Biblia na reference ya vitabu vya kipagani

Na kuna other schools of thoughts kuwa Noah aliingiliwa kimwili na kuhasiwa na mwanawe ili asipate mtoto wa nne ndio hasira zake kumlaani mtoto wa nne.
Google.com.Catholic dictionary.
Duuh dunia ina mengi sikuwahi isikia hii mkuu
 
Mkuu nilifikiri pia hata waislam huwa wanaquote hadeeth kadha wa kadha ili kupanua uelewa wa masuala fulani ya imani yao
Ndio wanaquote lakini ni tofauti na Bible ambayo km ulivyonukuu inakuambia uende kwenye kitabu fulani, Qur'an yenyewe ina conclude yenyewe haiitaji msaada wa nyongeza kwenye vitabu vyengine .
 
kwani kwenye huo mkutano wa Nicea walitaja sababu ya kuviita hivyo vitabu kuwa ni apokrifa??
Yes kwamba havikuwa na uvuvio wa Roho mtakatifu na havikuandikwa na manabii wanaotambulika na vingine viliitwa forgery kabisa..... Ndio maana hata kwenye Biblia ya ya Vulgate apokrifa vilitengwa kabisa havikupewa hadhi ya Vitabu vile 66 vya Biblia!!
 
Kungezea kidogo hapa, mtoa mada au mtu mwingine yyte anatakiwa afahamu kuwa kuwa biblia inajitosheleza ktk kumpeleka mtu mbinguni ambapo ndiyo lengo na msingi wa ukristo. Inawezekana vitabu vikawepo sawa lakini ktk kujenga msingi wa safari yetu vitabu hivi vinatosha na ilishatambulika kadhia kama hizi zitatokea na hivyo kukawa na stance ktk bible kuwa usiongeze hata nukta moja. Siyo usisome, unaweza kusoma lakini usii distort bible iache kama ilivyo ipo ktk msingi sahihi.
 
Mkuu labda hoja yangu haikueleweka ni hivi Yuda alimquote Book of Enoch sura ya 6 ili kujengea hoja kuhusu kurudi kwa Yesu na pia Joshua alijengea hoja kutumia reference ya kitabu cha Yashari

Sasa mimi zitto junior nauliza je nikiquote let's say Book of Enoch kuhusu malaika kuzaa na wanadamu.... Au kitabu cha Yashari kuwa Kaini aliuawa na mwanae ntakuwa nafanya makosa

Hapa ndipo napouliza
 
Mkuu nimeelewa hoja yako sana tuu bosi na Mimi pia nielewe. Mfano biblia haijatoa taatifa ya vifo vya mitume wengi wa Kanisa la kwanza aliloacha Yesu lakini Mimi na wewe tunajua kwa wakati ulivyokuwa ingewezekana kila ntume wa baada ya Yesu kujulikana vifo vyao na vingewekwa ktk bible lakini hilo halukufanyika. Vifo vyao vipo ktk historia za machapisho mbali mbali na yameweza kuthibitika kbsa. Point yangu hapa ni hii mengi yalioandikwa ktk bible yanalenga kumshape mtu aelekee ktk njia ya kwenda mbinguni. Pia kuna mengi y ukweli yameachwa, yale yaliyowekwa yanakidhi na kujitoshelza kikamilifu ky serve the purpose ya Ukristo. Sikatai uwepo.

Kukwoti hivyo vitabu??
Hapa inahitajika uthibisho sana kuhakiki kuwa kweli kitabu cha Gadi ni kile kile au kitabu cha fulani alichokiandika ni kilekile. Pia kumbuka vitabu vya kifalme si kazima viwe vinafaa kwa fundisho la neno la Mungu. Ndiyo maana kwa maneno yako ktk bandiko lako umekwoti yakihusisha habari za vizazi nafkiri biblia ilitaka ktk msingi wake tufahamu hicho tu ktk hicho kitabu labda mengine yanawalakini au hizo rekodi nyingine hazijafaa kwa fundisho
 
Mkuu mitale na midimu nimekuelewa hoja yako ila labda nigusie mambo machache

1. Unaposema kuwa hakatazwi mtu kuquote "nje ya Biblia"as long as unaangalia context..... Je ni wakati gani ambapo manabii walijua Biblia inasema A na wao wakaandika B ilihali mpaka Yesu anakuja hakukuwa na standard bible?? Nachojua ni kwamba baada ya wote kuandika ndio wakatokea watu miaka 300 baadae wakasema huyu anakinzana na huyu ndio maana vikatolewa na vingine vikaachwa Ndio kina Enock na Mwandishi wa Jasher na vitabu vingine vya kufanana wakawa victims wa hilo tokea mwanzo kabisa.

