Ben Saanane anavyoteseka na kivuli cha unafiki...

Ben Saanane anavyoteseka na kivuli cha unafiki...

slaa na yeye anashuhudia huu mnyukano lakini inaonekana kaamua aangalie tu mpaka mwisho kila mwenye lake aweke hapa aone itakuwa je.......

Ndiye mwasisi wa vita hivi

Chama
Gongo la mboto DSM
 
----- Forwarded Message -----
From: Ben Saanane <bensaanane@yahoo.com>
To: mchangehabibu@yahoo.com; mchangehabibu@gmail.com
Sent: Friday, June 10, 2011 1:52 AM
Subject: V4V values & Objctvs


The tragedy of Tanzania is a pervasive pathology. Its leadership selection process
excludes its best while celebrating mediocrity. The incremental influence of that
pathology has created a failing state that is unable to do much more than uphold the
conclave of looters that hold the country hostage. In many ways, every election
process turns out to be much worse than the preceding cycle.
Upon taking power after stolen polls, the new leadership often proceeds to enthrone
a ruling ethos that is defined by a searing contempt for the people. That is why,
despite the billions of dollars that the Tanzania state has earned over five decades,
Tanzania remains at the bottom of the human development league. It is a fate that
Tanzania must reject because a better life is possible.​
Fifty years into Tanzania’s attainment of nationhood, it still has the status of what
domestic and international observers call a failed state, failing state, or failed asset.
Tanzania’s failure to belong to the comity of successful and functional states that
obtained the status of independent nationhood within the same decade is not
attributable to the lack of material and human resources. On the contrary, the
country’s economic, social, and political failure has resulted from the non-adherence
to the practice of true federalism and the consequent mismanagement of the nation’s
resources by most of its political managers since independence. Such managers have
ranged from military dictators to civilian presidents and governors imposed on the
electorate through rigged elections

What to do now?
What is direly needed now is how to get
Tanzania out of the hole of underdevelopment, corruption, and mismanagement.
Now is the time for truly patriotic Tanzanians to join the movement to save Tanzania
from its current state of failure by joining forces with the Voice for the Voiceless Tanzanians (V4V) Group.
Now is the time to liberate Tanzania from the grips of its predators. V4V believes that​
Tanzanias’s failure is avoidable; that Tanzania can be saved. But to stop the politics of
self-imposed failure, a new crop of leaders with a patriotic outlook and a
transformational vision from those of its predatory leaders must move to the centre
of the country’s political space to re-engineer it away from chronic failure and chart
a new course in the direction of success. The V4V is blazing the trail of change and
transformation in Tanzania. V4V values has been designed to bring liberty,
security, and prosperity to all Tanzanians, is being made available to all Tanzanians, through building strong citizens to create wealth and
make contributions to modern global civilization.


wewe usaliti wako unakutafuna!!!!
Toka usiku unaulizwa ulichukua hatua gani?
 
----- Forwarded Message -----
From: Ben Saanane <bensaanane@yahoo.com>
To: mchangehabibu@yahoo.com; mchangehabibu@gmail.com
Sent: Friday, June 10, 2011 1:52 AM
Subject: V4V values & Objctvs


What to do now?
What is direly needed now is how to get
Tanzania out of the hole of underdevelopment, corruption, and mismanagement.
Now is the time for truly patriotic Tanzanians to join the movement to save Tanzania
from its current state of failure by joining forces with the Voice for the Voiceless Tanzanians (V4V) Group.

......

Huyu BEN mtazamo wake ulikuwa kama wa Mapalala: alitaka kuazisha chama ndani ya chama.
 
Nadhani uongozi wa juu wa chadema ukae chini na kuwadhibiti watu wa namna hii na naona kazi walisha ianza,hawa waliotumwa kuharibu mwelekeo wa chama ni kuwadhibiti pasi ya kuwaangalia usoni,rungu lifanye kazi,ni bora chama kibaki na watu wachache lakini waaminifu na wenye malengo ya kukiendeleza chama,kuliko kuwa na kundi kubwa la watu lenye malengo yasiyokitendea haki chama.

