Ulukolokwitanga
JF-Expert Member
- Sep 18, 2010
- 8,397
- 7,979
Kama jangili kuu Kinana ni sehemu ya serikali hatuna ujanja wa kupambana nalo. Acha Clintoni atusaidie maana akina Kinana wakiguswa nchi itayumba
Marekani haina maraisi watatu,yupo mmoja tu.
.....taarifa hizi zinawajia kwa HISANI/KODI YA/ZA WATU WA MAREKANI?....lini nasi tutawafadhili wengineo
Utawala wa JK utaingia katika historia ya kutembelewa na Marais wawili wa Marekani walioko madarakani na Marais wawili wastaafu wa Marekani. Na pia ndani ya kipindi kisichozidi mwezi mmoja Tanzania kutembelewa na rais wa Marekani aliyepo madarakani na Marais wawili wastaafu! Hata kama ni gas mbona hawajaenda Msumbiji ambako nako kuna gesi?
Acheni ushamba...
Acha U Zoba
nitajie nchi iliyoendelea kuizidi tanzania hapa africa chini ya jangwa la sahara (ukiondoa south africa). Nitajie ambayo ina siasa nzuri kuliko tanzania (africa nzima) mpaka useme tuna siasa za ovyo!, pinda kusema wapigwe ndio unadhani tumekua ovyo sana? Tembelea nchi zinazokuzunguka halafu fikiria tulikua vipi mwaka 1995 wakati mwinyi anaondoka ndio utajua tunapiga hatua kwa kasi ya ajabu! Fikiria secta zote za elimu, kilimo, afya, barabara, biashara (makampuni yameongezeka je) na usisahau kuhesabu ni watu wangapi wamepanda daraja kutoka kwenye level ya kumiliki baiskeli mpaka kumiliki pikipiki, bajaji na gari. Usifikiri mpaka kuwa kati ya '7 fastest growing economies in the world' ni kubahatisha au kupendelewa. Tulia 2015 usifanye makosa tu, chagua atakae kemea rushwa, atakaeondoa tatizo sugu la umeme (kama litakuwepo bado maana juhudi zilizopo ni kubwa sana) na kuondoa tatizo la maji (safi na taka)
tanzania iko imara, iko vizuri na inaenda pazuri zaidi, ndio maana viongozi weeengi wa nje ya africa wanalala waiota huku watoto wa africa wakitamani wangezaliwa tanzania!
Go my dear tanzania!
Karibu nyumbaniCLINTON ATUA NCHINI,
Rais Mstaafu wa Marekani Bill Clinton yuko nchini kukagua miradi inayofadhiliwa na Plan International, pia kuzungumza na akina mama Vikoba.
![]()
Rais Kikwete akiwa na Rais Mstaafu wa Marekani Mhe Bill Clinton ambaye yuko nchini kwa ziara ya kukagua miradi inayoendeshwa na taasisi yake ya Clinton Foundation katika nchi kadhaa za Afrika
================
Akiwa Vingunguti:
================
RAIS WA ZAMANI WA MAREKANI BILL CLINTON AFANYA ZIARA YA KUKITEMBELEA KIKUNDI CHA UPENDO HISA GROUP CHA JIJINI DAR ES SALAAM
Rais wa zamani wa Marekani Bw Bill Clinton akizungumza na wanachama wa Upendo Hisa Group alipotembelea kikundi hicho kilichopo Vingunguti jijini Dar es Salaam. Kulia kwake ni Meneja Miradi wa Shirika la kimataifa la Plan International Bw Paul Lusato na Catherine French Mkuu wa wafanyakazi ofisi ya Mtendaji Mkuu wa Barclays.
Rais wa zamani wa Marekani Bw Bill Clinton pia alitembelea moja ya saluni ya kutengenezea nywele ya Bi Zainabu Rashidi (kulia) ambaye ni mmoja wa wanakikundi cha Upendo Hisa Group cha Vingunguti Mtambani, DSM.Baadhi ya wakazi wa Vingunguti Mtambani wakimsubili Rais wa zamani wa Marekani Bill Clinton (hayupo pichani).
Rais wa zamani wa Marekani Bw Bill Clinton akitembelea baadhi ya mitaa ya Vingunguti kwa Mtambani jijini Dar es Salaam.