Kuhusu kuquote nachojiuliza sio tu kwa kuangalia muktadha ila Biblia mfano kwa story ya Daudi inasema historia ya Daudi MWANZO MWISHO na hata Rehoboam MWANZO MWISHO vimeandikwa kwenye kitabu cha Gadi n.k sasa je hapo nikienda kusoma na nikagundua inconsistency juu ya story ya daudi katika kitabu cha samweli/wafalme na kitabu cha gadi/Nathan je ntakuwa nina makosa kushikilia msimamo wa kitabu hicho???

2. Mkuu wanaosema vimepotea sio mimi ni hao hao waliocompile Biblia kuna apokrifa zilikuwa termed as LOST BOOKS yaani vilipotea katika uso wa dunia mfano kitabu cha shemaya kipo katika kundi hilo na ushahidi wote wa kiachiolojia unaonyesha manuscript zake zilishapotea kitambo unless una ushahidi mwingine kuwa Manuscript za book of shemaya,Gadi na Nathan bado vipo unaweza kutusaidia mkuu.

3. Mkuu kuhusu uandishi hilo jambo halipo kwenye Book of Enock pekee hata Wimbo ulio bora au barua kama 7 za paulo ni pseudepigrapha yaani havina ushahidi kuwa viliandikwa na paulo au paulo maana vimeandikwa vingi baada ya kifo cha paulo..... Mfano waebrania ni pseudepigrapha ila kwenye bible kipo hivyo sidhani kama hoja hii ya uandishi au backdating ya apokeifa ina mashiko tena hasa ukizingatia backdating/auhtorship crisis hata ndani ya Bible vipo according to theologians.

Ubarikiwe
 
Yes kwamba havikuwa na uvuvio wa Roho mtakatifu na havikuandikwa na manabii wanaotambulika na vingine viliitwa forgery kabisa..... Ndio maana hata kwenye Biblia ya ya Vulgate apokrifa vilitengwa kabisa havikupewa hadhi ya Vitabu vile 66 vya Biblia!!
doh!
ufafanuzi kwenye hiyo biblia ya Vulgate mkuu
 
Allah anasema hichi ni kitabu kisicho na shaka ndani yake
Na pia akasema "wanasema hii Quran umeindika wewe muhammad basi walete mfano wa kitabu hichi watafute na wasaidizi
Pia akasema walete mfano wa sura moja kama wanasema kweli

Pia akaseama hata tungelishusha Kitabu hichi kwa mfumo karatasi bado wasingesadiki

Na akasisitiza "hich ni kitabu chetu na tutakilinda kwa na aina upotofu"

Mtume Muhhamad aliteua waandish 12 akiwemo Uthuman na Zeyd ambae ndio anatajwa kuwa hafidh mkubwa wa Quran...wakati mtume yupo Quran ilikiwa imeandikwa kwenye magome ya miti na majani na na nyingine imehifadhiwa kwenye maktaba ya kiislam, wakati Umary ndio khalifa alimua kuiweka Quran katika mpangilio wake sababu wakati wa Umar tecnolijia ya kuandika kwenye ngozi ngumu ilikuwa imenza so akaamua kuipangilia kwa mfumo wa kitabu baada ya umary kuondoka akachukua madaraka Uthuman ambae alikiwa msomo na mmoja wa waandish wa Quran wakati wa mtume, alipoluwa safarin oman alikuta Watu wanasoma Quran amabayo imekosewa baashi ya matamshi kwa sababu wakati Muhhamad amewateua wale 12 hakuzuia wengine wanaoweza kuandika waandike wengine walikuwa wapita njia na walikuta muhhamad anateremsha aya nao waliziandika ila mtu ali double check tu kwa wale aliowateua so sababu kubwa ya hao watu kuwa na Quran yenye mapungufu ya kimtamsh ambayo yangebadili maana....

Ndipo Uthaman akarud Makka na akawaita wale waandishi by that time walikuwa wamebaki sita wakaandika Quran Upya kwenye ngozi kwa kipindi hicho teknolojia ilikuwa ime advance na kaagiza watu wote kwa kipindi hicho waende waka copy Quran ile walioyoiandika wao na kila mtu achome moto copy yoyote ambayo yupo nayo iwe ina mapungufu au haina mapungufu...na Quran ile aliyoiandika Uthaman ipo had leo maktaba ya Uturuki na ipo sawa sawa had leo ukilinganisha na Quran tuliyonayo leo..

Uthaman amendika Quran hiyo miaka 10 tu baada ya kufariki muhammad so watu wengi walihifadh Quran walikuwa bado wapo ndio maana hakujatokea utata qa copy za Quran na ukiitazama Quran kwa structure utagundua hakuna mwanadamu anaweza kuindika hata Uthaman angejaribu kuhujumu bado angeshindwa...kasome kitu kinairwa Quran in Numbers utaona miujiza ya kimoangilio na ndio maana Mungu kajitapa anaeweza alete japo mfano wa kitabu hiki,baadae akasema alete mfano sura moja baadae akasema alete mfano wa aya kumi baadae akasema alete japo mfano wa aya moja...hii yote ni kwa sababu ya structure yake na mahesabu ukiacha ujumbe uliyoibeba humu ndani...ndio maana inaitwa LIVING MIRACLE..!

