake, wadogo zake pamoja na mkewe kipenzi Janiphar mwanamke alikuwa akimpenda kupita maelezo, kijana wake Poul alikuwa mdogo sana leo hii anakwenda kuishi maisha ya mzazi mmoja kwa miaka saba daaaah! hakika alikuwa na haki ya kulia .
" jikaze mkubwa "
" naumia sana kaka "
"najua ila tambua wewe ni mwanaume na ukizaliwa mwanaume lazima uyapitie haya hapo utakuwa umekamilika na kuitwa mwanaume piga moyo konde kaka "
kwa mara ya kwanza toka aingie ndani ya gereza hilo alijikuta akiongea na mtu, kwani toka afike ndani humo hakupenda kuongea chochote zaidi ya kulia kila alipopata muda wa kufanya vile.
" Omar nashindwa kuelewa madawa yaliingiaje ndani ya begi langu na pia askari walijuaje? "
" daaaa!, je kwani nguo alipanga nani? "Omari aliuliza huku akikaa chini pembeni akiweka fagio lake
 
BLOOD DEAL
Author: Teddy
Cont:0655 202 285.
Whatsapp :0756 202 284
KWA MWENYE UHITAJI WA RIWAYA HII, AWASILIANE NA MWANDISHI KWA NAMBA HIZO JUU.

SEHEMU YA 3

" jikaze mkubwa "
" naumia sana kaka "
"najua ila tambua wewe ni mwanaume na ukizaliwa mwanaume lazima uyapitie haya hapo utakuwa umekamilika na kuitwa mwanaume piga moyo konde kaka "
kwa mara ya kwanza toka aingie ndani ya gereza hilo alijikuta akiongea na mtu, kwani toka afike ndani humo hakupenda kuongea chochote zaidi ya kulia kila alipopata muda wa kufanya vile.
" Omar nashindwa kuelewa madawa yaliingiaje ndani ya begi langu na pia askari walijuaje? "
" daaaa!, je kwani nguo alipanga nani? "Omari aliuliza huku akikaa chini pembeni akiweka fagio lake
" mke wangu na nilikuwa namshuhudia na hata asubhi yake nililifungua na kukagua upya lakini sikuona chochote"
"mmmh!., kweli? "
" ndio!"
" je huna adui yeyote na kabla hujasafiri nani aliijua safari yako? "
"aaaah!, mke wangu na mdogo wangu wa kiume "
" je uhusiano wako na mdogo wako ukoje? "
" hakuna shida tunapendana japo ni mvivu kujituma lakini nishamzoea"
Kuanzia siku hiyo Omari aliekuwa raia wa Omani mfungwa wa maisha ndani ya gereza hilo kwa kosa la mauaji makubwa alijikuta akipatana na Emanuel mtu mweusi aliekuwa hathaminiki mbele ya waarabu ,muda mwingi alitumia kumfariji na kumsihi kutokata tamaa kweli Emanuel alijikuta akianza kuyazoea maisha ya jela na kila kulipopambazuka hakusita kupunguza siku katika karenda iliyokuwa ndani ya kila chumba cha wafungwa.
" mambo Ema "
"sa... safii t... u."
Alijikuta akipata kigugumizi kujibu salamu hiyo kutokana na lugha iliyozungumzwa hakuamini Kama siku moja angeweza sikia mtu akizungumza kiswahili ndani ya nchi hiyo
" najua utanishangaa sana ila fahamu nami ni mtazania natoka mkoa wa Tabora wilaya ya Nzega " kijana huyo alizidi kuongea kiswahili fasaha huku akiwa amesimama karibu kabisa na mlango wa kuingilia chooni, mkononi akiwa na kopo pamoja na fagio ilionekana alitoka kufanya usafi
"aise karibu kabisa na nyumbani kwetu mie natokea Shinyinga wilayani Simiyu (kabla ya kupewa heshima ya mkoa),nashukuru kukufahamu "
Emanuel aliongea huku akinyosha mkono kumsalimia vizuri, siku hiyo alifurahi sana kukutana na mtanzania mwenzake, huo ukawa mwanzo wa urafiki wao.
Siku ya tano toka Mtanzania huyo aliekuwa akifahamika kwa jina la Yuda kuingia gerezani humo Emanuel alitekwa usiku wa saa tano saa za huko, akiwa usingizini aliamshwa na Yuda aliemuomba amsindikize chooni kwakuwa alimpenda na kumjali kama ndugu yake Emanuel alijikuta akitoka nje, bila kujua chochote hata kabla hajafika katikati ya uwanja alishangaa kuona vijana wawili wakimsogelea na kumkabwa wakiwa wamefunika sura zao, walimbemba mzobemzobe hadi nje ya jengo hilo kwa kuruka ukuta akiwa hajitambui baada ya kupigwa kitu kizito kisogoni kilichosababisha apoteze fahamu kwa muda wa dakika saba, fahamu zilipomrudia alijikuta akiwa katikati ya vijana saba ndani ya jengo bovu, Yuda mtanzania aliekuwa akiishi Afghanistan kwa kazi ya ujambazi, Murtaza, Hamayoun na wenzao wanne
"Yuda nimekukosea nini lakini? ,upendo wangu leo unaniua? "
" kaka sio mie " Yuda alizungumza huku akimpiga teke la mbavu
"mmmmmh,!! achaaaaa! "
Sauti hiyo ilipenya vyema katika ngoma za masikio ya Emanuel hali iliyopelekea Emanuel kugeuza haraka shingo maana haikuwa ngeni masikioni
"David!?,Mdogo wangu!??? "
Alishangaa kupita Maelezo kumuona mdogo wake wa damu toka nitoke akiwa maeneo hayo,, akijaribu kunyanyuka lakini ilishindikana kutokana na kamba akizokuwa amefungwa miguuni na mikononi
" ndio ni mie bwana mkubwa "
David alizidi kuongea huku akimsogelea kabla hajamfikia vizuri alimpiga teke la kifuani lililopelekea kutema damu
" kaka ulijifanya mjanja sana leo umepatikana sali sala yako ya mwisho "
" la... khooo! khooo.... lakini sijui kosa langu mdogo wangu, kipi ulikikosa toka kwangu, leo hii unaniua kweli, ok niambie chanzo cha wewe kunifanyia hivi? "
Emanuel aliongea kwa taabu kutokana na kuzidiwa maumivu ndani ya kifua chake
"mali nataka kumiliki zote, siwezi miliki ukiwa hai nitakuteketeza wewe na familia yako "
" kweli!? "
"ndio "
"niko radhi kukuandikisha kila kitu naomba usiniue tafadhali "
" safi sana andika "
Emanuel alikabidhiwa kalamu na karatasi akawa ameandika mali zote kumkabidhi mdogo wake David
" safi sana kaka naomba umsalimie babu na bibi Nyambele "
David aliachia risasi sita zilizokitoboa vibaya kifua cha Emanuel na kupoteza maisha papo hapo, David aliwaamru vijana wake kumpeleka gerezani usiku huo na kumtupia ndani ya ngome kisha wao walitokomea.
*****
Siku iliyofuata David ambaye ni Mdogo wake Emanuel alifika nyumbani kwa kaka yake kama walivyoahidiana na Shemeji yake usiku wa jana yake, swala lililompeleka hapo ni kupanga mikakati ya yeye kwenda Afghanistan kumsaidia kaka yake, Janiphar ambaye ni shemeji yake alikuwa teyari keshajianda kwenda benki kuchua pesa kwa ajili ya Safari hiyo
" usilie shemu, hata sie tunaumia sana "David aliongea huku akijifuta machozi ya kinafiki ili asijulikane
" naumia shemu "
"nafahamu"
Walifka mjini majira ya saa tatu na nusu asubuhi na kupaki gari lao kisha Janiphar akashuka na kuusogelea mlango wa benki ya CRDB, iliyopo jengo la PPF karibu kabisa na GOLD CREST HOTEL barabara ya Kenyatta.
Kwa kuwa siku hiyo hakukuwa na foleni alijikuta akitumia dakika kumi kuchukua pesa kwa ajili ya safari ya shemeji yake
" milioni sitini hizi hakikisha unarudi na kaka yako "
" sawa shemu "David aliongea huku akiipokea bahasha hiyo akijivika sura ya uchungu kupita maelezo
Baada ya kukabidhiana walielekea hofisi za ukataji wa tiketi za ndege mita chache kutoka hapo jengo moja na Mwanza Hotel kwa mkono wa kulia, kushoto kwake kuna tawi la benki ya NMB Kenyatta road.
Japo hakukuwa na nafasi ya kupata nafasi kwa ajili ya David, Janiphar alijikuta akinunua tikeki kwa malipo ya mara tatu ili mradi tu mmewe akasaidiwe. Siku hiyo jioni ya saa moja David aliondoka Tanzania, japo Janiphar alijua shemeji yake anaelekea Afghanistan kama walivyokubaliana lakini alijikuta akiishia Kanya akikoanza kusuka mipango ya kumuangamiza Kaka yake huko huko,
Kwanza kabisa aliwapa kazi vijana wake murtaza na Hamayoun kufatilia kesi ya kaka yake, kujua gereza gani alifungwa, baada ya kufahamu hilo alitulia kwanza kwa muda wa miezi miwili ndipo alipomtuma Yuda kufanya fujo ili tu aingie ndani ya gereza hilo kweli siku saba tu Yuda alifungwa siku mbili baada ya Yuda kufungwa David alisafiri hadi Afghanistan alikokwenda kuungana na vijana wake waliomteka Emanuel gerezani wakisaidiwa na Yuda kisha alimuua.

Hadi kunapambazuka mwili wa Emanuel ulikuwa bado uko pale pale nje, askari wa zamu ndio aliekuja kuuona ukiwa umetapakaa damu ukitisha pia
"kule kuna mfungwa ameuawa "
"wapi? " mkuu wa gereza aliuliza akiwa haamini alichokisikia
" kwenye domu la watukutu, na ni yule mwafrika toka Tanzania "
" mmmh! " mkuu wa gereza alishusha pumzi ndefu kabla ya kusema chochote , alikikuna kichwa chake kilichokuwa na upala kidogo huku nywele karibia zote zilikuwa zumeanza kujaa mvi,
" twende! "
Alinyanyuka kutoka katika kiti ndani ya hofisi yake Safari ya kwenda ndani ya hospitali ndogo iliyokuemo ndani ya gereza hilo ilianza huku kila mtu akiendelea kuwaza Lake
" inaonekana ameuawa kwa kupigwa risasai na mbaya zaidi macho nayo yametobolewa "alizungumza daktari aliekuwa akifahamika kwa jina la Mohammed Said baada ya kufika kwa asksri magereza hao
" je wafungwa wote wapo? "
" hapana mkuu yule mwafrika mpya nae hayupo "
" aaaah,! shida kweli "
Baada ya maongezi hayo waliondoka eneo hilo wakiwa na wazo la kuutarifu ubalozi wa Tanzania nchini humo kuhusiana na tukio hilo, hakika zilikuwa taarifa za kusikitisha masikioni mwa balozi huyo baada ya kupewa taarifa hizo nae aliamua kuwasiliana na serikali yake kuhusiana na tukio hilo la kuuawa kwa Emanuel.
Taarifa zilipoifikia familia yake hakuna alieamini hata kidogo mke wake alilia kupita maelezo achilia mbali ndugu jamaa na marafiki ,ulikuwa msiba mkubwa sana uliolikumba taifa la Tanzania hata serikali iliumia sana kumpoteza kijana aliekuwa akiingiza pato la taifa kila iitwapo leo ,mji wa mwanza ulijaa wangeni kutoka mikoa mbalimali.
"Mama mme wangu wamemuua mamaaa! "
Janiphar alikuwa akimlilia Mama mkwe mara baada ya wazazi wa Emanuel kufika nyumbani kwake majira ya saa tisa alasili wakitokea Simiyu, kilio ndicho kilichowapokea ndugu hao waliokuwa wamekonda kutokana na kulia kwa muda mrefu sana , toka siku waliyopata habari ya msiba huo kilichokuwa kikifanyika ni kilio tu .
"pole mamaaaa ha.. hata... sisi linatuumiza sana nimempoteza Emanuel wangu " Mama mkwe aliongea kwa huzuni huku akilia kama mtoto mdogo akiwa amekumbatiana na mke wa Emanuel
"shemeji nae amepigwa vibaya sana"
"nani David! !?"
"ndio mama walitekwa wote usiku "
" masikini watoto wangu "
Hakika yalikuwa maumivu yasiyopimika ndani ya mioyo yao kuuawa kwa Emanuel na kupigwa kwa David kama walivyopata habari kutoka Afghanistan iliwaumiza sana, hakuna hata mmoja aliekuwa anaujua ukweli . Baada ya David kutekereza adhima yake aliamua nae ajiumize kiaina ili kuficha ukweli halisi ,kweli usiku huo huo aliiamua kujipiga risasi ya mguuni sehemu aliyona ingepona mapema, mikono nayo aliijeruhi achilia mbali usoni japo aliumia lakini hakujali roho ya dhuruma ilikuwa imemtawala kupita maelezo.
****
 
BLOOD DEAL
Author: Teddy
Cont:0655 202 285.
Whatsapp :0756 202 284
KWA MWENYE UHITAJI WA RIWAYA HII, AWASILIANE NA MWANDISHI KWA NAMBA HIZO JUU.

SEHEMU YA 4

" masikini watoto wangu "
Hakika yalikuwa maumivu yasiyopimika ndani ya mioyo yao kuuawa kwa Emanuel na kupigwa kwa David kama walivyopata habari kutoka Afghanistan iliwaumiza sana, hakuna hata mmoja aliekuwa anaujua ukweli . Baada ya David kutekereza adhima yake aliamua nae ajiumize kiaina ili kuficha ukweli halisi ,kweli usiku huo huo aliiamua kujipiga risasi ya mguuni sehemu aliyona ingepona mapema, mikono nayo aliijeruhi achilia mbali usoni japo aliumia lakini hakujali roho ya dhuruma ilikuwa imemtawala kupita maelezo.
****
" bwana alitoa na bwana ametoa jina lake lihimidiwe, najua tunaumia sana kumpoteza mpendwa wetu ila kazi ya mola haina makosa, leo Safari ya mpendwa wetu Emanuel imeishia hapa nasi tumuombe mungu atusaidie kuishi maisha ya utakatifu hapa duniani, zaidi na zaidi tumuombe mungu ampumzishe pahali pema peponi ndugu yetu alietutangulia "
Yalikuwa ni maneno ya kuhuzunisha na kufariji kiasi flani kutoka kwa Padri Biruru ndani ya kiwanja cha kanisa kathoric bugando jijini mwanza, kutokana na idadi kubwa ya waombolezaji kufurika kanisani hapo misa ya mazishi ilifanyika nje ya kanisa ndani hakukufaa kabisa. Hakuna mtu alieshindwa kutoa machozi pindi alipoyatupia macho yake katika jeneza la Emanuel kipenzi cha watu mkoani hapo, mashirika mbalimbali nayo hayakuwa nyuma, vituo vya watoto yatima alivyokuwa akivisaidia navyo havikukosa kumsindikiza mpendwa wao.
" Mama Baba atakuja lini? "
"sass! ha..... "Janiphar alishindwa kujibu swali hilo kutoka kwa mwanae mdogo poul aliekuwa na miaka mitatu tu, swali hilo lilizidi kuumiza moyo wake, hakujua ajibu vipi ama aseme nini
" mama baba mbona haji? "
Poul alizidi kumsumbua mama yake aliekuwa hajiwezi kwa lolote na kila alipoyaruhusu macho yake kulitazama jeneza alipoteza fahamu.
Baada ya misa hiyo kumalizika safari za kuelekea makaburi ya Kangae wilaya ya Ilemela ilianza wakipitia barabara ya musoma, walipofika buzurunga walikata kushoto kuitafuta nyakato mecca, papo hapo kituo cha mecco walikata kushoto tena wakifuata barabara ya vumbi hadi makaburini, zoezi la kumhifadhi Emanuel halikuchukua muda mrefu hivyo Safari ya bwana Emanuel tajiri kijana ikawa imefika mwisho
" hakikisha unaitunza hiyo hati ya hoteli "
" sawa baba, ila vipi kuhusu hizo zingine? "
Msichsna wa kazi alimuuliza David ambaye hakuhuzuria maziko ya kaka yake kuanzia kanisani hadi makaburini akijifanya kuzimia kutokana na kulia sana hivyo ndugu hao waliamua kumuacha nyumbani, nusu saa baada ya kutoka nyumbani waombolezaji hao alizinduka na kuelekea chumbani kwa kaka yake alikoiba kila nyaraka za maana akiwa dakika za mwisho Vero msichana wa kazi alimfumania.
"zipo... zipooo kwani... vipi? "
Alishindwa kuongea vizuri baada ya kukaziwa macho makali na msichana huyo aliekuwa ameanza kumstukia muda mrefu hata kabla ya kifo cha boss wake ila hakuwa na uhakika hata kidogo.Hakutaka kukaaa tena chumbani humo alitoka akiwa anachechemea akielekea chumbani kwake
" huyu hanijui eeeh! ,nampa masaa 120".

