Ghazwat
JF-Expert Member
- Oct 4, 2015
- 23,718
- 66,262
Gereza la kilimo la songwe lililoko mjini Mbeya litahamishwa ili kupisha uchimbaji wa madini ya Niobium yaliyopo eneo hilo.
Taarifa hiyo ilitolewa mjini hapa jana na mwakilishi wa kampuni ya panda hill, inayotarajia kuchimba madini hayo Bw. Emmanuel Kisasi.
Kisasi alisema kwamba watahamisha pia nyumba za wafanyakazi wa gereza hilo, alitoa kauli hiyo jana wakati wa ziara ya mkuu wa mkoa wa Mbeya, Amos Makalla.
Kwa kuwa eneo lilipo gereza hilo kuna madini kampuni yetu ya Panda Hill imetenga shilingi bilioni 400 kwa ajili ya kuhamisha gereza hilo,ikiwa na pamoja na nyumba za wafanyakazi kwa umbali wa kilometa tano.
Sambamba na hilo zaidi ya wananchi 467 waliopo maeneo ya mgodi wanatarajia kunufaika kwa kupata ajira mara tu uchimbaji utakapoanza mwaka 2017
Madini hayo tunatarajia kuyachimba yatatumika kutengeneza vitu chuma, kulainisha chuma na kuwa imara zaidi pia yatatumika kwenye ujenzi wa nyumba.
Pia yatatumika vifaa vya ndege, mabomba ya mafuta, mabomba ya gesi lensi za kamera pamoja na vifaa vya kompyuta, kwahivyo tafiti tumegundua tani milioni 96.3 za madini hayo yatachimbwa kwa zaidi ya miaka 30 alisema Kisasi.
Chanzo : Mtanzania
Taarifa hiyo ilitolewa mjini hapa jana na mwakilishi wa kampuni ya panda hill, inayotarajia kuchimba madini hayo Bw. Emmanuel Kisasi.
Kisasi alisema kwamba watahamisha pia nyumba za wafanyakazi wa gereza hilo, alitoa kauli hiyo jana wakati wa ziara ya mkuu wa mkoa wa Mbeya, Amos Makalla.
Kwa kuwa eneo lilipo gereza hilo kuna madini kampuni yetu ya Panda Hill imetenga shilingi bilioni 400 kwa ajili ya kuhamisha gereza hilo,ikiwa na pamoja na nyumba za wafanyakazi kwa umbali wa kilometa tano.
Sambamba na hilo zaidi ya wananchi 467 waliopo maeneo ya mgodi wanatarajia kunufaika kwa kupata ajira mara tu uchimbaji utakapoanza mwaka 2017
Madini hayo tunatarajia kuyachimba yatatumika kutengeneza vitu chuma, kulainisha chuma na kuwa imara zaidi pia yatatumika kwenye ujenzi wa nyumba.
Pia yatatumika vifaa vya ndege, mabomba ya mafuta, mabomba ya gesi lensi za kamera pamoja na vifaa vya kompyuta, kwahivyo tafiti tumegundua tani milioni 96.3 za madini hayo yatachimbwa kwa zaidi ya miaka 30 alisema Kisasi.
Chanzo : Mtanzania