Bentley la Joseph Kusaga kupigwa mnada

Bentley la Joseph Kusaga kupigwa mnada

Duh....anaisoma namba na yeye?
Ndomanake kitu ambacho mpaka sasa nimemsifu Magufuli....niile Style yake takutoingilika kiRAHIS kuna jamaa 1 Mzee wa matamasha alipiga Hela sana Enzi ya Mkwere sasa alipoingia Magufuli alijipitisha sana kutaka akubalike kwake lkn kaangukia PUA mbwembwe zote zimekwisha so hao jamaa waliwekeza sana kuinadi CCM wakiamini wataendeleza kula peke yao
 
Atalinunua mnadani kwa bei ya kutupwa
hakuna bei ya kutupwa tra wanataka kodi yao tu hata akinunua atakuwa kalipa kodi ambayo kashindwa sasa ukijumlisha na heka ya kuagiza inarudi palepale.
 
Ebu tupe thamani ya kodi ya gari linalo nunuliwa tuseme £70000 halafu tuone fairness na kama kweli sera ni encouragement ya magari mapya. Kitu kingine sio magari yote yana equal durability mtu anaenunua range rover lenye miaka kumi na Noah ujue kuna gap kubwa sana ya life span hapo sasa una limit mtu kuleta gari ambalo bado lina maisha zaidi ya kumi mingine katika nchi maskini kisa kodi.

Bandari aiwezi kutumika kama n'gombe wa maziwa serikari lazima ibuni vyanzo vya mapato kupitia uzalishaji wa ndani hizo ndio reliable sources sio kutaka kukamua watu wamoja wamoja wanaotaka kujipongeza kwa ubunifu wao wakati bado wanalipa kodi na wana ajiri watu.
Hio gari ya £70,000 kama imezidi miaka 8 kabla ya kodi yoyote inatozwa 25% ya uchakavu,hio ni £17500. Wakati gari mpya ya £70,000 haitakuwa na hio 25% ya uchakavu.
 
Usishangae siku ya mnada usiolione kwenye list, nimeshahudhuria minada mingi sana pale, kuna figisufigisu nyingi mno, kuna gari zile kali kali kamwe hutaziona zikua kwenye list siku ya mnada, ukifuatilia unaambiwa kuwa "mwenyewe kalipia" au unaambiwa kaununa waziri Fulani au hii ni ya mwenyekiti
 
Eric cartman unachoongea wanatumia Botswana kwa sasa gari unachajiwa Kodi kutokana na invoice utakayoonyesha hata uingize vogue uonyeshe invoice ya usd 10,000 wanaangalia iyo tuu watswana na ukiona magari imara na mapya ni mengi sana pia hapa kwetu huo mfumo haufai hata kidogo kinachotakiwa ni kupunguza kiwango cha kodi kwa yale magari imara zaidi na mapya..Zambia wamepunguza kodi ya Nissan Navara wamegundua ni gari imara unaweza ukaendesha km za kutosha wewe ni kubadili diesel fielter,sterling oil na blake fluid tuu na ni msaada kwa jamii kwa shughuli zoote kodi yake kwa ss ipo kidogo sana...hapa kwetu mengi ya magari ni garage,ofisi nyumbani..kodi ndogo lakini matatizo madogo madogo ni meengi sana..waangalie upya huo mfumo wa kodi uwe rafiki kwa walipa kodi ambao ni watanzania..
 
Hio gari ya £70,000 kama imezidi miaka 8 kabla ya kodi yoyote inatozwa 25% ya uchakavu,hio ni £17500. Wakati gari mpya ya £70,000 haitakuwa na hio 25% ya uchakavu.
Binafsi naona kama vile hizi kodi azijazingatiwa in terms of volume kama lengo ni mapato zaidi ninachoweza kusema sidhani kama kwa mwaka kuna magari mia yanaingia yenye gharama hizo kwa Tanzania (rough guess) ina maana hakuna faida ya vile za kodi zaidi ya kudeter tu uagizaji wake research inahitajika bandarini ya counter view kupima faida ya kodi za sasa kwa kuangalia upya kipi kinakuja na largest possible estimators ili kuzipanga upya hizi kodi kuna watu wanaacha kuleta magari ya maana kisa kodi tu na valuation za TRA.
 
Huyu jamaa ni mtu wa Mbwembwe nyingi sana lakini sasa hivi anaisoma namba.
 
Nimehudhuria hio minada kuna magari nilitaka kununua nikashindwa yaliuzwa kwa gharama zake za ushuru tu sasa sijui ilikuwaje.
Watu wanadhani kuwa minada ya tra ni mteremko. Sio hivyo.
 
Haha sawa Shark ,huyo jamaa sidhani kama amekosa hela ya kulipia hiyo gari ,sema ni kwa sababu alizoea vya kunyonga ndio alikua anacheki upepo unaelekea wapi

Hebu cheki hiyo list ya used Bentley continental kabla ya kulipiwa ushuru halafu piga na mahesabu baada ya kulipiwa ushuru ,niambie unanunua Virtz ngapi

Mileage 5,646? Dah hiyo si mpya kabisa na sio used, sie used ni Mileage 150,000 hahah
 
Back
Top Bottom