" huyu hanijui nampa masaa 120"
David aliwaza maneno hayo huku akitembea kwa kuchechemea kutoka ndani ya chumba cha kaka yake, moyo wake ulijaa hasira isiyoelezeka hata kidogo aliona kila kitu kitaenda fyongo na siri yake ingetambulika na hilo hakutaka litokee hata kidogo.
" puuuuuuh! "
Alivuta pumzi ndefu baada ya kufika chumbani kwake alikojitupia kitandani kama mzigo puuu akiwa chali macho yake akiyaruhusu kutazama dali lilokuwa limenakishiwa kwa jipsamu rangi nyeupe ikiwa imepambwa vyema na maua ua. Dakika saba alitumia kufikiri ni kifo gani kingemfaa Vero tena kisicho na makelele ama maumivu
" hahaha! "
David aliachia cheko changa lenye maumivu ndani yake baada ya kupata jibu la kazi yake.
" Hail poison itamtosha huyu "
Hii ilikuwa ni sumu hatari sana yenye asili ya hewa hewa ambayo mtu ama kiumbe hai kikipewa sumu hii dakika tatu kinapoteza maisha huku akikiwa amebadirika rangi ya ngozi kuwa nyeusi, sumu hiyo aliipata nchini Austaria kwa gharama kubwa sana ndio aliona suruhisho tosha kutekeleza adhima yake aliyokuwa amekusuudia ya kumuangamiza Vero.
" atakoma" aliongae huku akinyanyuka kitandani hapo na kuliendea Begi lake dogo lililokuwa na sumu hiyo lakini kabla hajafanya chochote alipatata wazo la kurudisha nyaraka alizokuwa aneziiba chumbani kwa shemeji yake ,kweli alikubaliana na wazo hilo alinyanyuka haraka sana.
" sijui nimweleze Mama" Vero aliwaza akiwa bado amesimama ndani ya chumba cha boss wake mkononi akiwa bado ameshikilia hati ya hoteli aliyokuwa amepewa na David baba mdogo wake, kilichomshitua ni kufunguliwa kwa mlago tena kwa kasi ya ajabu haraka aliigeuza shingo yake na kukutana na David akiwa ameshika karatasi tano
" unafanya nini "
" aaaaah!, ba... baba.. nina... "
Vero ama Veronica alishindwa kuongea baada ya kukaziwa macho makali na Baba yake huyo Mdogo aliekuwa bado asimama katikati ya mlango
" pishaaa"
Aliongea huku akianza kutembea kuliendea kabati, Vero hakutaka kuendelea kubaki hapo aliondoka na ile hati hadi chumbani kwake na kuificha ndani ya begi lake dogo la nguo aina ya Omega rangi ya ugoro lililokuwa sakafuni bila kuwekewa kitu chochote chini .
" kazi ipo hapa daaa sijui tutasalimika huyu ni nyoka tena koboko daaa!. yawezekana hata Baba alimuua huyu "
Kwa kuwa Vero alikuwa Binti aliejitambua na kujaliwa uelewa mkubwa alianza kumstukia David na kupanga mikakati ya kupambana nae bila kujua kama mwenzake alikuwa mafia na jambazi mkubwa.
" kesho nakiondoa duniani kijinga sana "
Aliwaza huku akiondoka chumbani humo kwa Mara ya pili.
*****
Kesho nakiondosha duniani kijinga sana "
Aliongea huku akiondoka chumbani humo kwa Mara ya pili.
Baada ya lisaa limoja kuondoka waombolezaji walilejea kutoka makaburini hivyo David aliendelea kujiuguza tena.
Kesho yake kikao cha familia kilichukua nafasi na pendekezo lililopatikana Janiphar ataendelea kuwa msimamizi mkubwa wa mali zote akisaidizana na David, kwa kuwa hakuna na shaka nae yeyote akuwa na budi kumkataa na ukizingatia walikuwa wakifanya kazi nae muda mrefu hata kabla ya kifo cha mmewe.
"afadhali mambo yangu yameanza kwenda vyema sasa"
" kiaje David? " Eric miongoni mwa marafiki zake waliokuwa hawafanyi kazi zaidi ya kutegemea kodi kutoka kwenye nyumba zao za uridhi zikizokuwa mtaaa wa uhuru mkabara na mount meru university
" si kuhusu yule demu? " David alisema huku akichukua kipande cha nyama choma ndani ya sahani wakiwa Kumalija Hoteli iliyoko nyegezi stendi usiku huo
"aaah!,sikia huwezi kukiua kibinti kizuri kama kile bila kukila kwanza, tukiteke kikiwa kinaenda sokoni tukakibake kwanza harafu ndo tukiue "
" kile hakifai kichafu "
"mie naugwadu mtu wangu nipe nipunguze mafuta mwilini "
" basi poa kesho jiandae, "
Japo zilikuwa siku mbili tu baada ya kuzikwa kwa Emanuel David alikuwa tayari ameanza kunywa pombe, hakuwa na huruma hata chembe na mbaya zaidi alikuwa akianza kumuwinda Vero ambaye nae alikuwa amedhamilia kupambana nae.

kikao kati ya David na Eric kilivunjwa baada ya wao kwa wao kuanza kutoleana maneno ya kashifa usiku huo, hakiri ya David ilikuwa ikifanya kazi zaidi ya computer, vyovyote vile aliamini lazima Erick angemsaliti na hilo huwa hakubaliani nalo hata siku moja
" lest in peace Erick ( pumzika kwa amani Erick) "
David alizungumza maneno hayo huku akiwa anatoa machozi ya hasira iliyochanganyikana na uchungu, mkononi alishika bastola yake aina ya Berreta isiyo na sauti, aliibusu huku akiendelea kuiomba ifanye kazi yake sahihi,japo Erick hakuepo lakini tayari alishapanga kumuua usiku huo huo. Aliwasha gari na kuondoka hotelini hapo akiwa na hasira zisizo elezeka safari yake iliishia mtaa wa uhuru nyuma ya Wande hoteli hapo ndipo Erick alikuwa akiishi zaidi ya dakika 180 alikuwa eneo hilo akiwa anaendelea kuvuta sigara aina ya ESM ndani ya gari la kaka yake.
" safi sana " aliongea peke yake mara baada ya kumuona Erick akija eneo hilo, papo hapo aliichomoa bastola yake iliyokuwa kiunoni , aliikagua kama ilikuwa na risasi, alitabasamu mara baada ya kukutana na risasi tatu alimulenga Erick kichwani ,risasi moja tu ilikimaliza kichwa chake kisha aliondoka eneo hilo bila mtu yeyote kuona hiyo ilisababishwa na hali ya mvua usiku huo. Hakuwa na hofu yeyote dhidi ya vyombo vya dola, zaidi ya viogozi wakubwa walikuwa marafiki zake, pia heshima ya marehemu kaka yake aliitumia kufanyia uovu na uozo uliopindukia.
******
"lete bia hapa wewe kahaba! "
Erick aliongea kwa Sauti ya kilevi iliyochanganyikana na ukali kiasi,
"mshikaji punguza maneno machafu"
" wewe acha kuongea pumba hawa ni mamalaya tu yanat **** ,kila siku "
Erick aliendelea kuporomosha maneno makali dhidi ya wasichana wale hasa hasa akina Dada waliokuwa wamebarikiwa ama kujaliwa makalio makubwa ,hakujali maneno yake kwamba yalikuwa mwiba kwa wengine, yeye aliona kila muhudumu ndani ya kumalija hoteli alikuwa malaya.
 
BLOOD DEAL
Author: Teddy
Cont:0655 202 285.
Whatsapp :0756 202 284
KWA MWENYE UHITAJI WA RIWAYA HII, AWASILIANE NA MWANDISHI KWA NAMBA HIZO JUU.

SEHEMU YA 5

"lete bia hapa wewe kahaba! "
Erick aliongea kwa Sauti ya kilevi iliyochanganyikana na ukali kiasi,
"mshikaji punguza maneno machafu"
" wewe acha kuongea pumba hawa ni mamalaya tu yanat **** ,kila siku "
Erick aliendelea kuporomosha maneno makali dhidi ya wasichana wale hasa hasa akina Dada waliokuwa wamebarikiwa ama kujaliwa makalio makubwa ,hakujali maneno yake kwamba yalikuwa mwiba kwa wengine, yeye aliona kila muhudumu ndani ya kumalija hoteli alikuwa malaya.
Wakiwa wanaendelea kunywa na kutafuna nyama choma ghafla alitokea Diana rafiki yake na Erick, David alipomtazama tu alihisi mapigo ya moyo kuongezeka, kutokana na uzuri wa Diana alianza kutumia nguvu za kumchukua Diana hali hiyo Erick hakukubaliana nayo hivyo nae alianza kumrushia maneno bila kujua kama mwenzake hakuwa mtu wa kawaida hata kidogo
"tena umkome Diana muone kama kituo cha polisi nakuambia hujui tulikotoka "
" wewe unahela gani ya kumpa mtoto mkali Kama huyu, hebu njoo mchumba " aliongea huku akianza kumfuata Diana, alifika na kumkumbatia kwa lazima , mikono yake akipapasa mgongoni kwa Diana aliekuwa ametulia kama maji mtungini, kitendo hicho kilimkera sana Erick alinyanyuka katika hali ya kilevi levi akiwa na chupa mkononi hata kabla hajawafikia vyema aliirusha ile chupa iliyotua vyema kichwani kwa David na kusababisha mpasuko kidogo
" mtu mbaya sana wew izoee familia yako, hapa umefika nitakuua muuaji mkubwa wew "
"Erick!!!!!!!!!? "
"ndio hivyo nakueleza si umezoea kuua wengine kwangu huwezi, nitakuonesha na kesho unaenda kuishi nyuma ya nondo "
Erick alizidi kutoa maneno makali sana yaliyozidi kuukera moyo wa David, tayari ndani kwa ndani alianza kutoa machozi, alihisi moyo wake ukivuja damu, macho yalianza kuona ukungu ukungu achilia mbali nyota nyota zisinzo na idadi, kwa hasira akitoka ndani ya Hoteli akiwa anaendelea kulia kimoyo moyo akimuhurumia Erick .
*****
"Mama naomba uwe makini sana na ba Mdogo "
" kwanini vero? "
Aliuliza Janiphar akiwa anaendelea kupanga panga vitu ndani ya chumba chake
" aaaah! ,basi tu ila nakuomba tu ufanye hivyo laz..... "alishindwa kuendelea baada ya kuhisi nyayo za mtu zikitembea kuja eneo hilo
" aaaah!, shemu nakuona uko.... "
David aliyakatisha maneno yake baada ya kukutana na macho makali kutoka kwa Vero
"wewe mshenzi wewe utanikoma nakuondoa duniani leo "David aliwaza ndani ya moyo wake huku akimtazama Vero macho makali sana.
" niambie shemu najiandaa wiki ijayo niruhusu baadhi ya hofisi ziendelee na kazi na wew utakuwa unasimami nikiwa bado sijaanza kutoka "
"sawa sawa shemu tena itakuwa njema vipi Vero huendi sokoni nataka kukuagiza "
"haendi leo anasafari ya kwenda kwao mara moja "
"aaaah!, sa.. wa ,ataondoka saa ngapi? "
"yuko tayari muda huu huu Dominic ndie anaemchelewasha "
"anaondoka nae ama? " Erick alizidi kupeleleza ili ajue jinsi ya kummaliza Vero kabla hajafungua mdomo wake , japo alikuwa akitumia mdomo kuongea lakini hakiri iliwaza njia ya kummaliza Vero
"atampeleka Buzuruga stendi , kisha ataondoka kwa bus la Zakaria "
Masikini Janiphar hakujua kama alikuwa akimua Vero tena bila huruma.
"oky, Vero nakutakia safari njema yenye mapumziko ya amani ila tutakukumbuka sana "
Vero hakuyajibu maneno hayo maana yalikuwa na ujumbe mzito ila umkiyachukulia poa yalikuwa ya poa tu.
" shemu baadae "
" haya shemu "
"lakini Mama David sio mtu mzuri hata kidogo sikiliza maneno yangu "
Vero alizungumza huku akitia huruma alimuonea huruma tajiri yake , hakujijali yeye maana uwezo wa kupambana na David alikuwa nao, na kilichomuuma zaidi ni poul kitoto kilichokuwa kidogo sana lakini kilikuwa kinapelekwa kubaya kama Mama yake asipokuwa makini
"Vero sipuuzii maneno yako ila David tumefanya nae kazi muda mrefu sana, na tabia yake naijua sio mtu mbaya kama unavyofikiria , istoshe nikimfukuza mapema hii huoni nitamtenga mwanangu na ndugu zake, hapana Vero "
"sawa Mama acha niondoke naona Domi keshafika " aliagana na ndugu waliokuwa bado wapo nyumbani hapo kisha aliondoka
" naomba tupitie barabara ya Igogo kisha tukaikamate ile ya kutoka Shinyanga inayoelekea airport ,tutaiacha baada ya kufika kona ya kuelekea kilimahewa kisha tunaekekea Nyasaka man... "
"sina mafuta ya kuchezea Vero "
"oky niache nichukue pikipiki"
"lakini Mama kadai nikupelekea Buzuruga "
"nifuate nisemacho kama hutaki acha "
Vero alizungumza kwa ukali huku akifungua mlango wa gari akiwa na nia ya kushuka, kabla hajafanya hivyo Dominic alimzuia na kuwasha gari akifuata maelezo ya Vero.
Dakika sirufuri wao kuondoka David nae aliondoa gari lake eneo alilokuwa amejificha akiwafatilia kwa nyuma nyuma huku akiendelea kuwasiliana na vijana wake ambao tayari walikuwa wameshafika Buzuruga stendi.

