Biblia na reference ya vitabu vya kipagani

Ukweli sijakisoma na wala hata sijui vinakopatikana though bado ninashawishika kuamini kua "haviwezi kua vya kipagani" kwasababu ya waandishi wake! Hapa na refer vitabu ulivyo vitaja, sina hakika na vingine ambavyo either sivifahamu au ambavyo hujavitaja kwenye UZI wako!
 
Kwa mtazamo wangu (najua Wakristo wengi, sio wote watakubaliana na mimi). Quran na Biblia havijatokana na source moja; Hakuna Mkristo wa kweli anae amini kwamba Quran ni kitabu cha Mungu wa mbinguni aliyeziumba mbingu na nchi, siwezi zungumzia msimamo wa Uislamu kuhusu Biblia, hilo wao ndio wanaweza kusema and this is why, huwezi kumkuta Mkristo anafanya reference ya Mungu through Quran ingawa wapo Waislam wengi hufanya reference ya mambo ya Mungu kupitia Biblia. Kwenye hili tunaweza kufungua UZI tofauti na hu na tukaendeleza mjadara huko na mimi nina ahidi kutokashfu IMANI ya yeyote
 
Mkuu Zitto Jr, kwanza niseme wazi, nimependa jinsi unavyo dadavua, hushindani bali unajenga HOJA, something which I also like. Wakristo wanao bisha hapo kwenye Bold, waende wakasome kwenye Biblia tena kitabu cha Mwanzo sura ya 6 kama sikosei, inasema the same thing na alicho kisema Henoko, na hapo kwenye italic, again sioni kama ni tofauti na Biblia, the issue is, hivi kwa mfano leo hi wanajeshi wote wa JMT (police, wanajeshi, mgambo, TISS, magereza etc) wote wauawe kwenye battle (nasema battle na sio vita) na amiri jeshi mkuu ndio awe amewatuma, tafsiri yake kwa mkuu wa nchi hapo ni ipi kama sio KUFA tu!? Nasema kafa kwasababu hawezi tena kutamba kwa lolote maanake hana security (kauri kama, ningeanza na shangazi zao hawezi tena kuzitamka zaidi tu ya kwenda kupiga magoti kwa huyo aliye ua hao askari wake) Remember Biblia inasema, nguvu ya mfalme ni watu wake, hivi kwa sisi tusio jua kutumia bunduki tunawezaje kua "nguvu ya mfalme?" But again, Kibiblia kuna namna 3 ya mtu kufa! Ya kwanza ni hiki kifo mtu anakufa na tunakwenda kumzika, ya pili ni mtu wa Mungu kumuacha Mungu na kurudia DHAMBI, hicho nacho ni KIFO na aina ya tatu ni hiki, mtu aliyekua MPAGANI (with this case is Pharao) na kumrudia Mungu, huyu nae amekufa, yaani matendo yake ya mwili yamekufa na kule kubatizwa ndio anazikwa na kufufuka na kua mwili mpya. SO bado sijaona tofauti ya Henoko na Biblia (ingawa hicho kitabu sijakisoma)
 
Hakuna wakujibu hilo swali

Ila tunaomba ututoshelezee tamaa yetu ya kuunga Doti

Mwagika mkuu....[emoji101][emoji101][emoji101][emoji101]
 
Kumbe kila kitabu nje ya Biblia ni cha kipagani?? Na kama vitabu ulivyoorodhesha hapo vipo, ungetoa ushahidi kama mfno!
 
nimerekebisha,wanasema linazama kwenye bwawa la maji
jua linazama kwenye bwawa tokea lini?
Wanaosema hivyo nani? mbona nishakwambia sijawahi kusikia waislamu kufundishana kuwa jua huwa linazama kwenye matope wala kwenye bwawa la maji,Ni wewe ndio nakusikia ukisema hayo.
 
labda nikwambie kwamba hawakupata tabu sana,wali-plagiarize maandiko yaliyokuwepo kabla mfano maandiko ya wamisri kwenye kitabu kinachoitwa the papayrus of ani
Hayo maandiko yalikuwepo kabla ya nini?
 
Mtume hakuwahi andika Quran, alikuwa anateremsha maneno kwa imla (anapandwa na mzuka/anawehuka kwa kiswahili kibovu).
Kwani ndugu yangu huwezi kujadili kwa lugha ya staha? Au ni hasira kwakishindwa kumjibu Zito junior?
 

