Bei kubwa za dawa Nigeria zimewafanya baadhi ya wagonjwa kugeukia tiba asili

JanguKamaJangu

JF-Expert Member
Feb 7, 2022
2,308
5,460
Gharama za kubwa za baadhi ya dawa nchini Nigeria kiwango ambacho kimepanda takribani mara kumi katika miezi michache iliyopita, kimewalazimisha baadhi ya wagonjwa kupunguza dozi au kugeukia tiba asilia.

Maafisa wa sekta ya dawa wamesema kushuka kwa thamani ya Naira baada ya kuondolewa katika udhibiti wa sarafu mwezi Juni kumefanya bei za bidhaa mpya kupanda.

Wakati Sodiq Ajibade alipokuwa akitoka katika duka la dawa mjini Lagos alikuwa ameshika dawa za pumu, aina moja ya dawa hakuwa nayo mkononi mwake kwa sababu hana pesa za kuinunua.

“Nilikuwa nikinunua dawa nilizoandikiwa na daktari za aina tatu, lakini sasa nimepunguza na kununua mbili ambazo ni penicillin na aminophylline” alisema Ajibade.

Rais wa Jumuiya ya Famasia ya Nigeria Cyril Usifoh, amesema dawa nyingi zinatoka nje ya nchi wakati watengenezaji wa ndani wanategemea uagizaji wa malighafi za kutengenezea dawa kutoka nje.

Tangu mwezi Juni, Naira imepoteza nusu ya thamani yake, na kuongeza bei ya kila kitu kuanzia dawa za maumivu mpaka dawa za magonjwa sugu.

“Ninacho khofia hasa ni vitu kama dawa za kansa, dawa za kuzuia shinikizo la damu, dawa za kisukari. Bei zimepanda sana” alisema Usifoh.

Dawa ya pumu ya Seretide inayotengenezwa na kampuni ya GSK kwa mfano mwezi April ilikuwa ikigharimu Naira 8,000 lakini sasa katika maduka ya rejareja inauzwa kwa Naira 70,000. Bei za dawa za antibiotic kama vile augmentin zimepanda na kufikia Naira 25,000 kutoka Naira 4,500 mwezi Julai.

Waziri wa Afya wa Nigeria na Shirika la Taifa la Chakula pamoja na Utawala na Udhibiti wa dawa haukuweza kujibu maombi ya maoni.

Msemaji wa GSK amesema uhaba wa fedha za kigeni umeathiri uwezo wa GSK kusambaza dawa na chanjo katika masoko, na kusababisha kutoweka kwa dawa madukani.

==================

Nigerian patients feel pain of soaring drug prices

When Sodiq Ajibade emerged from a Lagos pharmacy holding asthma medication, one drug on his prescription was missing because he did not have the money to buy it.

The price of some medicines has risen almost tenfold in Nigeria in the past few months, forcing patients like Ajibade to cut his dose or turn to traditional alternatives.

Pharmaceutical industry officials said the plunge in the value of the naira after the removal of currency controls in June has sent prices of new stocks rocketing.

British drug maker GSK (GSK.L) is moving from GSK-controlled local operating companies in Nigeria to a third-party direct distribution model. Some industry officials said this was also adding to woes, which GSK denied.

"I used to buy three medicines prescribed to me but now I have reduced to two, that is penicillin and aminophylline," said Ajibade.

Research firm Statista says only 3% of Nigerians have health insurance, meaning patients must find the money themselves to buy medication.

Nigeria's health ministry and National Agency for Food and Drug Administration and Control did not respond to requests for comment.

A GSK spokesperson said foreign currency shortages had affected GSK's ability to maintain consistent supply of medicines and vaccines in the market, leading to stockouts.

"The price increases we are seeing in Nigeria are not as a result of the decision to change the business model, and we regret that market forces outside our control have impacted the price of remaining stock in the market," the spokesperson said.

Cyril Usifoh, president of the Pharmaceutical Society of Nigeria said most drugs were imported while local makers relied on imports for the pharmaceutical ingredients to produce medicines.

he naira has lost half its value since June, raising prices of everything from pain killers to drugs for chronic disease.

A Seretide asthma inhaler manufactured by GSK, for example, cost up to 8,000 naira ($9.42) in April but now retails for up to 70,000 naira. Antibiotics like augmentin cost as much as 25,000 naira, up from 4,500 naira in July.

Source: Reuters
 
Hatari sana Mkuu.

GHARAMA ZA MAISHA ZINAONGEZEKA KILA UCHWAO.

KaziKweliKweli/JobTrueTrue
 
images (30).jpeg
baado hamjasema.
 
Back
Top Bottom