Bill Clinton atembelea tena Tanzania

Bill Clinton atembelea tena Tanzania

Nchi yangu Tanzania;nchi ya maziwa na asali, wanakuja kwa wingi, wote wakubwa wa dunia, kulikoni Tanzania?

Wamegundua udhaifu wenu uko kwa watawala wenu na huko ndiko wanakopitia kulinyonya Taifa lenu!!!
 
Uchaguzi, Olevaroya and others, HATA mimi napata wasiwasi! Kutakua na siri nzito sana kuhusiana na huu ugeni mfululizo.Kinachosikitisha ni kama kunakua pia na usiri fulani! Mbona taarifa zingine za ujio zinapatikana very late!Mbona nchi zingine huko hawaendi?Kama 'tumeshauzwa' tuambieni shs ngapi ili tudai chetu.. Halafu mbona huku mbagala hawafiki?hakuna mvuto au?'Ole wenu...'
 
Kaja kukagua miradi yake...

Period....

Khaa!!

Ngoja niwahi zangu Uswisi nikakague zile accounts zangu.

Hawa watawasaidia na projects zao kupiga deki nyumba zenu za udongo.
 
mi.naona tz usa waichukue na kuifanya state yao tu
 
Kaja na "cigar" zake? Haya, wapenda "cigar" muanze kujipitisha.
 
Huyu ni msimamizi wa miradi gani hapa Tz, na hiyo miradi mwananchi wa kawaida ananufaika vipi, hivi mataifa ya kigeni yanazamia Tz kwani nchi yetu in vito vya manemane, yakuti samawi, na zabarajadi?

inayofadhiliwa na plan international ila hiyo haitoshi lazima tufikirie beyond the box kwa sababu kuanzia gesi na uranium yetu igunduliwe imewachanganya mataifa ya magharibi na kusababisha kutokwa na udenda mara obama mara bush mara waziri mkuu wa thailand daah kweli wanaitamani sana resource yetu sio siri.
 
xi jinping, obama, bush, clinton, na tony blair wote wameitembelea tanzania kwa kipindi kifupi tuu kilichopita.

Kiudaku, kagame lazima ahusike hapo. Tunafuatwa fuatwa kwa sababu, recently we're become more attractive and sexy than them.

Niambie ni nchi gani duniani imetembelewa na watu hao wote ndani ya miezi sita tuu? Kagame lazima ahusike hapo. Lol.
kaka yangu naona na wewe umeanza ukorofi lol!!
 
Huyu siyo Clinton,huyu ni msukule. Kuwafahamu miksukule,tazama picha zao,linganisha masikio katika kila picha.
 
hivi hapa kuna ajenda gani? Maana mimi naanza kupatwa na wasiwasi ndani ya mwezi mmoja tu hivi tunatembelewa na maraisi 3 wa Marekani! i doubt if this is a health relationship, something fishy might be going on under the carpet! TUAMKE!!
 
IMG_1416.jpg


Katika msafara wa Mhe Bill Clinton kuna mastaa kadhaa wa sinema basketball ambao wameongozana na Rais huyo mstaafu wa Marekani aliye katika ziara ya kikazi kukagua na kuendeleza kazi za maendeleo zinazofanywa barani Afrika na taaisis yake ya Clinton Foundation. Pichani juu kulia ni mcheza sinema nyota Dakota Fanning akiongea na mcheza sinema mwingine nyotaJesse Eisenberg na nyuma yao aliyekwenda juu ni mcheza basketball katika NBA Brook Lopez

IMG_1644.jpg

Jesse Eisenberg na Dakota Fanning wakishuhudia utiwaji saini wa mkataba wa maelewano kati ya Serikali ya Tanzania na tasisi ya Clinton Foundation Ikulu jijini Dar es salaam
 
kwa taarifa tu,wamerekani nao wako na hazina kubwa tu ya gesi,wala hawaitaji kuja kuchukua gas ya hapa.gas yetu itatumika kuzalisha nishati,na kwa matumizi mengine ya nyumbani.

mbona wana hazna kubwa ya mafuta lakin wanataka kutawala maeneo yanayozalisha mafuta? Tuachane na gas, Uranium je? Hawa wakubwa wanajaribu kugombea maliasili tulizonazo thats why akitoka huyu anaingia huyu kwan Kikwete anakubaliana nao kila waingiapo.
 