{KUANZA UPYA SIO UJINGA,by mrisho mpoto} wakati chama kina jiandaa na chaguzi ni vyema kuondoa hawa watu mapema ili mwaka 2013 chama kiwe na watu wenye msaada na chama.

kulea haya makundi ama watu wa namna hii ni kulea mchawi mwenye malengo ya kuroga na kuharibu malengo mazuri ya chama,chama hakiwezi kuendelea kwa kulea mamruki tena wanaotumiwa kwa faida ya wachache.

Tunaelewa kuwa uongozi wa Chadema unatumia sana JF na hili nzuri sana kwa mstakabari wa chama,maana hata serikali ya uchina wao wanatumia sana Sina WeiboChinesemicroblogging (weibo) na kupambana na walarushwa na habari nyingi huanzia huko.

Nanyi viongozi wachadema ni vyema mkaendelea kutumia JF kama sehemu ya kupata habari na kuzitumia vyema kupambana na hawa wasiokitakia mema chadema.

Walisema mwisho wa dunia ulikuwa jana,lakini sasa naona si mwisho wa dunia bali ni mwisho wa wanafiki ndani ya chadema,sasa wameanza kuonekana kwa kurunzi na kiukweli huu ni mda wa kuwatokomeza kabisa bila hata kuwaonea huruma.
 
Hapa kuna uhuni mwingi sana.
Ben unaweza kutuambia kwanini Friends of Slaa walikutimua?
Unajua uasisi wa M4C?"..........Ben acha uhuni wewe.
 
Ndiye mwasisi wa vita hivi

Chama
Gongo la mboto DSM......

Mkubwa chama; hebu tupe mwongozo jinsi Slaa alivyohusika kuuanzisha myukano huu ili tuweze kupata mwangaza zaidi juu ya kile kinachojiri.
 
Mchange,zitto kabwe,nyie ni wanafiki katika chama chetu,Chadema mliikuta na mtaiacha,na mjue hamna wafuasi wanaowaunga mkono\.

Watanzania wana elimu kubwa sana,wanajua kila kitu,na endeleeni na ushirikina wenu we na Zitto,sisi tunamwamini Mungu! Its shame to Zitto to say ameaga kigoma na atakagusa kwao watapukutika kama panya,kiongozi anayeamini ktk ushirikina si kiongozi.

.......

Walimshindwa watu Zitto,utaweza wewe sisiminzi?Uongo wa saa nane umewekwa wazi.
 
Tumekesha siku 2, asubuhi nikaamka labda nitakuta watu hawa wameshikana mikono ya amani-IT'S OK, lakini waaaaapi. Jamani tuoneeni huruma wengine tumedoji lectures,

Hauna tape recorder? Hapa ni moto tu mkuu!! Kushikana mkono na mnafiki ili iweje?

Chama
Gongo la mboto
 
ndio maana mimi nasema tukiwa watulivu tutasikia mengi sana hapa, na mimi leo silali mpaka aje saa nane nimsikie anakimbiaje humu. duh


Kwani wa kukimbia peke yake wapo wengi tu ila kitaeleweka tu .........:israel:
 
mkubwa chama; hebu tupe mwongozo jinsi Slaa alivyohusika kuuanzisha myukano huu ili tuweze kupata mwangaza zaidi juu ya kile kinachojiri.

Jifundisheni kuunganisha channel sio mnakwenda kama vipofu; Ben Saanane anautaka uraisi?

Chama
Gongo la mboto DSM
 
Last edited by a moderator:
Habari, nimeona mchango wangu huu niuanzishie uzi ili tujadiliane kwa mapana..

Mpaka tuufikie tunaouita ukombozi wa pili, basi tuna kazi na safari ndefu sana!

Kama vijana tunaweza tukainuka na kuanza kuporomosha mashtaka na kutaja majina ya watu bila hata facts, basi kazi ipo ndugu zangu.

Ufahamu wangu ni kuwa ili tufanikiwe kuwaondoa CCM madarakani lazima tufanye kazi hiyo kama timu moja, mawazo yangu ni kuwa hatutaweza kufikia hatua yoyote ikiwa tutakuwa na vijana wa namna hii.

