Fidel80
JF-Expert Member
- May 3, 2008
- 21,945
- 4,506
Nahisi Chiku yupo humu ndani....Lol
Komredi umegundua anapiga piga misele humu...hehehe
Nahisi Chiku yupo humu ndani....Lol
kwikwikwikwikwikwi si unajua tz ukiongea ngeli unaonekana msomi.......
......... Kwa nafasiNi vituko vya pwani, umbea lakini si uchonganishi,mipasho, unataka kujua ukweli wa mambo basi umefika...michezo ndio kwao, burudani za kumwaga...yote kwa yote mambo ya pwani yanapewa kipaumbele hapa....asikwambie mtu mambo haya ni zaidi ya chakula....matamu lakini ukiyakosa mdomo wachahuka kama umeona kiembe ngwadu.
Dina Marios......
ushaenda mlimani city pale? usipoweka this what unaonekana mshamba....hehehehehe kha! si mchezo mambo ya ung'eng'e noma mazee.
Komredi umegundua anapiga piga misele humu...hehehe
Dada Belinda na wewe anzisha ya kwako blog mm nitakuwa mod. au unaonaje?
Tulijaribu kwa kumpa Zakia akataka aifilisi nchi kabisa tukamshtukia mm naamini wanawake wa Kitanzania kuongoza bado sana.
dada mtarajiwa hatuwezi kuwa na taifa la type za akina dada wa kitanzania......tutapotea....imagine
raisi.....rachel temu
makamu.......teddy kalonga
waziri mkuu........dina marios
gavanawa pesa.....kelly01
waziri wa fedha......kui
......nchi itakuwa imeshafika kuzimu......
Inachekesha kuona ati Dina Marios na wenzie wanaonekana ndiyo wawakilishi wa wanawake wa kitanzania! Kwani hakuna the likes of Dina wa kiume...mbona kuna wanaume wengi tu wako clueless kwenye mambo mengi na hatuwasemi?
Hebu tuwaache watu wawe huru na maisha yao jamani.
tutakupa ww uwakilishi
That is not the point.The point is...let everyone live his/her life bila kulinganishwa na mwingine.Mwache Dina na wengine wenye blogs wafanye vitu vyao.... na msiwakebehi kwa kuwapa nafasi za uongozi wa kitaifa kama vile hao ndio walioonekana miongoni mwa wanawake wa Tz.Kuanzisha blog is not a big deal afterall wala siyo achievement.
Ni kweli generalization ni mbaya, japo kwa kutumia sample ya YO YO mtu anaweza ku-conclude kirahisi zaidi kwamba akina dada blogs zao zikoje ama zinaongelea nini.
Lakini inabidi pia tuangalie upeo wao wa elimu, malengo ya kuanzisha blogs zao na background za hao bloggers. Ukichunguza kwa makini wengi wao elimu yao ni F4 au wakijitahidi sana ni F6, na kozi za miezi 3 kwenye vyuo vya uandishi wa habari vya mtaani, akitoka hapo anajiita mwandishi wa habari.
Kuna akina mama/dada wengi ambao wako makini sana kwenye issues mbali mbali lakini hawana muda wa kuanzisha blogs. Hao walio na blogs wana muda lakini matumizi yake ndo kama wanavyojua wao.
Chukua blogs za Kalonga, Temu, na Kimambi (kabla hajaifuta) zilikuwa zimejaa umbea na kusemana na inawezekana walizianzisha kwa malengo yao na yale yaliyokuwa yanaandikwa kwenye hizo blogs yanakupa picha halisi ya background zao, wala huhitaji kuuliza huyu mtu yukoje awe ni msomi ama yuko nje ya Tanzania, hapo nikimaanisha kwamba elimu na/au exposure havijamsaidia. Mtu aliyeelimika/mstaarab/mwenye exposure hawezi kukaa kusemana/kutukanana na mwingine kwenye blogs, kwa faida ya nani kama siyo kujianika?
Kundi jingine ndo hilo la "waandishi wa habari" akina Dina Marious, Shamimu, Dinahicious, Diva, na wengineo wana malengo yao binafsi ambayo nadhani wanayajua wao ndani ya nafsi zao.
