Pakome
JF-Expert Member
- Dec 8, 2024
- 1,541
- 916
Binadamu ana tabia ya kugeuza matumizi ya vitu na sijajua hii tabia inatokana na nini
Anaweza hata akavaa chupi kichwani au akajipaka mafuta ya kulainisha break ilimradi tu ageuze matumizi ndipo aridhike
Lengo la kuundwa kwa bunduki halikua kuonea watu bali lilikuwa kujilinda na maadui lakini wale maadui wanaoweza kutoa uhai sio kila adui ni wakupigwa risasi wengine wanachapwa tu fimbo na kurushwa kichura
Nadhani aliko mgunduzi wa bunduki anajuta sana kwasababu ugunduzi wake umeleta madhara makubwa zaidi ya faida
Habari kubwa tuliyonayo duniani ni binadamu kutoana uhai kwa risasi kwenye makosa ambayo yalihitaji tu fimbo na kurushwa kichura
Tukitazama tasnia ya Hip Hop Marekani tunaona idadi kubwa ya Wasanii kupoteza maisha kwa njia ya risasi na mambo mengi chungu nzima tusiyoweza hata kumaliza kutaja endapo tutaanza
Imekuwa ni kawaida ya binadamu kugeuza matumizi anaweza hata kuweka sukari kwenye supu ilimradi aharibu maana ya vitu
Ifike mahali tuache kugeuza matumizi ya vitu kwasababu kama tukiendelea hivi ipo siku tutaweka Petrol kwenye chakula itutoe uhai
Anaweza hata akavaa chupi kichwani au akajipaka mafuta ya kulainisha break ilimradi tu ageuze matumizi ndipo aridhike
Lengo la kuundwa kwa bunduki halikua kuonea watu bali lilikuwa kujilinda na maadui lakini wale maadui wanaoweza kutoa uhai sio kila adui ni wakupigwa risasi wengine wanachapwa tu fimbo na kurushwa kichura
Nadhani aliko mgunduzi wa bunduki anajuta sana kwasababu ugunduzi wake umeleta madhara makubwa zaidi ya faida
Habari kubwa tuliyonayo duniani ni binadamu kutoana uhai kwa risasi kwenye makosa ambayo yalihitaji tu fimbo na kurushwa kichura
Tukitazama tasnia ya Hip Hop Marekani tunaona idadi kubwa ya Wasanii kupoteza maisha kwa njia ya risasi na mambo mengi chungu nzima tusiyoweza hata kumaliza kutaja endapo tutaanza
Imekuwa ni kawaida ya binadamu kugeuza matumizi anaweza hata kuweka sukari kwenye supu ilimradi aharibu maana ya vitu
Ifike mahali tuache kugeuza matumizi ya vitu kwasababu kama tukiendelea hivi ipo siku tutaweka Petrol kwenye chakula itutoe uhai