Biashara ya nguo, viatu, mikoba na cosmetics kutoka Uganda

nimesoma nacheka huu uzi. Wewe dada nikiacha mengine yote ya kupata waliokupa namba za simu, mara sijui pm muwasiliane mara mkutane mwanza mie nakushauri kama ifuatavyo.

Kuna Uzi humu ukiutafuta unaelezea sana habari za Uganda na Wengine tumetoa uzoefu wetu wa kwenda mara ya kwanza.

Nakusisitiza nenda peke yako. (Sijui umenielewa)?

Siku ya kwanza nilienda peke yangu, sikutaka kupelekwa na mtu nisiyemfahamu. Sasa ukiona yafaa wewe pelekwa na mnaokutana humu uone. (Utaliwa mpk ushangae) we si mwanamke wewe

Sikwambii ufanye nn, ila soma nilivo safiri itakusaidia. Nilienda kukata uhamiaji hati ya dharula ya kusafiria. Kama sikosei ilikuwa 15000/=

Nikapanda gari ubungo, safari ikaanza, nikalala kahama, hapo nimevaa soksi ndefuuu mpk mapajani za mpira humo nimepanga maburungutu ya millions zangu, alafu nikavaa suruali pana tu.

Kesho yake asbh tulitoka kahama nikaingia kampala saa 9 au 10 hivi. Safarini tayari kwenye gari kuna wafanya biashara tulianza kupiga stori njiani (huwakosi) ila sikuwaonesha mie ndio first time

Katika stori tu njiani, nilijua gest ya katikati ya mji, majengo ya bidhaa, lakini pamoja na yote nilitoka na ramani ya hivyo vyote hapa jamii forum (uzi upo) unaeleza mpaka gesti.

Tuliposhuka stand nikachukua boda nikamwambia nipeleke gest flan, alipojua mie Mtanzania akabadili lugha akaanza kugonga kiswahili (kibovu lakini). Prrrrrrrrri tuk tuk mpaka gesti nikalipia elfu 25 ya Uganda ilikuwa kama elfu 15/16 ya Tanzania. Nikalala

Hii gesti niliolala ingekuwa Tanzania basi nimelala karikakoo kabisaa, ukitoka nje ni maduka. Basi asbh mzee nikaanza kukata mitaa mwenyewe napita jengo mpk jengo na study. Lakin nilipolala hapo walilala pia watanzania wawili waanya biashara wazoefu, na mkongo mmoja ambao jioni ile kulikuwa na match chini sehemu ya chakula tukakaa tunapiga stori kabla ya kulala

Aisee katika story walinipa madini sana ya biashara, zinavofanyika, kupita mpakani, na kuongeza kipato kwa kubeba mzigo unapokuja uganda na unabeba unaporudi. So hakuna kusafiri kiboya.

Aisee ni mengi, siwezi eleza yote. Kesho yake kama nilivoeleza hapo juu nikafanya kuzunguka mwenyewe nikajua mengi, nikarud kulala kuwa sasa kesho naenda kununua. Usiku huo pia wakaja watanzania watatu wanawake pale lodge. Wawili toka dar, mmoja kigoma.

Aisee wale wadada tulikaa tujapiga story wakanipa ramani hadi nikahsi naamka tajiri leo. Kesho yake nikaingia nao madukani japo tuliachana, kila mtu akawa bize kufunga mzigo, ukishafungwa moja kwa moja kwenye gari. Kesho yake alfajiri safari

Hapo mnarudi njiani mko wengi, na stori kama zote (naimani ushanisoma eeh?) Utapewa mbinu na kila ujanja.

Dada imetosha. Ondoka nenda, mpk unafika ushakuwa mwenyeji. Kila la kheri.

Dumelang
Nimekielewa ulichokiandiaka mkuu.
 
Habarini wakuu wa Jamvi nilisahau kuleta mrejesho ...nilikwenda UG na mambo ni mazuri sanaaa... Nilifata ushauri wenu na sana sana Dumelang ulitoa ushaur mzuri na niliufanyia kazi 100% .. Na nshapiga trip za kutosha na mwezi November nasafir tena Mungu akinibariki uzima ....
Asanteni sana kwa muongozo
Hongera sana
 
Narudia kukujibu tena ukiona sikujib vizur kuna wengi walioshaur mwanzo kwnye huu Uzi sawa boss ...sina uzoefu na border kma m nimeenda kuchukua nguo za m2 na ww ukaenda kununua spear unategemea waangalia mtaji wako au wanaangalia bei ya vitu ulivinunua shngap huko UG , second m sio TRA sina nguvu ya kuongea chochote kuhus kodi jomba ...nenda kapambane na ww ujue border inauzoefu gni
Mmhh
 
Uganda nguo ni bei nafuu sana kwa sababu nchi za America,Asia na Europe zimefanya uganda kama sehemu ya kupeleke nguo ,begi,viatu etc kutokana na kuwa hawana urasimu wa biashara na kodi ni kidogo sana.Tanzania kuna urasimu na kukandamiza sana wafanyabashara kwa njia za kodi.kule wanasapoti wafanyabiashara kwa vitendo.

