Iselamagazi
JF-Expert Member
- Sep 26, 2011
- 5,922
- 6,009
Nimesikia msemo huu mara kadhaa katika jamii zetu.
Week- end moja hivi nilitoka out na rafiki yangu. Tulitafuta sehemu nzuri ktk pub moja hivi na kuagiza vinywaji; taratibu tuliendelea kubadilishana mawazo kuhusu mustakabari wa nchi yetu pamoja na mambo mbali mbali ya kisiasa yanayoendelea hapa nchini kwetu.
Katika meza ya jirani, walikaa wanaume wanne na wanawake wawili. Walikuwa wakibadilishana mawazo kama sisi
kwa sauti za kawaida. Baadae kilevi kilipokolea wanaume wawili katika ile meza jirani yetu walianza kubishana kwa kutumia nguvu nyingi na kwa sauti kubwa. Mmoja kati ya wale wanaume wawili waliokuwa wakibishana aliamua kusimama huku akiyumba na kubadilisha lugha; alizungumza hivi: " Listen, I am a successful man, but behind me are my books. No woman there. Woman are overrated. Mr. Kimaro please refute your argument otherwise................ " Baadaye mwanamke mmoja katika lile group, alimsihi sana yule bwana aliyekuwa amesimama, hatimaye alimsikiliza na kukaa. Baadaye ilijulikana kuwa mabishano yao yalihusu usemi huu; Behind every successful man there is a woman.
WANA JF KUNA UKWELI KTK USEMI HUU? LET US COMMENT.
Week- end moja hivi nilitoka out na rafiki yangu. Tulitafuta sehemu nzuri ktk pub moja hivi na kuagiza vinywaji; taratibu tuliendelea kubadilishana mawazo kuhusu mustakabari wa nchi yetu pamoja na mambo mbali mbali ya kisiasa yanayoendelea hapa nchini kwetu.
Katika meza ya jirani, walikaa wanaume wanne na wanawake wawili. Walikuwa wakibadilishana mawazo kama sisi
kwa sauti za kawaida. Baadae kilevi kilipokolea wanaume wawili katika ile meza jirani yetu walianza kubishana kwa kutumia nguvu nyingi na kwa sauti kubwa. Mmoja kati ya wale wanaume wawili waliokuwa wakibishana aliamua kusimama huku akiyumba na kubadilisha lugha; alizungumza hivi: " Listen, I am a successful man, but behind me are my books. No woman there. Woman are overrated. Mr. Kimaro please refute your argument otherwise................ " Baadaye mwanamke mmoja katika lile group, alimsihi sana yule bwana aliyekuwa amesimama, hatimaye alimsikiliza na kukaa. Baadaye ilijulikana kuwa mabishano yao yalihusu usemi huu; Behind every successful man there is a woman.
WANA JF KUNA UKWELI KTK USEMI HUU? LET US COMMENT.