Pascal Mayalla
Platinum Member
- Sep 22, 2008
- 50,467
- 113,578
Mkuu Kokola, asante kwa hoja murua kuzungumzia harakati za uhuru bila mrengo wa udini.Bwana Mohamed Said "upuuzi" hapa halikuwa tusi ni kinyume cha hoja yenye mantiki ile isiyo na maana ndio upuuzi sio tusi kamwe!! We ndugu yangu nilichosema mimi sio kuwa hatupendi au hatuwaenzi wapigania uhuru wetu la hasha!! Tena ifike mahali wapewe hadhi ya manabii wetu lakini katika context ya Utaifa na sio udini au ukabila Kaka!! Waikela kama yeye ni shujaa wa kumtoa mkoloni kwangu na naamini kwa Watanzania wengi ni mtu muhimu sana bila kujali dini yake au kabila lake. Hapo pia, haitegemei kutembelewa kwake na "mwanasiasa kijana aliye mashuhuri - Zitto Kabwe". Historia yetu imeandikwa na wageni sisi ndio sasa tunaamka kama anavyotaka kuamka rafiki yangu Paskali. Kama hao mashujaa hawakuthaminiwa au hawakutanjwa kwenye historia basi isiwe kuwa tuone ni kwa ajili ya dini zao bali tu kwa ajili ya kile walichokuwa wanakipigania ambacho mgeni alieandika historia hakukipenda. Wewe kama kijana wa sasa rekebisha ukisisitiza Utaifa na sio udini.
Paskali