Vijana wa aina ya Ben Saanane wanaoweza kukaa, kutengeneza mgogoro, kubuni njia za kuuendesha mgogoro, kutafuta suluhu na hatimaye kwenda kuuza huo mgogoro kwa viongozi wengine huku akiamini kuwa anakinusuru chama hakika anakosea sana.

Vijana wa aina ya Saanane ambao kazi yao nikutumia muda na akili zao nyingi kuwarubuni na kuwagombanisha vijana wa chama na viongozi wa chama ni hatari pengine kuliko ukoma.

Kwa kuwa mara kadhaa amekuwa akinitaja kwenye mijadala yake yote. Bila hata kuangalia namna ninavyohusika, na kwa kuwa na leo hii ameamua kunitaja na kunihusisha moja kwa moja, na kwa kuwa viongozi, vijana na wanachama wengi wa chadema wamekuwa wakinihusisha mimi kuwa karibu sana na zitto kabwe. leo nitasema kitu kwenye hili.

1. Naomba niweke wazi hapa leo, kuwa sikuwahi kumfahamu mtu anayeitwa Ben Saa nane kabla mwezi wa nne 2011.
sijawahi kumsikia jina wala kumuona sura yake.(hawezi kubisha kwenye hili)

2. Ben ndiye alikuwa wa kwanza kunipigia simu, kati kati ya kipindi cha kampeni za uchaguzi wa BAVICHA - 2011 mimi nikiwa nagombea uenyekiti na yeye akiwa ni mgombea wa kimkakati(alitumwa na baadhi ya viongozi kuja kuuvuruga uchaguzi-uthibitisho upo) ambapo aliponipigia simu na kunieleza kuwa tuna haja ya kukaa kama wagombea na kuangalia namna tunaweza shiriki salama kwenye huo uchaguzi kwa madai kuwa amepata tetesi makao makuu wanamgombea wao na wanajiandaa kukata majina ya watu, jina lake na langu yakikiwemo. Nilimsikiliza na kumpuuza.

3. Baada ya hapo sijawahi kuwasiliana nae tena ben saa nane, mpaka usiku wa siku jina langu limekatwa na kamati kuu ya chama, tena aliwasiliana na mimi kupitia grayson nyakarungu, aliyekuwa swahiba wake&#8230;cha kusikitisha ni kuwa mwana mkakati ben aliwashauri mwampamba, nyakarungu na kisandu kuungana, akanishirikisha na mimi. Huku nikijua dhamira yake kuwa ni unafiki. Nikamsikiliza kwa kuwa sikuwa tena na cha kupoteza (nimeshaenguliwa tayari).

Masikini ya mungu BEN akawahadaa vijana wa watu (Mwampamba na Nyakarungu) wakaenguliwa huku yeye akiwa ni wa kwanza kukiri kuwa wameamua kuongeza nguvu.

4. Unafiki wa Saanane uliendelea siku ya tatu baada ya kuisha kwa uchaguzi wa BAVICHA maana baada ya kukatwa jina langu, wanafiki wengi walifikiri ningetoa tamko la kukipinga chama ama kuhama chama, sikufanya hivyo, kwangu mimi uchaguzi ule haukuwa ligi, ilikuwa ni mechi tu ya kirafiki. Hapo mwenyekiti wa chadema wilaya ya Kibaha akaomba kukutana namimi, nikakubali, nikakutana nae ubungo plaza, tukiwa hapo tulikuwa na mwampamba na nyakarungu, aliposimuliwa saa nane kuwa tunaenda kukutana ubungo Plaza, akaandika humu jamii forums kwa kutumia ID fake yake kuwa tumekutana na mimi nina mpango wa kuhama chama.

Nlimwambia Mwampamba kuwa saa nane ana kazi maalum, mwampamba hakunielewa, akanipinga sana sana sana, naamini leo atanielewa vizuri sasa.