"Domi hebu simama kwanza "
Vero aliongea huku macho yake yakiwa bado yametazama setimira, kana kwamba alikuwa ameona kitu
"Vero acha usumbufu bhana ndo kwanza dakika kumi tu, toka tumeanza Safari tambua na mambo ya kufanya si kukupeleka wew tu "
Domi alizungumza bila kumtazama usoni, ila muonekano wake tu ulionesha dhahili alikuwa amechukizwa na kitendo kile
"Domi nisikilize kuna kitu sikielewi kabisa "
" kiaje? "
"nahisi nafuatiliwa sasa fanya hivi endesha gari kwa kasi, ukifika pale kwenye kona punguza mimi nitaruka " Vero alizungumza huku akitoa begi lake nyuma ya siti aliyokuwa amekaa, japo kilikuwa kitendo cha hatari sana lakini hakujali bora afe kwa ajali ila si kifo cha mateso kutoka kwa David .
" unajua sikuelewi Vero? "
" utanielewa muda mfupi fuata ninachokuambia Domi "
Japo aliongea lakini macho yake hayakutulia upande mmoja, kila sekunde alitazama nyuma kupitia setimira,
" punguza mwendo Domi "
"unajua u..... "
hata kabla hajamalizia sentesi yake, tayari Vero alikuwa ameshafungua mlango akijilazimisha kuruka ndani ya gari, ilibidi Domi apunguze mwendo akiwa hajui kinachoendelea
" maisha mema Domi, ila nakuomba usimwambie mtu chochote, pia ondoka eneo hili kabla ya David kufika "
"Vero.. Vero sikuelewi jamani "
"ondokaaaaaa "
Aliongea huku akikimbia kuelekea ndani ya makazi ya watu eneo hilo la Igogo sehemu inayosifika kuwa na idadi kubwa ya watu, wenye hali ya chini kabisa ndani ya jiji la mwanza ama unaweza ukapaita uswahini. Kwa kuwa hakukuwa na njia ya moja kwa moja zaidi ya vichochoro chochoro vilivyompa Vero nafasi ya kutokomea ndani ya dakika mbili tu.
"piiiiii!, piiiii!"
Sauti kali na yenye kustua ilimshitua Dominic aliekuwa bado amesimama eneo hilo asijue cha kufanya
".........nakuomba uondoke eneo hili mapema kabla ya David haja.... "
Alijikuta akiyakumbuka maneno ya Vero aliyokuwa amezungumza nae muda mfupi kabla ya kutokomea uswahilini, nae hakutaka kuendelea kusisimama tena eneo hilo wala hakujali mfurulizo wa honi kutoka kwa David aliekuwa akija kwa kasi sana.
"duuu! hatari" David aliongea peke yake huku akizidi kumfukuza Dominic, lakini ajikuta akiambulia patupu hiyo ilisababishwa na uwezo mdogo wa gari lake kupambana na landcurser vus8 aliyokuwa nayo Dominic .
"shitii! mfyuuuuuuuu"
David alijikuta akisonya kwa hasira baada ya kumkosa Dominic , aliupiga ngumi usukani kwa hasira zisizoelezeka, tayari uso wake ulikuwa umeanza kutengeneza matuta matuta, mishipa ya shingo nayo haikuwa nyuma kuisindikiza hasira hiyo, alijihisi joto jepesi jepesi japo ndani ya gari hilo kulikuwa na ac.
" siwezi nikazidiwa ujanja na mafala hao " aliongea huku akiongeza gia, hakiri yake ilishahama tayari. Kutoka Igogo hadi Buzuruga stendi hapakuwa mbali sana ukizingatia mji wa mwanza hauna foleni sana hivyo alijikuta akitumia dakika kumi na tano tu.
"vipi mmemuona? "
"hapana hajafika mtu yeyote,kwani vipi ?"
" vimenitoroka, sasa fanyeni hivi jigaweni kuanzia hapa hadi kisesa hakikisheni kila basi linalopita mnalisimamisha na kulikagua lazima atapatikana tu "
Sawa boss ".
Vijana wale hawakutaka kupoteza muda walitekeleza maelezo hayo kutoka kwa boss wao lakini hadi inaingia usiku Vero ama Dominic hakuonekana, ikambidi David kuahilisha adhima yake na kulejea nyumbani kwake akiwa amekasirika bila kipimo.
*****
Vero alizidi kukimbia bila kutazama nyuma,hakujali michubuko aliyokuwa anaipata pindi alipokuwa akijikwaa, muda mwingine alianguka lakini alinyanyuka na kuendelea kukimbia akizidi kutumbukia ndani ya makazi hayo. Dakika thelathini ndipo aliposimama na kukaa sehemu iliyokuwa imejificha,huku akihema mithili ya mbwa aliekuwa akikimbiza mwizi,
" sasa nitetokaje ndani ya mji huu? ,au eeeeh! "aliwaza peke yake huku akisimama tayari alikuwa ameshapata wazo la kutoka mwanza akiwa salama, hofu tena ya kukamatwa na David ilikuwa imetoweka kivyovyote vile asingeweza kumpata uchochoroni humo . Alinyanyuka na kujipangusa vumbi lililokuwa limeushambulia mwili wake kisha alinyanyua begi lake alijitwika na kuanza kusonga mbele bila kufahamu ni wapi angetokea, zaidi ya saa moja alitumia kutembea bila kuona barabara yeyote zaidi ya vichochoro
"hujambo mtoto mzuri "
"sijambo shikamoo dada "
"mar -haba , hivi hii njia inaelekea wapi? "
Vero aliuliza huku akiwa amesimama mzigo kichwani
"kwani wew unaenda wapi? "
"nataka barabara kubwa ya kwenda nyegezi stendi "
"ooooh!, umepitiliza njoo nikuoneshe, kwanza umeshafika kona ya butimba "
Kile kitoto cha kiume kilichokadiriwa kuwa na miaka saba ama nane kilimuonesha Vero njia ya kutokea kona ya butimba, kichwani akiwa na dhamira ya kwenda Kwao akipitia barabara ya busangala.
Baada ya kupata maelekezo hayo alikapatia noti ya shilingi mia tano kama ishara ya shukurani, kweli kalifurahi sana na kumuombea safari Norma, dakika tatu tu alijikuta alitokea barabarani hapo alipochukua daladala hadi Nyegezi stendi kisha alitafuta usafiri uliompeleka busangala, alishuka hapo na kugojea usafiri wa aina yeyote utakaompeleka Bunda , bahati ilikuwa yake ndani ya dakika kumi alipata lori lililokuwa likielekea Musoma, Vero alishukuru sana pia alijipa ushindi wa kutoka ndani ya jiji la mwanza akiwa salama.
 
BLOOD DEAL
Author: Teddy
Cont:0655 202 285.
Whatsapp :0756 202 284
KWA MWENYE UHITAJI WA RIWAYA HII, AWASILIANE NA MWANDISHI KWA NAMBA HIZO JUU.

SEHEMU YA 6

Baada ya kupata maelekezo hayo alikapatia noti ya shilingi mia tano kama ishara ya shukurani, kweli kalifurahi sana na kumuombea safari Norma, dakika tatu tu alijikuta alitokea barabarani hapo alipochukua daladala hadi Nyegezi stendi kisha alitafuta usafiri uliompeleka busangala, alishuka hapo na kugojea usafiri wa aina yeyote utakaompeleka Bunda , bahati ilikuwa yake ndani ya dakika kumi alipata lori lililokuwa likielekea Musoma, Vero alishukuru sana pia alijipa ushindi wa kutoka ndani ya jiji la mwanza akiwa salama.
"kaka ahsanteni sana mungu awabariki "
"usijali Dada "
Aliwashukuru vijana wale kwa msaada waliompatia kutoka Busangala hadi kona ya kwenda Tarime bila malipo yeyote
"je nitapata usafiri kweli? "
"aaaaah! mapema hii ,bando kuna basi la Zakaria linalotoka mwanza saa kumi na mbili na la kutoka Musoma kwenda Tarime halijapita ondoa wasiwasi dada ".
Baada ya mazungumzo hayo Vero alishuka ndani ya lori hilo na kutafuta sehemu ya wazi, alikaa, huku akiendelea kuwatazama wafanyabiashara wadogo wadogo waliokuwa wakifanyaka biashara eneo hilo .
"Tarime tarime elfu tano "
Sauti ya konda ndiyo iliyomsitua Vero kutoka katika lindi la mawazo alinyanyuka na kuelekea ndani ya basi huku akiwa haamini kama kweli alikuwa amesalimika.
*****
Usiku mzima David hakupata lepe la usingizi hata kidogo zaidi ya kujigeuza kila upande wa ubavu wake, hali ilipozidi kuwa mbaya zaidi alinyanyuka kitandani hapo na kuelekea sebuleni, kilichokuwa kikimuumiza zaidi ni jinsi ya kumpata Vero, uwepo wake duniani ungechangia yeye kutopata kile alichokuwa amekisudia
"nitakamalizaje? "
David alizidi kuongea peke yake huku akiwasha television usiku huo wa saa tisa , japo macho yalikuwa yakiitazama television hiyo lakini mawazo hayakuepo hata kidogo,
"acha niongee na Deus atajua nini cha kunishauri ".
Aliongea huku akinyanyuka kitini hapo ,alielekea chumbani kuifuata simu yake ili aongee na Deus mwananaume aliemfundisha kazi ya ujambazi, pia Deus huyo huyo alikuwa rafiki wa kaka yake Emanuel lakini walikosana baada ya Deus kumzurumu Emanuel kiasi kikubwa cha pesa.
"niambie kaka? "
Upande wa pili ulisikika ukiongea baada ya simu kupokelewa
"si kama nilivyokueleza mchana kaka kile kimalaya kimenipotea sasa nahofia usalama mjomba "
"hahahaha kweli wew hujakomaa , lala kesho njoo hofisi nikupe njia "
Deus alizungumza hayo kisha alikata simu, akimuacha David njia panda.

David alibaki ameishikilia simu sikioni kana kwamba alikuwa bado anaongea na mtu ,zaidi ya dakika tatu alikuwa bado yuko katika hali hiyo hiyo.
"puuuuu! ".
Alishusha pumzi ndefu kisha aliutoa mkono wake, alichukua rimoti na kuizima television, taratibu alianza kutembea kuelekea chumbani kwake akiwa bado amechanganyikiwa, hakujua ni kipi Deus angeenda kuongea nae hiyo asubuhi tarajiwa ,alifika na kujitupia kitandani huku sendozi zikiwa bado miguuni, macho yake yaliendelea kulitazama dari, kila alilowaza halikufanya kazi muda mwingine alitamani kulia lakini alishindwa .
" au nikifuate kijijini kwao?, ila sipafahamu! "swali na jibu alilipata yeye, hadi inaingia saa kumi na mbili asubuhi hakuwa amepata usingizi, aliamka na kuelekea bafuni alionga kisha alielekea jikoni alikoandaa chai, baada ya kuvaa alilejea na kukuta chai ikiwa tayari, hakutaka kuelekea kokote pale pale jikoni ndiko alikonywea chai na kipande kimoja cha mkate.
" Baba uko hofisini kwako? "
aliuliza David huku akiingia ndani ya gari lake
"aaaah dogo mie hadi muda huu niwe sijafungua hofisi, nina pesa gani, ninyi ndo wenye utajiri sema mnauchezea "
"hahahaha, una masihara mtoto wa kasuru wewe, unatafuta pesa kama mchanga ?"
"nimetoka kigoma kutafuta pesa sio kushangaa rami, kata simu njoo "
"poa kaka dakika ishirini ".
"puuuuu! "David alishusha pumzi ndefu kisha alichomeka funguo wa gari na kuwasha, Safari ya kuelekea hofisini kwa Deus hofisi zilizokuwa mtaaa wa rumumba katikati ya jiji la mwanza ilianza, njiani alikuwa na mawazo chungu nzima, zaidi na zaidi alimuwazia Deus, hakumuelewa mtu huyu japo walikuwa marafiki wa muda mrefu sana lakini hakuwa akimfahamu zaidi, alikuwa na pesa nyingi sana lakini kilichokuwa kikimshangaza zaidi ni tabia ya rafiki yake huyo kufungua hofisi yake asubuhi ya saa kumi na moja, huku wafanyakazi wake wakiingia kuanzia saa moja na robo hadi saa mbili.
"kila mtu na maisha yake bhana kivyake "ilibidi David ayapuuzie mawazo yake yaliyokuwa yakimuumiza bila kupata jibu, mji wa mwanza hauna foleni sana na hata ikiwepo huwezi tumia muda mrefu sana barabarani, David alijikuta akitumia dakika arobani tu kufika hofisini hapo akitokea pansiasi soko jipya huko ndiko alikokuwa amejengewa na kaka yake marehemu Emanuel.
"habari yako dada "
"nzuri,mambo kaka "
"safi tu sijui boss yupo? " David aliuliza baada ya kufika hofisini hapo, japo alikuwa akifahamu uwepo wa Deus, lakini alitaka kujihakikisha zaidi.
" yupo tena huyooo aaah! "
Dada aliekuwa akifanya kazi ya ulinzi hofisini hapo nyakati za usiku aliongea huku akiendelea kunywa kahawa, modomo ukiwa umejaa tabasamu tele , kwa kuwa David hakuwa mgeni hofisini hapo mara moja akipandisha ngazi kuelekea hofisini humo.
"aaah! Kaka niambie,"
"safi tu, karibu dogo nipe michakato"
Deus aliongea huku akimimina kawa ndani ya kikombe kidogo na kumkabidhi David alieipokea kwa mkono wa kushoto, na kunywa fundo moja, kabla ya kukaa, alikiweka mezani kikombe hicho, akinyosha mkono kusalimiana na Deus.
"eeeh!, leta habari bwana mdogo "
"sina mengi ni kuhusu kile kitoto"
"aaah hicho achana nacho, hakiwezi kuongea chochote, kwanza kishamba kipotezee, fuata taratibu ya pili ambayo ni ya muhimu zaidi na ndo itakayokupa maisha sawa dogo"
"nakuelewa ila... "
"toa neno ila David, kama uliweza kumuua fala utawezaje kukimalizi hiki kidogo ,ondoa mawazo fanya kazi, "
"basi sawa "
******
Baada ya wiki tatu hofisi zote za marehemu Emanuel zilikuwa zikiendelea kufanya kazi zikiwa chini ya usimamizi wa David kwa huo muda mfupi, hakuwa na roho mbaya kama kipindi cha mwanzo enzi ya uhai wa kaka yake, hali hiyo Iliwashangaza baadhi ya wafanyakazi ndani ya hofisi hizo tatu mbili zikiwa za usafirishaji na moja ikijihusisha na mitandao achilia mbali hoteli na maduka ya nafaka pamoja na ya simu, ilikuwa ni lazima jioni apite kila hofisi kuangalia biashara ilikwendaje, hali hiyo ilianza kuibadili hakiri yake, tamaa mbaya ikaanza tena kuuandama ubongo wake dhidi ya shemeji yake.
"babu shukamoo "
"Mar haba mjukuu wangu vipi ulifanikisha? "
"ndio babu ila natatizo tena "
"niambie nitakusaidia "
"nataka kukamaliza katoto ,ila kwa njia ya ajari, huwa kinakwenda shule kwa gari je babu unaweza ukanitengenezea ajari katika mambo yako ".
David aliongea bila huruma usiku huo baada ya kutoka kazini, hakuwa na hofu na mganga wake mwenyeji wa kasuru mkoa wa kigoma, mzee huyo alikuwa akifahamika Kwa jina la Songoro aliekuwa amejaliwa ujuzi mkubwa katika ulozi, na ndo huyo huyo aliempatia David dawa za kujikinga endapo yangetokea ya kutokea baada ya kumua kaka yake.
"usijali mjukuu nitumie picha yake ndani ya siku moja " aliongea mganga huyo kwa kujiamini
"sawa nitaituma kesho mchana "
David alikata simu ,alipiga makofi ya ushindi, picha ya poul mtoto wa kaka yake aliekuwa ndani ya jeneza ilianza kupita ndani ya ubogo wake.
Kwa kuwa hakuwa na picha yeyote ya mtoto huyo ndani ya nyumba yake alipanga kesho kwenda nyumbani kwao kuchukua picha hiyo ili akamilishe mambo yake.

kichwa chake kiliendelea kuwaza mambo mengi sana , taswila ya kumiliki utajiri tayari ilianza kupita ndani ya ubongo wake ,alijiona jinsi anavyomiliki utajiri huo, akiwa kama boss, hakika David alikuwa duniani nyingine kabisa! Hakutaka kulala mapema alichofanya ni kwenda kuonga kisha alivaa pensi yeusi ya jinsi , tsheti nyeupe aliyoiambatanisha na marashi aina ya blue men, alichukua saa na kuitazama.
"aaah! Bado mapema sana , acha nimtafute salama " David aliwaza huku akifunga mlango , Safari yake iliishia katika gari lake aina ya Rav4 ,alibinya ufunguo kabla ya kuingia lilifunguka kisha alifungua na kuingia.
"Salamaa mtoto wa kimanga njoo Villa tutafune duniaa "
David aliongea baada ya simu kupokelewa, upande wa pili, katika wanawake David aliokuwa akiwakubali Salama alikuewemo, kwanza alijua kutumia pesa, pili alijipenda, hakuwa mtu wa mariongo ,alijariwa umbo zuri ambalo kila mwanaume aliepita mbele yake lazima shingo igeuke , sauti yake tu ilikuwa na uwezo wa kumtoa nyoka pangoni , kitandani usiniulize.
Kutoka pansiasi hadi Villa hakukuwa mbali sana na ukizingatia usiku hakuna foleni, alijikuta akitumia dakika saba tu, akawa ameegesha gari lake,sehemu sahihi, hakuta kushuka haraka, alichofanya alikiegemeza kichwa chake, juu ya kiti baada ya kukikunjua, alifungua radio pole pole alianza kusikiliza mziki huku akiendelea kumsubili Salama.
"khoook!Khoook!"
Sauti ya kugongwa kwa dirisha la gari lake ndio iliyomshtua David, hakuwa na haraka sana maana alijua ni Salama tu ,kweli mawazo yake hayakukosea alimfungulia mlango.
"niambie mme wa mie "
Salama alizungumza huku akimbusu David mdomo, nae hakuwa nyuma alimpokea kwa mikono miwili
"leo kula pesa yangu kadri unavyojua, jichetue ujuavyo linga mtoto wa kike" David alizungumza hayo baada ya wote kuachiana, hakutaka kukaa sana ndani ya gari,walishuka na kuingia ndani ya Club hiyo, ambayo ni maarufu na ni pendwa kwa wakazi wa mji wa mwanza.
 