Judaism has as its holy book the Hebraic Bible. This differs from the Old Testament of
the Christians in that the latter have included several books which did not exist in Hebrew.
In practice, this divergence hardly makes any difference to the doctrine. Judaism does not
however admit any revelation subsequent to its own.
 
Kwani ndugu yangu huwezi kujadili kwa lugha ya staha? Au ni hasira kwakishindwa kumjibu Zito junior?
zitto junior ni jamaa yangu sana humu JF 🙂.
Kuna manabii kama Daniel walikuwa wanapewa ufunuo kupitia ndoto, yani mpaka walale ndio wanaoteshwa then asubuhi wanakuja ongea walichoota!. (Ni simple kuelezea hili tendo eeehh!?).
Sasa kuna huyu Mtume Muhammad yeye alikuwa halali kuelezea taarifa anazopewa!. Nikuombe unisaidie kuielezea hiyo hali 'kwa lugha ya staha' unayoielewa wewe babu na mjukuu ila kumbuka kuweka hii hoja "mtoa taarifa hakuwa anajua kusoma wala kuandika!".
Sijashindwa kumjibu zitto junior sababu hoja zake zilibase kwa watu mnaotaka referance za kwenye bible pekee!. Ukiiifatiria michango yangu humu Intelligence Forum utajua nipo upande upi wa story!.
 
Sasa kama Lutu aliweza kulala na binti yake kwanini unaamini daudi hawezi fanya uhuni?? Mbona alimlala mke wa mwanajeshi wake na baadae akamuua kabisa?? Who is David mpaka asifanye huo uhuni??
Lutu alilala na binti yake kwa kupenda mwenyewe!
 
Dini inaingiaje hapa?? Tujikite kwenye hoja kwamba JF wafia dini mbadilike mfungue akili yenu na mkubali maarifa kutoka vyanzo tofauti sio kila hoja mpaka bible

Anyway nimeweka hapo maswali labda tusaidiane kujadili hayo tupate majibu
Weee niajenti wa shetani utawapata wajinga kama wewe pepo kabisa wewe.
 
Wewe unajua kabisa kuwa kulikuwa na mitume na walikuwa na vitabu,sasa hoja ingekuwa kipi kimepotoshwa na yapi yameongezwa katika hayo mafundisho yaliyo kwenye hivyo vitabu?
Ila waliotangulia ni wayahudi as wayahudi kupitia Tanakh/Torah ambayo Biblia pia imeazima na kutumia kwenye agano la kale lakini kuanzia agano la jipya maandiko ya wayahudi na wakristo yanakinzana then baadae wanakuja waislam nao wanakinzana na both jews and christians hivyo kama hoja ni kwamba wa kwanza ndio mkweli basi dini ya wayahudi ambayo haimtambui Yesu kama messiah ndio inayosema ukweli if at all tutachukua definition yako kwamba wa kwanza kuandika ndio mkweli.
 
Kweli
vidole vyenu havina macho
na macho yenu hayana nuru
na akili zenu,hazina akili

Ipo siku,tutajua tu
uliempanda ni Punda au Farasi!!!
Lutu alilala na binti yake kwa kupenda mwenyewe!
 
Nimeviita vya kipagani sababu vinapingana na Biblia ndio maana nikakuhoji kama sio vya kipagani ina maana Book of enoch ni sahihi licha ya kupigana na Biblia?? Je ina maana Book of Jasher ni sahihi licha ya kupingana na Biblia

Kwa mtazamo wako maneno ya Mungu yanaweza kukinzana?? Kama hayawezi niyaitaje hayo maandiko yanayopinga Biblia bila kujali ni ya Nabii gani??

Naomba unisaidie jina la kutumia ili mods waedit kichwa cha habari
 
Nimekuwekea link ukavisome na hivyo jasher na enock sijavitaja ila nimesummarise kuwa viko zaidi ya 20 vingine..... Ndio hivi viwili vinaingia ingawa na vyenyewe vinakinzana na Bible hivyo unaposema sio vya kipagani unaniacha na maswali mengi sana kwamba je maneno ya Mungu yanakinzana??

Alafu kwanini tunatishika na majina?? Ina maana leo mwakasege akisema HAKUNA MBINGU hutomuita ni mpagani kisa ni "mtumishi" wa Mungu

Upagani hatuangalii status ya mtu bali tunajali KAZI yake.... Hivyo haijalishi kama Enoko/Gad/Nathan alikuwa ana status gani ila kwa wakristo wanaamini as long as anakinzana na Biblia basi anageuka MPAGANI by his writings.