5. Kwa kipindi chote hicho saa nane alikuwa anaitisha vikao vya kila aina, saa nane anatukana na kutoa kejeli za kila aina kwa viongozi wa kuu hasa katibu mkuu na mwenyekiti (lengo ni kutaka kluthibitisha kuwa kuna vijana wanawapinga viongozi hawa). Ninataja maeneo machache ambayo saa nane alipenda kuitishia vikao vyake, KWA JOHN FEDHA-KINONDONI, BLUE PEARL HOTEL-UBUNGO PLAZA na LUCH TIME HOTEL-UBUNGO EXTERNAL&#8230;.naomba nikiri hadharani hapa, si mimi, mwampamba wala Juliana anayemsema aliyewahi kwenda kukutana na saa nane akajinunulia kinywaji wala chakula&#8230;kwa saa nane huwa tukifika tunakula, tunakunywa mpaka tunapochoka saa nane yeye hulipia-tukambatiza jina tukamwita manji. (lakini siku zote nimekuwa nikiwaambia wenzangu kuwa kaeni chonjo na huyu jamaa ana kazi maalum---leo wamejionea)

6. kati kati mwaka jana 2011 mwenyekiti wetu wa taifa freeman mbowe alikamatwa kwa kilichodaiwa kutokutii amri ya mahakama hapa napo saa nane akafanya vitu vyake, kama kawaida yake, akawakusanya vijana wake wote ambao yupo nao kwa kazi maalum akaanza kuwajaza ujinga&#8230;naomba nikiri tena hapa kuwa usipokuwa makini ni rahisi sana kuingia kwenye kumi na nane za huyu jamaa. Ni lalzima uwe makini kama mchange kumshinda na ndio maana ananichukia sana sana.

Mimi nimefundishwa kuwafahamu wanafiki. Hasa ninapokuwa naongea nao uso kwa macho saa nane kwangu alikuwa mnafiki kwa hiyo sikumpa nafasi hata chembe.

7. katika kipindi chote hiko sijawahi kumsikia mwana mkakati saa nane akiwasema vizuri viongozi wa chadema. Mtu pekee aliyekuwa anamsifia alikuwa ni zitto.

SAA NANE NA ZITTO
Nimeshtushwa sana na maandishi aliyoyaandika Saanane leo, hii inatokana na ama kuchanganyikiwa au kujihami kutokana na kushushuliwa na kuonekana mwongo. Naomba nieleze vizuri hapa.

1. Ben Saanane ndiye alikuwa muitishaji mkuu wa vikao vya hotelini(makutano) akiwa na saa yake ya kurekodi aliyonunuliwa na kiongozi mmoja wa chama kwa kinachoitwa kazi ya ushushu. Yeye ndiy aliyekuwa mwenyekiti wa vikao na mwandishi wa kila kinachosemwa.

2. Ni BEN SAANANE ndiye aliyewashawishi na kuwalazimisha wenzie anaowasema leo ni wasaliti waunde kikundi. Hakuishia hapo, akakitunga mpaka na jina. Kuwa ni ''patriotic movement seven'' na akakifupisha PM7.(V4C-VOICE FOR VOICELESS) Akashawishi kikundi hicho kizunguke nchi nzima kuhamasisha viongozi wa huko kufanya mageuzi ndani ya chama. Saa nane unafiki utakupeleka pabaya.

3. Ni BEN SAANANE ndiye aliyegawa majina ya kuitana miongoni mwa wana kikundi hiko, yeye akajipa jina la COBRA, mimi akanipa MDUDE (kwa kuwa nilikuwa naijua dhamira yake niliendelea kumkeli)

4. Ni BEN SAANANE ndiye aliyeshauri namna ya kuhakikisha kikundi hicho kinapata pesa, wakati mimi nilimpinga ku anzia kuanzisha hiko kikundi mpaka namna ya kukusanya kwake pesa..wakati yeye alikuwa anasisitiza kwenye njia ya kukusanya michango, tena tuwachangishe viongozi wa chama na watu wengine maarufu.

5. Akiwa mkweli atakumbuka na kukiri kuwa nilimwambia kuanzisha kikundi hicho ni sawa na kuanzisha chama ndani ya chama, aliumizwa na misimamo yangu sana.