.....taarifa hizi zinawajia kwa HISANI/KODI YA/ZA WATU WA MAREKANI?....lini nasi tutawafadhili wengineo
 
ktk lile linaloonekana si la kawaida Tanzania inaingia mkataba na familia ya rais mstaafu wa marekani Clinton kwa ajili ya kusaidia ulinzi wa majangili ambalo limekuwa ni tatizo kubwa hapa tanzania,Hv sisi watanzania tunaweza kufanya lipi kama mpaka hata hl la ulinzi wa mali asili tunahtaji watu wa nje watulindie,Marekani wanataka nini hasa ktk nch hi?eti kutulindia majangili? Kweli watanzania tupime uelewa wa viongoz wetu,ukoloni unarudi kwa kasi kupitia mlango wa nyuma,tumeshndwa hata kulinda uingza na usafirishaji wa madawa ya kulevya,
 
hakika tanzania tunatawaliwa kifikra ,ni hatari ukifungwa kifikra .
 
Harafu pamoja na ukarimu wetu na ugeni wao hata kunyonyesha watoto wetu hatujui, achia mbali elimu ya bora liende, siasa za hovyo, mpira hatujui, yaani shida tu. ....bin short ugeni wao hautusaidii tutaikomboa Tz yetu na hayo yote sisi wenyewe...

Nitajie Nchi iliyoendelea kuizidi Tanzania hapa Africa chini ya jangwa la Sahara (Ukiondoa South Africa). Nitajie ambayo ina siasa nzuri kuliko Tanzania (Africa nzima) mpaka useme tuna siasa za ovyo!, Pinda kusema wapigwe ndio unadhani tumekua ovyo sana? Tembelea nchi zinazokuzunguka halafu fikiria tulikua vipi mwaka 1995 wakati Mwinyi anaondoka ndio utajua tunapiga hatua kwa kasi ya ajabu! Fikiria secta zote za Elimu, kilimo, afya, barabara, biashara (Makampuni yameongezeka je) na usisahau kuhesabu ni watu wangapi wamepanda daraja kutoka kwenye level ya kumiliki Baiskeli mpaka kumiliki Pikipiki, bajaji na gari. Usifikiri mpaka kuwa kati ya '7 fastest growing economies in the world' ni kubahatisha au kupendelewa. Tulia 2015 usifanye makosa tu, chagua atakae kemea Rushwa, atakaeondoa tatizo sugu la umeme (kama litakuwepo bado maana juhudi zilizopo ni kubwa sana) na kuondoa tatizo la maji (Safi na Taka)

Tanzania iko Imara, iko vizuri na inaenda pazuri zaidi, ndio maana viongozi weeengi wa nje ya Africa wanalala waiota huku watoto wa Africa wakitamani wangezaliwa Tanzania!

Go my dear Tanzania!
 
.....taarifa hizi zinawajia kwa HISANI/KODI YA/ZA WATU WA MAREKANI?....lini nasi tutawafadhili wengineo

Ambacho tuko tunafanya Congo na Sudani sio ufadhili kuliko hata huo uliotaja? Tulichofanya Comoro sio ufadhili? Tulichofanya South Africa, Msumbiji, Zimbabwe, Uganda, Zambia, angola na Burundi sio ufadhili? Ufadhili gani unauzidi huo?

Jiamini na uiamini nchi yako!
 
Serikali DHAIFU, Clinton hawezi kuwa na uchungu wa nchi yetu na kutoa ulinzi wakati yeye ni mstaafu labda kama amekuja kununua mbuga ya wanyama ili aweke walinzi wake tuambiwe hivyo.
Hivi Tanzania imekuwa nchi ya kusaini mikataba kila siku ya Mungu, huwa inaandaliwa baada ya kutangazwa TENDA au kila ajaye akishawapa fungu viongozi wanampa mkataba wa kuuza nchi.
Juzi UTURUKI wametoa gari la doria wakati wapokeaji wa gari hilo POLISI ndio majambazi, kazi itafanyikaje?
 
Wako sahihi, watawalinda majangili kwa faida ya pande mbili na siyo kuwashughulikia kisheria, majangili wenyewe na viongozi wakubwa wa chama twawala na wengine ni wanajeshi na wanatumia magari ya kijeshi kusafirisha wanyamapori.Nani atamvisha paka kengele?
 
kinanaaaaaaaaa........... Weka mbali na Tembo.......
 
Back
Top Bottom