BLOOD DEAL
Author: Teddy
Cont:0655 202 285.
Whatsapp :0756 202 284
KWA MWENYE UHITAJI WA RIWAYA HII, AWASILIANE NA MWANDISHI KWA NAMBA HIZO JUU.

SEHEMU YA 7

"khoook!Khoook!"
Sauti ya kugongwa kwa dirisha la gari lake ndio iliyomshtua David, hakuwa na haraka sana maana alijua ni Salama tu ,kweli mawazo yake hayakukosea alimfungulia mlango.
"niambie mme wa mie "
Salama alizungumza huku akimbusu David mdomo, nae hakuwa nyuma alimpokea kwa mikono miwili
"leo kula pesa yangu kadri unavyojua, jichetue ujuavyo linga mtoto wa kike" David alizungumza hayo baada ya wote kuachiana, hakutaka kukaa sana ndani ya gari,walishuka na kuingia ndani ya Club hiyo, ambayo ni maarufu na ni pendwa kwa wakazi wa mji wa mwanza.
Saa kumi na moja alfajili ndipo walipotoka ndani ya club hiyo, David alimpitisha Salama nyumbani kwao kisha alielekea kwake!,Kwa kuwa ilikuwa jumapili, hakuwa na haja ya kuamka mapema sana, alilala hadi saa sita mchana, kisha alielekea nyumbani kwa marehemu kaka yake, kichwani akiwa na lengo la kupata picha ya Poul kwa njia yeyote.
"waaooooo Baba shikamooo "
"mar -haba hujambo mzee wetu "
David alijibu salamu hiyo huku akimnyanyua kutoka chini na kumpakata, kisha alianza kuelekea ndani.
"Safi sana umekwisha! " Alijikuta akiwaza maneno hayo huku macho yake yakimtazama mtoto Poul aliekuwa amejawa na tabasamu usoni mwake, laiti angefahamu huyo alikuwa adui yake namba moja duniani, asigedhubutu kumsogelea,
"Mama yuko wapi? "
"Kalala "
"aaaah!, Kamwambie nimekuja "
"sawa "
Poul aliondoka eneo hilo akikimbia kuelekea ndani, huku nyuma, David akimtazama kwa uchu kana kwamba alikuwa akitamani kumtafuna mbichi mbichi!. Akiwa katika lundo la mawazo Janiphar shemeji yake alitokea sebuleni hapo.
"nakuona mke mwema "
"shemu huuishiwi na maneno " Janiphar aliongea huku akikaa na kumpakata mwanae.
"Unajua nataka nikuridhi, hahahaha! "
David alichomeka utani hali iliyopelekea wote kucheka kwa furaha, ili asijulikane adhima yake, alishinda hapo siku nzima huku tayari akiwa amefanikiwa kuchukua picha ya Poul, kupitia simu yake ya mkononi.Safari yake ilianzia studio iliyopo karibu kabisa na sheli ya moili raundi abauti ya mwalimu Nyerere, mkakabala na benki ya stabick.
"Babu kila kitu kipo tayari, na nimeituma kabisa ipokee kesho katika basi la Zuberi "
David aliongea baada ya kukamilisha zoezi la uchapishaji wa picha hiyo, kisha alielekea hofisi za mabasi yaliyokuwa yakienda kigoma, mtaa wa natta barabara ya Igoma.
"Sawa babu kesho kutwa utaona jibu, si tayari na majina yake umeyaandika kama nilivyokueleza? "
"Ndio! "
"Tegemea ushindi, mjukuu wangu "
"nitafurahi sana babu! "
"Lazima ufurahi "
"hahahaha! "
David alimalizia kwa cheko, kubwa na lenye ushindi mkubwa ndani yake, siku hiyo hakutaka kwenda kokote, kutokana na uchovu wa jana aliamua kwenda nyumbani kwake moja kwa moja bila kumpitia msichana yeyote.
******
"Mama leo siendi shule "
Kwanini Poul? "
Mama yake alimuuliza huku akiendelea kunyosha nguo za shule za mwanae, asubuhi ya jumanne.
"sitaki tu nimemkubuka Baba, harafu hutaki kuniambia baba yuko wapi? "
"Puuuuh!,
Mama yake alishusha pumzi ndefu, kisha aliichomoa pasi kwenye soketi na kumsogelea mtoto wake ,aliekuwa amelala chali macho yakimtazama Mama yake.
"Nikweli mwanangu, naomba uende shule ukirudi tu nitakuelezea kuhusu Baba atarudi lini, sawa Baba? "
Japo Janiphar alizungumza maneno hayo, huku akitoa tabasamu, tabasamu hilo lilikuwa la bandia tu , moyoni aliumia alihisi moyo ukivuja damu, lakini hakutakiwa kumuonesha picha hiyo mwanae.
"Kweli Mama na utanipeleka? "
"Ndio, ni.... nit.. akupe.... leka "
Alijikuta akishindwa kuongea vizuri, baada ya kukabwa na kitu kizito kooni.
"Naenda kuoga mwenyewe leo "
Poul alizungumza huku akitupa pembeni shuka, alivua pensi na kujifunga taulo la Baba yake , vitendo vyote hivyo mama yake alikuwa akivitazama tu, ila kilichomuhuzunisha zaidi ni kitendo cha mwanae kujifunga taulo la mmewe, chozi jembamba lilianza kutiririka na kulowanisha kope zake.
"Masomo mema baba "
"haya Mama, nikirudi unaniambia sawa? "
Mtoto Poul aliongea, maneno hayo huku akimbusu mama yake mkononi, kisha alipanda ndani ya school bus, safari ya kuelekea Alliance international school ilianza. Hadi bus hilo linapotea machoni mwake Janiphar alikuwa bado ameganda eneo hilo akiyatafakari maneno ya mwanae!, Taratibu alianza kuondoka eneo hilo kwa unyonge usioelezekea, hofu kubwa ikaanza kuushambulia moyo wake, mawazo mabaya kwa mwanae yakaanza kupita ndani ya kichwa chake.
"Kunanini? "
"Kwani vipi Mama? "
Janiphar alijikuta akishtuka ,baada ya kuulizwa swali hilo na Mama mkwe wake ambaye alikuwa bado nyumbani hapo pamoja na baadhi ya ndugu wengine. Alibaki ameduwaa asijue cha kuongea, hata hakujua amefikaje sebuleni hapo, alichokuwa akikikumbuka ni uwepo wa yeye barabarani, sasa ndani humo ameingiaje?, nani aliemfungulia geti?.
Kutokana na mawazo mengi kumzidia alijikuta akitembea bila kujua.
"Tuambie mama tatizo nini? "
Mama mkwe aliendelea kumdadisi baada ya kumuona amebadirika ghafla,
"hata sijui nasikia moyo ukiniuma sana "
"Pole sana mama punguza mawazo mwanangu "
Mkwe wake alisema hayo huku akimkalisha chini.
"Griiiiiii! Griii"
Mlio wa simu ya Janiphar ndio uliowashtua wote , haraka bila kuchelewa aliichukua kutoka juu ya meza, alimwangalia mpigaji, lahaullaa! Alihisi moyo ukichomoka ndani ya kifua chake, baada ya kukuta jina la dereva wa poul, hakuweza kuipokea simu hiyo kutokana na mikono kutetemeka, moyo ukienda mbio, taarifa za habari mbaya zilianza kujitengeneza ndani ya hakiri yake, iliita hadi ilikatika yenyewe.
"Mama mbona hujapokea si... ?"
Hakumalizia , mara simu iliita tena, mama mkwe ilibidi aichukue na kubofya kitufe cha kupokelea, kisha aliiweka sikioni.
"Halo! "
"Kuna tatizo limeji.... "
Hakuweza kumalizia alikatishwa
"nini? "
"Ndio, tumepata ajari hapa Natta, mtoto wenu ame.... "
"mamamamamamama weeeee Poul mwanang... "
Mama mkwe alishindwa hata kusikiliza vizuri, alijikuta akilia kwa sauti ya juu, hali hiyo ilipelekea kila mtu kuacha kile alichokuwa akikifanya, kelele za vilio zianza kusikika ndani ya nyumba hiyo, kila mtu alijua Poul amefariki, Mama yake tayari alikuwa ameshazimia ,alijuta kumlazimisha mwanae kwenda shule, laiti angemsikiliza yote hayo yasingetokea.
Ilibidi dereva wa familia hiyo aliekuwa akifahamika kwa jina la Dominic, atoke nje akiwa na simu ya boss wake, ndani hapakufa tena, alitafuta namba za Dereva huyo katika kitabu cha namba, huku akitetemeka alitafuta jina hilo na kupiga kabla ya kuweka sikioni.
"Niambie mwanangu Poul amekufa?"
Domi aliuliza huku naye akilengwa lengwa na machozi, miguu ikikosa nguvu,
"hajafa ila yupo hospitali ya Aghakhan hali yake mbaya sana, katika wote yeye ndie alieumia sana"
Dereva aliongea huku akitetemeka kupita maelezo,
"daaaah! Ilikuwaje mwanangu? "
"Hata sijui lori lilitokea wapi?, nimeingia freshi barabara ya Igoma, ghafla lori lilitoea ubavuni na kunigonga kwa nyuma hali iliyopelekea bus letu kuanguka, huku Poul akikandamizwa na kiti kifuani ."
Alitoa Maelezo hayo kisha alikata simu.
"Jamani Poul hajafa yuko Aghakhan, twendeni "
Hakuna alietaka kubaki nyumbani hapo, kwa masada wa ndugu Janiphar alisaidiwa kutembea, kuelekea kule gari lilikuwa limepakiwa.
Kweli walifanikiwa kumkuta Poul akiwa katika hali mbaya sana, mwili wake karibia wote ulijaa madonda, jinsi alivyokuwa akitisha haikuwa rahisi, kuamini kama alikuwa mzima,
Ilibidi wakae kidogo kusubili majibu ya daktari, nusu saa waliweza kuonana nae, aliwapa matumaini ya mwanao kupona japo alikuwa ameumia sana kifuani , kisha wengine waliondoka wakimuacha Mama yake na Bibi yake kumuangalia.
*****
Kazi ya kutengeneza ajari ya kiini macho haikuwa ngumu sana kwa mzee Songoro, baada ya kuipokea picha hiyo majira ya saa mbili usiku, hakutaka kulala , aliichukua na kuitumbukiza ndani ya dawa nyeusi, huku akizunguka zunguka eneo hilo, mkononi alishika usinga mweusi, dakika tano aliitoka na kuiweka ndani ya ungo uliokuwa umejaa kila aina ya dawa, alileta kioo kilichokuwa kimevikwa kitambaa chekundu na cheupe nacho alikitumbukiza ndani ya ungo huo, alichukua dawa iliyokuwa na asili ya kimiminika, kidogo alimimina ndani ya kiganja chake na kukipakaza kioo hicho kwa juu huku chini yake akiwa amekandamiza picha ya Poul, vitendo hivyo viliambatana na maneno aliyokuwa akiyatamka kumuita Poul.
Dakika saba, sura ya mtoto Poul ilitokea juu ya uso wa kioo, hapo hapo aliachia tabasamu, alichukua dawa nyeupe na kuipaka sura hiyo, dawa hiyo ilimsaidia kuyatambua majina yote ya koo mbili ,kwa Mama na kwa baba, akiwa katika zoezi hilo ghafla yalitokea majina yote, hivyo akawa ameimchoma kisu kikali picha ya Poul sehemu ya kifua.
Baada ya zoezi hilo alichukua, ile picha na kuifunga ndani ya karatasi kisha aliweka tena, juu ya kioo na kuanza kuongea maneno yake, mara juu ya kioo ilianza kuonekana school bus ya akina Poul, hapo hapo alianza kutengeza ajari ,kwanza alitengeneza eneo sahihi la ajari itakapotokea, akimpiga upofu dereva, baadae alichomeka lori feki litakalo ingonga gari la shule. Hakutaka kulala aliondoka kigoma usiku huo hadi jijini mwanza akiwa ndani ya umbo la bundi, safari yake ilianzia Natta alipopawagia, kisha alienda kuliwangia school bus na hata kiti alichota mtoto Poul kukaa alikiwangia, akiuchochochea moyo wake kukaa pale pale.
"nimemaliza subili matokea kesho! "
"Kweli mzee? "
David aliuliza kwa shauku ya hali ya juu, hakuamini kama kazi hiyo ingekuwa rahisi kiasi hicho . Furaha ilizidi kuongezeka kadri muda ulivyokuwa ukiyoyoma, hakuweza kupata usingizi mapema hadi jongoo wa kwanza kuwika alikuwa macho , saa kumi na nusu ndipo alipopitiwa na usingizi, alikuja kushituka jua likiwa limechomoza.
"acha nimpigie Baba simu, najua ataniambia tu "aliwaza hayo huku akiiangalia saa iliyokuwa ikionesha saa mbili na nusu asubuhi.
"Shikamo Baba "
David alisalimia baada ya simu kupokelewa, sauti yake tu ilionesha hali mbaya
"vipi mzee mbona unaongea kinyonge hivyo? "
David aliuliza swali hilo ma kusudi ila tayari alikuwa ameshaanza kuhisi jambo.
"Poul amepata ajali hali yake mbaya sana, kaumia kifuani ya... "
Mzee huyo alishindwa kuongea vizuri, maumivu ya kuondokewa kwa mwanae yalikuwa bado yakiisumbua hakiri yake, leo tena mjukuu wa pekee alieridhi jina lake nae amepata tatizo kubwa, na linaweza kupelekea kupoteza maisha yake! Kweli alikuwa na haki ya kulia.
"Pole sana Baba je yuko wapi kwa sasa?".
Aliuliza David huku akiwa amechanganyikiwa, hakupendezwa na taarifa hizo, alichotaka yeye ni kusikia taarifa ya kifo si majeruhi.
"nitaenda kuongea na daktari "
Aliwaza hayo huku akinyanyuka kitandani.
 
BLOOD DEAL
Author: Teddy
Cont:0655 202 285.
Whatsapp :0756 202 284
KWA MWENYE UHITAJI WA RIWAYA HII, AWASILIANE NA MWANDISHI KWA NAMBA HIZO JUU.

SEHEMU YA 8

Ilikotoka....

Ajali ya kiini macho iliyotengenezwa na mganga Songoro toka Kigoma, inatokea maeneo ya Natta barabara ya Igoma, mtoto Pool anaumia vibaya Sana, hali inayopelekea alazwa ndani ya hospitali ya Aghakhan mita chache kutoka eneo la ajali ilipotokea, taarifa hizo zinamfukia David baba mdogo ya Poul anaeumizwa sana na kitendo hicho kwani yeye alitarajia kusikia habari ya msiba lakini si, habari ya majeruhi, anapanga moyoni Kuzungumza na daktari.Je nini kitatoea?.

SONGA NAYO.