Ujinga ujinga mwingi unaandikwa juu ya Quran na watu wengi tu ila ukiamua kufata vyanzo sahihi utaupata ukweli Quran ni moja tu duniani
 
Hapa Mkuu umezalisha maswali mengi kuliko majibu,kwa sababu sio lengo la Uzi huu kujadili Quran na uandishi wake! Basi Inshallah! upo wakti wake.
 

Thank you again Zitto Jr.
From today I shall be calling you - Zitto Jr. The Athenian.
Nijikite kwenye mada na kujaribu kujibu Maswali ya Msingi ninayodhani ndio kichocheo cha Mada.
BIBLIA NA REFERENCE YA VITABU VYA KIPAGANI.
Kwanza kabisa hakukuwahi kuwa na Vitabu vya Kipagani kabla ya dola ya Warumi kutawala.
Vitabu vyote! Hoja zote na Mabishano yote hasa wakati wa dola ya Wayunani walihoji kila kitu na Maswali ya Msingi yalikuwa juu ya Mungu ni nani na ni nini hatma ya Maisha haya baada ya Kifo.

Neno Upagani ni neno lililotoka katika lugha ya Kirumi "Paganus" Mtu wa kijijini / mtu wa shamba! Hii ilihusishwa mtindo wa Maisha na Uelewa wa wahusika hao wa shambani (Villagers) na imani yao( Believing differently from the popular belief).
Wapagani walidharauliwa na hata vitu walivyoviamini havikuheshimika kabisa;ikawa basi kila andiko na falsafa isiyo popular ina be termed as Upagani.Leo picha haijabadilika sana! mpagani yuleee! haamini unachoamini wewe! Sio Mkristo wala Muislam! (katika Mazoea ya Kitz).Vitabu vya Kipagani ni Vile Vilivyoandika mambo tofauti na Mazoea ya Jamii fulani.
Neno Upagani limepata nguvu na ushabihi kwa vile vitabu vilivyoandika tofauti na Biblia ama vimeandika kupinga hoja ya Biblia kimantiki.

Ili kufahamu sasa! Iwapo Kitabu hiki ni cha kipagani ama la? yaani kimebeba Ukweli au shaka ni kwa kuilewa Biblia yenyewe kwanza.

Biblia ni mkusanyiko wa Vitabu Vingi.Wanatheolojia wengi ( ingawa sio wote) na wakristo wanaamini kabisa kuwa Biblia Haina makosa! (inerrancy).Nisijadili sana hili kwa leo.

Wakristo baadae wanakuja kutofautiana - Waprotestanti wanavikataa baadhi ya Vitabu kuwa haviko sawa (Apocrypha) Wakatoliki wanavikubali kuwa havina shida na kila upande unatoa sababu zake za msingi.
Ukielewa Asili ya Vitabu vya Biblia na uandishi wake na mamlaka ya uandishi huo unakuweka huru kabisa.
Vipo Vitabu vya Sheria,Historia,Hekima,Vitabu vya manabii wakubwa na wadogo ( agano la kale) - Zipo Injili,Nyaraka za paulo na nyaraka zingine.(agano jipya).
Uandishi na Uhalali wake Unapimwa kwa Vigezo na ushahidi mbali mbali likiwemo hili la ku-Cross -reference out of the bible.
Bible survey na Historicity ni Ngao kuu katika Kupima andiko hili linamashiko ama la?


Twende kwenye Hoja ya Mfalme Daudi alikuwa na mahusiano ya Jinsi moja! Hii haina mashiko kabisa.
Biblia haina lengo la Kuficha Uchafu wa mtu hapa! Iwapo Daudi aliiba Mke wa Uria na Biblia(Vitabu vya Historia) vikaibua jambo hili kwa uwazi na adhabu iliyofuatia! sembuse Swala la ushoga ambalo Biblia imesema kabisa Wafiraji hawataurithi Ufalme wa Mungu na Torati(Vitabu vya sheria) ilikuwa wazi kabisa juu ya watu wenye tabia kama hizo - Miji ya Sodoma na Gomora iliteketezwa kwa sababu ya Ushoga na matendo ya Dhambi kinyume cha asili; leo hii jambo kama hilo liwepo Biblia ifiche au labda waandishi waruke?Hapana.

Vitabu nje ya Biblia Vilivyokataliwa Vilishindwa Kujitetea Vyenyewe hivyo vikakosa hadhi ya Kuwa sehemu ya Maandiko ya Biblia na Moja ya Sababu ni Historicity of the Events and Bible survey. Ukianza kuchambua kitabu kimoja baada ya kingine Tutachangia hapo mkuu.