I hope tunaelewana hapa
 
Ikiwa akili haina sifa timilifu
Hata kama watakusanyika watu wote,Bado sifa itabaki pale pale,nayo ni kutotimia asilimia 100
Unapomuoma mtu,anakuwa na jeuri na nguvu bandia,mpaka kumjadili Muumba mbingu na ardhi au kuwajadili Manabii wa Mola
Basi,sifa yake ya upunguani,ndio inajidhihirisha kidogo kidogo
atafika sehemu
atamkana mpaka Mama yake mzazi,na kukana haki zake
atakuja kumuoa Mama yake,huku akiuliza
Ni nani ameweka sheria hizi?!!
atamuoa mpaka Dada yake tumbo moja
huku akijiona kuwa yupo sawa

Tunamshukuru Muumba mbingu na ardhi,kwa kutupa mwangaza sahihi wa kumtumia yeye tu
Hakuna Mola apasae kuabudiwa kwa Haki,isipokuwa Mola mmoja tu,na Mohammad ni Mtume wake
Shukran
 
1: Hadi Yesu anakuja Standard bible ilikuwepo. Walikuwa hawasomi kila kitu mwenye masinagogi kama maandiko matakatifu.
Hicho kilichokuwepo kwenye Hekalu na masinagogi ambacho hata Yesu alikisoma na akasema kinamuelezea yeye ndio bibilia ya wakati huo.
Kama nilivykupa mfano wa jinsi yalivyohifadhiwa. Ndio maana Yesu alisema '' Mwayachunguza maandiko'' alikuwa hazungumzii vitabu vya kufikirika kila andiko lililokuwepo. na hivyo unavyosema sijawahi kujifunza popote kuwa enzi za Yesu vulikuwa ni maandiko matakatifu na Yesu hakuwahi kuviquote au kuviendorse.

Bibilia inasema maneno ya manabii huwatii manabii ikitokea kuna ukinzani hapo kuna sababu ya kujiuliza kwa nini. Ila ikiwa maelezo na mafunzo ya samweli yanaumana na waandishi wenzake wa bibilia ila yanakinzana na huyo Gadi. Muamini Samweli. Kuhusu daudi kutenda dhambi haijalishi ziliandikwa zote au kadhaa, ikiwa alitembea katika mwili alikuwa prone kufanya kila aina ya uovu. Ila ukweli ni kwamba alimrudia Mungu, na Mungu akasema hakuna mtu aliyenipenda na kunitii kama Daudi kuonyesha Mungu anasemehe na kutupilia mbali makosa ya kale.
Katika maandishi ya kiyahudi ambayo yalitambuliwa kama Maandiko matakatifu kwa Uongozi wa Mungu, Unaushahidi wowote kuwa walikuwa wanakitabu CHA GADI, au tukienda kwenye masinagogi yao Tutaambiwa hilo? kama sio Basi Kitabu cha Gadi kitabaki kuwa kitabu ambacho sio Maandiko matakatifu. Ukiambiwa habari za mkwawa utazikuta kwa mchawi mkuu wake haimaanishi kila kilichoandikwa na mchawi huyo ni sahihi.

2: Wakinanani hao, unaweza kufunguka zaidi. maana compilation ya bibilia inamambo mengi ya kuzungumzia.

3: Licha ya hiyo changamoto. Kikubwa ambacho nakisisitiza ni doctrinal consistence ya hivyo vitabu 66 ya bibilia. Fact kuu ni kuwa hakuna og mauscript
hivyo ushahidi wa kuungana mkono kwa vitabu hivyo, Lakini pia magombo mengi ya kale yanayovumbuliwa yanaonyesha kuwepo kwa barua nyingi zilizokuwa zikisambaa katika makanisa ya awali na ufanano wa kimafundisho na misistizo ambayo inaungana kama mnyororo kuanzia mwanzo hadi ufunuo. Usadikisho wa Lengo kuu la Mungu kwa mwanadamu mdambi unapatikana katika vitabu vyote. Ila hivyo unavyotaka viingizwe kama authority sawa na bibilia ambavyo havina idadi na vingine licha ya kuwa na sehemu chache zinazungana na bibilia tunayoiamini vina mavitu mengi ya ajabu yasiokidhi viwango vya kuingia katika mnyororo wa Mwanzo hadi Ufunuo. Yaani anguko la mwanadamu, Wokovu kupitia Yesu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…