Pia soko ni kubwa kuna watu toka tanzania,Kenya ,rwanda,Congo,Burundi,Eritrea,Ethiopia,China,India etc na hakuna sheria kali za uhamiaji kama tanzania kwa ufupi kule hakuna kufatiliana utaifa ni free kabisa.Twende kwenye maswali yako sasa,

Sehemu ambazo unaweza nunua mzigo ni city centre lakin mitaa ya Ben Kiwanuka,Tax park,Copper complex,Arua park na Owino market na sehemu jiran na Owino market.
Kwa vile unataka mitumba ingia Owino Market uko vitu ni bei rahis sana ila inahitaji ubageini na ni lazima ubageini,viatu ( TimberLand )ambavyo nanunua Tanzania 90,000 tzsh kule nanunua kwa 15,000-18,000 tzsh ila wanakuanzia mbali unaomba upunguziwe.
Uko Owino wafanyabiashara wanajua kiswahili vizuri ila ukiambiwa bei,wewe sema ambayo ni kidogo sana kutegemea na mzigo pia wakat unanunua ndio wakat mzuri wa kujua pia utauza kiasi gani.
Tshirt ya 15,000 tzsh pale unapata kwa 1,500 tzsh tena hiyo bei rejareja kwa wewe ukinunua kwa uwingi bei ni rahis sana.Uganda imefanywa kama dampo la bidhaa hizo na watu wa ulaya,asia na america.

Sehemu ya kulala maeneo ya copper complex kuna guest nzuri moja inaitwa Galaxy Guest house ni nzuri sana,bei zake ni ndogo sana kutegemea na unachukua room gani bei uanzia 15,000 ugsh hadi 30,000 Ugsh ndio bei ya juu kabisa.
room zipo ghorofan chini ni mgahawa,pia ukikuta imejaa jiran na hapo kuna nyingine Boston guest house ni nzuri pia na ata wafanyakaz wa hapo uongea kiswahili .bei zake ni ndogo.na hizo sehemu ni jiran na shoprite pia kutoka hapo hadi owino ni dakika 2 tu kutembea na hizo sehemu ndio kwenye maduka mbalimbali.

Kuhusu kodi,kuna mbinu inafanyika nitaku pm si vizuri nikieleza hapa.Kuna njia mbili za kwenda uko kuna njia ya kupitia Nairobi hadi Kampala na kuna jia ya kati hadi Bukoba kisha unapanda bus za Friends huondoka saa moja asubuh kutoka bukoba kwenda kampala,na saa sita na nusu uko kampala,ukifika hapo chukua bodaboda hadi Galaxy Guest house au Boston zipo maeneo ya copper complex jiran na shoprite ambapo kwa bodaboda haizid 2000 ugsh.

Pia ata maeneo ya Arua park kuna guest za kulala pia. ( hayo maeneo ni kama unavyoona kariakoo majina ninayotaja ni kama mitaa tu mfano msimbazi etc hizo sehemu ziko jiran jirani )

Rate za ubadilisha pesa ni 1.5 hadi 1.6
yani 1,000 Tzsh ni 1550-1600 Ugsh.
wakat ambapo shule zinafunguliwa rate inashuka sababu wanafunz wengi wa kitanzania wanakuja na pesa na wanachange inaweza pungua hadi 1.5 au 1.55.

kuna bus kama Falcon utoka dar kupitia njia ya kati hadi bukoba kisha kampala.
njia ya nai mfano kuna spider utokea dar-nairob-kampala.

ni wewe sasa kuamua,nawajua watu wengi wanawake/wanaume wamefanikiwa sana kimaisha kupitia biashara hii.cha muhimu ukinunua kitu uombe sana kupunguziwa pia usiingiwe tamaa za kununua vitu ambavyo hukupanga kuna vitu vizuri sana kule na cha muhimu kuwa makini ili usiibiwe pesa,uporaji kule hakuna labda mtu achane pochi yake bila wewe kujua.

mkiwa na swali ulizeni
maelezo safi sana haya
 
@Moneystunna alipoteaga mda mrefu,sijui ilikuaje,ile ndege ya malaysia ilipopotea tu na yeye hakuonekanaga humu tena
 
Samahani dada masai can I get your phone number plz,, I need more clarification about this business
Sikufanikiwa kuenda ila rafiki yangu anaenda huko kufata mashuka..next year naenda..so hata nikichukua namba yako sitakupa mchanganuo dhahiri ila mwakani mapema kabisa naenda ug
 
Sikufanikiwa kuenda ila rafiki yangu anaenda huko kufata mashuka..next year naenda..so hata nikichukua namba yako sitakupa mchanganuo dhahiri ila mwakani mapema kabisa naenda ug
Muombe rafikiyo atupe mrejesho
 
Back
Top Bottom