6. Ni BEN SAANANE ndiy aliyekuwa anasisitiza tuombe kukutana na zitto kabwe ili tumuombe ufadhili wa kufadhili kikundi chetu kilichoasisiwa na SAANANE na akanipa jukumu la kuhakikisha ninamwambia na kumshawishi zitto tukutane nae tufanye nae kikao, sababu yake kubwa ni kwamba Zitto ni rafiki yangu sana na itakuwa rahisi kumpata. Hapa tulirumbana sana, mimi nilielewa dhamira yake na nikiri leo hadharani kuwa nilimshauri zitto asikubali kukutana na kikundi hiki, na niukamwambia kabisa kuwa lengo la kikundi hiki ni kuthibitisha makundi ndani ya chama.-leo yametimia.

7. Ni SAANANE aliyewaapia kujito a kwenye kikundi alichokianzisha mwenyewe kwa sababu ya kutokumpata zitto kwenye kikao, siku ambayo saa nane alipendekeza zitto tukutane naye zitto alikwenda marekani kuzindua tawi la chadema, ni saa nane ndiye aliyenilaumu sana kuwa kwa nini sikumuarifu kuwa zitto hatokuwepo, nilimjibu sio wajibu wangu kuwaambia watu kuwa zitto yupo ama hayupo.

8. Ni Saanane huyu huyu mnafiki tuliyerumbana naye hasa mimi nay eye juu ya namna ya kumshirikisha zitto kwenye michango ya kikundi chake cha PM7. Naomba ninukuu mabishano yetu..mimi '' kama swala ni kukusanya pesa, kwanini tumfuate Zitto kwanza na sio mtu mwengine yeyote''?...saa nane..''kwa sababu zitto ni kijana na ana mitazamo chanya kwa vijana wenzie na pia tunafanana nayo mitazamo hiyo sio kamakina mnyika wao status quo''&#8230;mimi..''kama Zitto tumemwomba tuonane naye na amesafiri bila kutujibu hauoni kuwa anatuudharau, kwanini tujipeleke kwa zitto tunayemnung'unikia kila leo?''..saa nane.. '' hapana ni lazima atusaidie, zitto kwa vyovyote lazima agombee uenyekiti, na hatuwezi fanya hii kazi tukamfungulia milango bila nay eye kutoka jasho lake, ni lazima atupe pesa''&#8230;.mimi sasa kwanini tunakataa wenzetu kutumiwa halafu na sisi tunajitumikisha wenyewe kwa zitto?''&#8230;saa nane..''Mchange, hakuna jinsi tunaweza acha mshirikisha zitto, mwisho wa siku zitto atakuwa beneficiary kwenye huu mpango''&#8230; &#8230;&#8230;&#8230;&#8230;&#8230;&#8230;&#8230;ukifuatilia kwa makini mazungumzo yetu ambayo kwa bahati nzuri nimeyarekodi kuanzia siku ya kwanza mpaka ya mwisho utaweza kumuelewa SAANANE kuwa alikuwa na kazi maalum.

Niseme hapa kuwa wote kwa pamoja, saa nane na zitto kila mmoja ameniambia kwa mdomo wake kuwa hawajawahi kuonana uso kwa macho, zitto yeye anasema kuwa anaweza akakutana leo na saa nane barabarani na akapishana nae bila kumfahamu.

Wote kwa pamoja wameniambia kuwa mawasiliano yao huwa ni kwa simu hasa SMS na mara chache kwa emails.

Na moja kati ya malalamiko aliyokuwa ananipa saa nane nimpe zitto ni kuwa..
1.kwa nini hapokei simu za wapiganaji wake akiwemo yeye?...
2..kwanini anakuwa na mpiganaji kama saa nane na hataki kuonna nae&#8230;.
3&#8230;kwanini hataki kukifadhili kikundi cha PM7. a.K.a V4C(VOICE FOR VOICELESS)?

Kwa mtiririko wa matukio ulivyo, na kwa jinsi SAA NANE alivyoandika mashtaka yake dhidi ya zitto huku akizani anamchafua, hakika amejidharirisha sana.