Alibaki ameduwaa kama dakika tano baada ya kukata simu, taarifa za kujeruhiwa kwa mtoto Poul hazikukaa vyema ndani ya mtima wake, pamoja na kichwani, alichokuwa akifikiria yeye ni kifo tu! Si majeruhi.
"Nitaongea na dokta ".
Alizidi kuisistiza kauri yake, hakutaka tena kulala, alinyanyuka na kuelekea bafuni alikokoga haraka haraka na kutoka, alivaa vazi la kinaijeria alilowahi kununuliwa na kaka yake pindi alipohitimu shahada ya biashara, miaka miwili iliyopita.
"sijui nianzie hofisini? Au acha nielekee hospitali. "
Njia nzima aliongea peke yake, muda mwingine aliweza kutoa maneno ya kashfa pindi alipokwaruzwa kidogo, hakuwa David wa siku zote, hasira alizokuwa nazo dhidi ya Poul hazikuelezeka.
"Shikamoo mama "
"mar haba, kwema huko? "
"Kwema tu, vipi anaendeleaje? "
David aliuliza huku usoni akiweka huzuni ya bandia, baada ya kufika hospitalini hapo,
"Bado mtoto kaumia vibaya sana, lakini majibu ya daktari yanatushangaza!"
"Kwani vipi? "
"Inaonekana hajaumia kokote, wakati yupo katika hali mbaya sana, kila kipimo alichofanyiwa hakuna tatizo, Chest T-scan nayo wamefanya kuangalia kama kuna mfupa uliovunjika ama la, jibu hakuna, hakuna damu iliyovujia kwa ndani, hata hatuelewi "
Aliongea bibi yake Poul kwa majonzi makubwa.
"Mama yake yuko wapi "
Alioneshwa na kuelekea eneo alilokuwa Janiphar, waliongea mawili matatu kisha aliomba kumuona mtoto aliekuwa Icu, kwakuwa ilikuwa hospitali binafsi hakukuwa na pingamizi. Macho yake yalikereka sana kumkuta Poul akiwa hai japo alikuwa akipumlia mashine ya oxygen, dripu za maji na damu zikiendelea kuingia ndani ya mwili wake, wa kitoto kupitia mishapa ya damu .
"Pole sana shemeji, mungu atatusimamia, je kuna daktari yeyote aliechukua jukumu la kumhudumia?"
Aliuliza David, wakiwa wanatembea kutoka ndani ya wodi hiyo
"ndio nimemkabidhi kwa Dokta Atanasi rafiki mkubwa wa marehemu mme wangu, najua hataniangusha "
"aaaah! Kwe..kweli, umefanya vyema " alijikuta akipata kigugumizi cha ghafla mara baada ya kusikia njina hilo.
Dokta Atanasi alikuwa rafiki mkubwa sana na marehemu Emanuel , urafi wao ulizaliwa siku ambayo mzee Poul ,Baba mzazi wa marehemu Emanuel na David, alipougua ghafla presha ya kupanda, majira ya sasa mbili usiku, wakiwa ndani ya gari wakielekea nyumbani. Japo Dk. Atanasi alikuwa bingwa wa upasuaji, alijikuta akiwaonea huruma kutokana na hali mbaya akiyokuwa nayo mzee huyo, alichofanya usiku huo huo alimpingia simu Dk. Andrew akimsistiza kufika hospitali hapo, ilikuwa ngumu sana kwa Dk. Andrew kufika hospitali hapo usiku huo, ukizingatia tayari alikuwa amelala, kitendo hicho kilimfanya Emanuel kuwa karibu sana na Dk. Atanasi kwa muda wote aliokuwa amelazwa mzee wake hospitalini hapo.Hata baada ya kuagwa Emanuel hakusita kumsalimia japo kwa simu na muda mwingine waliweza kukutana na kuzungumza.
Taarifa za kukabidhiwa mtoto huyo kwa Dokta huyo, hazikumfurahisha David hata kidogo, toka uhai wa kaka yake, David na Dk. Atanasi walikuwa paka na panya kisa kikiwa msichana, japo Dk. Atanasi alikuwa ameoa lakini michepuko haikukosekana na mbaya zaidi aliwahi kuchepuka na msichana wa David aliemtoa kijijini kwao Simiyu. David alibaki na hasira hiyo hadi leo, hakuwa na roho ya kusamehe.
"nifanyeje? "
Alijikuta akiwaza peke yake, lakini hakupata jibu, ghafla alitoka ndani ya hospitali hiyo kwa kasi ya ajabu, lakini kabla hajatoka nje ya geti, alikutana na kijana, mwembamba na mrefu, macho yake yalipendezwa sana na sura ya kijana huyo, alionekana ni mwanafunzi wa udaktari, japo alikuwa mwanafunzi akiekuwa akisomea udaktari ,pia alionekana wa hali ya chini sana, hata mavazi yake tu yalitosha kumtambulisha haiba yake,
"yes (ndio) nitamtumia huyu huyu! "
David alijisemea peke yake, kisha aligeuka na kuanza kumfuata,
"samahani Dokta "
"bila samahani ndugu "
"sijui naweza kuongea na wew? "
David aliongea huku akiwa amemkazia macho, alichongundua haraka sana kutoka kwa Daktari huyo alikuwa akisumbuliwa na njaa, pamoja na mawazo yaliyopelekea kuonekana kijana kama mwanzo alivyomtazama, kumbe hakuwa kijana wala mwanafunzi, ila ukata ulimfanya apoteze hadhi yake.
"kwa sasa sina muda, nipe dakika ishilini nitakutafuta baada ya kutoka kunywa chai "
"aaah! Ingekuwa vyema sote tungeambatana, maana hata mie sijapata huduma hiyo "David aliongea huku akiachia tabasamu, uso wake akiupamba kwa furaha ya ulaghai laghai.
"mie naenda kunywa chai ya hofisi ina... "
"aaaah! Dokta heshima yote hiyo bado unakunywa chai ile ile ya mandazi ya mia na vitumbua vya mamantilie jamaniii "
"hahahaha (alicheka kwa aibu ),heshima wapi kaka njaa tupu "
Nae alijaribu kuongea huku akibandika tabasamu usoni, ambalo David alilitambua haraka sana.
"wew wa kunywa supu, bhana twende " aliongea huku akianza kuondoka eneo hilo, akimuacha Dokta huyo akijishauri, mita chache David aligeuza Shingo na kumtazama Dokta huyo, nae kuona vile alianza kumfuata.
"Hapa hapa! " Aliwaza hayo huku akimfungulia Daktari huyo mlango, kisha nae alizunguka upande wake
"nimesahau nikatoka na koti hili "
"unaweza ukalivua, wala usijali "
Hakuna alieongea tena, hadi gari hilo linafunga breki ndani ya maengesho ya Glod crest hoteli, mkabara na mwanza hoteli, walishuka na kuingia ndani.
"Agiza unachotaka, mie nipe maji makubwa ya Kilimanjaro na supu ya mbuzi bila chochote ".
Nusu saa tayari walikuwa wameshamaliza kunywa supu, Safari ya kulejea hospitali ilianza, lakina kabla hawajafika hospitalini hapo, David aliegesha gari lake na kumtazama Dokta huyo, alieonekana bado anasumbuliwa na kitu flani
"naitwa David naishi pansias , kazi yangu biashara , sijui unaitwa Dokta nani? "
"Dokta Eddyson Swai, mwenyeji wa mkoa wa moshi, kwa hapa mwanza naishi Nyakabungo "
"haaaaa! Dokta? "
David alishangaa, hadi alishika kichwa, hakuamini ,Kama Daktari huyo anaweza kuishi eneo hilo, Nyakabungo ilisadikiwa kuwa ni mtaa uliojaa vibaka si mchana wala usiku, uswahili uliopitiliza na sifa nyingine ni idadi kubwa ya kabila la wakurya, ambao husemekana ni wakorofi kupita maelezo , zaidi na zaidi hakukuwa na majengo mazuri zaidi ya vijumba vidogo na vifupi, vilivyojengwa bila utaratibu ,kwa wakazi wa mwanza Nyakabungo ilitambulika kama ushashini.
"Nini?"
"wewe wa kuishi Nyakabungo? "
"Eeeh !"
"Hapana, naomba nikupatie nyumba ya kuishi, iko Nyakato National kama utakuwa tayari, na je umeoa? " Safari hii aliongea kwa upole na umakini wa hali ya juu , alikuwa na kazi moja tu, ya kumrubuni Dokta huyo, kwa kutumia umasikini wake ama tamaa ya pesa, angeweza kufanikisha adhima yake.
"Ndio namke na watoto wanne, pia nipo tayari kupokea msaada huo " alizungumza kwa sauti ya chini, yenye asili ya kukata tamaa kabisa.
"Hata leo naweza kukupa nyumba hiyo endapo utanisaidia nami kitu kidogo " David alizungumza bila kumtazama
"nini hicho? Nitakusaidia, maana hata wewe umenisaidia pia "
"ok sawa, je upo Aghakhan kwa muda gani? "
"Miezi ishirini na sita sasa "
"sawa mshahara unalipwa bei gani? "
Dk. Eddyson alijikuta akikaa kimya kwa muda huku macho yakiwa yametazama nje , alipokuja kumtazama David alikuwa akilengwa lengwa na machozi.
"Silipwi mshahara wowote kwa sasa hadi miaka mitatu ipite... "alianza kusimulia
"kwanini? "
"Miezi tatu kuajiriwa hapa nilijikuta nikipoteza mashine ya T-scan baada ya kuvamiwa na majambazi , majira ya saa tano asubhi nilipokuwa natoka uwanja wa ndege kuipokea, kwa kuwa nilikuwa Daktari mkubwa kuliko wote katika swala la upasuaji, nikitokea hospitali ya Muhimbili, hofisi iliniamini sana kutokana na utendaji wa kazi toka nikiwa Muhimbili"
"kwanini ulitoka Muhimbili? "
"masirahi yalikuwa madogo na mbaya zaidi mshahara hautoki wakati mwafaka, ukitoka ni wa mwezi mmoja tena wa deni, sasa unajikuta hujapata mshahara wako hata miezi sita! "
Dk Eddyson alizidi kuongea kwa hisia ya hali ya juu.
"Pole sana ,hiyo mitihani midogo midogo tu, na tambua wakati wako wa kufurahi umewadia! Endapo utanisaidia tu!".
*****
"Nitakusaidia! "
"Ahsante sana, kuna mtoto ameletwa hapo leo asubuhi, akiwa na hali mbaya chanzo kikiwa ni ajari, sijui umemsikia? "
"Si kumsikia tu bali nimehusika hata kumtibu nikiwa na Dk Atanasi , si kile cha kiume kirefu maji ya kunde? "
"Eeeeh!, hicho hicho "
"vipi nikisimamie kwa hali ya juu? "
"Hapana, nataka ukamchome sindano ya sumu itakayomuua baada ya miaka mitano ,mama yake nae mchome damu ya virusi vya ukimwi, utapata nyumba na gari hili".
Aliongea huku akiwa amemtazama machoni, maneno yake hayakuwa na utani hata kidogo, akichokuwa akisema alikimanisha.
"puuuuuuuh! "Dk. Eddyson alishusha pumzi ndefu, kabla ya kuongea chochote.
"kwanini? "
"Wazazi wake wamehusika kumuua kaka yangu, huko Afghanistan, sijui unamfahamu tajiri Emanuel Poul anaemiliki kampuni la sasatel hapa Tanzania? "
"hua nasikia tu, ukizingatia mie mgeni hapa "
"basi huyo alikuwa kaka yangu, ameu.... "
David hakuweza kuongea , alijikuta akianza kulia, kilio cha utapeli wa fikla, na ili lengo lake litimie alitakiwa acheze na hakiri za Dokta huyo.
"pole sana"
"naumia sana kuwaona wakiishi duniani, huku familia yake ikiteseka "
"kimoja nitakusaidia, ila kingine sidhani "
"kipi? "David akiuliza, huku mkono wake ukiyafuta machozi bandia
"dhambi kumuua malaika, ila kwa mama yake ni kazi rahisi sana, kazi hiyo nitaifanya baada ya mtoto kutolewa icu, najua Mama yake atakuwa akilala na mwanae "
Dokta Eddyson alijikuta akikubali Kumuangamiza Janiphar bila kujua chanzo sahihi cha yote hayo! Hali ngumu ya kimaisha inapelekea yeye kutaka kufanya ukatili huo.
"kuua hapana! Naogopa, ila ukimwi kawaida tu maana siui atakufa mwenyewe taratibu "
Dk.Eddyson aliwaza hayo,picha ya maisha mazuri ilianza kuutesa moyo wake,
"sio mbaya tekereza kama ulivyokusudia, ukienda tofauti na hilo tusilaumiane , pia utakuwa rafiki yangu mkubwa na nitakufanya uache kazi hiyo ya kusubili pesa mwisho wa mwezi , tena ukiwa na mawazo chungu nzima "
"nitashukru sana "
"kingine tunza siri hiyo ".
Ilibidi David akubaliane na wazo la Dk. Eddyson, kuondoka kwa Janiphar kungemsaidia kumuua Poul kiurahisi sana , pia angejikuta akiziendesha biashara zote na mwisho wa siku angekuwa ndie mmiliki halali wa mali hizo. Ilibidi David amrudishe Dk Eddsyson kazini kwake, kisha nae aliondoka , akiwa na mawazo chungu nzima.
 
BLOOD DEAL
Author: Teddy
Cont:0655 202 285.
Whatsapp :0756 202 284
KWA MWENYE UHITAJI WA RIWAYA HII, AWASILIANE NA MWANDISHI KWA NAMBA HIZO JUU.

SEHEMU YA 9.

Ilikotoka......

Mpango wa hatari Kati ya Dk. Eddyson na David umesukwa tena kwa lengo la kmuangamiza Janiphar kwa kumuchoma damu yenye maambukizi ya virusi vya Ukimwi , kabla ya kutoka ndani ya Aghakhan, huku poul nae akiwa bado ndani ya hati hati ya kuchomwa sindano ya sumu, je nini kitatokea?.

SONGA NAYO.

