happyxxx
JF-Expert Member
- Nov 14, 2020
- 568
- 1,847
Mh Judge Biswalo ni kiongozi muadilifu, mchapakazi, mtenda haki.
Aliopokuwa DPP aliifanya kazi yake kwa weledi mkubwa. Alihakikisha mafisadi wanaonja uchungu wa kuiba mali za watanzania bila kuonea mtu.
Sasa mafisadi na majizi yanatumia nafasi waliyopewa kulipiza kisasi kwa kumchafua na kumdhalilisha.
Biswalo kama mzalendo alikuwa anatimiza wajibu wake wa kisheria kwa kusimamia sheria iliyotungwa na bunge.
Ripoti ya CAG haijaonesha sehemu yoyote kuwa Biswalo kaiba pesa. Kilichotokea ni issues za procedures tu ila pesa inayozungumzwa kwa mujibu wa CAG ipo kwenye akaunti ya serikali kilichotokea ni kuweka akaunti tofauti na ilivyozoeleka.
Biswalo angekuwa ana makosa kama angeweka pesa kwenye akaunti yake binafsi au angetorosha.
Sisi wazalendo tunasema pamoja na kampeni chafu dhidi yako wananchi tuko pamoja na wewe na uendelee kufanya kazi uliyoaminiwa na Rais.