Mtu mmoja mpinzani mkubwa sana wa zitto amenitumia sms kwenye facebook, ananiambia JF vipi maana COMPUTER YANGU HAIFUNGUI..huyu nae ni mjinga sababu anashabikia ujinga.

Kumshambulia zitto kwa mashtaka ya uwongo namna hii kuna mfanya zitto awe na nafasi ya kuonekana anasingiziwa mamba mengi sana hasa ndani ya chama.

Kwa mimi ninayemfahamu Saanane nje na ndani, na ninayefahamiana na kufanya kazi na Zitto, kwa mashtaka haya ya uwongo, basi hakika nitazidi kumuamini Zitto.

Nitazidi kuamini kuwa Zitto amesingiziwa mambo mengi sana ndani na nje ya chama, ninazidi kumuamini na kumtia moyo kwamba hizi ni hatua za mwisho za watu wanaokupinga, wakishindwa kukupinga kwa facts, watakupinga kwa uwongo&#8230;saa nane amekubali kutumika vibaya kwa kisingizio cha kuwa anakilinda chama na viongozi wake.

Napata mashaka kama anakielewa anachokisema, huwezi kumtenganisha zitto na uongozi wa chama. Zitto ni naibu katibu mkuu wa chama, hivyo sio rahisi kumchafua zitto ukaacha kukichafua chama.

Nimemwona saa nane anajitetea kutishiwa kuuawa, saa nane, ZITTO akiwa na mimi amenusurika kuuawa kwa ajali ya gari hivi karibuni tukitokea morogoro kwenda iringa(siku ya kumbukumbu ya kifo cha mwalimu nyerere) baada ya wapinzani wake ndani ya chama kwenda kufungua nati za tairi la nyuma ili afe, kweli zitto ameaga kwao, kweli zitto hataweza kufa kwa mipango ya mungu, hatukufika mbali tuliushtukia mchezo tukarudi morogoro mjini na zitto akaendelea na retreat yao mpaka kesho yake tukarudi dar wala hakuitangaza hii sababu aliwadharau na mbinu dhaifu.

Sio rahisi kuitoa roho ya mwanadamu mwenzio, sio rahisi kumuua zitto kama mlivyojaribu mara kadhaa na timu yenu ..

Nasikitika sana kama vijana sasa tunaeza kusimama kidete na kuandika uwongo na kuutetea bila hata woga kama ndugu yangu Saanane.

Hasira yako ya mimi kukushtukia na kuwaambia kina Mwampamba na Juliana kuwa wewe kila siku una warekodi na kwenda kuuza habari kwa kiongozi mmoja wa juu ambaye humtumia HAWARA WAKE kutuma SMS za matusi kwa watu, isiwe sababu ya kuanza kuwachafua watu ndugu yangu.

Mchafue Zitto kama unahisi una sababu ya kufanya hivyo kwa mambo ambayo una ushahidi nayo.

SAANANE acha tabia ya KUBUNI MGOGORO, KUUANZISHA, KUUENDELEZA, NA KISHA KUUTUMIA KAMA CHANZO CHAKO CHA KUPATA PESA.

SAA NANE, Waislam wanasema sifa za mnafiki tatu (ayatul munafiq tharasa).
1. akiongea huongea uwongo..
2..akiaminiwa hajiaminishi/hudhiaki..na ..
3..akiahidi hatimizi..

KATIKA KUUTHIBITISHA UNAFIKI WA SAA NANE KWA WALIOMTUMA. NAOMBA NIWEKE NAKALA YA EMAIL ALIYONITUMIA JUU YA KUANZISHA KIKUNDI CHA PM7 AMBACHO ALITAKA TUKISAJILI KAMA NGO IITWE VOICE FOR VOICELESS KISHA IZUNGUKE MIKOANI KUFANYA USHAWISHI KWA VIONGOZI WA CHAMA WA HUKO...