DK Eddyson alianza kutembea taratibu kuingia hofisini kwake, mkononi alishika koti lake la kazi, alionekana mtu mwenye mawazo sana, kweli hakiri yake ilikuwa imevurugwa kupita maelezo, nafsi mbili zilizidi kushindana , moja ikipinga shauri hilo, ila nyingine ilizidi kumtia nguvu, ikimtamanisha maisha mazuri.
"puuuuuuuuuh! ".
Alishusha pumzi ndefu, akiwa ameegemeza mikono yake juu ya meza, akiwa amesimama, hakujua achague lipi kati ya kutekeleza ama kukataa.
"my Jesus (Yesu wangu), lakini kanuni na taratibu za udktari hazi r..... " alishindwa kuyaendeleza mawazo yake, baada ya kukatishwa na ujumbe mfupi uliongia katika simu yake. Ukitoa sauti ya juu sana.
Haraka sana aliitoa simu hiyo ndani ya mfuko wa shati, alienda moja kwa moja upande wa meseji, ili kujua ujumbe huo ulitoka wapi,
"mmmmmh "aliguna baada ya kuona Meseji hiyo, akiwa haamini hata kidogo, kitendo cha kupokea laki tisa kutoka kwa David, kama moja ya malipo kilimtisha na kumshangaza sana, alibaki ameduwaa huku akiwa ameitumbulia macho simu yake.
"duuu! Mtihani kweli, huu je nimchome? Aaah! Potelea mbali dhambi ngapi nimefanya?, pesa kwanza maisha yangu "
Dk. Eddyson alijikuta akidhamiria kufanya kazi aliyotumwa na David, na kilichomchanganya zaidi ni zile laki tisa, tayari zilikuwa zimeshapata kazi, jioni hiyo hiyo alipanga kupita bar kidogo, kama ishara ya kujipongeza! Kwa kazi ndogo iliyokuwa mbele.
******
Baada ya David kumrudisha Dk. Eddyson kazini kwake, yeye alielekea moja kwa moja Nyakato National majanini, huko kulikuwa na moja ya nyumba aliyokuwa ameijenga marehemu kaka yake, bila kumshirikisha mkewe zaidi ya kumshirikisha mdogo wake David,hata hati za nyumba alikuwa nazo David. Kama ujuavyo wanaume huwa hawana utaratibu wa kuwashirikisha wake zao baadhi ya mali, wakiamini mwanamke hatakiwi kutambua kila kitu anachokifanya mwanaume, hivyo hata Emanuel hakuwahi kumshirikisha mkewe baadhi ya mali, ikiwemo nyumba hiyo, iliyokuwa bado haijakamilika vyema,
"nitampa hii hii itamtosha ,ila akinizingua namuondoa duniani! "
David aliongea huku akiuma meno kwa hasira, safari yake iliishia hapo alishuka na kuikangua ,baada ya zoezi hilo aliondoka akipitia ATM alikotoa kiasi cha shilingi milioni moja na laki mbili, laki tisa alimrushia ,Dk. Eddyson na zilizobaki alimtumia shemeji yake.Akimpumbaza.
"Umeiona picha ya nyumba? "
"Ndio!, Tena nzuri sana, tajarajia ushindi ndani ya siku tano, ama tatu"
"mimi nimeshamaliza ,kazi imebaki kwako, unatakiwa ufanye sio ombi tena, tambua kuanzia sasa upo ndani ya Blood deal, nikimanisha mpango wa damu, maana kile unachokwenda kukifanya lazima damu imwagike ndo mpango wako ufanikishe, kuwa makini, nakupenda sana "
David aliongea kwa msistizo sana, akimanisha alichokizungumza, daima hakuwa mtu wa kukata tamaa, ama kughairi, hakuwa na tabia hiyo , lazima afanye alichokiamu hata kama kingehatarisha maisha yake, ilikuwa ni lazima. Alikata simu na kuuma kidole gumba cha mkono, huku akiwaza kupita maelezo, dakika tano alipata wazo la kumtafuta Deus rafiki yake mkubwa.
"Acha nimtafute Deus "
Hapo hapo alichukua simu yake na kulitafuta jina la Deus, dakika moja alilipata , alibonyeza kitufe cha kijani kisha aliweka sikioni, sekunde mbili simu ilianza kuita .
"Dogo Safari hii umeamua sio masihara ".
Deus aliongea baada ya kupokea simu
"hasira niliyonayo hata nikikupunguzia, huna pa kuiweka kaka "
"safi sana, huo ndio uanaume, mwanaume lazima awe shujaa , mwenye kujitoa tena kwa viungo vyote, na ikiwezekana hata kupoteza maisha yake, babu alinieleza kila kitu "
Eeeeh! Kaka lazima nimalizie ,kama damu tayari nimeshamwanga, na mpango utimie "
"hahahahaha! "
Deus alicheka kwa furaha sana, hali iliyopelekea hata David kuunganisha cheko hilo. Kisha alielekea hofisini kwake bila kujua tena habari za Poul zaidi ya kusikia taarifa za kifo kutoka hospitali hiyo , muda mwingine alidriki hata kusali akimuombea mtoto Poul afe.
******
Siku tano baada ya ajari, Poul aliruhusiwa kutoka ndani ya chumba cha wagonjwa mahuti huti, baada ya hali yake kutengamana, kwa asilimia sabini lakini alikuwa bado akilalamika kifua kilikuwa bado kikimsumbua sana, kwa upande wa Dk. Atanasi alikuwa makini sana kuhakikisha Poul anakuwa nafu kama si kupona kabisa ndani ya muda mfupi tu! Kila baada ya masaa matatu ilikuwa lazima apite kitandani hapo, ukaribu huo na umakini huo ndio uliochangia mtoto Poul kupata nafu kwa asilimia kubwa.
"Mama "Poul alimuita Mama yake kwa sauti ya chini yenye maumivu ndani yake ,dakika moja Janiphar alibaki kimya bila kuitika akimtazama mwanae, hakuamini kama kijana wake angeweza kutoa kauri, picha ya ufu aliyokuwa nayo ndani ya chumba cha wagonjwa mahuti huti ilikuwa bado ikimsumbua.
"Abee Baba "
Alitika kwa unyonge huku akimtazama machoni, hakika alikuwa na huruma sana na maumivu makubwa ndani ya mtima wake , muda mwingine alitamani mmewe angekuepo.
"niambie kuhusu baba ,siku ile ulikataa ndo maana niliumia "
"hapana, sikukataa mwanangu "
"haya Mama , baba yuko wapi? "
Poul aliuliza huku akimtazama Mama yake usoni, macho yenye usiriazi na kile alichokiuliza, hakujali maumivu aliyokuwa akiyapata pindi alipozungumza, yeye alihitaji kufahamu wapi Baba aliko, tayari moyo na masikio yake vilichoka kusikia taarifa za Baba kuja kesho.
"Pona kwanza mwanangu "
"hapana mama ,niambie natakaaa"
Poul alizungumza huku akianza kulia, Mama yake hakutaka hali hiyo itokee, kulia huko kungezidi kuongeza maumivu ndani ya kifua chake, ilibidi ambembeleze akimuahidi kumueleza ukweli wote, japo aliamini kufanya vile kungezidi kumuumiza hata yeye mwenyewe.
"Baba hayupo mwanangu "alianza Kuongea, bila kumtazama mwanae, maumivu aliyokuwa akiyapata pindi asimuliapo habari hiyo ilikuwa siri yake na mungu wake
"atakuja lini? "
"Haji mwanangu "
"kwanini Mama, inamana hatupendi tena? Kumbe Baba mbaya akinidanganya ataniletea baskeli ha... "
"shiiii! Sio hivyo Poul "
"kumbe? "
"Baba amefariki mwanangu "
"amefariki? Ndo kwenda wapi? "
Poul alikuwa na maswali kama mtu mzima, hata mama yake alimshangaa kupita maelezo , umri wake haukuendana na maswali hayo.
"kufariki ni kuondoka duniani, hatakuja tena kutuona, hawezi kuja mwanangu, huna Baba tena, mpende Baba mdogo David, huyo ndie aliebaki pamoja na anti Agnesi, Babu na Bibi, sawa mwanangu "ilibidi Janiphar ajikaze .
"Amefarikiiiiii, haji aaaaaah! "
Poul alishindwa kuvumila alianza kulia sana, neno kutomuona Baba yake tena lilimuumiza sana, haikuwa kazi rahisi kumtuliza, alipotulia alipitikiza kusinzia kabisa.
Janiphar alinyanyuka na kuelekea bafuni, alioga na kurejea, alijilaza pembeni ya mwanae aliekuwa bado amesinzia, akiwa ndani ya mawazo nae alijikuta akipitiwa usingizi, hiyo ndo ikawa nafasi ya Dk. Eddyson kutekele kazi yake, aliyokuwa ameipanga kwa muda mrefu, kila kitu kilikuwa tayari, damu yenye maambukizi ya virusi vya Ukimwi ilikuwa imeshaandaliwa siku moja nyuma, tena ikiwa ndani ya chupa. Siku hiyo hakutoka hospitalini hapo, mara baada ya kugundua uwepo wa Poul ndani ya vyumba vya kawaida , kila hatu iliyokuwa ikitendeka alihakikisha anaifatilia.
Baada ya kumuona Janiphar amepitiwa na usingizi alinyanyuka haraka sana akiwa na bomba mbili zenye damu hiyo pamoja na kichupa kidogo kilichokuwa na dawa ya usingizi, ndani ya koti lake, alitazama huku na huko kuhakikisha usalama wake, alipogundua hakuna akiemuona alinyata kuingia ndani ya chumba cha Poul na Mama yake ,taratibu akiurudisha mlango, kisha akitoa kichupa cha dawa ya usingizi , aliitikisa na alipohakikisha imekaa sawa alimpulizia Janiphar kidogo sana, maana ilikuwa Kali sana kisha alitoa bomba la damu iliyokuwa na maambukizi ya virusi vya Ukimwi na kumchoma nayo Janiphar kupitia ndani ya mshipa mkubwa wa mkono wake wa kushoto , huku akiwa amefumba macho, kiwa anamalizia kuchomoa sindano ya pili mara mlango ulifunguliwa, alihisi haja kubwa ikizichafua nguo zake, mwili wote ulianza kutetemeka asijue la kufanya.

Dk. Eddyson hakujua afanye kipi? Moja kwa moja alijua ni Dk. Atanasi, haraka bila kuchelewa alizirushia bomba za sindano ndani kabisa ya shati lake , lililokuwa limechomekwa ndani ya suruali, kisha likafungwa kwa mkanda, kwa muonekano huo isingekuwa rahisi mtu yeyote kufahamu kilichokuwa kikiendelea.
"Khook! Khoook! ".
Alikohoa kikoozi kikavu, ili kumshitua mtu aliekuwa bado akiusukuma mlango
"vipi Mama? "
Dk. Eddyson aliuliza, mara baada kuufungua na kukutana macho kwa macho na mama mkwe wa Janiphar, kiasi alihisi, mwili wake ukipoa, mapigo ya moyo yaliyokuwa yanaenda kwa kasi, sasa yalipungua, picha ya kufumaniwa iliondoka hakirini mwake.
"Aaaah!, Nilikuja kumuaga mie nataka kuondoka! "
"OK, sawa ila kalala, sijui utafanyanje? "Dk Eddyson alizungumza huku macho yake makubwa kiasi , yalikuwa makini kumtazama mwanamke huyo, kujua kama aligundua ama la.
"Basi nisimchoshe, kesho nayo siku nitakuja kuwatazama "
"haya mama ".
Kwa pamoja walitoka ndani ya chumba hicho, wakimuacha Poul na Mama yake wakiwa ndani ya usingizi,
"haloo boss mambo tayari"
"kweli? "
"Ndio sasa nikutanie, keshaisha huyo, na nzuri zaidi nimemchoma chupa moja kabisa "
Dk. Eddyson aliongea huku akicheka cheka, furaha aliyokuwa nayo, ndani ya moyo wake aliifahamu mwenyewe.
"daaah!, safi sana, cha muhimu tunza siri hiyo milele "
"kutunza siri, ni moja ya sheria ya udaktari, kwa hilo ondoa wazo "
"basi sawa, naomba nikutakie usiku mwema, kesho tukutane Nyakato nikumalize kabisa "
"haya ".
Dk. Eddyson alikata simu na kubaki amesimama, moyo wake ulijaa furaha, hakuamini kama zoezi hilo lingekamilika salama, hakutaka tena kukaa neno hilo ,alianza kujiandaa kuelekea kwake, moyoni akiwa na amani sasa. Usiku mzima ulikuwa wa furuha kupita maelezo, hadi kunapambazukua alikuwa na tabasamu tu, hali hiyo ilimshangaza hata mke wake, lakini hakuweza kumuuliza .
 
BLOOD DEAL
Author: Teddy
Cont:0655 202 285.
Whatsapp :0756 202 284
KWA MWENYE UHITAJI WA RIWAYA HII, AWASILIANE NA MWANDISHI KWA NAMBA HIZO JUU.

SEHEMU YA 10.