Chemi, Katabazi, na Subi blogs zao zimetulia na zinaweza kusomwa na mtu yeyote. Mfano, baba anaweza kufungua webpage ya Katabazi na akasoma kwa uhuru hata kama mwanae yuko around, lakini hizo nyingine huwezi kufungua mbele ya mwanao ama mzazi wako, ni aibu tu.
Niungane na WomenOfSubstance kwamba blogs ambazo tunaziona zina utata inawezekana wenye kuzimiliki wamekosa pa kutokea na sasa wanatafuta namna ya kutoka (umaarufu?) ama kupata umaarufu wa aina fulani na inawezekana wengine walikosa kazi na wakaamua kuanzisha vitu kama hivyo. Nakumbuka Dinahicious alipoanzisha blog yake alienda kuitangaza DarHotBoard (DHB) ya zamani. Alisema kwamba, ninamnukuu lakini siyo neno kwa neno, "jana baada ya kukosa cha kufanya niliamua kuanzisha kitu kama hiki, karibuni mje muone nilichofanya". Wengi wa wana DHB walimsagia sana walipokuta ameweka picha ya msichana aliyevaa chupi tu (wanaomfahamu walisema ni yeye na yeye mwenyewe alikomaa kwamba anajiamini na ndiyo maana aliweka picha yake na haoni ubaya kufanya hivyo!).
Kwa hiyo tusije tuka-conclude kwa kuangalia hao walioanzisha blogs bila kuangalia melengo, elimu, background zao na mengineyo. Wako wamama/wadada ambao wako serious sana lakini hawana nafasi ya kuanzisha blogs, kwa wale wanaofanya vyema tuwaunge mkono na wale wanaoharibia wengine tuwaseme wazi ili wabadilike na kufanya mambo mengine mazuri yenye tija na maendeleo kwa jamii na nchi yetu kwa ujumla.
Ningependa kukujibu kuwa, nani kasema kuwa wanaume hawana cha kufanya hadi waanzishe na kumiliki blog zao? Mpoki aliwahi kuhojiwa majuzi na kusema kuwa kwa kweli ni kazi kuendesha blog na kufanya kazi za kiandishi. Naye angesema kuwa yuko bize, na mwingine, na mwingine je?
Nimesema hapo awali, wanawake wanapenda kufanya yale yaliyo karibu nao. Hivyo bado changamoto ziko pale pale. Suala si kuwatetea eti wako bize na mambo yao mengine kiasi cha kuwaachia kina Dina kuvurunda.
Nao wajitoe kama wanaume. Si wanataka 50/50?
Ninakubaliana na Mpoki kwamba kuendesha Blog na kuifanya iwe active inahitaji muda wa kutosha na kujitoa. Michuzi akihojiwa na Bongo Celebrity Blog alisema kwamba huwa analala baada ya saa saba usiku kila siku na kuna siku nyingine huwa anakuwa macho mpaka saa tisa za usiku ili angalau aweke taswira alizonazo na kupitia comments za wadau. Je, akina mama walio na responsibilities za kazi, familia, watoto na mengineyo wana nafasi hiyo? Ukisema waende 50/50, maana yake na responsibility za ndani nazo ziwe 50/50 of which hakuna mwanaume ambaye yuko tayari kwa hilo.
Hata wanaume nao wanafanya yale yaliyo karibu nao, na ndiyo maana nikasema tuangalie background za bloggers, elimu na malengo ya kuanzisha blogs. Michuzi, Mjengwa, Mroky, MichuziJr, Mpoki na wengineo wa jamii hiyo walianzisha blogs za picha kwa kuwa kupiga picha ni sehemu ya fani/hobby/ajira yao. So hizo picha ni mojawapo ya vitu vilivyo karibu nao. Wachangiaji kwenye hizo blogs ndiyo wameongeza mijadala ya uchumi, jamii, na mengineyo.