Basi, Paulo alisimama mbele ya baraza la Areopago, akasema, “Wananchi wa Athene! Ninaona kwamba nyinyi, kwa vyovyote, ni watu wa dini sana, 23.maana nilipokuwa napita huko na huko nikiangalia sanamu zenu za ibada niliona madhabahu moja ambayo imeandikwa: ‘Kwa Mungu asiyejulikana.’ Basi, huyo mnayemwabudu bila kujua, ndiye ninayemhubiri kwenu. 24.Mungu, aliyeumba ulimwengu na vyote vilivyomo, ni Bwana wa mbingu na dunia; yeye hakai katika hekalu zilizojengwa na watu. 25.Wala hatumikiwi kwa mikono ya watu kana kwamba anahitaji chochote kile, kwa maana yeye mwenyewe ndiye anayewapa watu uhai, anawawezesha kupumua na kuwapa kila kitu. 26.Kutokana na mtu mmoja aliumba mataifa yote na kuyawezesha kuishi duniani kote. Aliamua na kupanga kabla kabisa lini na wapi mataifa hayo yangeishi. 27.Alifanya hivyo, ili mataifa hayo yapate kumfuata, na kama vile kwa kupapasapapasa, yapate kumfikia. Hata hivyo lakini, Mungu hayuko mbali na kila mmoja wetu. (Matendo 17:22- 27.)

Asante Kiongozi.
 
Mkuu nafikiri bado kuna kitu tunakiacha.... Unaposema biblia ilitaka tufaham hicho tu ila mafundisho mengine yana walakini hapo unaniacha njiapanda mfano

1 wafalme 11:41
41 Nayo yaliyosalia ya Sulemani, mambo yake na yote aliyoyafanya, na hekima yake, je! Hayo siyo yaliyoandikwa kitabuni mwa mambo yake Sulemani (Book of Acts of Solomon)

Hapa Bible iko clear kabisa kwamba YOTE ALIYOFANYA.... YALIYOSALIA.... Ikimaanisha story ya solomon in depth imekuwa referred kwenye hicho kitabu kizima na sio part ya hicho kitabu. Same kwa story ya daudi na rehoboam. Sasa basi kama kitabu kizima kimekuwa referred hapa je ina maana tukigundua hicho kitabu kina incosistency na kitabu cha wafalme (Maana bible haikuwepo bado) tuchukue msimamo wa kitabu gani?? Wafalme au acts of solomon,Book of Gad etc???

Na ndio hapo narudi kwenye swali la msingi kwamba kama manabii walikuwa huru kurefer biblical stories kwa vitabu ambavyo havitambuliki na Biblia ya sasa je na sisi tukifanya itakuwa kosa?? Na kama ni kosa why kwa manabii haikuwa kosa wakifanya hivyo??

Pia kuhusu credibility ya kama hivyo vitabu ndio hivi vilivyopo nafkiri huo ni mjadala mwingine sababu wanatheolojia wengi leo wanakiri hata barua za paulo hakuandika zote yeye as yeye na badhi ya tafiti zinaonyesha barua hizo ziliandikwa kuwa kwenye mfumo wa ''kitabu'' miaka mingi baada ya paulo kufa kwahiyo tukijikita kwenye hoja hii itabidi hata tuwekee mashaka baadhi ya vitabu vya bible juu ya uandishi wake.

Lakini pia kama hivyo quoted vitabu vitakuwa vimechezewa kama unavyohisi labda niulize je nini hatma ya maneno ya Mungu kama yanaweza kuchezewa na wahuni wachache??ina maana mwanadamu anaweza pambana na maneno ya Mungu hadi afanikiwe?

Mkuu embu tuwekane sawa hapo
 
Matope ya wapi hayo mkuu na hadi leo hayo matope hayajakauka?
inachekesha san
hawa watu hawaelewi kuwa nikiweka mada humu au comment nakuwa nimeifanyia utafiti
wa kuijibu hadi sasa sijamuona zaidi ya kurukaruka tu,ukristo na uislamu wote wanatia huruma na kuxhekesha tu

kuna watu humu wanaleta nyuzi humu ingawaje wanaujua ukweli kuwa biblia na quran ni upuuzi mtupu lakini wanataka kuwa 'politically correct" mfano zitto junior ambaye ni mtoto wa juzi tu kwenye haya mambo ukilinganisha na sisi watata wa siku nyingi
anaujua ukweli lakini anaogopa kupoteza wafuasi
mimi namshauri aache kuwapq matumaini ambayo hayapo sababu nikimsoma naona anaujua ukweli ila hataki kupoteza wafuasi wapuuzi aliojijengea humu wanaoamini hadithi za biblia na quran ambazo kudebate na mimi wanaogopa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…