----- Forwarded Message -----
From: Ben Saanane <bensaanane@yahoo.com>
To: mchangehabibu@yahoo.com; mchangehabibu@gmail.com
Sent: Friday, June 10, 2011 1:52 AM
Subject: V4V values & Objctvs


The tragedy of Tanzania is a pervasive pathology. Its leadership selection process
excludes its best while celebrating mediocrity. The incremental influence of that
pathology has created a failing state that is unable to do much more than uphold the
conclave of looters that hold the country hostage. In many ways, every election
process turns out to be much worse than the preceding cycle.
Upon taking power after stolen polls, the new leadership often proceeds to enthrone
a ruling ethos that is defined by a searing contempt for the people. That is why,
despite the billions of dollars that the Tanzania state has earned over five decades,
Tanzania remains at the bottom of the human development league. It is a fate that
Tanzania must reject because a better life is possible.​
Fifty years into Tanzania's attainment of nationhood, it still has the status of what
domestic and international observers call a failed state, failing state, or failed asset.
Tanzania's failure to belong to the comity of successful and functional states that
obtained the status of independent nationhood within the same decade is not
attributable to the lack of material and human resources. On the contrary, the
country's economic, social, and political failure has resulted from the non-adherence
to the practice of true federalism and the consequent mismanagement of the nation's
resources by most of its political managers since independence. Such managers have
ranged from military dictators to civilian presidents and governors imposed on the
electorate through rigged elections

What to do now?
What is direly needed now is how to get
Tanzania out of the hole of underdevelopment, corruption, and mismanagement.
Now is the time for truly patriotic Tanzanians to join the movement to save Tanzania
from its current state of failure by joining forces with the Voice for the Voiceless Tanzanians (V4V) Group.
Now is the time to liberate Tanzania from the grips of its predators. V4V believes that​
Tanzanias's failure is avoidable; that Tanzania can be saved. But to stop the politics of
self-imposed failure, a new crop of leaders with a patriotic outlook and a
transformational vision from those of its predatory leaders must move to the centre
of the country's political space to re-engineer it away from chronic failure and chart
a new course in the direction of success. The V4V is blazing the trail of change and
transformation in Tanzania. V4V values has been designed to bring liberty,
security, and prosperity to all Tanzanians, is being made available to all Tanzanians, through building strong citizens to create wealth and
make contributions to modern global civilization.


aiseee, mpaka emails tena alikuwa anatuma utafikiri mzalendo kweli!..mungu atakuwa kaahepusha na hatari kubwa sana.
 
Mkuu kunasehemu umeona Zitto amehusika na kuonana au kuzungumza au kufanya chochote na kikundi hicho au hao vijana?
Zitto hahusiki na huu upuuzi,Sema uimara wake kisiasa Ben saanane akaona ni muhimi aushushe kwa aina hii aliyoihagua.

Taswira, tuseme Zitto hakuonana na kikundi cha saa nane, Je unakubali kuwa alishiriki kumhujumu Lema na Chama kule Arusha ???? na mbaya zaidi akamhusisha na mshauri wa Chama???
Ukweli unabaki kuwa Zitto, Ben na akina Mchange, Juliana ni wasaliti tofauti iliyopo ni kwamba Ben kakiri, wengine wanajitahidi kujisafisha na wewe Taswira U mmoja wao wa wanaojisafisha.
Usaliti ni usaliti tu. Kwa kifupi- kuku hapakwi rangi mdomoni.
 
inaonekana ngoma unaijua kuicheza ndio sababu akili yako imeleekea huko; wajinadi hujaonja tamu pilipili ilhali waogopa makali ya pilipili? Ulijuaje kama pilipili kali? Yakhe karibu usiogope sisi waungwana tutakufundisha maadili mpaka jina utabadili badala ya kujiita Msemaovyo utajiita waridi.

Chama
Gongo la mboto DSM
Mkuu Chama,

maneno yako na hekima zako muda si mrefu huyu kasuku atakuimbia nyimbo mwanana.

Mmmhh!!!
 
