Habari za uhakika kabisa kutoka kwa kada mbalimbali ndani ya CCM Mwanza zinasema sherehe hizi zilipangwa kufanyika Mza kwa sababu kuu zifuatazo:KWANZA taarifa za ndani kabisa zinadai wenyeviti wale wa mashina walitakiwa kujieleza ni kwanini chama kilipoteza majimbo,kulikuwa na taarifa kuwa nao WAVUE MAGAMBA,baadae waliona chama kitakufa kabisa,hali hii iliongeza mpasuko,sasa kwa "Chakula hiki cha CCM Kirumba"tuwe pamoja na Wanachama.PILI:Kuzindua harakati za kupata kiti cha udiwani cha kata ya Kirumba ambacho diwani wake(CHADEMA) alifariki dunia.Ni moja kati ya kata muhimu sana kwa CCM.TATU:Makovu makubwa yanayotokana na uchaguzi uliopita,wanachama,viongozi na wangineo......UTANI KIDUCHU,Ni kwamba Baadhi ya wafuasi wa CHADEMA wanasema CCM imekuja kujifanyia"HITMA" na kwamba wamekuja kuwapumbaza watu kwa nyama,kuwafanya "Mazuzu"
Source:MWANACCM Aliyeasi-Kirumba
Wanaweka malengo bila kufikiria au wamechoka kufikiria. Inakuwaje wana lengo hilo halafu wanajaza watu kutoka sehemu za mbali ambao si wapiga kura wa kata hiyo?!!!!!!.