Dk. Eddyson alikata simu na kubaki amesimama, moyo wake ulijaa furaha, hakuamini kama zoezi hilo lingekamilika salama, hakutaka tena kukaa neno hilo ,alianza kujiandaa kuelekea kwake, moyoni akiwa na amani sasa. Usiku mzima ulikuwa wa furuha kupita maelezo, hadi kunapambazukua alikuwa na tabasamu tu, hali hiyo ilimshangaza hata mke wake, lakini hakuweza kumuuliza .
Safari ya kwanza, asubuhi hiyo ilikuwa ni kuelekea Nyakato national majanini, huko alikutana na David, aliekuwa amemsubili muda mrefu.
"Nakupa nyumba hii, ila hati sitakupatia leo, utazipata baada ya kifo cha Janiphar, hapo ndipo nitakapoamini, na kuanzia muda huu, umeshakuwa rafiki kwangu na ndani ya Blood deal, hutakiwi kukataa kufanya chochote, ukienda nje ya utaratibu, kichwa chako kitakuwa chakula cha hii "
David alizungumza huku, akitoa bastola ndani ya suruali yake, wote wakiwa ndani ya gari lake, alianza kuipangusa pangusa, akiwa ameitumbulia macho, upande wa Dk. Eddyson, hali haikuwa nzuri, kulikuwa na nafsi iliyoanza kumbeza na kumsunta, muda mwingine alijuta kukutana na David, kukubali kufanya kazi yake, alidhani mambo yatakuwa rahisi sana! Masikini Dk Eddyson alianza kutetemeka, bila mwenyewe kutegemea.
"Sasa unatetemeka nini? Mbona unakuwa kama mwanamke! Daima mwanaume huishi popote, hufanya lolote, na tambua mwanajeshi hachagui adui wa kumshambulia hata mtoto mdogo anaweza kushambuliwa akiwa upande wa adui, wewe mwanaume kaza mjomba " alizungumza maneno hayo David akiwa anakipiga piga kifua cha Dk Eddyson, kilichokuwa kidogo na cha kawaida sana .
"Lakini makubaliano yetu hayakuwa hivyo? "Alizungumza kwa unyonge, muda mwingine alitamani kuitoa damu yenye maambukizi ya virusi vya Ukimwi ndani ya mwili wa Janiphar, lakini haikuwezeka, tayari maji yalikuwa yamemwangika ndani ya bahari, na ni ngumu sana kuyachota yaleyale, lazima utoke na mengine, majuto ambaye ni mjukuu tayari ,alikuwa rafiki yake kuanzia dakika hiyo.
"hahaha Dk Eddyson!! Hahahaha! Unanifurahisha kweli baadala ufu....."
David alicheka kwa furaha, huku akiongea, aliyakata maneno yake, baada ya kuchukua mzinga wa konyangi, aliutikisa tikisa kama dakika moja, huku macho yake yakiendelea kumtathimini Dk. Eddyson ,aliekuwa mnyonge kupita maelezo ,
"puuuuh! Sikiliza bwana mkubwa, siku zote ahadi huvunjwa kutokana na sababu za kila mmoja, hujawahi kuona penzi la watu waliokuwa wakipendana sana, na kila mtu akiwatamani lakini mwisho wa siku wanaachana? Na hata wakikutana hawasemeshani? "
"kweli "
"sasa Kama ni kweli!, Je mimi nitakuachaje, na tayari umeshafahamu kila kitu changu, ukitaka nikuache labda nikuue "
"nini? "Dk. Eddyson alipayuka kupita maelezo,
"ndio lazima ufe, ndipo utakuwa huru la sivyo karibu ndani ya Blood deal, kuna swali?"
"ha.... hap... aaana "
Alijikuta akishindwa kujibu vyema, zaidi ya kuendelea kutetemeka, ile furaha ya asubuhi aliyoamka nayo ilotoweka ghafla.
"Basi kama hakuna, karibu kwako, unaweza ukarudi kuishi hapa kuanzia leo, fanya usafi, tutazidi kuwasiliana, unaweza kuondoka chukua pikipiki wahi hofisini "
David alimkabidhi noti tatu za elfu tano tano mpya, Kama nauli.
*****
Usiku mzima hakuna alieshituka, zaidi ya kujigeuza geuza, saa kumi na mbili, Poul alikuwa wa kwanza kuamka, aliyafuta macho yake ili kuiondoa hali ya usingizi singizi, kisha alinyanyuka na kuketi, hakutaka kumuamsha mama yake, muda huo, alichofanya alishuka taratibu hadi chini alikoanza kufanya mazoezi kama Dk. Atanasi alivyokuwa amemweleza,
"Mama nataka kuoga "
Poul alimuongelesha Mama yake, huku mikono yake ikimtikisa tikisa, dakika mbili alishituka akiwa mchovu mchovu sana,
"shikimoo Mama "
Mar- haba ,umeamka salama? "
"Ndio mama, wewe je? "
"Salama ila nahisi, mwili mchovu, na mkono unauma hapa "aliongea huku akipashika shika eneo lililokuwa likimuuma, hakujua ni kipi kilimpata zaidi ya kuhisi uchovu tu, hakuta kulala tena, alimchukua mwanae na kumpeleka bafuni alimsafisha, kisha nae alijisafisha, baada ya kumrudisha chumbani huko,dakika kumi wasalimiaji waliingia, hata kabla hawajakaa Dk. Atanasi alifka chumbani humo kumjulia hali rafiki yake Poul, aliwaomba wampishe kidogo na baada ya vipimo aliondoka, akiahidi kurudi mchana huku akiwapa matumaini ya kuondoka siku chache.
Ilikuwa jumatano asubuhi Janiphar alikuwa akijiandaa kuelekea kazini, baada ya wao kuruhusiwa kutoka hospitali siku tano nyuma, hakuwa na furaha hata kidogo, kutokana na upweke uliokuwa ukimsumbua, siku zote alizoea kuondoka na mmewe ,tena wakiwa wanacheka kwa furaha,
"mpenzi nilikuzoea sana, sikujua kama siku moja utaniacha peke yangu, nilijua tutaishi milele ndani ya vicheko na tabasamu zisizo na kikomo, leo umeondoka na kuniachia mtoto, leo umeondoka na kuniachia lawama na hata uaduni, laiti ningekuwa na uwezo ningekufuata, nit...... "Janiphar alishindwa kuongea, alijikuta akilia sana huku akiwa ameikumbatia picha ya mmewe, siku wakifunga ndoa, miaka mitatu nyuma, hakiri yake, moyo wake vyote vilishindwa kuzoea kabisa, kila siku kwake kilikuwa kilio,tena kibichi, muda mwingine alidhani ni ndoto, ama yuko Safari na siku moja angelejea, lakini haikuwa hivyo, Emanuel alikuwa ameshafariki! Na asingeonekana tena ndani ya uso wa dunia.
Taratibu aliitoa picha hiyo kifunia kwake, aliibusu, kisha aliirudisha ndani ya kabati lake la nguo, hakutaka tena kuiona kwa muda huo,
"bwana nipe uvumilivu "papo hapo alichukua funguo za gari lake aina ya BMW ,mkoba mkono wa kushoto na kutoka chumbani humo, aliwaga ndugu waliokuwepo kisha aliondoka, bila kuyafuta machozi yaliyokuwa yamesambaza sambaza powder yake.
Kila mtu alifurahi kumuona, neno Pole ndilo aliloshinda nalo masikioni mwake, siku hiyo alishinda mnyonge sana, lakini kadri siku zilivyozidi kusonga alijikuta akianza kuzoea zoea na kusahau ,ndani ya miezi mitatu alikuwa keshazoea, kule kulia lia kulipungua kiasi, tabasamu likaanza tena kuonekana usoni mwake, ngozi nayo ikaanza kukujuka na kurudi katika muonekano wake, wa kawaida.
Mwezi wa sita alianza kuugua ugua hovyo hovyo, muda mwingine alihisi ni maralia hivyo alinunua dawa, ama aliongea na Dk. Atanasi aliemshauri cha kufanya, lakini hakupona akawa mtu wa homa homa baada ya muda mfupi, hali ilivyozidi kuendelea ilibidi aende Aghakhan kuchukua vipimo.
"Janiphar Emanuel! "
" Abeee Dk "
Akiitika Janiphar huku akinyanyuka na kuelekea chumba alichokuwa Dk Larry, raia wa Hindia
"karibu Janiphar "Dk. Larry aliongea kiswali chenye rafudhi ya kihindi hindi huku akimtazama machoni ,
"ahsante "
Kimya kilitawala huku Dk. Larry akikagua kagua karatasi zake,
"Dk. niambie vipi namaralia sugu nini ? "
Aliuliza Janiphar baada ya kuona kimya kimetawala muda mrefu.
Dk Larry hakutaka kuongea chochote zaidi ya kumtazama kama dakika tatu, kisha aliachia kikohozi kikavu kutengezeza koo lake,
"Janiphar "alianza kwa kuita, kisha akiendelea
"majibu yako utapata, ondoa wasiwasi, hebu niambie mmeo alikufa kwa ugonjwa gani? "
"aaaah! Aliuawa nchini Afghanistan, kwa ufupi hakufa kwa ugonjwa wowote "
"sawa, na kabla ya kifo chake, aliwahi kuugua ugua kitu chochote?"
"mmmmmh! Hapana, mme wangu hakuwa na tabia ya kuugua hovyo hovyo, kwani vipi? "
"hakuna tatizo, nilikuwa nataka kujua tu, je wew hukuwa ukiugua chochote? "
"hapo nyuma hapana!, ila miezi mitano ama sita baada ya mme wangu kufariki, mwili wangu ulianza kuumwa umwa hovyo, mwanzo nilijua mawazo, lakini hali iliendelea endelea tu "
"ok sawa, samahani kwa swali hili, sina nia mbaya, je baada ya kufiwa uliwahi kushiriki tendo la ndoa na mtu mwingine? ".Safari hii Janiphar alishituka, hakujua kwanini Daktari huyo alikuwa na maswali, mengi kiasi hicho!.
"Hapana sijawahi, na siko tayari kwa muda huu, nampenda mme wangu sana, je nimeonekana na Ukimwi? "
"mmmmmh! Janiphar ondoa wasiwasi, bado tunashughulikia vipimo, na hatuwezi tukakueleza, kuwa umeambukizwa ila njoo baada ya miezi mitatu tutajua zaidi "
Maneno ya Dk. Larry alimchanganya sana Janiphar, hakutaka kuendelea kukaa tena ,chumbani humo alitoka mbio mbio hadi ndani ya gari lake, safari ya kuelekea mwananchi hospital ilianza, njia nzima alikuwa akitoa machozi, hakujua alifikaje hapo, alipaki gari lake mbele ya jengo la zamani la Tanesco,alishuka haraka, huku akikimbia kukifuata kijia cha kuingia soko la makoroboi, lakini hakufika huko ,alikunja mkono wa kushoto na kuingia ndani ya hospitali hiyo iliyojificha ficha, kwa mtu mgeni jiji la mwanza ni vigumu sana kuifahamu.
"Agines ninaukimwi! "Janiphar aliongea bila hata kukaa, Wifi yake Agines aliekuwa daktari mpya ndani ya hospitali hiyo alimshangaa, haikuwa kawaida ya Janiphar kwenda pale bila kumtarifu.
"nani kakueleza wifi? "Agnesi aliuliza kwa upole, huku akiacha kumuhudumia mgonjwa aliekuwemo ndani,
"nimetoka Aghakhan dakika hii nimeelezwa, ninaukimwi wifiiii, na nani kaniambukizaaaa"Janiphar alishindwa kuongea vizuri, zaidi ya kulia, alikiona kifo kikimkabili muda si mrefu , kifua nacho kilichemka kupita maelezo .
"Mamy tulia Kwanza, acha nimalizie kumuhudumia huyu nije tujue zaidi " Agnes alizungumza hayo, huku akimalizia kumuhudumia mgonjwa wake, dakika kumi alianza kuongea na wifi yake ,Janiphar alianza kumuelezea kila kitu, huku akitia huruma,
"acha tuchukue kipimo ".
Papo hapo alichukua damu kutoka kwa Janiphar, na kuipeleka sehemu husika, dakika mbili alilejea kuongea na wifi yake, akimtia moyo, kidogo Janiphar akianza kufarijika, wakiwa wamezama ndani ya mazungumzo, majibu ya Janiphar yaliletwa na kukabidhiwa Dk. Agines ambaye ni wifi yake kabisa, kabla hajafanya chochote Janiphar alimnyakua na kuyasoma, papo hapo alidondoka chini kama mzigo puuuu, na kupasuka kichwa upande wa kisogoni, Agines alibaki amepigwa bubuwazi, hakujua afanye nini, zaidi ya sekunde arobani na tano alikuwa hajielewi ,alikuja kushituka baada ya kuona damu nyingi zikiipamba taizi, kelele akizozipiga zilichangia kujaza watu, dakika saba ndizo zilizotumika kumsaidia Janiphar aliekuwa akihema kwa mbali sana ,huku akiwa amepoteza fahamu , huduma ya kwanza ilitolewa ,kabla ya kwenda Bugando hospitali kwa uchunguzi zaidi.
Machozi na kamasi nyepesi nyepesi hazikukatika machoni, na puani kwa Agines pindi alipogundua majibu ya wifi yake, yaliyokuwa yakionesha maambukizi ya virusi vya ukimwi, hakujua muda gani walifika Bugando, wakiwa bado getini Janiphar alipandisha kifua juu, macho yakiwa yametoka, huku mdomo ukiachama na alipokuja kushusha kifua tayari alikuwa amefariki, kila mtu ndani ya ambulance hiyo hakuamini hasa hasa wifi yake, alieona kama maigizo flani lakini ukweli ndo ulikuwa huo.
 
BLOOD DEAL
Author: Teddy
Cont:0655 202 285.
Whatsapp :0756 202 284
KWA MWENYE UHITAJI WA RIWAYA HII, AWASILIANE NA MWANDISHI KWA NAMBA HIZO JUU.

SEHEMU YA 3

" jikaze mkubwa "
" naumia sana kaka "
"najua ila tambua wewe ni mwanaume na ukizaliwa mwanaume lazima uyapitie haya hapo utakuwa umekamilika na kuitwa mwanaume piga moyo konde kaka "
kwa mara ya kwanza toka aingie ndani ya gereza hilo alijikuta akiongea na mtu, kwani toka afike ndani humo hakupenda kuongea chochote zaidi ya kulia kila alipopata muda wa kufanya vile.
" Omar nashindwa kuelewa madawa yaliingiaje ndani ya begi langu na pia askari walijuaje? "
" daaaa!, je kwani nguo alipanga nani? "Omari aliuliza huku akikaa chini pembeni akiweka fagio lake
" mke wangu na nilikuwa namshuhudia na hata asubhi yake nililifungua na kukagua upya lakini sikuona chochote"
"mmmh!., kweli? "
" ndio!"
" je huna adui yeyote na kabla hujasafiri nani aliijua safari yako? "
"aaaah!, mke wangu na mdogo wangu wa kiume "
" je uhusiano wako na mdogo wako ukoje? "
" hakuna shida tunapendana japo ni mvivu kujituma lakini nishamzoea"
Kuanzia siku hiyo Omari aliekuwa raia wa Omani mfungwa wa maisha ndani ya gereza hilo kwa kosa la mauaji makubwa alijikuta akipatana na Emanuel mtu mweusi aliekuwa hathaminiki mbele ya waarabu ,muda mwingi alitumia kumfariji na kumsihi kutokata tamaa kweli Emanuel alijikuta akianza kuyazoea maisha ya jela na kila kulipopambazuka hakusita kupunguza siku katika karenda iliyokuwa ndani ya kila chumba cha wafungwa.
" mambo Ema "
"sa... safii t... u."
Alijikuta akipata kigugumizi kujibu salamu hiyo kutokana na lugha iliyozungumzwa hakuamini Kama siku moja angeweza sikia mtu akizungumza kiswahili ndani ya nchi hiyo
" najua utanishangaa sana ila fahamu nami ni mtazania natoka mkoa wa Tabora wilaya ya Nzega " kijana huyo alizidi kuongea kiswahili fasaha huku akiwa amesimama karibu kabisa na mlango wa kuingilia chooni, mkononi akiwa na kopo pamoja na fagio ilionekana alitoka kufanya usafi
"aise karibu kabisa na nyumbani kwetu mie natokea Shinyinga wilayani Simiyu (kabla ya kupewa heshima ya mkoa),nashukuru kukufahamu "
Emanuel aliongea huku akinyosha mkono kumsalimia vizuri, siku hiyo alifurahi sana kukutana na mtanzania mwenzake, huo ukawa mwanzo wa urafiki wao.
Siku ya tano toka Mtanzania huyo aliekuwa akifahamika kwa jina la Yuda kuingia gerezani humo Emanuel alitekwa usiku wa saa tano saa za huko, akiwa usingizini aliamshwa na Yuda aliemuomba amsindikize chooni kwakuwa alimpenda na kumjali kama ndugu yake Emanuel alijikuta akitoka nje, bila kujua chochote hata kabla hajafika katikati ya uwanja alishangaa kuona vijana wawili wakimsogelea na kumkabwa wakiwa wamefunika sura zao, walimbemba mzobemzobe hadi nje ya jengo hilo kwa kuruka ukuta akiwa hajitambui baada ya kupigwa kitu kizito kisogoni kilichosababisha apoteze fahamu kwa muda wa dakika saba, fahamu zilipomrudia alijikuta akiwa katikati ya vijana saba ndani ya jengo bovu, Yuda mtanzania aliekuwa akiishi Afghanistan kwa kazi ya ujambazi, Murtaza, Hamayoun na wenzao wanne
"Yuda nimekukosea nini lakini? ,upendo wangu leo unaniua? "
" kaka sio mie " Yuda alizungumza huku akimpiga teke la mbavu
"mmmmmh,!! achaaaaa! "
Sauti hiyo ilipenya vyema katika ngoma za masikio ya Emanuel hali iliyopelekea Emanuel kugeuza haraka shingo maana haikuwa ngeni masikioni
"David!?,Mdogo wangu!??? "
Alishangaa kupita Maelezo kumuona mdogo wake wa damu toka nitoke akiwa maeneo hayo,, akijaribu kunyanyuka lakini ilishindikana kutokana na kamba akizokuwa amefungwa miguuni na mikononi
" ndio ni mie bwana mkubwa "
David alizidi kuongea huku akimsogelea kabla hajamfikia vizuri alimpiga teke la kifuani lililopelekea kutema damu
" kaka ulijifanya mjanja sana leo umepatikana sali sala yako ya mwisho "
" la... khooo! khooo.... lakini sijui kosa langu mdogo wangu, kipi ulikikosa toka kwangu, leo hii unaniua kweli, ok niambie chanzo cha wewe kunifanyia hivi? "
Emanuel aliongea kwa taabu kutokana na kuzidiwa maumivu ndani ya kifua chake
"mali nataka kumiliki zote, siwezi miliki ukiwa hai nitakuteketeza wewe na familia yako "
" kweli!? "
"ndio "
"niko radhi kukuandikisha kila kitu naomba usiniue tafadhali "
" safi sana andika "
Emanuel alikabidhiwa kalamu na karatasi akawa ameandika mali zote kumkabidhi mdogo wake David
" safi sana kaka naomba umsalimie babu na bibi Nyambele "
David aliachia risasi sita zilizokitoboa vibaya kifua cha Emanuel na kupoteza maisha papo hapo, David aliwaamru vijana wake kumpeleka gerezani usiku huo na kumtupia ndani ya ngome kisha wao walitokomea.
*****
Siku iliyofuata David ambaye ni Mdogo wake Emanuel alifika nyumbani kwa kaka yake kama walivyoahidiana na Shemeji yake usiku wa jana yake, swala lililompeleka hapo ni kupanga mikakati ya yeye kwenda Afghanistan kumsaidia kaka yake, Janiphar ambaye ni shemeji yake alikuwa teyari keshajianda kwenda benki kuchua pesa kwa ajili ya Safari hiyo
" usilie shemu, hata sie tunaumia sana "David aliongea huku akijifuta machozi ya kinafiki ili asijulikane
" naumia shemu "
"nafahamu"
Walifka mjini majira ya saa tatu na nusu asubuhi na kupaki gari lao kisha Janiphar akashuka na kuusogelea mlango wa benki ya CRDB, iliyopo jengo la PPF karibu kabisa na GOLD CREST HOTEL barabara ya Kenyatta.
Kwa kuwa siku hiyo hakukuwa na foleni alijikuta akitumia dakika kumi kuchukua pesa kwa ajili ya safari ya shemeji yake
" milioni sitini hizi hakikisha unarudi na kaka yako "
" sawa shemu "David aliongea huku akiipokea bahasha hiyo akijivika sura ya uchungu kupita maelezo
Baada ya kukabidhiana walielekea hofisi za ukataji wa tiketi za ndege mita chache kutoka hapo jengo moja na Mwanza Hotel kwa mkono wa kulia, kushoto kwake kuna tawi la benki ya NMB Kenyatta road.
Japo hakukuwa na nafasi ya kupata nafasi kwa ajili ya David, Janiphar alijikuta akinunua tikeki kwa malipo ya mara tatu ili mradi tu mmewe akasaidiwe. Siku hiyo jioni ya saa moja David aliondoka Tanzania, japo Janiphar alijua shemeji yake anaelekea Afghanistan kama walivyokubaliana lakini alijikuta akiishia Kanya akikoanza kusuka mipango ya kumuangamiza Kaka yake huko huko,
Kwanza kabisa aliwapa kazi vijana wake murtaza na Hamayoun kufatilia kesi ya kaka yake, kujua gereza gani alifungwa, baada ya kufahamu hilo alitulia kwanza kwa muda wa miezi miwili ndipo alipomtuma Yuda kufanya fujo ili tu aingie ndani ya gereza hilo kweli siku saba tu Yuda alifungwa siku mbili baada ya Yuda kufungwa David alisafiri hadi Afghanistan alikokwenda kuungana na vijana wake waliomteka Emanuel gerezani wakisaidiwa na Yuda kisha alimuua.