Mfano, siku Liverpool ikishinda ama Man U wakishindwa, immediately after the match utakuta taswira na matokeo ya game pale kwa michuzi, lakini siku Liverpool wakishindwa ama Man U akishinda utakutana na taswira kesho yake ama usione kabisa mpaka watu wamtumie e-mail za vijembe. Ni swala la interest na mazingira ya kazi. Hivi ulishaona kwa Michuzi kuna mada/comments za kukandia CCM ama serikali? Hujiulizi ni kwanini huwa hata comments za kukandia serikali huwa hazionekani? Mazingira ya kazi ndugu yangu.
The rest of bloggers wa kiume wengi wao ni waandishi wa habari by profession na wanachokiweka huko ni news wanazokutana nazo ama makala wanazoandaa ama wanaanzisha mijadala ili kupata maoni na mwelekeo wa wachangiaji na hivyo kuwapa nafasi ya kuandika makala ambazo ziko balanced.
Kwa hiyo hata wanaume nao wanafanya kile ambacho kilicho karibu nao, hakuna blogger ataanzisha blog ya fani ambayo siyo yake. Mchumi ataweka blog ya uchumi na ndicho kilicho karibu yake. Politician atakuwa na blog ya siasa ili kuangalia joto la siasa na mwelekeo ukoje. Kwa hiyo wenye blogs wengi wanaweka vitu ambavyo viko kwenye anga zao ama ambavyo ni sehemu ya maisha yao. Na ndiyo maana nikasema angalia BACKGROUND ya blogger, it tells a lot.
Sasa kama akina Kalonga and the likes wamekulia kwenye mazingira ya mashindano ya mavazi na mitoko, marafiki wa aina gani, mavazi ya aina gani na kwamba anam-date nani na wa class gani, what do you expect from them?
Ukienda kwa Mjengwa utakuta picha za Iringa na kama siyo Iringa basi ni Dar, hususani Kariakoo na Kinondoni Biafra au Bagamoyo, au vijijini iwapo atakuwa na safari za vijijini na hizo picha ndiyo ziko karibu na yeye. Picha nyingine tofauti zinakuwa zimetoka kwa wadau ambao hutuma kwenye hizo blogs na bloggers hutoa maelezo kwamba picha imetumwa na mdau.
Kwa wale walio kwenye ndoa wanaweza kujitoa iwapo mfumo dume utawaruhusu kufanya hivyo. Mfumo dume bado ni kikwazo kwa akina mama kufikia hiyo 50/50 unayosema ndugu yangu.
Nimalizie kwa kusema kitu kimoja, tunaposema akina mama/dada makini nao waanzishe blogs zao za ku-discuss mambo muhimu lazima tuelewe priorities zao, access ya mtandao na pia fursa ya kufanya hivyo. Hao walio na blogs unaweza kuta ama wako nje ya nchi au wako Bongo. Walio nje ya nchi wana access ya mtandao 24/7, na walio bongo wanaweza kuwa na access ya mtandao wakiwa ofisini na ndipo wanakofanya vitu vyao. Kwa hiyo kuna mengi sana ambayo yanaweza kuwa vikwazo kwao kuliko jinsi tunavyofikiria na inawezekana wana mambo mengine muhimu ambayo wanafanya ambayo ni mazito/makubwa na yana tija kuliko hata kuwa na blog ambayo inakuwa accessed na wale walio na mtandao tu.
Mfano Mama Hellen Kijjo-Bisimba ambaye ana kituo haki za binadam na amekuwa akifanya makubwa sana na outreach yake ni kubwa zaidi kuliko hata blog. Kuna wana harakati kibao ambao wana NGOs zao ambazo zimekuwa zikisaidia jamii na ziko karibu na watu kwa kuwa zinatoa msaada unaonekana. Mfano ni yule aliyekuwa house girl wa Mahita anatetewa na Kituo cha Mama Bisimba na si ajabu akapata haki yake. Mpaka sasa Mzee mzima Mahita ameingia mitini amegoma kwenda kufanyiwa DNA, sijui mahakama itaamua nini. Kwa hiyo kila mama anaangalia afanye kipi na kile kilicho ndani ya uwezo wake. Tusitumie hao wachache ambao walianzisha blogs bila kujua wanafanya nini na wakaishia kuzifanya ziwe za mipasho badala ya kuwa visima vya mijadala na maoni yenye kuleta maendeleo kwa jamii.