Binafsi maisha ya Dar es salaam yamenishinda

Binafsi maisha ya Dar es salaam yamenishinda

Burn the bridge _Tz

JF-Expert Member
Joined
Apr 15, 2021
Posts
2,247
Reaction score
6,615
Kuanzia suala Zima la imani, huku watu wengi hasa maeneo ya mjini na uswahilini hawana imani kabisa wako mbali na Mungu.

Suala la malezi ndio kabisaa mana watoto hujifunza kwa wanaowazunguka mtoto akikulia vingunguti Tabata au mbagala kazi ipo.

Suala la ajali ndo usiseme ajali za uzumbe kabisa kuanzia Bodaboda mpaka watembea kwa miguu. Ukikaa dar jiandae kuwa mlemavu mtarahiwa.

Uchafu, hapa sina maneno mengi kuanzia hewa mitaro mpaka makazi uchafu ndio uchafu.

Vyakula visivyo Bora kuanzia mboga za majani nk mambo hovyo kabisa

Pesa haina thamani kabisa, elfu 50k ya Dar sio sawa na Ile ya Tabora kabisa.

Kifupi ukitaka maisha ya amani raha na utulivu wa nafsi karibu mkoani ila kaam unataka shida na matatizo baki Dar.

Yani Dar es salaam ni mji wa matatizo TU
Kwahelini
Haya ni mawazo yangu ty kila mtu ana uhuru wake jamani msinitukane
,
 
Ukiwa na pesa huwezi kuona huo uchafu,huwez kupata ajali za kijinga,huwez kuhama na mwisho 50k ni hela ya backet moja ya BUDWEISER wala sio ya kufanyia mipango....
Rudi bush mzee mji unataka mahustler.
 
Umesema ukweli ila watu wa masaki hawaathiriwi na hayo uliyoyataja
 
Ukiwa na pesa huwezi kuona huo uchafu,huwez kupata ajali za kijinga,huwez kuhama na mwisho 50k ni hela ya backet moja ya BUDWEISER wala sio ya kufanyia mipango....
Rudi bush mzee mji unataka mahustler.
Nimemweleza hivo pia.

Nimemshauri tu arudi akatafute pesa then atakuja tutumie. Jiji linahitaji uwe na pesa and not otherwise
 
Tulisema baada uchaguzi mtarudishwa vijijini kwenu na hivi mlifanya fujo ndio kabisa mtakoma
Baada ya hapo wanafuata ni bodaboda
Mji utakuwa msafi sasa
 
Back
Top Bottom