Hadi kunapambazuka mwili wa Emanuel ulikuwa bado uko pale pale nje, askari wa zamu ndio aliekuja kuuona ukiwa umetapakaa damu ukitisha pia
"kule kuna mfungwa ameuawa "
"wapi? " mkuu wa gereza aliuliza akiwa haamini alichokisikia
" kwenye domu la watukutu, na ni yule mwafrika toka Tanzania "
" mmmh! " mkuu wa gereza alishusha pumzi ndefu kabla ya kusema chochote , alikikuna kichwa chake kilichokuwa na upala kidogo huku nywele karibia zote zilikuwa zumeanza kujaa mvi,
" twende! "
Alinyanyuka kutoka katika kiti ndani ya hofisi yake Safari ya kwenda ndani ya hospitali ndogo iliyokuemo ndani ya gereza hilo ilianza huku kila mtu akiendelea kuwaza Lake
" inaonekana ameuawa kwa kupigwa risasai na mbaya zaidi macho nayo yametobolewa "alizungumza daktari aliekuwa akifahamika kwa jina la Mohammed Said baada ya kufika kwa asksri magereza hao
" je wafungwa wote wapo? "
" hapana mkuu yule mwafrika mpya nae hayupo "
" aaaah,! shida kweli "
Baada ya maongezi hayo waliondoka eneo hilo wakiwa na wazo la kuutarifu ubalozi wa Tanzania nchini humo kuhusiana na tukio hilo, hakika zilikuwa taarifa za kusikitisha masikioni mwa balozi huyo baada ya kupewa taarifa hizo nae aliamua kuwasiliana na serikali yake kuhusiana na tukio hilo la kuuawa kwa Emanuel.
Taarifa zilipoifikia familia yake hakuna alieamini hata kidogo mke wake alilia kupita maelezo achilia mbali ndugu jamaa na marafiki ,ulikuwa msiba mkubwa sana uliolikumba taifa la Tanzania hata serikali iliumia sana kumpoteza kijana aliekuwa akiingiza pato la taifa kila iitwapo leo ,mji wa mwanza ulijaa wangeni kutoka mikoa mbalimali.
"Mama mme wangu wamemuua mamaaa! "
Janiphar alikuwa akimlilia Mama mkwe mara baada ya wazazi wa Emanuel kufika nyumbani kwake majira ya saa tisa alasili wakitokea Simiyu, kilio ndicho kilichowapokea ndugu hao waliokuwa wamekonda kutokana na kulia kwa muda mrefu sana , toka siku waliyopata habari ya msiba huo kilichokuwa kikifanyika ni kilio tu .
"pole mamaaaa ha.. hata... sisi linatuumiza sana nimempoteza Emanuel wangu " Mama mkwe aliongea kwa huzuni huku akilia kama mtoto mdogo akiwa amekumbatiana na mke wa Emanuel
"shemeji nae amepigwa vibaya sana"
"nani David! !?"
"ndio mama walitekwa wote usiku "
" masikini watoto wangu "
Hakika yalikuwa maumivu yasiyopimika ndani ya mioyo yao kuuawa kwa Emanuel na kupigwa kwa David kama walivyopata habari kutoka Afghanistan iliwaumiza sana, hakuna hata mmoja aliekuwa anaujua ukweli . Baada ya David kutekereza adhima yake aliamua nae ajiumize kiaina ili kuficha ukweli halisi ,kweli usiku huo huo aliiamua kujipiga risasi ya mguuni sehemu aliyona ingepona mapema, mikono nayo aliijeruhi achilia mbali usoni japo aliumia lakini hakujali roho ya dhuruma ilikuwa imemtawala kupita maelezo.
****

Inasikitisha sana...

Ila malipo ni hapa hapa duniani...
Kaka mtu (David) Kaenda kuumua mdogo wake (Emanuel) kisa mali...


Cc: mahondaw
 
BLOOD DEAL
Author: Teddy
Cont:0655 202 285.
Whatsapp :0756 202 284
KWA MWENYE UHITAJI WA RIWAYA HII, AWASILIANE NA MWANDISHI KWA NAMBA HIZO JUU.

SEHEMU YA 4

" masikini watoto wangu "
Hakika yalikuwa maumivu yasiyopimika ndani ya mioyo yao kuuawa kwa Emanuel na kupigwa kwa David kama walivyopata habari kutoka Afghanistan iliwaumiza sana, hakuna hata mmoja aliekuwa anaujua ukweli . Baada ya David kutekereza adhima yake aliamua nae ajiumize kiaina ili kuficha ukweli halisi ,kweli usiku huo huo aliiamua kujipiga risasi ya mguuni sehemu aliyona ingepona mapema, mikono nayo aliijeruhi achilia mbali usoni japo aliumia lakini hakujali roho ya dhuruma ilikuwa imemtawala kupita maelezo.
****
" bwana alitoa na bwana ametoa jina lake lihimidiwe, najua tunaumia sana kumpoteza mpendwa wetu ila kazi ya mola haina makosa, leo Safari ya mpendwa wetu Emanuel imeishia hapa nasi tumuombe mungu atusaidie kuishi maisha ya utakatifu hapa duniani, zaidi na zaidi tumuombe mungu ampumzishe pahali pema peponi ndugu yetu alietutangulia "
Yalikuwa ni maneno ya kuhuzunisha na kufariji kiasi flani kutoka kwa Padri Biruru ndani ya kiwanja cha kanisa kathoric bugando jijini mwanza, kutokana na idadi kubwa ya waombolezaji kufurika kanisani hapo misa ya mazishi ilifanyika nje ya kanisa ndani hakukufaa kabisa. Hakuna mtu alieshindwa kutoa machozi pindi alipoyatupia macho yake katika jeneza la Emanuel kipenzi cha watu mkoani hapo, mashirika mbalimbali nayo hayakuwa nyuma, vituo vya watoto yatima alivyokuwa akivisaidia navyo havikukosa kumsindikiza mpendwa wao.
" Mama Baba atakuja lini? "
"sass! ha..... "Janiphar alishindwa kujibu swali hilo kutoka kwa mwanae mdogo poul aliekuwa na miaka mitatu tu, swali hilo lilizidi kuumiza moyo wake, hakujua ajibu vipi ama aseme nini
" mama baba mbona haji? "
Poul alizidi kumsumbua mama yake aliekuwa hajiwezi kwa lolote na kila alipoyaruhusu macho yake kulitazama jeneza alipoteza fahamu.
Baada ya misa hiyo kumalizika safari za kuelekea makaburi ya Kangae wilaya ya Ilemela ilianza wakipitia barabara ya musoma, walipofika buzurunga walikata kushoto kuitafuta nyakato mecca, papo hapo kituo cha mecco walikata kushoto tena wakifuata barabara ya vumbi hadi makaburini, zoezi la kumhifadhi Emanuel halikuchukua muda mrefu hivyo Safari ya bwana Emanuel tajiri kijana ikawa imefika mwisho
" hakikisha unaitunza hiyo hati ya hoteli "
" sawa baba, ila vipi kuhusu hizo zingine? "
Msichsna wa kazi alimuuliza David ambaye hakuhuzuria maziko ya kaka yake kuanzia kanisani hadi makaburini akijifanya kuzimia kutokana na kulia sana hivyo ndugu hao waliamua kumuacha nyumbani, nusu saa baada ya kutoka nyumbani waombolezaji hao alizinduka na kuelekea chumbani kwa kaka yake alikoiba kila nyaraka za maana akiwa dakika za mwisho Vero msichana wa kazi alimfumania.
"zipo... zipooo kwani... vipi? "
Alishindwa kuongea vizuri baada ya kukaziwa macho makali na msichana huyo aliekuwa ameanza kumstukia muda mrefu hata kabla ya kifo cha boss wake ila hakuwa na uhakika hata kidogo.Hakutaka kukaaa tena chumbani humo alitoka akiwa anachechemea akielekea chumbani kwake
" huyu hanijui eeeh! ,nampa masaa 120".

" huyu hanijui nampa masaa 120"
David aliwaza maneno hayo huku akitembea kwa kuchechemea kutoka ndani ya chumba cha kaka yake, moyo wake ulijaa hasira isiyoelezeka hata kidogo aliona kila kitu kitaenda fyongo na siri yake ingetambulika na hilo hakutaka litokee hata kidogo.
" puuuuuuh! "
Alivuta pumzi ndefu baada ya kufika chumbani kwake alikojitupia kitandani kama mzigo puuu akiwa chali macho yake akiyaruhusu kutazama dali lilokuwa limenakishiwa kwa jipsamu rangi nyeupe ikiwa imepambwa vyema na maua ua. Dakika saba alitumia kufikiri ni kifo gani kingemfaa Vero tena kisicho na makelele ama maumivu
" hahaha! "
David aliachia cheko changa lenye maumivu ndani yake baada ya kupata jibu la kazi yake.
" Hail poison itamtosha huyu "
Hii ilikuwa ni sumu hatari sana yenye asili ya hewa hewa ambayo mtu ama kiumbe hai kikipewa sumu hii dakika tatu kinapoteza maisha huku akikiwa amebadirika rangi ya ngozi kuwa nyeusi, sumu hiyo aliipata nchini Austaria kwa gharama kubwa sana ndio aliona suruhisho tosha kutekeleza adhima yake aliyokuwa amekusuudia ya kumuangamiza Vero.
" atakoma" aliongae huku akinyanyuka kitandani hapo na kuliendea Begi lake dogo lililokuwa na sumu hiyo lakini kabla hajafanya chochote alipatata wazo la kurudisha nyaraka alizokuwa aneziiba chumbani kwa shemeji yake ,kweli alikubaliana na wazo hilo alinyanyuka haraka sana.
" sijui nimweleze Mama" Vero aliwaza akiwa bado amesimama ndani ya chumba cha boss wake mkononi akiwa bado ameshikilia hati ya hoteli aliyokuwa amepewa na David baba mdogo wake, kilichomshitua ni kufunguliwa kwa mlago tena kwa kasi ya ajabu haraka aliigeuza shingo yake na kukutana na David akiwa ameshika karatasi tano
" unafanya nini "
" aaaaah!, ba... baba.. nina... "
Vero ama Veronica alishindwa kuongea baada ya kukaziwa macho makali na Baba yake huyo Mdogo aliekuwa bado asimama katikati ya mlango
" pishaaa"
Aliongea huku akianza kutembea kuliendea kabati, Vero hakutaka kuendelea kubaki hapo aliondoka na ile hati hadi chumbani kwake na kuificha ndani ya begi lake dogo la nguo aina ya Omega rangi ya ugoro lililokuwa sakafuni bila kuwekewa kitu chochote chini .
" kazi ipo hapa daaa sijui tutasalimika huyu ni nyoka tena koboko daaa!. yawezekana hata Baba alimuua huyu "
Kwa kuwa Vero alikuwa Binti aliejitambua na kujaliwa uelewa mkubwa alianza kumstukia David na kupanga mikakati ya kupambana nae bila kujua kama mwenzake alikuwa mafia na jambazi mkubwa.
" kesho nakiondoa duniani kijinga sana "
Aliwaza huku akiondoka chumbani humo kwa Mara ya pili.
*****
Kesho nakiondosha duniani kijinga sana "
Aliongea huku akiondoka chumbani humo kwa Mara ya pili.
Baada ya lisaa limoja kuondoka waombolezaji walilejea kutoka makaburini hivyo David aliendelea kujiuguza tena.
Kesho yake kikao cha familia kilichukua nafasi na pendekezo lililopatikana Janiphar ataendelea kuwa msimamizi mkubwa wa mali zote akisaidizana na David, kwa kuwa hakuna na shaka nae yeyote akuwa na budi kumkataa na ukizingatia walikuwa wakifanya kazi nae muda mrefu hata kabla ya kifo cha mmewe.
"afadhali mambo yangu yameanza kwenda vyema sasa"
" kiaje David? " Eric miongoni mwa marafiki zake waliokuwa hawafanyi kazi zaidi ya kutegemea kodi kutoka kwenye nyumba zao za uridhi zikizokuwa mtaaa wa uhuru mkabara na mount meru university
" si kuhusu yule demu? " David alisema huku akichukua kipande cha nyama choma ndani ya sahani wakiwa Kumalija Hoteli iliyoko nyegezi stendi usiku huo
"aaah!,sikia huwezi kukiua kibinti kizuri kama kile bila kukila kwanza, tukiteke kikiwa kinaenda sokoni tukakibake kwanza harafu ndo tukiue "
" kile hakifai kichafu "
"mie naugwadu mtu wangu nipe nipunguze mafuta mwilini "
" basi poa kesho jiandae, "
Japo zilikuwa siku mbili tu baada ya kuzikwa kwa Emanuel David alikuwa tayari ameanza kunywa pombe, hakuwa na huruma hata chembe na mbaya zaidi alikuwa akianza kumuwinda Vero ambaye nae alikuwa amedhamilia kupambana nae.

kikao kati ya David na Eric kilivunjwa baada ya wao kwa wao kuanza kutoleana maneno ya kashifa usiku huo, hakiri ya David ilikuwa ikifanya kazi zaidi ya computer, vyovyote vile aliamini lazima Erick angemsaliti na hilo huwa hakubaliani nalo hata siku moja
" lest in peace Erick ( pumzika kwa amani Erick) "
David alizungumza maneno hayo huku akiwa anatoa machozi ya hasira iliyochanganyikana na uchungu, mkononi alishika bastola yake aina ya Berreta isiyo na sauti, aliibusu huku akiendelea kuiomba ifanye kazi yake sahihi,japo Erick hakuepo lakini tayari alishapanga kumuua usiku huo huo. Aliwasha gari na kuondoka hotelini hapo akiwa na hasira zisizo elezeka safari yake iliishia mtaa wa uhuru nyuma ya Wande hoteli hapo ndipo Erick alikuwa akiishi zaidi ya dakika 180 alikuwa eneo hilo akiwa anaendelea kuvuta sigara aina ya ESM ndani ya gari la kaka yake.
" safi sana " aliongea peke yake mara baada ya kumuona Erick akija eneo hilo, papo hapo aliichomoa bastola yake iliyokuwa kiunoni , aliikagua kama ilikuwa na risasi, alitabasamu mara baada ya kukutana na risasi tatu alimulenga Erick kichwani ,risasi moja tu ilikimaliza kichwa chake kisha aliondoka eneo hilo bila mtu yeyote kuona hiyo ilisababishwa na hali ya mvua usiku huo. Hakuwa na hofu yeyote dhidi ya vyombo vya dola, zaidi ya viogozi wakubwa walikuwa marafiki zake, pia heshima ya marehemu kaka yake aliitumia kufanyia uovu na uozo uliopindukia.
******
"lete bia hapa wewe kahaba! "
Erick aliongea kwa Sauti ya kilevi iliyochanganyikana na ukali kiasi,
"mshikaji punguza maneno machafu"
" wewe acha kuongea pumba hawa ni mamalaya tu yanat **** ,kila siku "
Erick aliendelea kuporomosha maneno makali dhidi ya wasichana wale hasa hasa akina Dada waliokuwa wamebarikiwa ama kujaliwa makalio makubwa ,hakujali maneno yake kwamba yalikuwa mwiba kwa wengine, yeye aliona kila muhudumu ndani ya kumalija hoteli alikuwa malaya.

Uchu na uroho wa mali ni mbaya sana...

Na dhambi ya kuua ni mbaya sana... ukianza kuua kila utakayekutana nae utamuona mbaya wako au anajua maovu yako, utaendelea kuua hutokaa kuishi kwa amani...

Ndicho kinachomtoea David...


Cc: mahondaw
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom