Ndio mimi nilikua nawaambia watu humu ndani wana misconcept unplanned settlements na slums.Wewe huenda huijui Manzese na hujui maana ya 'Slum' zinazozungumziwa hapa, unaisikia.
Mazingira ya Manzese kwa zaidi ya 80% yameboreshwa vizuri huenda kuliko makao ya miji mingi hapa Tanzania.
Wewe ulishawahi kuona wapi slum ambayo:
1. Imejaa barabara za lami mitaani
2. Imejaa nyumba za maghorofa za kisasa
3. Utitiri wa hoteli za kisasa, lodge, bar, migahawa, mini supermarkets, kumbi za starehe nk.
4. Imejaa taa za barabarani za usalama za usiku.
5. Imejaa miundo mbinu ya mabomba ya maji, umeme na mitaro ya maji machafu.
6. Kuna shule binafsi nyingi la 'English medium'
7. Utiriri wa misikiti na makanisa makubwa/kisasa.
Nenda manzese utaona hayo.
Characteristics za slums;
*Low/poor building quality.
*Lack of sanitation.
*Lack of electricity.
*Lack of essential infrastructures like roads,hospitals,schools e.t.c.
*Lack of pure,clean and safe water.
Sasa Manzese,Tandale,Buguruni,Mwananyamala huko kuna nyumba za tofali,Kuna barabara,Kuna shule,Kuna hospitali,Kuna maji safi na salama,Kuna mfumo wa maji taka,Kuna umeme n.k n.k.
Je hivi vitu Kibera unaviona!??
Kibera Kuna nyumba za mabati,umeme hakuna wa uhakika,hakuna barabara za uhakika,hakuna mfumo wa maji taka hata picha zimeonesha watu wengine wamejenga pembeni ya maji taka yaliyosambaa.
Halafu mtu anafanananisha Kibera na Mwananyamala.
Tanzania Kuna UNPLANNED SETTLEMENTS TU.
Ila sio slums.