Katika maelezo ya Ben Saanane, kuna mahali anakiri alikuwa kwenye kundi la mpango 'maalum'. Na kundi hili liliota mizizi wakati wa uchaguzi wa BAVICHA. Lakini pia Ben anasema kwa sasa ameshajitoa kwenye hilo kundi. Mambo ambayo ningetaka kusikia toka kwa hawa wengine waliotajwa kwenye hii list na hasa hawa wanajitokeza kujibu ni haya:

1. Ni kweli walikuwa kwenye kundi moja na Ben Saanane?
2. Kwa sasa bado wanaendelea kuwa wanachama wa huo mpango 'maalum?
3. Kama hawajajitoa (au walau kutanganza kujitoa kama alivyofanya Ben Saanane), wanasubiri nini?

Kwa kifupi ndugu Mchange anatakiwa kusema kama V4V bado iko hai na wanachama wake ni wakina nani? Ni lini mara ya mwisho wana V4V walikutana na waliafiki nini?

Nasema haya kwa sababu 'normally' wakati wa campign za chaguzi (kwa kundi lolote lile, iwe chama cha siasa au hata mwenyekiti wa mtaa) kila mgombea anakuwa na kundi lake la kumfanyia campaign. Hivyo kuundwa kwa vikundi its ok to some extent. Shida tuliyonayo hapa Tanzania - na hii kwa kwa vyama vyote vya siasa, ni tabia ya kuendeleza makundi hata baada ya kumalizika uchaguzi. Watu wanaendelea na vikumbo utadhani uchaguzi bado haujafanyika. Tumeona madhara ya 'mimtandao' CCM, na sasa naona CHADEMA wanaanza kuugua ugonjwa huo huo wa 'mitandao'. Hili ni tatizo kwenye siasa zetu.
 
Asante sana kamanda Mchange kwakuleta huu ufafanuzi, maana haya uliyoyaandika ndiyo nilkiyotaka kuyatolea ufafanuzi japo bado nitatoa ufafanuzi wangu kuhusu hizi shutuma ambazo kwangu mimi nachokiona ni sawa na mtu kuchimba shimo halafu akatumbukia yeye mwenyewe.

Suala la Ben kutumiwa kimkakati katika harakati zakumchafua zitto na sisi ambao wao hutuita masalia wala halijaanza leo, huu ni mkakati unaoratibiwa dhidi ya Zitto pamoja na vijana ambao wanamuunga mkono Zitto, nazidi kusisitiza kwamba Ben Saanane anatumia uongo kuuaminisha umma kwamba anamfahamu Zitto kitu ambacho hata nafsi yake nina hakika inamsuta.

Ben acha kukimbia kivuli chako, sio rahisi kumchafua Zitto kama unavyoweza kudhani, japo mnajitahidi sana lakini hamtofanikiwa.

Palipo ukweli, uwongo hujitenga .
daaah!inaonekana ulikuwa unasubiri post ya mchage kwa hamu sana na wewe toa ya kwako mama
 
mhh makubwa mkuu,saanane inaonekana anapenda sana totoz

sio anapenda watotoz ndio wanampenda eti ni hb...ndio maana wanakamua wauza sura wenye channel wanamuuzia mafile saaa8..saa8 ana mafile mengi sana ya wauza sura hadi wa magamba mtakomaa hii ndio jf watu watajua yote aha hah ahah
 
Leo hapa ngoma inogile maana kwa mujibu wa sub tetesi hapa kwamba kuna audio na Video ambazo zitamwaga hapa very soon na kumuweka mtu mzima uchi.........
Waongo endele sana na uongo ila kama nilivyokesha siku 2 basii leo hakuna kukesha kwai mambo yote yataenda kuwa hadharani na intelejensi ya chama iwe makini kuchukua kila data ila tusiingie na wanafiki ktk nchi ya ahadi.
 
slaa na yeye anashuhudia huu mnyukano lakini inaonekana kaamua aangalie tu mpaka mwisho kila mwenye lake aweke hapa aone itakuwa je.


chama hakina nafasi kwenye huuuuuu uuuuupuuuuzi wacha wachambane dhambi ni mbaya hawakuutumwa na chama kufanya haya usihusishe kabisaaaaaaaaaaa yaani cdm

 
Back
Top Bottom