Bill Clinton atembelea tena Tanzania

Bill Clinton atembelea tena Tanzania

habariyamujini

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2013
Posts
3,094
Reaction score
457
CLINTON ATUA NCHINI,

Rais Mstaafu wa Marekani Bill Clinton yuko nchini kukagua miradi inayofadhiliwa na Plan International, pia kuzungumza na akina mama Vikoba.

IMG_1700.jpg

Rais Kikwete akiwa na Rais Mstaafu wa Marekani Mhe Bill Clinton ambaye yuko nchini kwa ziara ya kukagua miradi inayoendeshwa na taasisi yake ya Clinton Foundation katika nchi kadhaa za Afrika

================
Akiwa Vingunguti:
================

RAIS WA ZAMANI WA MAREKANI BILL CLINTON AFANYA ZIARA YA KUKITEMBELEA KIKUNDI CHA UPENDO HISA GROUP CHA JIJINI DAR ES SALAAM


Rais wa zamani wa Marekani Bw Bill Clinton akizungumza na wanachama wa Upendo Hisa Group alipotembelea kikundi hicho kilichopo Vingunguti jijini Dar es Salaam. Kulia kwake ni Meneja Miradi wa Shirika la kimataifa la Plan International Bw Paul Lusato na Catherine French Mkuu wa wafanyakazi ofisi ya Mtendaji Mkuu wa Barclays.
Rais wa zamani wa Marekani Bw Bill Clinton pia alitembelea moja ya saluni ya kutengenezea nywele ya Bi Zainabu Rashidi (kulia) ambaye ni mmoja wa wanakikundi cha Upendo Hisa Group cha Vingunguti Mtambani, DSM.
Baadhi ya wakazi wa Vingunguti Mtambani wakimsubili Rais wa zamani wa Marekani Bill Clinton (hayupo pichani).

Rais wa zamani wa Marekani Bw Bill Clinton akitembelea baadhi ya mitaa ya Vingunguti kwa Mtambani jijini Dar es Salaam.



 
Clinton yupo nchini na mkewe kwaajili ya kukagua miradi ambayo iko chini ya ufadhili wake.

sasa nauliza kwani hapo Kagame anahusikaje??
 
Huyu ni msimamizi wa miradi gani hapa Tz, na hiyo miradi mwananchi wa kawaida ananufaika vipi, hivi mataifa ya kigeni yanazamia Tz kwani nchi yetu in vito vya manemane, yakuti samawi, na zabarajadi?
 
Hawa wamarekani kutusaidia vizuri, na hasa kwa hii issue inayotusumbua ya muungano, wangechukua haka kanchi kawe state yao nyingine.

Mara Bush, mara Obama, hatujakaa sawa Clinton. Vigesi vyetu na urani vinawatoa macho
 
CLINTON ATUA NCHINI: Rais Mstaafu wa Marekani Bill Clinton yuko nchini kukagua miradi inayofadhiliwa na Plan International, pia kuzungumza na akina mama Vikoba.
CC. KAGAME

source. mwananchi/vodacom news alert.

Hivi kati ya hawa viongozi wote mbona sija wahi kuona Rais au kiongozi wa Ufaransa aikija kupiga mahera bongo isipokuwa hawa kina obama, hu jintao, mam tony blaire, bush, m .singh (india), mama thailand, mama uturuki, wen jiabao, etc. hakika katika nchi zinzopaswa kuwa na tuzo nyingi za ukarimu duniani ni TZ kwani mnene ajaye atakuja kununua hadi wafuasi wa magamba na kujimilikisha kwa miaka kadhaaa.
 
Anakagua miradi inayofadhiliwa na taasisi yake. Na Rwanda pia atapita.
 
...mzee wa kuchukua faida Kagame ameshasikia kuna mafuta zanzibar na huko mtwara na kwenye ziwa malawi,na migodi ya dhahabu huko shy, anataka kuja kuchimba, lazima atuchape tu...

Mkuu kagame anaiweza drc tu.. huko ka vuna kweli ila hapa atapinda....
 
Hivi kati ya hawa viongozi wote mbona sija wahi kuona Rais au kiongozi wa Ufaransa aikija kupiga mahera bongo isipokuwa hawa kina obama, hu jintao, mam tony balire, bush, m .singh, wen jiabao, etc. hakika katika nchi zinzopaswa kuwa na tuzo nyingi za ukarimu duniani ni TZ kwani mnene ajaye atakuja kununua hadi wafuasi wa magamba na kujimilikisha kwa miaka kadhaaa.

Harafu pamoja na ukarimu wetu na ugeni wao hata kunyonyesha watoto wetu hatujui, achia mbali elimu ya bora liende, siasa za hovyo, mpira hatujui, yaani shida tu. ....bin short ugeni wao hautusaidii tutaikomboa Tz yetu na hayo yote sisi wenyewe...
 
Nchi yangu Tanzania;nchi ya maziwa na asali, wanakuja kwa wingi, wote wakubwa wa dunia, kulikoni Tanzania?
 
Harafu pamoja na ukarimu wetu na ugeni wao hata kunyonyesha watoto wetu hatujui, achia mbali elimu ya bora liende, siasa za hovyo, mpira hatujui, yaani shida tu. ....bin short ugeni wao hautusaidii tutaikomboa Tz yetu na hayo yote sisi wenyewe...
kumbe kweli roma hakukosea kwenye wimbo wake wa sema tanzania.
 
Rais mstaafu wa marekani billy clinton yuko mchini kukagua miradi inayofadhiliwa na plan international,pia kuzungumza na akina mama vikoba,ndgu zangu watanzania wenzangu kunani hapa tanzania mbona kuanzia gesi igundulike marais kibao wa nchi mbali mbali wanakuja tanzania,tujiulize kama watanzania tumeshauzwa au lah!mwenye majibu naomba tusaidie kujua.

Aluta continua.
 
anakuja kuchukua vyake hivi huji kwa tanzania uraisi ni u agent??
 
salaam ziwafikie majirani zetu wenye husda na nchi yetu wanaoleta chokochoko
 
olevaroya

Kwa sasa yupo mkoa gani? Nina haja ya kusema naye mawili matatu bila shaka.
 
Last edited by a moderator:
Ni kweli hiyo taarifa ya kuwepo kwa Bill Clinton nimeipata kupitia Breaking News ya Mwananchi kama ulivyoiandika hapo, ametembelea miradi inayofadhiliwa na kusimamiwa na Plan International maeneo ya Vingunguti, na atakutana na akina mama wa Vikoba anaowafadhili, kama kuna mengine kuhusu ziara hiyo tufahamishane.
 
Back
Top Bottom